Taarifa rasmi ya kusitisha mgomo kutoka chama cha madaktari 10/03/2012

Kenya, Chadema, Madaktari!
Ama kweli JK ni moto wa kuotea mbali! Mkishajipeleka kumuona tu lazima mlainike wenyewe!

Hongera sana JK..wewe ni DR kwa ukweli!
 
Anatafuta data za marehemu? Wafe wangapi ndiyo inatosha kuingilia kati? Kwa mtawala makini hata roho ya mtu mmoja inatia uchungu haipaswi kuachiwa
 
JK never fails in negotiation and this was expected, if you don't agree with this, ask Kenyans. They know him very well. We've lost our fellow Tz lives unnecessarilly for things that would have been solved soft on the table.
 
Hii inadhihirisha Pinda si lolote, si chochote.
Nasema hivi kwa sababu, tangu Jan amewahadaa madaktari, mara vitisho, mara tunajipanga, .... huku wananchi wakiendelea kufa. Angemwambia tu tangu wakati huo bosi wake kuwa suala hilo hawezi kulishughulikia, hana nguvu ya ofisi...Nawapongoza madaktari kwa hatua hiyo. Natumaini JK hatawaangusha watanzania.
Pia ni matumaini yetu kuwa Mponda na Nkya wataachia ngazi, bila kusubiri kufukuzwa. Mungu awabariki na wote mlioshirikiana nao katika kulifikisha zoezi hili hapa.

Kuna wakati huwa najiuliza hivi washauri wa Pinda ni kina nani? Nina wasiwasi na huyu jamaa kama sana. Naona kama busara iko mbali na yeye! Ningekuwa miye saa hizi nshaacha kazi! Hakuna alilolisema ameweza kulitekeleza. Wale ndugu zetu Albino aliishia kulia tu! Jairo oooh kama namsubiri mkuu atue! Wapi! Madaktari wasiporudi kazini wamejifukuza kazi! Amemfukuza nani mpaka sasa. Juzi kaja na mpya eti serikali imejipanga! Mara kaingia kizani. Ni aibu!
 
Kenya, Chadema, Madaktari!
Ama kweli JK ni moto wa kuotea mbali! Mkishajipeleka kumuona tu lazima mlainike wenyewe!

Hongera sana JK..wewe ni DR kwa ukweli!

Kikwete is running straight back to what we ran away from 50 years ago under the reign of our dear Mwalimu.
 
Nafahamu msimamo wenu ulikua kwamba hamtaji mazungumzo hadi mponda na huyo mama watimuliwe...sasa iweje mmeruhusu iyo stej ya pili ya mazungumzo kabla hiyo ya kuwasimamisha kutekelezwa..unless j3 jk aseme amewasimamisha tofaut na apo hatutawaelewa...ikulu juice at work!!n

ikulu ni ofisi isiyotakiwa kudhalilishwa.kama wamepata fursa ya kuzungumza lazima kuna give n take.nawashukuru madaktari kwa uvumilivu walioonesha.
 
Hongera madaktari kwa uamuzi wenu tunasubiri utekelezaji tu na sio siasa za funika kombe.
 
Wengine wanasema jk angekutana na madaktari toka mwanzo, sasa wakina mponda na pinda wa kazi gani kama kazi zote atafanya mjomba? Idiot!
 
JK amechelewa mno kutoa suluhu mpaka baada ya pande zote kusuguana hadi zimechoka. Pili ni dalili kuonyesha kuwa yeye anafanya kazi peke yake pasipo kushishirikiana na Pinda ili jamii imuone Pinda ni dhalili. Hii ni hatari kiuongozi. Kama angeona Pinda hana uwezo basi angejadiliana na Madaktari bila kumtuma Pinda

Uliyoandikwa ni kweli kabisa lakini ni lazima tujue kuwa Kikwete ana what we call intrinsic defects as far as leadership is concerned! According to modern Costitutions, in any Republic the President is Executive in Chief but in our Republic Kikwete is not executive but CHIEF. Hii haina maana kuwa Katiba haikumpatia madaraka ya utendaji ispokuwa ni yeye au kwa makusudi au kwa kutokuwa kwake makini ameamua/amejikuta amezungukwa na watu wasio makini na wengi wao ni marafiki zake. Running a country is not like running a kiosk - Erdogan,PM Turkey: i really think that this is a message which should be delivered to Mr Kikwete. Tunapenda mara nyingi kusema kuwa Kikwete amezungukwa na watendaji wabovu, wengine wanapenda kusema kuwa Kikwete anapotoshwa na watendaji wake - lakini swali la kujiuliza ni nani anawateua hao watendaji??? Mwalimu J.K Nyerere(RIP) alwahi kusema viongozi wabovu ni kama mizoga wana tabia ya kukaribisha kunguru karibu nao. Je kikwete sio kiongozi mbovu?? na hao wanoumzunguka sio mizoga??? Mimi sioni sababu ya msingi iliyofanya rais akashindwa kuwafukuza Mponda na Nkya hasa baada ya ripoti yao bungeni ambayo ilikuwa haiendani na ukweli on the ground. Watu wakishakuwa ni "waskaji" zako inakuwa ni vigumu kuwafukuza.

Mimi nafikiri umefika wakati kwa Kikwete ku-behave like a President otherwise nchi itamshinda. Tanzania ya leo si Tanzania ya miaka 20 iliyopita haiongozeki kwa kutumia nguvu za dola bali kwa busara na hekima. Mgomo wa madaktari nafikiri utakuwa umetoa fundisho. Mwenye masikio na asikie....


 
And that is how the magic brain of the doctor works!!!

Hapo ndipo napompendea JK, Rais wangu. He always gives people what they want, well done Mr. President. Nadhani Pasco ameshaweka hili katika thread yake ya mazuri ya JK.
 
Waliomkimbia bungeni walimfuata ikulu wakanywa juice na pilau, nakumbuka kauli ya katibu wao "Eti mweshimiwa rais watu wanasema nilikukimbia... teh teh teheeee...... ".
Waliikataa rasimu ya katiba wakaikubali ikulu.
JK ni mwiba, hoja yao kuu madaktari ilikuwa mponda na nkya wapigwe chini! wamerudi kimyaaaa......
JK kiboko ya njia kwani madaktari i wazalendo kabisa nimewadharau hasa mnapoanza kujibembeleza kuwa lengo lenu sio kugoma Hawa mawaziri wanawahusu nini? km sio kutumwa kisiasa
Nyie daini yenu, mkafungue vidispensari hata mwenye mimba akija watoeni
 
Mwasi, kwani mwanzo alikuwepo?. Si alikuwa safarini!. Mara ya pili alikuwepo?.Si alikuwa Mlima Kilimanjaro!. Karudi, si kawaita Ikulu na kumaliza mambo!. Sometimes the end, justifies the means!. Mgomo umeisha!, tusonge mbele!.

Nina kila sababu ya kuamini kuwa mgomo haujaisha ila umehairishwa. Sababu zilizofanya mgomo uitishwe bado zipo palepale na zote ni za msingi as far as medical profession is concerned, ninachoamini Kikwete baada ya kusikiliza madai ya Madaktari atakuwa amewaomba wampe muda ili aweze kuyafanyia kazi. Kwahiyo logically utakuwa suspeded. So far hatujui wamekubaliana nini lakini nina uhakika kuwa miongoni mwa makubaliano yao kuna hata kuwapiga chini akina Ponda na Nkya na ndio maana Madaktari wameli-underline hilo hata ktk taarifa yao kwa vyombo vya habari. Hatuwezi kurisk maisha ya ndugu zetu kwasababu ya Nkya na Mponda, who are they by the way???

 
ni kama vile viongozi wa chadema walipoalikwa chai na juice pale ikulu na kuhidumiwa na JK basi mpaka leo hatuoni zile kelele tena! hekima itawale kwanza ili tushinde!

watu msiojua kufikirisha ubongo wenu ndio nyie,sijui mungu alikosea nini mpaka mkatokea hapa duniani. Hivi bila cdm kwenda ikulu yale mabadiliko yangepelekwa bungeni? Fuatilia mabadiliko aliyopendekeza lisu na yale ya bungeni. Werema alilazimishwa kula matapishi aliyoyakataa mpaka akawa anashindwa hata kutetea anachokilinda. Tuombe uzima nitakukumbusha mambo yatakavyonyooka, mtaishia kupiga kelele kwenye keyboard sie tunatetea mpate dawa,vipimo safi,mlale kwenye vitanda. Tutaendelea kutumia taaluma zetu kwa manufaa ya wananchi na familia zetu. Hao mnaowatuhumu kutoa mimba,sijui kuomba rushwa ndo hao waliokuwa wanatusaliti kwa sababu sio wasafi.
 
Tamko mlilotoa linaviashiria vya U-LOOSER!!
linafanana na yale majigambo wa watu waoga kwamba. umenipiga huku mtaani siku ukija kwetu utaniona!!

Ndugu yangu, ni bora ukose ushirikiano kutoka kwa polisi, maana unaweza kuupata kutoka kwa sungusungu au majirani. Lakini unapokosa ushirikiano kwa madaktari ujue ndo basi tena, maana uwezi kuupata kutoka kwa manesi au wafamasia, maana watakwambia (nesi) siwezi kutoa huduma kwa kuwa ukuonwa na daktari au (mfamasia) siwezi kukupa dawa kwa kuwa daktari hakuandika prescription. Ndugu yangu, tamko lao ni hatari kubwa kwa wahusika psychologically.
 
kiufupi mkuu mgomo huo mlichemka ile mbaya, kwani mlikuwa hamjaambiwa kuwa hatoondoshwa pale, majibu ya raisi hayajapingana na ya pinda. Pinda alisema madai ya kuwaondosha waziri na naibu wake yanashughulikiwa na serikali wala hakusema kuwa serikali imesema haitowaondosha pale. Jaziba na ukurupukaji wa kuona kuwa hamkosei ndio imewafanya mchukiwe na jamii, ndio maana hapo kwenye tamko lako umeanza kujitetea kwa jamii. Nyie madaktari ndio mnaoomba rushwa na sio Haji mponda, nyie ndio mnajifanya mko busy tunapokuja kwenye hospitali kupata huduma, nyinyi ndio wengi mnamiliki vituo vya afya,nyinyi ndio mnao kuwa mnawaelekeza wagonjwa wakanunue dawa kwenye farmacy zenu, nyie madaktari ndio mnaotoa mimba, nyie madaktari ndio mnaowauzia wagonjwa damu, yaani jamii ikipima makosa ya Hadji mponda na nyie, yaani nyie ndio mlipaswa kuondoshwa wote ila basi tu, nyie madaktari hamwajibiki vile inavyopaswa kwani mnafanya kazi zaidi ya hospitali moja hali ya kuwa nyie ni waajiliwa wa serikalini na mmesomeshwa bure na serikali, nyie madaktari ndio baadhi yenu huchukua dawa kwenye vituo vya serikali wanakofanyia kazi na kupeleka kwenye vituo vyao wanavyomiliki, sasa nataka mniambie je haya yote na mangine mengi tu mnayajua nyinyi wenyewe,kama yale ya muhimbili,mwananyamala na kungineko mnakojua wenyewe mlikuwa mnayafanya kwa sababu ya Hadji Mponda??? hasa wewe raisi uliyekuwa kinara wa kutangaza migomo nakushauri sana rudi kwa mola wako ukatubu ukweli wa kutubu kwani usidhani Mungu atakuacha ivi ivi kwa yaliyotokana na ujeuri wa cheo hicho. Kila unalolifanya kaka ujue linarekodiwa na mbele za Mungu utaulizwa. Kwahiyo kafanye toba ya kweli. na kama hamkuwa na chuki binafsi kwa waziri basi hamna sababu ya kumchukia ivo vyote kwani kama mnaona kafanya makosa basi jueni kuwa na yeye ni binadamu. ivi nyinyi ni wasafi kiasi gani mpaka mseme hamtotoa ushirikiano wa kibinafsi wala wa kiutendaji? ivi nyie Mungu nanyi akisema hatowasamehe makosa yenu mnayoyatenda kila kukicha mtafanya nini? kama Mungu mwenyewe Muumba wa mbingu na aridhi na vyote vilivyomo anasamahe je iweje nyie, ivi rais wa MAT huo ujeuri hasa unautoa wapi? mrudie Mungu wako ukatubu kwani duniani sisi ni wa kupita tu.
mkuu we mchungaji au?unafikiri unamjua sana Mungu kuliko watu wengine wote?nakushauri hii homily yako wapelekee family yako kwanza....who doesnt know kwamba duniani tunapita?wewe ndio lusekelo nini?
 
31 Reactions
Reply
Back
Top Bottom