Swala la kujiunga na OIC Hawajalipatia Ufumbuzi?

Mkuu pengine nazungumza lugha usoifahamu..Vatican ni Taasisi ambayo imeunda nchi ndani ya Italy..Labda nikuulize wewe kwa nini Vatican hakuna watoto wanaozaliwa? Kwa nini raia wa Vatican ni wazawa toka nchi tofauti duniani ambao uraia wao unatokana vyeo vyao ktk dini ya Katoliki..Au labda nambie wewe hao raia wake wanazaliana vipi? na pengine nijulishe kama wapo raia wasiohusiana kabisa na Kanisa! maanake nijuavyo mimi Vatican ni Taasisi iliyopewa au chukua eneo na kulifanya nchi ya utawala wa kanisa hilo.

Mkuu wangu tusibishane ili mradi kubishana kwa sababu swala la kuita nchi ni mfumo tu tuloweka sisi na umekubalika..Hata Macca wakiamua kuifanya nchi wanaweza ingawa najua fika itakuwa kaazi kubwa na wala sii utaratibu unaokubalika kiislaam. hivyo haiwezekanai kidini lakini kidunia inawezekana na ikakubalika.

Nitarudia kusema kama hakuna Taasisi ya Katoliki nchi hiyo haipo..hakuna vyama wala wananchi wanaozaana kujenga jamii hiyo. Hata wewe kesho unaweza kuwa raia wa Vatican pengine Pengo ana ganda la Vatican na kama hanaipo siku atakuwa..hakuzaliwa wala hana asili yoyote ya uzawa wala kuishi....who knows!

Vatican ni Taasisi iliyochukua eneo muhimu la kidini toka mji wa Rome na kuifanya nchi ili Pope aweze kuongoza dunia ya Kikatoliki..Hapa ndipo wanapoweza ku control makanisa yote duniani
na wafuasi wake ambao hata wewe pamoja na kuwa Mtanzania unashirikishwa ktk policies and authority of the papacy popote ulipo..
ifupi, Vatican wanaishi viongozi wa dini na raia wake ni waumini wote wa kanisa katoliki sehemu yoyote duniani....Go figure!

Kwanza nikushukuru kwa taarifa hizi nyingi na madai haya mengi juu ya Vatican na Ukatoliki ambayo umeyapendekeza kama ni ukweli kabisa. Ninaamini kuwa unayaamini uliyoyoyasema kuwa ni kweli na hivyo wengine wanaosoma wayapokee pia kama ni ukweli. Ni kusudio langu kuonesha kuwa yote uliyoyasema hayakubaliani na ukweli wa kihistoria na kihalisia kuhusu Vatican, Ukatoliki na Wakatoliki.

Umesema mambo kadhaa ambayo labda niyatenganishe kutoka insha fupi hapo juu. Umedai kwamba:


  1. Vatican ni Taasisi ambayo imeunda nchi ndani ya Italia baada ya kuchukua au kupewa ardhi ili Papa atawale dunia ya ukatoliki (hivyo Vatican siyo nchi)
  2. Vatican siyo nchi kwa sababu uraia wa wananchi wake hautokani na uzawa
  3. Mtu yeyote anaweza kuwa raia wa Vatican (kutumia maneno "hata wewe waweza"
  4. Vatican wanaishi viongozi wa dini
  5. Raia wake ni waumini wote wa Kanisa Katoliki sehemu yoyote duniani.

Hofu yangu ni kuwa baadhi ya watu ambao wamesoma maelezo yake yawezekana wameyachukulia kama ni ukweli bila kuhoji msingi wake au ukweli wake. Na kutoka katika kuyaamini kwa sababu yamekaa kama "facts" basi na wao wanaweza kujikuta wanayarudia kwa watu wengine na taarifa sahihi ikaendelea kupitisha kutoka mtu mmoja kwenda mwingine.

1. VATICAN NI TAASISI

Hili ni jibu rahisi ambalo mtu yeyote anaweza kuangalia kwa urahisi kwenye intaneti au maktaba. Jina kamili ni Nchi ya Vatican City (Vatican City State). Jina la "Vatican" ni la zamani na limetangulia Upapa kwani linatokana na jina la Kilatini "Mons Vaticanus" yaani "Mlima wa Vatican". Historia inasema ni katika mlima (kwa kweli ni kilima) ndipo Mt. Petro aliuawa kwa kusulubiwa kichwa chini miguu juu na ni juu ya kabuli lake ndipo kanisa la Mt. Petro lilijengwa ambalo baadaye limeendelea kukuzwa hadi kufikia hilo tunalolijua kama St. Peter's Basilica.

Mapapa kwa muda mrefu walikuwa na utawala wa Kanisa na utawala wa kisiasa (secular) na wakiwa na kazi hizo mbili waliweza kutawala maeneo mbalimbali ambayo yalijulikana kama "Majimbo ya Papa – Papal States". Mfumo huu wa upili (duality) wa Papa kuwa mtawala wa Kanisa na maeneo ulidumu kwa karibu miaka elfu hadi mwanzoni mwa karne ya 19 ambapo Ufalme wa Italia ulipoundwa. Tukumbuke kuwa Italia wakati huo ilikuwa ni mgawanyo wa falme na himaya ndogo ndogo kama za Sicily, Tuscany, Sardinia, Savoy, Nice n.k kila mmoja ikiwa na mkuu wake na Papa naye alikuwa na eneo lake.

Vita kati ya falme hizo na watawala wa Austria na Ufaransa na wenyewe kwa wenyewe ndizo zilizosababisha hatimaye Waitaliano kutaka kuungana chini ya kiongozi au uongozi mmoja. Hadi inafikia 1870 maeneo na mali ya Papa yalikuwa katika hatari ya kuchukuliwa na watawala wapya wakiongozwa na ufalme wa Piedmont (makao yake makuu Turin). Kuanzia wakati huo hadi 1929 kulikuwa na kile kinachoitwa na wanahistoria kuwa ni "Swali kuhusu Roma" yaani katika Italia hiyo mpya Papa (ambaye alikuwa anatawala pia maeneo yake akiwa na mabalozi na nchi nyingine zikiwa na ubalozi naye atakuwa nani wakati taifa sasa ni Ufalme wa Italia?

Na yeye Papa alikataa kuondoka hata Vatikani hadi suala hilo litatuliwe kwani kwa upande wake hakuwa tayari kumtambua mfalme mpya wa Italia. Kulikuwa na makubaliano ambayo yalimruhusu Papa kuendelea kufanya kazi zake kupokea mabalozi n.k kama wakuu wengine wa nchi.

Mfalme mpya wa Italia hakumnyanyasa sana Papa lakini alitaifisha mali kadhaa za Papa ikiwemo maskani yake ya Quirinal ambayo leo hii ndio maskani rasmi ya Rais wa Italia. Papa Pius IX ndiyo alikuwa mtawala wa mwisho wa tawala mbalimbali za kipapa (yale maeneo niliyoyataja hapo juu) baada ya Jiji la Roma nalo kuchukuliwa na kumfanya ajitangaze kuwa amekuwa "mfungwa ndani ya Kuta za Vatican".

Mgongano kati ya Ufalme wa Italia na Papa ulimalizika kwa makubaliano maarufu yajulikanayo kama Makubaliano ya Lateran (Unaweza kutafuta yanaitwa Lateran Treaty) ambayo yalimaliza swali la Uroma kwa kuitambua Vatican kama nchi hakimiya (sovereign state) na kuhakikisha mali zake nyingine hazichukuliwi n.k Kutokana na hilo Vatican siyo sehemu ya Italia ni nchi kamili iliyoundwa kwa mkataba halali uliouingiwa kati ya Benito Musolini kwa niaba ya Mfalme Victor Emmanuel III na Waziri wa Mambo ya Nje wa Papa Cardinali Gaspari kwa niaba ya Papa Pius IX.

Ni vizuri nitenganishe vitu ambavyo kwa mtu asiye Mkatoliki (na hata Wakatoliki wengine) hawavielewi. Kuna kitu tunakiita "Holy See" na kuna "Vatican City State". Mambo mengi tunayoyaona yanafanywa na Papa au Kanisa Katoliki n.k yanafanywa na Holy See na siyo nchi ya Vatican.

Holy See (Kiti cha Papa a.k.a Upapa) ni utawala wa kidini wa Baba Mtakatifu ndani ya Kanisa Katoliki ambao huundwa na Papa mwenyewe na Kuria ya Roma wakati Vatican City State inaongozwa na Gavana wa Vatican chini ya Papa. Vyote viwili vinahusiana lakini si kitu kimoja. Utawala wa Papa basi siyo jamhuri (yenye kuhitaji vyama vya siasa kupiga kura n.k) bali ni Ufalme kamili – absolute monarchy. Maana yake ni kuwa Papa ana mamlaka yote ya kutunga sheria, haki, na utawala. Kutokana na hili utaona kuwa mabalozi wote hupelekwa Holy See na siyo Vatican na hata kile tunachoita Ubalozi wa Vatican kimsingi ni ubalozi wa Upapa – mfalme.

Kanisa Katoliki la Tanzania au la mahali linauongozi wake katika mambo ya askofu wake. Hivyo balozi wa Holy See hayuko juu ya Pengo kwani yeye yuko kwa kumwakilisha mfalme (Papa) kwa serikali ya Tanzania na Tanzania inapeleka balozi wake huko. Kutokana na ukweli kuwa Holy See ndiyo yenye mlolongo wa huduma ya kibalozi ya zamani zaidi duniani kuliko nchi nyingine yeyote (kuanzia 325AD) nchi kadhaa zina mabalozi wake huko. Miongoni mwa nchi za Kiislamu ambazo zinatambua hili na zina uhusiano wa kibalozi na Holy See ni pamoja na:

Morocco
Misri
Iran
Iraq
Uturuki
Palestine
Azeirjabain

Tanzania kama nchi hizo nayo ina ubalozi kwa Papa na hili si tatizo kuwa na ubalozi na taifa la kidini. Tanzania ina balozi Saudi Arabia ambao ni ufalme, tuna ubalozi Jordani ambao ni Ufalme na tuna mahusiano ya kibalozi na Falme za Kiarabu. Hizi zote ni falme ambazo zina msingi wa kidini kama vile ulivyo Upapa na dini ya Kikatoliki. Hakuna mtu ambaye amewahi kuhoji kwanini Tanzania ina husiana na nchi hizi au kwanini Jordani ina ubalozi Tanzania wakati ni ufalme wa utawala wa Kiislamu? Kumbe la msingi ni kuwa kwa vile hizi zote ni nchi halali na tunazitambua hivyo hakuna tatizo la kuwa na balozi nazo. Hili ni kweli tangu wakati wa Nyerere hadi leo hii.
Kwa hiyo, Vatican siyo "taasisi" bali ni nchi kamili, iliyoundwa kufuatia mkataba wa Laterani ambaye mkuu wake ni Papa. Haijawahi kuchukua eneo la nchi nyingine au mtu mwingine ili liwe chini ya Papa bali Papa ndiye alinyang'anywa maeneo aliyokuwa akiyatawala kwa karibu miaka elfu kufuatia vita vya Waitalia vilivyoiunganisha Italia. Kwa mkataba wa Laterani na nyongeza yake aliachiwa hiyo Vatican City pamoja na maeneo mengine ambayo yako nje ya kuta za Vatican (kama maktaba, makanisa yaliyopo sehemu mbalimbali za Italia na magazi mengine ya kipapa).

Kwa mtu yeyote anayejisikia kubisha anatakiwa aeleze ni Vatican City imetoka wapi na ilikuwa taasisi kwa utaratibu gani?

2: HAKUNA URAIA WA KUZALIWA HIVYO SI NCHI

Kwanza, niseme si kweli; Uraia wa Vatican unaweza kupatikana kwa watoto na wenza wa maofisa wanaofanya kazi Vatican. Kwa watoto hadi watakapofikisha miaka 25. Uraia ni suala la kisheria na kila nchi ina utaratibu wake. Mkataba wa Laterani nilioutaja hapo juu ndio unasimamia uraia wa Vatican vile vile. Raia wa Vatican ambaye anapoteza uraia wa Vatican au wa nchi yake (kwa wale wenye uraia wa nchi mbili) basi kwa mujibu wa Laterani anapata uraia wa Italia automatically.

Hadi mwaka mwishoni mwa 2005 kulikuwa na watu 557 wenye uraia wa Vatican. Miongoni mwao ni:

Papa
58 -Makadinali (ambao wanaoishi au kufanya kazi karibu na Roma). Ni muhimu kutambua kuwa siyo makardinali wote wenye uraia wa Vatican. Kanisa Katoliki lina makardinali 199 walio hai (hadi naandika hii) ambao kati yao ni 109 ndio wanauwezo wa kupiga kura kumchagua papa (wapiga kura wanatakiwa wawe ni wale chini ya miaka 80).
293 Waklegi (mapadre, mashemasi) wanaofanya kazi katika balozi mbalimbali za Holy See pote duniani. Baadhi yao ndio kama yule Askofu Mkuu Novatus Rugambwa ambaye ameteuliwa mapema mwaka huu kuwa Balozi wa Papa huko Sao Tome na Principe.
62 Watendaji wengine wa kanisa wanaofanya kazi Vatican
101 Maafisa wa vikosi vya usalama vya Vatican wakiwemo wale Swiss Guard wanaomlinda Papa
43 Walei wengine wanaofanya kazi hapo au familia na watoto wao.

Na Vatican inatoa passport za utumishi na za kibalozi. Passport kama hizi hutolewa na taasisi kama Umoja wa Mataifa au na taasisi nyingine zinazotambulika kimataifa. Taasisi kama Umoja wa Afrika na yenyewe inatoa passport zake za utumishi na wakuu wa nchi zote 53 za Umoja huo wamepewa passport hizo pamoja na watendaji wake wengine na watu wengine mashuhuri. Kutolewa passport si lazima kuwa suala la uraia ni suala la kumtambulisha msafiri kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine na zinatumika kwa makubaliano ya kutambuliwa kwa taasisi inayotoa. Naamini hata OIC inatoa passport za namna hii kwa watendaji wake.


3: MTU YEYOTE ANAWEZA KUWA RAIA WA VATICAN
Ni kweli mtu yeyote anaweza kuwa "raia wa Vatican" endapo tu mtu huyo ametimiza masharti ya uraia huo kwa mujibu wa Katiba ya Vatican na makubaliano ya Vaticani. Siyo rahisi kuupata uraia wa Vatican. Kwani hautokani na damu tu au kuwa naturalized bali unatokana na huduma (service) au ofisi ya mtu na kutoka hapo ndipo kwa watoto au wenzi wanaweza kuupata uraia huo.

4: VATICAN WANAISHI VIONGOZI WA DINI
Hili ni kweli kiasi. Lakini siyo viongozi wa dini tu. Wanaishi wafanyakazi wa Taifa la Vatican na raia wake vile vile wakiwemo watoto wa wafanyakazi na watendaji wengine ambao si viongozi wa dini.


5:WAUMINI WAKATOLIKI POTE DUNIANI NI RAIA WA VATIKANI
Hii si kweli kabisa. Wakatoliki wote siyo raia wa Vatican. Kama nilivyosema hapo juu uraia wa Vatikani hauji kwa ubatizo au kwa kuitwa Mkatoliki unakuja kwa mujibu wa mkataba wa Laterani wa 1929. Hii ina maana kwamba Vaticani licha ya kuwa ni taifa dogo zaidi vile vile ni taifa lenye raia wachache zaidi (hawazidi 1000). Na Vatican City haina mamlaka ya aina yoyote juu ya Mkatoliki kuhusu uraia wake. Papa ana mamlaka katika masuala ya imani na dini kama kiongozi wa dini lakini siyo kama mfalme wa wakatoliki wote duniani.

Ni muhimu kutambua kuwa kama mfalme Papa ni sovereign (hakimiya) hivyo haitaji Vatican City ili kuwa sovereign. Lakini uwepo wa Vatican City unasaidia tu katika kutekeleza majukumu yake ya kisiasa na kiutawala.

Nitawaacha wengine waendelee kuchangia suala la kujiunga na OIC kwani nilishatoa maoni yangu miaka mitatu iliyopita na kujirudia itakuwa ni kurudia rudia kitu kile kile. Mjadala mzuri sana.
 
Mwanakijiji umetoa ufafanuzi mzuri sana!

Wengi huuongelea ukatoliki bila kuujua, halafu wanakuwa wabishi
Inafikia wakati unashindwa kuwaelewesha, unaamua kukaa kimya.
Na ukinyamaza ndo upotofu unaposhika kasi.

Kwa staili uliyotumia, taratibu tutawekana sawa!
 
Kwanza nikushukuru kwa taarifa hizi nyingi na madai haya mengi juu ya Vatican na Ukatoliki ambayo umeyapendekeza kama ni ukweli kabisa. Ninaamini kuwa unayaamini uliyoyoyasema kuwa ni kweli na hivyo wengine wanaosoma wayapokee pia kama ni ukweli. Ni kusudio langu kuonesha kuwa yote uliyoyasema hayakubaliani na ukweli wa kihistoria na kihalisia kuhusu Vatican, Ukatoliki na Wakatoliki.

Umesema mambo kadhaa ambayo labda niyatenganishe kutoka insha fupi hapo juu. Umedai kwamba:


  1. Vatican ni Taasisi ambayo imeunda nchi ndani ya Italia baada ya kuchukua au kupewa ardhi ili Papa atawale dunia ya ukatoliki (hivyo Vatican siyo nchi)
  2. Vatican siyo nchi kwa sababu uraia wa wananchi wake hautokani na uzawa
  3. Mtu yeyote anaweza kuwa raia wa Vatican (kutumia maneno "hata wewe waweza"
  4. Vatican wanaishi viongozi wa dini
  5. Raia wake ni waumini wote wa Kanisa Katoliki sehemu yoyote duniani.

Hofu yangu ni kuwa baadhi ya watu ambao wamesoma maelezo yake yawezekana wameyachukulia kama ni ukweli bila kuhoji msingi wake au ukweli wake. Na kutoka katika kuyaamini kwa sababu yamekaa kama "facts" basi na wao wanaweza kujikuta wanayarudia kwa watu wengine na taarifa sahihi ikaendelea kupitisha kutoka mtu mmoja kwenda mwingine.

1. VATICAN NI TAASISI

Hili ni jibu rahisi ambalo mtu yeyote anaweza kuangalia kwa urahisi kwenye intaneti au maktaba. Jina kamili ni Nchi ya Vatican City (Vatican City State). Jina la "Vatican" ni la zamani na limetangulia Upapa kwani linatokana na jina la Kilatini "Mons Vaticanus" yaani "Mlima wa Vatican". Historia inasema ni katika mlima (kwa kweli ni kilima) ndipo Mt. Petro aliuawa kwa kusulubiwa kichwa chini miguu juu na ni juu ya kabuli lake ndipo kanisa la Mt. Petro lilijengwa ambalo baadaye limeendelea kukuzwa hadi kufikia hilo tunalolijua kama St. Peter's Basilica.

Mapapa kwa muda mrefu walikuwa na utawala wa Kanisa na utawala wa kisiasa (secular) na wakiwa na kazi hizo mbili waliweza kutawala maeneo mbalimbali ambayo yalijulikana kama "Majimbo ya Papa – Papal States". Mfumo huu wa upili (duality) wa Papa kuwa mtawala wa Kanisa na maeneo ulidumu kwa karibu miaka elfu hadi mwanzoni mwa karne ya 19 ambapo Ufalme wa Italia ulipoundwa. Tukumbuke kuwa Italia wakati huo ilikuwa ni mgawanyo wa falme na himaya ndogo ndogo kama za Sicily, Tuscany, Sardinia, Savoy, Nice n.k kila mmoja ikiwa na mkuu wake na Papa naye alikuwa na eneo lake.

Vita kati ya falme hizo na watawala wa Austria na Ufaransa na wenyewe kwa wenyewe ndizo zilizosababisha hatimaye Waitaliano kutaka kuungana chini ya kiongozi au uongozi mmoja. Hadi inafikia 1870 maeneo na mali ya Papa yalikuwa katika hatari ya kuchukuliwa na watawala wapya wakiongozwa na ufalme wa Piedmont (makao yake makuu Turin). Kuanzia wakati huo hadi 1929 kulikuwa na kile kinachoitwa na wanahistoria kuwa ni "Swali kuhusu Roma" yaani katika Italia hiyo mpya Papa (ambaye alikuwa anatawala pia maeneo yake akiwa na mabalozi na nchi nyingine zikiwa na ubalozi naye atakuwa nani wakati taifa sasa ni Ufalme wa Italia?

Na yeye Papa alikataa kuondoka hata Vatikani hadi suala hilo litatuliwe kwani kwa upande wake hakuwa tayari kumtambua mfalme mpya wa Italia. Kulikuwa na makubaliano ambayo yalimruhusu Papa kuendelea kufanya kazi zake kupokea mabalozi n.k kama wakuu wengine wa nchi.

Mfalme mpya wa Italia hakumnyanyasa sana Papa lakini alitaifisha mali kadhaa za Papa ikiwemo maskani yake ya Quirinal ambayo leo hii ndio maskani rasmi ya Rais wa Italia. Papa Pius IX ndiyo alikuwa mtawala wa mwisho wa tawala mbalimbali za kipapa (yale maeneo niliyoyataja hapo juu) baada ya Jiji la Roma nalo kuchukuliwa na kumfanya ajitangaze kuwa amekuwa "mfungwa ndani ya Kuta za Vatican".

Mgongano kati ya Ufalme wa Italia na Papa ulimalizika kwa makubaliano maarufu yajulikanayo kama Makubaliano ya Lateran (Unaweza kutafuta yanaitwa Lateran Treaty) ambayo yalimaliza swali la Uroma kwa kuitambua Vatican kama nchi hakimiya (sovereign state) na kuhakikisha mali zake nyingine hazichukuliwi n.k Kutokana na hilo Vatican siyo sehemu ya Italia ni nchi kamili iliyoundwa kwa mkataba halali uliouingiwa kati ya Benito Musolini kwa niaba ya Mfalme Victor Emmanuel III na Waziri wa Mambo ya Nje wa Papa Cardinali Gaspari kwa niaba ya Papa Pius IX.

Ni vizuri nitenganishe vitu ambavyo kwa mtu asiye Mkatoliki (na hata Wakatoliki wengine) hawavielewi. Kuna kitu tunakiita "Holy See" na kuna "Vatican City State". Mambo mengi tunayoyaona yanafanywa na Papa au Kanisa Katoliki n.k yanafanywa na Holy See na siyo nchi ya Vatican.

Holy See (Kiti cha Papa a.k.a Upapa) ni utawala wa kidini wa Baba Mtakatifu ndani ya Kanisa Katoliki ambao huundwa na Papa mwenyewe na Kuria ya Roma wakati Vatican City State inaongozwa na Gavana wa Vatican chini ya Papa. Vyote viwili vinahusiana lakini si kitu kimoja. Utawala wa Papa basi siyo jamhuri (yenye kuhitaji vyama vya siasa kupiga kura n.k) bali ni Ufalme kamili – absolute monarchy. Maana yake ni kuwa Papa ana mamlaka yote ya kutunga sheria, haki, na utawala. Kutokana na hili utaona kuwa mabalozi wote hupelekwa Holy See na siyo Vatican na hata kile tunachoita Ubalozi wa Vatican kimsingi ni ubalozi wa Upapa – mfalme.

Kanisa Katoliki la Tanzania au la mahali linauongozi wake katika mambo ya askofu wake. Hivyo balozi wa Holy See hayuko juu ya Pengo kwani yeye yuko kwa kumwakilisha mfalme (Papa) kwa serikali ya Tanzania na Tanzania inapeleka balozi wake huko. Kutokana na ukweli kuwa Holy See ndiyo yenye mlolongo wa huduma ya kibalozi ya zamani zaidi duniani kuliko nchi nyingine yeyote (kuanzia 325AD) nchi kadhaa zina mabalozi wake huko. Miongoni mwa nchi za Kiislamu ambazo zinatambua hili na zina uhusiano wa kibalozi na Holy See ni pamoja na:

Morocco
Misri
Iran
Iraq
Uturuki
Palestine
Azeirjabain

Tanzania kama nchi hizo nayo ina ubalozi kwa Papa na hili si tatizo kuwa na ubalozi na taifa la kidini. Tanzania ina balozi Saudi Arabia ambao ni ufalme, tuna ubalozi Jordani ambao ni Ufalme na tuna mahusiano ya kibalozi na Falme za Kiarabu. Hizi zote ni falme ambazo zina msingi wa kidini kama vile ulivyo Upapa na dini ya Kikatoliki. Hakuna mtu ambaye amewahi kuhoji kwanini Tanzania ina husiana na nchi hizi au kwanini Jordani ina ubalozi Tanzania wakati ni ufalme wa utawala wa Kiislamu? Kumbe la msingi ni kuwa kwa vile hizi zote ni nchi halali na tunazitambua hivyo hakuna tatizo la kuwa na balozi nazo. Hili ni kweli tangu wakati wa Nyerere hadi leo hii.
Kwa hiyo, Vatican siyo "taasisi" bali ni nchi kamili, iliyoundwa kufuatia mkataba wa Laterani ambaye mkuu wake ni Papa. Haijawahi kuchukua eneo la nchi nyingine au mtu mwingine ili liwe chini ya Papa bali Papa ndiye alinyang'anywa maeneo aliyokuwa akiyatawala kwa karibu miaka elfu kufuatia vita vya Waitalia vilivyoiunganisha Italia. Kwa mkataba wa Laterani na nyongeza yake aliachiwa hiyo Vatican City pamoja na maeneo mengine ambayo yako nje ya kuta za Vatican (kama maktaba, makanisa yaliyopo sehemu mbalimbali za Italia na magazi mengine ya kipapa).

Kwa mtu yeyote anayejisikia kubisha anatakiwa aeleze ni Vatican City imetoka wapi na ilikuwa taasisi kwa utaratibu gani?

2: HAKUNA URAIA WA KUZALIWA HIVYO SI NCHI

Kwanza, niseme si kweli; Uraia wa Vatican unaweza kupatikana kwa watoto na wenza wa maofisa wanaofanya kazi Vatican. Kwa watoto hadi watakapofikisha miaka 25. Uraia ni suala la kisheria na kila nchi ina utaratibu wake. Mkataba wa Laterani nilioutaja hapo juu ndio unasimamia uraia wa Vatican vile vile. Raia wa Vatican ambaye anapoteza uraia wa Vatican au wa nchi yake (kwa wale wenye uraia wa nchi mbili) basi kwa mujibu wa Laterani anapata uraia wa Italia automatically.

Hadi mwaka mwishoni mwa 2005 kulikuwa na watu 557 wenye uraia wa Vatican. Miongoni mwao ni:

Papa
58 -Makadinali (ambao wanaoishi au kufanya kazi karibu na Roma). Ni muhimu kutambua kuwa siyo makardinali wote wenye uraia wa Vatican. Kanisa Katoliki lina makardinali 199 walio hai (hadi naandika hii) ambao kati yao ni 109 ndio wanauwezo wa kupiga kura kumchagua papa (wapiga kura wanatakiwa wawe ni wale chini ya miaka 80).
293 Waklegi (mapadre, mashemasi) wanaofanya kazi katika balozi mbalimbali za Holy See pote duniani. Baadhi yao ndio kama yule Askofu Mkuu Novatus Rugambwa ambaye ameteuliwa mapema mwaka huu kuwa Balozi wa Papa huko Sao Tome na Principe.
62 Watendaji wengine wa kanisa wanaofanya kazi Vatican
101 Maafisa wa vikosi vya usalama vya Vatican wakiwemo wale Swiss Guard wanaomlinda Papa
43 Walei wengine wanaofanya kazi hapo au familia na watoto wao.

Na Vatican inatoa passport za utumishi na za kibalozi. Passport kama hizi hutolewa na taasisi kama Umoja wa Mataifa au na taasisi nyingine zinazotambulika kimataifa. Taasisi kama Umoja wa Afrika na yenyewe inatoa passport zake za utumishi na wakuu wa nchi zote 53 za Umoja huo wamepewa passport hizo pamoja na watendaji wake wengine na watu wengine mashuhuri. Kutolewa passport si lazima kuwa suala la uraia ni suala la kumtambulisha msafiri kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine na zinatumika kwa makubaliano ya kutambuliwa kwa taasisi inayotoa. Naamini hata OIC inatoa passport za namna hii kwa watendaji wake.


3: MTU YEYOTE ANAWEZA KUWA RAIA WA VATICAN
Ni kweli mtu yeyote anaweza kuwa "raia wa Vatican" endapo tu mtu huyo ametimiza masharti ya uraia huo kwa mujibu wa Katiba ya Vatican na makubaliano ya Vaticani. Siyo rahisi kuupata uraia wa Vatican. Kwani hautokani na damu tu au kuwa naturalized bali unatokana na huduma (service) au ofisi ya mtu na kutoka hapo ndipo kwa watoto au wenzi wanaweza kuupata uraia huo.

4: VATICAN WANAISHI VIONGOZI WA DINI
Hili ni kweli kiasi. Lakini siyo viongozi wa dini tu. Wanaishi wafanyakazi wa Taifa la Vatican na raia wake vile vile wakiwemo watoto wa wafanyakazi na watendaji wengine ambao si viongozi wa dini.


5:WAUMINI WAKATOLIKI POTE DUNIANI NI RAIA WA VATIKANI
Hii si kweli kabisa. Wakatoliki wote siyo raia wa Vatican. Kama nilivyosema hapo juu uraia wa Vatikani hauji kwa ubatizo au kwa kuitwa Mkatoliki unakuja kwa mujibu wa mkataba wa Laterani wa 1929. Hii ina maana kwamba Vaticani licha ya kuwa ni taifa dogo zaidi vile vile ni taifa lenye raia wachache zaidi (hawazidi 1000). Na Vatican City haina mamlaka ya aina yoyote juu ya Mkatoliki kuhusu uraia wake. Papa ana mamlaka katika masuala ya imani na dini kama kiongozi wa dini lakini siyo kama mfalme wa wakatoliki wote duniani.

Ni muhimu kutambua kuwa kama mfalme Papa ni sovereign (hakimiya) hivyo haitaji Vatican City ili kuwa sovereign. Lakini uwepo wa Vatican City unasaidia tu katika kutekeleza majukumu yake ya kisiasa na kiutawala.

Nitawaacha wengine waendelee kuchangia suala la kujiunga na OIC kwani nilishatoa maoni yangu miaka mitatu iliyopita na kujirudia itakuwa ni kurudia rudia kitu kile kile. Mjadala mzuri sana.

So what is the difference between alichosema Mkandara na wewe!!! Mkataba wa Laterai unahusu utambuliko wa nchi but hilo linaweza kufanya but chini yake ikawa ni taasisi ya kimafia iliyo na uhuru wa kufanya jambo lolote duniani?
 
Mwanakijiji umetoa ufafanuzi mzuri sana!

Wengi huuongelea ukatoliki bila kuujua, halafu wanakuwa wabishi
Inafikia wakati unashindwa kuwaelewesha, unaamua kukaa kimya.
Na ukinyamaza ndo upotofu unaposhika kasi.

Kwa staili uliyotumia, taratibu tutawekana sawa!

Kabwenge ufafanuzi upi???
 
Mwanakijiji umetoa ufafanuzi mzuri sana!

Wengi huuongelea ukatoliki bila kuujua, halafu wanakuwa wabishi
Inafikia wakati unashindwa kuwaelewesha, unaamua kukaa kimya.
Na ukinyamaza ndo upotofu unaposhika kasi.

Kwa staili uliyotumia, taratibu tutawekana sawa!

.......Kweli katoa maelezo mazuri sana. Tena kwa kusisitiza tu, ni kuwa Vatican City ni kitongoji kidogo sana chenye ukubwa wa kama ekari 100 tu katika jiji la Roma; kadri nilivyowahi kusoma haopa JF, kuna waoadhani kuwa hilo ni taifa lenye raia kama lilivyo taifa la Tanzania, no it is just an institution, ila haiingiliwi na dola za nchi yoyote duniani kama alivyofafanua MKJJ.
 
.......Kweli katoa maelezo mazuri sana. Tena kwa kusisitiza tu, ni kuwa Vatican City ni kitongoji kidogo sana chenye ukubwa wa kama ekari 100 tu katika jiji la Roma; kadri nilivyowahi kusoma haopa JF, kuna waoadhani kuwa hilo ni taifa lenye raia kama lilivyo taifa la Tanzania, no it is just an institution, ila haiingiliwi na dola za nchi yoyote duniani kama alivyofafanua MKJJ.

Je Institution sio Taasisi na what is the difference between mnachokisema na alichokisema Mkandara???
 
Mimi siku zote nashindwa kuelewa kwa nini watu wanakuwa wanatokwa mapovu " literally" tunapoanza kuzungumzia hizi dini mbili zilizoletwa na Wazungu na Waarabu. Nadhani Waafrika tumekuwa brainwashed vibaya sana inapokuja kwenye masuala ya imani.
 
Hahaha! nimefurahi saana, Thanx Mkandara kwa maelezo mazuri,naona M/kijiji amekuja kuweka wazi zaidi ufafanuzi wako,sioni kipya alichozungumza M/kijiji ni yale yale uloongea Mkandara, nahisi itachukua mda mrefu kwa wenzetu hawa kuweza kupambanua haya masuala,labda mpaka siku ambayo wale maaskofu tunaowaona kwenye TV wakinyanyua mikono,watu walokuwepo pale wanaanguka chini,iwe wakinyanyua mikono watu hawaanguki tena lkn naona itachukua mda saana...
 
Nimefuatilia mjadala na kuona wengi wa wachangiaji eidha hawajui sheria ya nchi yetu au labda pia wana muono finyu wa mambo.
Mimi navyofahamu nchi yeyote inapotaka kutengeneza uhusiano na nchi nyingine au Taasisi yeyote ni lazima kwanza kuzingatia mambo makuu yafuatayo
  1. Sheria za nchi husika- hasa sheria Mama (KATIBA)
  2. Sheria za kimataifa zilizoridhiwa na Umoja wa Mataifa
  3. Kanuni/sheria na Malengo ya Muungano husika
  4. Faida na Hasara za muungano huo -Kiuchumi, Kijamii, Kisiasa,n.k
Mada yetu ilikuwa Suala la kujiunga na OIC halijapatiwa uvumbuzi.
Maswali ya kujiuliza ni
kujiunga na OIC Tanzania au Zanzibar inavunja kipengele gani cha Sheria.
Je kujiunga na OIC ni sheria gani za kimatifa zinavunjwa. Hivi kunafaida kujiunga na jumuiya yenye wanachama 57 jumuiya ya pili kwa ukubwa duniani baada ya Umoja wa Mataifa. Je hakuna faida za kiuchumi kwa wanachama wa juiya yenye Pato la wastani wa U$D 10,140,000,000/=.
lakini najua kuna wale wataojibu kwa jazba kwa kusema Katiba ya Jamhuri ya muungano Ibara ya 19 (2) inazuia. mimi nasema mtu huyo anakosea na hajaisoma vizuri katiba. labda kwa faida ya wengine ibara hiyo inasema hivi..."Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya
Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.



Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.

Ukisoma kwa makini utaona katiba imetoa uhuru kwa mtu bianafsi kufanya yafuatayo
1. kazi ya kutangaza dini,
2. kufanya ibada
3. kufanya ibada
4. kueneza dini
wakati huo huo ifahamike katiba pia imezuia serekali kufanya yafuatayo:
1. kazi ya kutangaza dini,
2. kufanya ibada
3. kueneza dini
4. shughuli na uendeshaji wa Jumuiya za dini

Swali la kujiuliza ni je kwa Tanzania/Zanziba kiujiunga na OIC je mamlaka ya nchi itakuwa inafanyakazi ya kutangaza dini, kueneza dini, kufanya ibada au inajishughulisha na uendeshaji wa Jumuiya za dini.

Jibu si kweli kwasababu moja tu kuu, OIC sio Shirika linalofanyakazi ya kutangaza dini, kueneza dini, kufanya ibada au linalojishughulisha na uendeshaji wa Jumuiya za dini. Na hii inathibitishwa na malengo ya Shirika la OIC ebu yapitie bila chuki binafsi za kidini wala uzandiki. Malengo yanasema hivi:

Chini ya Mkataba, Shirika lina malengo yafuatayo:
1. Kuboresha na kuimarisha kwa Mahusiano ya udugu na mshikamano kati ya Nchi Wanachama;
2. Kuhifadhi na kulinda maslahi ya pamoja na kulinda harakati halali za nchi wanachama na kuratibu na kuunganisha juhudi za Nchi Wanachama katika mtazamo wa changamoto zinazokabili hasa ulimwengu wa nchi za Kiislamu na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla;
3. Kuheshimu haki ya maamuzi binafsi na yasiyoingiliwa katika mambo ya ndani na kuheshimu uhuru, na uadilifu na uhuru wa mipaka wa eneo la kila nchi wanachama.
4. Kuhakikisha ushiriki wa Nchi Wanachama katika kisiasa za dunia, kiuchumi na kijamii na kushiriki katika mchakato wa maamuzi ya kijamii kupata maslahi yao ya kawaida;
5. Kuthibitisha uungaji mkono wake kwa haki za watu kama ilivyoelezewa katika Mkataba wa Umoja wa Mataifa na sheria za kimataifa.
6. kuimarisha mahusiano ya chumi za kiislamu na ushirikiano wa kibiashara, ili kufikia muungano wa kiuchumi kupelekea kuanzishwa soko la pamoja la kiislamu.
7. Kuweka juhudi za kufikia maendeleo endelevu na mapana ya kibinadamu na maendeleo na ustawi wa kiuchumi kwa nchi wanachama.
8. Kulinda na kutetea sura ya kweli ya Uislamu, ili kukabiliana na udhalilishaji wa Uislamu na kuhimiza mazungumzo kati ya staarabu mbalimbali na dini.
9. Kuimarisha na kuendeleza sayansi na teknolojia na kuhimiza utafiti na ushirikiano kati ya nchi wanachama katika maeneo hayo.

Sasa ebu niambie ni wapi katika malengo haya shirika la OIC linalofanyakazi ya kutangaza dini, kueneza dini, kufanya ibada au linalojishughulisha na uendeshaji wa Jumuiya za dini. Na Shirika kama hili haliwezi kufanya hivyo kwani limesha ainisha katika lengo namba 3 na 5.

Wananchi wenzangu jaribuni basi hata kupitia Mkataba wa Umoja wa Mataifa na sheria za kimataifa kuhusu haki za binaadamu ambazo OIC wameahidi kuzilinda na kuzisimamia kati ya nchi wanachama.

MAAJABU
Mbali ya kukosekana sababu za Tanzania kutojiunga na OIC lakini miongoni mwetu bado tunaamini nchi kujiunga na OIC ni kinyume na Katiba na wapo wale wahafidhana wa chuki za kidini ambao wao kubwa ni kuwa kujiunga na OIC ni kutusilimisha KIAINA kwa jina la misaada

Chuki hizi au ufinyu huu wa mawazo unatokana na sababu kuu zifuatazo

Jina lenyewe ni Organization of "ISLAMIC" Conference. Yaani hawa chochote kile chenye kuashiria uislamu kwao ni sumu lakini sio dini nyingine ni uislamu tu. Vita yao ni dhidi ya Uislamu na waislamu na hapa nitatoa mfano. Tanzania kuana mengi yanafanyika yenye sura za dini lakini kundi hili sijawasikia wakikosoa mfano:
i. UWEPO WA UBALOZI WA HOLLY SEE:
Kuna wachangiaji wengi wameandika kuwa Tanzania inaubalozi na VATICAN napenda hapa kurekebisha Tanzania hatuna ubalozi na VATICAN kama vile ambavyo VATICA haina ubalozi na nchi yeyote.
Tanzania tuna ubalozi na Holly see. Holly see ipo chini ya utawala wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki la Roma, ambapo Askofu wake anajulikana kama Papa. Ni Maaskofu mtakatifu wa Kanisa Katoliki, anayetengeneza serikali kuu ya Kanisa.(Kwa maneno mepesi holly see ni serekali kuu ya kanisa katoliki)

Kwa maana hiyo Tanzania kuwa na ubalozi wa Holly see maana yake ndani ya jamhuri ya muungano tuano ubalozi wa serekali kuu ya kanisa katoliki


Hebu tizama :
Although it is often referred to by the ambiguous term "the Vatican", the Holy See is not the same entity as the Vatican City State, which came into existence only in 1929, while the Holy See dates back to early Christian times.
Ambassadors are officially accredited not to the Vatican City State but to "the Holy See", and papal representatives to states and international organizations are recognized as representing the Holy See, not the Vatican City State.

Tafsri binafsi:
Ingawa mara nyingi huitwa kwa jina lenye utata "Vatican", Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) ni kitu tofauti kabisa na serekali ya mji wa Vatican, Mji ambao (VATCAN) ulianza kuwepo tu mwaka 1929, wakati Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) ilianza mapema ulipoanza ukristo.
Mabalozi wenye vibali rasmi si kwa ajili ya kuwakilisha Taifa la mji wa VATICAN bali Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki)", na wawakilishi wa Papa kwa nchi na mashirika ya kimataifa wanatambuliwa kama wawakilishi wa Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) nasio serekali ya mji wa Vatican.
Tembelea website ya Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki): Bilateral and Multilateral Relations of the Holy See, update on October 22, 2009. imetaja nchi zenye ubalozi na Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki): Tanzania imetajwa ni nchi ya 159.
Lakini ukitaka kujua ubalozi huo upo wapi basi website hii Embassy of Vatican in Tanzania itakusaidia.
Ubalozi wa Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) Tanzania:
Apostolic Nunciature of Holy See (Vatican City) in Dar-es-Salaam, Tanzania
Plot N. 146
Haile Selasie Road
Oyesterbay
P.O. Box 480
Dar-es-Salaam
Tanzania
Phone:
+255-22-266 6422
+255-22-266 7771
Fax:
+255-22-266 8059
Email:
nunzio@cats-net.com
SWALI 1
Wale wazandiki wa dini na chuki za kimadhehebu ebu niambini serekali yetu kujiunga na Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) Tanzania tunafaidi kitu gani kiuchumi (Kijinchi chenyewe ni kina eneo za mraba kilometa 0.44), Idadi ya watu wake kwa sense ya mwaka 2010 inakadiriwa kuwa na watu 829, Uchumi wake unategemea uuzaji wa stampu, na michango ya wakristu duniani, tambua ina bajeti ya wastani wa Trilioni 1.2 watatusaidia nini nchi yenye bajeti inayokadiriwa kufikia Trilioni 11

SWALI 2
Je tunaijua misingi inayoongoza Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) haipingani na Katiba yetu ibara niliyoitaja hapo juu. http://en.wikipedia.org/wiki/Canon_law_(Catholic_Church)


ii. WIMBO WA TAIFA
Tanzania ni nchi yenye makabila mbali mbali na dini tofauti, swali la kujiuliza katika kuupata wimbo wa taifa ilitumika mbinu gani kuuchagua huu tulionao. Hivi kwa makabila zaidi ya 120 tuliyonayo na jadi na tamaduni zetu, watunzi wetu hatukuona inafaa mpaka kuutafuta kuutafsiri wimbo wa Enoch Sontonga Mnajua kuwa asili ya wimbo huu unatokana na wamishionari wa kanisa la Methodist.
Mnajua lakini asili ya wimbo huu Huko Finland wimbo huu unatokana na sala za makanisa makuu ya Finland.
Mbona sisi hatusemi huku ni kubatizwa au tatizo ni Uislamu ikiwa ukatoliki, Umethodist sawa kabisa na ni kwa mujibu wa sheria lakini islamu Marufuku?
Mungu ibariki Afrika - Wikipedia, the free encyclopedia


iii. MAPUMZIKO JUMAPILI NA JUMAMOSI
Kitaifa serekali ya jamhuri ya muungano hupumzika kufanya kazi za kitaifa Jumamosi na Jumapili. Lakini siku hizi mbili ni mapumziko kwa watu wa madhehebu ya Katoliki na Sabato. Hivi dini zingine waliulizwa au ndo hivyo tena la Mkiristo ndio sawa na sheria?
Mifano ipo mingi.....
 
Nimefuatilia mjadala na kuona wengi wa wachangiaji eidha hawajui sheria ya nchi yetu au labda pia wana muono finyu wa mambo.
Mimi navyofahamu nchi yeyote inapotaka kutengeneza uhusiano na nchi nyingine au Taasisi yeyote ni lazima kwanza kuzingatia mambo makuu yafuatayo
  1. Sheria za nchi husika- hasa sheria Mama (KATIBA)
  2. Sheria za kimataifa zilizoridhiwa na Umoja wa Mataifa
  3. Kanuni/sheria na Malengo ya Muungano husika
  4. Faida na Hasara za muungano huo -Kiuchumi, Kijamii, Kisiasa,n.k
Mada yetu ilikuwa Suala la kujiunga na OIC halijapatiwa uvumbuzi.
Maswali ya kujiuliza ni
kujiunga na OIC Tanzania au Zanzibar inavunja kipengele gani cha Sheria.
Je kujiunga na OIC ni sheria gani za kimatifa zinavunjwa. Hivi kunafaida kujiunga na jumuiya yenye wanachama 57 jumuiya ya pili kwa ukubwa duniani baada ya Umoja wa Mataifa. Je hakuna faida za kiuchumi kwa wanachama wa juiya yenye Pato la wastani wa U$D 10,140,000,000/=.
lakini najua kuna wale wataojibu kwa jazba kwa kusema Katiba ya Jamhuri ya muungano Ibara ya 19 (2) inazuia. mimi nasema mtu huyo anakosea na hajaisoma vizuri katiba. labda kwa faida ya wengine ibara hiyo inasema hivi..."Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya
Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.



Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.

Ukisoma kwa makini utaona katiba imetoa uhuru kwa mtu bianafsi kufanya yafuatayo
1. kazi ya kutangaza dini,
2. kufanya ibada
3. kufanya ibada
4. kueneza dini
wakati huo huo ifahamike katiba pia imezuia serekali kufanya yafuatayo:
1. kazi ya kutangaza dini,
2. kufanya ibada
3. kueneza dini
4. shughuli na uendeshaji wa Jumuiya za dini

Swali la kujiuliza ni je kwa Tanzania/Zanziba kiujiunga na OIC je mamlaka ya nchi itakuwa inafanyakazi ya kutangaza dini, kueneza dini, kufanya ibada au inajishughulisha na uendeshaji wa Jumuiya za dini.

Jibu si kweli kwasababu moja tu kuu, OIC sio Shirika linalofanyakazi ya kutangaza dini, kueneza dini, kufanya ibada au linalojishughulisha na uendeshaji wa Jumuiya za dini. Na hii inathibitishwa na malengo ya Shirika la OIC ebu yapitie bila chuki binafsi za kidini wala uzandiki. Malengo yanasema hivi:

Chini ya Mkataba, Shirika lina malengo yafuatayo:
1. Kuboresha na kuimarisha kwa Mahusiano ya udugu na mshikamano kati ya Nchi Wanachama;
2. Kuhifadhi na kulinda maslahi ya pamoja na kulinda harakati halali za nchi wanachama na kuratibu na kuunganisha juhudi za Nchi Wanachama katika mtazamo wa changamoto zinazokabili hasa ulimwengu wa nchi za Kiislamu na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla;
3. Kuheshimu haki ya maamuzi binafsi na yasiyoingiliwa katika mambo ya ndani na kuheshimu uhuru, na uadilifu na uhuru wa mipaka wa eneo la kila nchi wanachama.
4. Kuhakikisha ushiriki wa Nchi Wanachama katika kisiasa za dunia, kiuchumi na kijamii na kushiriki katika mchakato wa maamuzi ya kijamii kupata maslahi yao ya kawaida;
5. Kuthibitisha uungaji mkono wake kwa haki za watu kama ilivyoelezewa katika Mkataba wa Umoja wa Mataifa na sheria za kimataifa.
6. kuimarisha mahusiano ya chumi za kiislamu na ushirikiano wa kibiashara, ili kufikia muungano wa kiuchumi kupelekea kuanzishwa soko la pamoja la kiislamu.
7. Kuweka juhudi za kufikia maendeleo endelevu na mapana ya kibinadamu na maendeleo na ustawi wa kiuchumi kwa nchi wanachama.
8. Kulinda na kutetea sura ya kweli ya Uislamu, ili kukabiliana na udhalilishaji wa Uislamu na kuhimiza mazungumzo kati ya staarabu mbalimbali na dini.
9. Kuimarisha na kuendeleza sayansi na teknolojia na kuhimiza utafiti na ushirikiano kati ya nchi wanachama katika maeneo hayo.

Sasa ebu niambie ni wapi katika malengo haya shirika la OIC linalofanyakazi ya kutangaza dini, kueneza dini, kufanya ibada au linalojishughulisha na uendeshaji wa Jumuiya za dini. Na Shirika kama hili haliwezi kufanya hivyo kwani limesha ainisha katika lengo namba 3 na 5.

Wananchi wenzangu jaribuni basi hata kupitia Mkataba wa Umoja wa Mataifa na sheria za kimataifa kuhusu haki za binaadamu ambazo OIC wameahidi kuzilinda na kuzisimamia kati ya nchi wanachama.

MAAJABU
Mbali ya kukosekana sababu za Tanzania kutojiunga na OIC lakini miongoni mwetu bado tunaamini nchi kujiunga na OIC ni kinyume na Katiba na wapo wale wahafidhana wa chuki za kidini ambao wao kubwa ni kuwa kujiunga na OIC ni kutusilimisha KIAINA kwa jina la misaada

Chuki hizi au ufinyu huu wa mawazo unatokana na sababu kuu zifuatazo

Jina lenyewe ni Organization of "ISLAMIC" Conference. Yaani hawa chochote kile chenye kuashiria uislamu kwao ni sumu lakini sio dini nyingine ni uislamu tu. Vita yao ni dhidi ya Uislamu na waislamu na hapa nitatoa mfano. Tanzania kuana mengi yanafanyika yenye sura za dini lakini kundi hili sijawasikia wakikosoa mfano:
i. UWEPO WA UBALOZI WA HOLLY SEE:
Kuna wachangiaji wengi wameandika kuwa Tanzania inaubalozi na VATICAN napenda hapa kurekebisha Tanzania hatuna ubalozi na VATICAN kama vile ambavyo VATICA haina ubalozi na nchi yeyote.
Tanzania tuna ubalozi na Holly see. Holly see ipo chini ya utawala wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki la Roma, ambapo Askofu wake anajulikana kama Papa. Ni Maaskofu mtakatifu wa Kanisa Katoliki, anayetengeneza serikali kuu ya Kanisa.(Kwa maneno mepesi holly see ni serekali kuu ya kanisa katoliki)

Kwa maana hiyo Tanzania kuwa na ubalozi wa Holly see maana yake ndani ya jamhuri ya muungano tuano ubalozi wa serekali kuu ya kanisa katoliki


Hebu tizama :
Although it is often referred to by the ambiguous term "the Vatican", the Holy See is not the same entity as the Vatican City State, which came into existence only in 1929, while the Holy See dates back to early Christian times.
Ambassadors are officially accredited not to the Vatican City State but to "the Holy See", and papal representatives to states and international organizations are recognized as representing the Holy See, not the Vatican City State.

Tafsri binafsi:
Ingawa mara nyingi huitwa kwa jina lenye utata "Vatican", Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) ni kitu tofauti kabisa na serekali ya mji wa Vatican, Mji ambao (VATCAN) ulianza kuwepo tu mwaka 1929, wakati Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) ilianza mapema ulipoanza ukristo.
Mabalozi wenye vibali rasmi si kwa ajili ya kuwakilisha Taifa la mji wa VATICAN bali Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki)", na wawakilishi wa Papa kwa nchi na mashirika ya kimataifa wanatambuliwa kama wawakilishi wa Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) nasio serekali ya mji wa Vatican.
Tembelea website ya Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki): Bilateral and Multilateral Relations of the Holy See, update on October 22, 2009. imetaja nchi zenye ubalozi na Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki): Tanzania imetajwa ni nchi ya 159.
Lakini ukitaka kujua ubalozi huo upo wapi basi website hii Embassy of Vatican in Tanzania itakusaidia.
Ubalozi wa Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) Tanzania:
Apostolic Nunciature of Holy See (Vatican City) in Dar-es-Salaam, Tanzania
Plot N. 146
Haile Selasie Road
Oyesterbay
P.O. Box 480
Dar-es-Salaam
Tanzania
Phone:
+255-22-266 6422
+255-22-266 7771
Fax:
+255-22-266 8059
Email:
nunzio@cats-net.com
SWALI 1
Wale wazandiki wa dini na chuki za kimadhehebu ebu niambini serekali yetu kujiunga na Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) Tanzania tunafaidi kitu gani kiuchumi (Kijinchi chenyewe ni kina eneo za mraba kilometa 0.44), Idadi ya watu wake kwa sense ya mwaka 2010 inakadiriwa kuwa na watu 829, Uchumi wake unategemea uuzaji wa stampu, na michango ya wakristu duniani, tambua ina bajeti ya wastani wa Trilioni 1.2 watatusaidia nini nchi yenye bajeti inayokadiriwa kufikia Trilioni 11

SWALI 2
Je tunaijua misingi inayoongoza Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) haipingani na Katiba yetu ibara niliyoitaja hapo juu. http://en.wikipedia.org/wiki/Canon_law_(Catholic_Church)


ii. WIMBO WA TAIFA
Tanzania ni nchi yenye makabila mbali mbali na dini tofauti, swali la kujiuliza katika kuupata wimbo wa taifa ilitumika mbinu gani kuuchagua huu tulionao. Hivi kwa makabila zaidi ya 120 tuliyonayo na jadi na tamaduni zetu, watunzi wetu hatukuona inafaa mpaka kuutafuta kuutafsiri wimbo wa Enoch Sontonga Mnajua kuwa asili ya wimbo huu unatokana na wamishionari wa kanisa la Methodist.
Mnajua lakini asili ya wimbo huu Huko Finland wimbo huu unatokana na sala za makanisa makuu ya Finland.
Mbona sisi hatusemi huku ni kubatizwa au tatizo ni Uislamu ikiwa ukatoliki, Umethodist sawa kabisa na ni kwa mujibu wa sheria lakini islamu Marufuku?
Mungu ibariki Afrika - Wikipedia, the free encyclopedia


iii. MAPUMZIKO JUMAPILI NA JUMAMOSI
Kitaifa serekali ya jamhuri ya muungano hupumzika kufanya kazi za kitaifa Jumamosi na Jumapili. Lakini siku hizi mbili ni mapumziko kwa watu wa madhehebu ya Katoliki na Sabato. Hivi dini zingine waliulizwa au ndo hivyo tena la Mkiristo ndio sawa na sheria?
Mifano ipo mingi.....

Excellent explanation at least umejaribu kufafanua na kwa kuongeza nawashauri mkasomi vitabu vya Davinci na Opec Dei ndio mtajua kama je vatican ni state au institution???
 
Mzee Mwanakijiji,
Shukran kwa maelezo yako nadhani majibu yako yangemlenga Mwanafalsafa1 ambaye ameendelea kudai Vatican ni NCHI wakati nchi ni Vatican City..Hili jina limetokana na kitu gani sii sababu kwani hata wewe Mwanakijiji jina lako limetokana na kitu fulani. Nitaendelea kusisitiza kwamba Vatican sio nchi ni Taasisi ya Kikatoliki - Period.

Katika maswala ya citizenship Mkuu wangu hili halihusiani kabisa na kuijua dini ya katoliki, kwa sababu huu ni utaratibu wa Utawala wa Pope.. Ndio maana wanaopewa Uraia wa pale ni wale tu wanaofanya kazi za Kanisa Katoliki...

Hao wale watoto wanaozaliwa hapo na wafanyakazi hupewa uraia wa muda. Swiss Guard anakuwa raia hadi siku akiacha kazi, uraia wake pia unakoma sawa na wafanyakazi wengine woote isipokuwa Papa tu ndiye mwenye Uraia wa kudumu..Ni uraia wa Muda ambao tunaweza sema ni kitu Residential Permit kutokana na mujibu wa sheria zetu..

Hata passport za kusafiria wanapewa pindi tu mtu akisafiri kwa kazi za kikanisa nchi za nje..Kila raia hakai na passport nyumbani kwake kama ilivyo kwetu.
Hao watoto wa wafanyakazi nao ni yale yale as long as wazazi wake bado ni wajiriwa wanakuwa raia lakini akisha fIka utu uzima tu Uraia wake pia unaondolewa vile vile hata kama wazazi wake bado wameajiriwa na kanisa.

Mkuu wangu , unajua fika kwamba hata ikitokea mtoto akazaliwa Vatican City na mzazi au wazazi wako sii wafanykazi wa kanisa, mtoto huyo hapewi Uraia hata wa muda. Kifupi utaratibu woote wa kiutawala unaotumika Vatican City ni wa kidini unaolingana na imani yao ya dini sii mfumo wa kawaida kama nchi nyinginezo. Kuna wanasiasa wanaodai kwamba nchi yeyote pasipo demokarasia hakuna haki na Uhuru wa kweli kwa raia wake! - maneno haya huwezi kuyatumia ktk Utawala wa Vatican City kwa sababu nchi hii haiundwa kwa misingi tunayoijua sisi.

Tunarudi pale pale Vatican sio nchi, na Tanzania tuliingia mkataba na Taasisi ya Vatican hivyo sioni makosa yoyote Zanzibar wakiingia mkataba na OIC maadam ni kwa faida yao. Mkuu wangu, Ukristu au Uislaam hauwezi kutofautiana penye haki na Uhuru...Tunachokifanya Bara ni ule msemo wa - CHAKO CHANGU - CHANGU CHANGU, yaani kila linaloanzishwa Zanzibar tunataka tushirikishwe ni chetu, lakini Ya bara ni yetu sisi pekee, Wazanzibar hawahusiki labda tutawamegee kidogo tukipenda. Huu ndio Ubinafsi na umaskini wa mwafrika kiakili.. Tunapofikia hapo hushindwa kabisa kufikiria nje ya Ufinyu wa fikra za kimasikini na kitumwa yaani kila mtu atabeba msalaba wake.

Mkuuu hii sii haki hata kidogo na hakika hata kama Zanzibar ingekuwa nchi ya Kikristu bado ningesimama na mtazamo wangu pasipo kusita kwani swla sio dini ila haki na uhuru wa wananchi wa nchi hiyo. Natazama haki ya wahusika na sii watu hao ni kina nani kufikiria kama wanastahili haki hiyo!. Hapa JF tuna tabia za Chuki binafsi ambazo ndizo huwasukuma wengi kutoa mchango wao wenye kuelemea chuki binafsi. Na siwalaumu kwani Umaskini huja na mengi sana yaliyolaaniwa na moja kubwa ni kujipendekeza ktk dini ambazo hata kuzifuata zinatushinda isipokuwa kulia na Mungu ktk sala za usiku wa manane -UNAFIKI!

Nafikiri tumemaliza hili La OIC na haki ya Wazanzibar isipokuwa - Thanks to You again kwamba ulituwekea kale ka kitabu ka Nyerere na hatma ya Uongozi Tanzania. Ndipo nilipokuja gundua kwamba hili sii swala dogo isipokuwa ni kubwa kuliko tunavyofikiria..

Bara tulitaka serikali ya tatu kwa sababu Zanzibar ilijiunga na OIC - Mgogoro ukawa mkubwa hadi kumshinda Mwinyi kwa sababu wakati ule Zanzibar ilikuwa na rais wake na waziri kiongozi kisha bara nako tungekuwa na rais na waziri mkuu sijui kiongozi halafu tena Rais wa Jamhuri na makamu wake yaani vurugu tupu. Ndipo Mwalimu na rais Mwinyi walipoamua kuvunja Uanachama wa Zanzibar OIC pamoja na kwamba ilikuwa haki yao na kwa upande wa pili wa madai ya serikali tatu kina Malecela ndio akawavua na kuwaacha uchi kuua hoja ya serikali tatu...

Hivyo hii kitu ni kubwa kuliko kufikiria maswala ya Udini, na hakika this will be the second biggest Nyerere failure baada ya Ujamaa, kwani wale waliotaka serikali tatu wamerudi madarakani na wana nguvu na Zanzibarians keep on fighting for their freedom and rights..
 
So what is the difference between alichosema Mkandara na wewe!!! Mkataba wa Laterai unahusu utambuliko wa nchi but hilo linaweza kufanya but chini yake ikawa ni taasisi ya kimafia iliyo na uhuru wa kufanya jambo lolote duniani?

kama huoni tofauti basi sina namna ya kukusaidia. Vatican ni nchi kama Tanzania, na ni ufalme kama Swaziland! Kanisa Katoliki ndiyo Taasisi!!! Kanisa Katoliki siyo Vatican City.
 
Mzee Mwanakijiji,
Shukran kwa maelezo yako nadhani majibu yako yangemlenga Mwanafalsafa1 ambaye ameendelea kudai Vatican ni NCHI wakati nchi ni Vatican City..Hili jina limetokana na kitu gani sii sababu kwani hata wewe Mwanakijiji jina lako limetokana na kitu fulani. Nitaendelea kusisitiza kwamba Vatican sio nchi ni Taasisi ya Kikatoliki - Period.

Sasa kusisitiza unaweza kabisa lakini utakuwa unasisitiza kutokana na hisia bila ushahidi wa historia nyuma yako, wa kisheria au wa kihalisia. Sasa msisitizo wa namna hiyo ni msisitizo mgumu kuushinda kwa sababu hautokani na ukweli halisi. Ni sawa na mtu atoke na "kusisitiza" kuwa kwenye mwezi kuna mwanamke kabebeshwa kuni na ana mtoto mgongoni. Sasa akiendelea kusisitiza kwa nguvu zote hakufanyi msisitizo kuwa ukweli. Hakuna mahali pamoja unapoweza kupata katika historia au vinginevyo ambavyo patakupa chembe ya ushahidi kuwa Vatican (tunavyofupisha kuhusu Vatican city) kuwa siyo NCHI.


Katika maswala ya citizenship Mkuu wangu hili halihusiani kabisa na kuijua dini ya katoliki, kwa sababu huu ni utaratibu wa Utawala wa Pope.. Ndio maana wanaopewa Uraia wa pale ni wale tu wanaofanya kazi za Kanisa Katoliki...

Uraia unatokana na utaratibu wa nchi husika na Vatican ina utaratibu wake wa uraia kwa mujibu wa Mkataba wa Laterani wa 1929. Kila nchi ina utaratibu wake wa Uraia.

Hao wale watoto wanaozaliwa hapo na wafanyakazi hupewa uraia wa muda. Swiss Guard anakuwa raia hadi siku akiacha kazi, uraia wake pia unakoma sawa na wafanyakazi wengine woote isipokuwa Papa tu ndiye mwenye Uraia wa kudumu..Ni uraia wa Muda ambao tunaweza sema ni kitu Residential Permit kutokana na mujibu wa sheria zetu..

Hapana, uraia wa mtu yeyote ule ni uraia wa muda (unaweza kubadilisha) na wengine uraia wao ni wa kudumu (kama Papa) na ndiyo hukoma baada ya huduma yao kwa sababu ndivyo utaratibu wa uraia wa nchi ya Vatican. Tatizo unaangalia "kwa mujibu wa sheria zetu". Vatican haifuati sheria zetu inafuata "sheria zake" na kwa mujibu wa sheria zake uraia wake ni uraia kamili kama uraia wa Kenya, US, Iraq au nchi nyingine yeyote. Hatuwezi kuhukumu uraia wa Vatican kwa kupitia "sheria zetu".

Hata passport za kusafiria wanapewa pindi tu mtu akisafiri kwa kazi za kikanisa nchi za nje..Kila raia hakai na passport nyumbani kwake kama ilivyo kwetu.

Absolutely wrong; wanapewa passport za kwao wanalala nazo, wanasafiri nazo na si kwamba kila wakitaka kusafiri ndio wanaenda kuchukua passport zao. Passport zao ni hati kamili za kusafiria na wanakuwa nazo kwa muda wote wanaokuwa ni raia wa Vatican. Hawana mtu anayewashikilia passport zao.

Hao watoto wa wafanyakazi nao ni yale yale as long as wazazi wake bado ni wajiriwa wanakuwa raia lakini akisha fIka utu uzima tu Uraia wake pia unaondolewa vile vile hata kama wazazi wake bado wameajiriwa na kanisa.

Hili ni utaratibu wa kisheria tu, hata sisi mtoto aliyezaliwa na wazazi wenye uraia wa nchi nyingine lakini amezaliwa Tanzania anakuwa na uraia wa wazazi wake badi akifikisha miaka 18 anatakiwa kuukana uraia wa wazazi wake na kuchukua wa kwetu au kuukana uraia wetu. Huu ni utaratibu tu wa uraia. KILA nchi ina utataratibu wake wa kupitisha uraia na taratibu hizo hazifanani.


Mkuu wangu , unajua fika kwamba hata ikitokea mtoto akazaliwa Vatican City na mzazi au wazazi wako sii wafanykazi wa kanisa, mtoto huyo hapewi Uraia hata wa muda. Kifupi utaratibu woote wa kiutawala unaotumika Vatican City ni wa kidini unaolingana na imani yao ya dini sii mfumo wa kawaida kama nchi nyinginezo. Kuna wanasiasa wanaodai kwamba nchi yeyote pasipo demokarasia hakuna haki na Uhuru wa kweli kwa raia wake! - maneno haya huwezi kuyatumia ktk Utawala wa Vatican City kwa sababu nchi hii haiundwa kwa misingi tunayoijua sisi.

Bado unapima kwa "misingi tunayoijua sisi"; Vatican ni absolute Monarch ni ufalme. Ni sawa na Saudia na ni sawa na Swaziland sasa kwa vile nchi hizo hazina utaratibu kama wa kwetu hatuwezi kusema siyo "nchi". Saudi Arabia ni absolute Monarch kama ilivyo Vatican na inaongozwa na Qurani kama Katiba yake. Haijaundwa kwa "misingi tunayoijua sisi", hakuna haki na uhuru wa kweli kwa raia wake" kama ilivyo kwetu. Lakini kwa mujibu wa sheria zake wako sahihi na sisi tunaitambua kama nchi na kuwa na mahusiano nayo kama nchi. Vatican ni hivyo hivyo.


Tunarudi pale pale Vatican sio nchi, na Tanzania tuliingia mkataba na Taasisi ya Vatican hivyo sioni makosa yoyote Zanzibar wakiingia mkataba na OIC maadam ni kwa faida yao.

Kama nilivyosema hapo awali, unaweza kusisitiza, kurudia rudia au hata kurejea mara kwa mara kwua "Vatican siyo Nchi" lakini haiondoi ukweli kuwa ni nchi. Ni sawa na mtu mwingine aje na kusema Saudia siyo nchi ati kwa sababu haifanani na ya kwetu, inaongozwa na Mfalme na Katiba yake ni Qurani! Hapana ni nchi. Tanzania haijawahi kuingia Mkataba na Taasisi ya Vatican. Siyo wakati wa Nyerere hadi sasa. Nakupa changamoto utudokeze tu Mkataba na "Taasisi" ya Vatican uliingiwa lini, wapi na nani?

Mkuu wangu, Ukristu au Uislaam hauwezi kutofautiana penye haki na Uhuru...Tunachokifanya Bara ni ule msemo wa - CHAKO CHANGU - CHANGU CHANGU, yaani kila linaloanzishwa Zanzibar tunataka tushirikishwe ni chetu, lakini Ya bara ni yetu sisi pekee, Wazanzibar hawahusiki labda tutawamegee kidogo tukipenda. Huu ndio Ubinafsi na umaskini wa mwafrika kiakili.. Tunapofikia hapo hushindwa kabisa kufikiria nje ya Ufinyu wa fikra za kimasikini na kitumwa yaani kila mtu atabeba msalaba wake.

Hivi Tanzania imeungana na Nchi ya Kikatoliki ya Vatican? La hasha. Tanzania na Vatican vina uhusiano wa kibalozi kama nchi mbili zilivyo au kama ilivyo Uhusiano wa Kibalozi kati ya Tanzania na nchi ya Kiislamu ya Saudi Arabia. Tanzania haijaungana na Saudi Arabia bali lina ushirikiano. Lakini kwenye OIC watu hawataki kuwa na uhusiano wa kibalozi (kwani inawezekana) lakini wanataka tujiunge kama nchi. Hapa ndipo mgogoro wote ulipo. Binafsi (kama nilivyosema miaka minne iliyopita) ningependa Tanzania iwe na uhusiano wa kibalozi na OIC kama US ilivyo na balozi wake pale. Tunaweza kukaribisha OIC kufungua ubalozi wao wa kwanza katika Afrika ya Mashariki.

Lakini vile vile sina tatizo hasa la kujiunga na OIC isipokuwa mpaka wabadilishe sehemu ya Katiba yao kuruhusu non-islamic countries wenye kukubaliana na malengo yao kuweza kujiunga bila kuonekana wanajiunga kwa sababu ya Uislamu wao. Kwa mfano, Msumbiji na Rwanda zimejiunga na Jumuiya ya Madola, lakini zote mbili hazijawahi kuwa makoloni ya Uingereza. Zimejiunga kwa sababu katiba ya Commonwealth inaruhusu uwezekano huo.

Mkuuu hii sii haki hata kidogo na hakika hata kama Zanzibar ingekuwa nchi ya Kikristu bado ningesimama na mtazamo wangu pasipo kusita kwani swla sio dini ila haki na uhuru wa wananchi wa nchi hiyo. Natazama haki ya wahusika na sii watu hao ni kina nani kufikiria kama wanastahili haki hiyo!. Hapa JF tuna tabia za Chuki binafsi ambazo ndizo huwasukuma wengi kutoa mchango wao wenye kuelemea chuki binafsi. Na siwalaumu kwani Umaskini huja na mengi sana yaliyolaaniwa na moja kubwa ni kujipendekeza ktk dini ambazo hata kuzifuata zinatushinda isipokuwa kulia na Mungu ktk sala za usiku wa manane -UNAFIKI!

Hili nitakuachia mkuu.


Nafikiri tumemaliza hili La OIC na haki ya Wazanzibar isipokuwa - Thanks to You again kwamba ulituwekea kale ka kitabu ka Nyerere na hatma ya Uongozi Tanzania. Ndipo nilipokuja gundua kwamba hili sii swala dogo isipokuwa ni kubwa kuliko tunavyofikiria..

Kwanini iwe ni haki ya Wazanzibari tu na isiwe haki ya Watanzania wote? Binafsi ningependa huo uhusiano uwe kati ya Tanzania na OIC. sehemu sehemu moja tu ya muungano kwani kama Waislamu wapo pande zote mbili au tunataka Waislamu wa Zanzibar tu ndio wanufaike na "misaada" hiyo ya OIC. Kwanini tusipiganie kuwa Tanzania nzima ishirikiane na OIC?


Bara tulitaka serikali ya tatu kwa sababu Zanzibar ilijiunga na OIC - Mgogoro ukawa mkubwa hadi kumshinda Mwinyi kwa sababu wakati ule Zanzibar ilikuwa na rais wake na waziri kiongozi kisha bara nako tungekuwa na rais na waziri mkuu sijui kiongozi halafu tena Rais wa Jamhuri na makamu wake yaani vurugu tupu. Ndipo Mwalimu na rais Mwinyi walipoamua kuvunja Uanachama wa Zanzibar OIC pamoja na kwamba ilikuwa haki yao na kwa upande wa pili wa madai ya serikali tatu kina Malecela ndio akawavua na kuwaacha uchi kuua hoja ya serikali tatu...

Bara hatukutaka serikali tatu kama umesoma vizuri kile kijitabu. Kulikuwa na kundi la watu wachache tu waliotaka kufanya hivyo. CCM haikutaka serikali tatu, Tume ya Kisanga haikutaka hivyo na NEC haikutaka hivyo. Watu wa bara hatujawahi kudai serikali tatu.

Hivyo hii kitu ni kubwa kuliko kufikiria maswala ya Udini, na hakika this will be the second biggest Nyerere failure baada ya Ujamaa, kwani wale waliotaka serikali tatu wamerudi madarakani na wana nguvu na Zanzibarians keep on fighting for their freedom and rights..

Nimekupata vizuri sana. Lakini sisi Watanzania wengine tunapigania haki na uhuru wetu vile vile. Haki ya kulazimisha Tanzania au sehemu yake kuingizwa pasipo masharti kwenye taasisi ya kidini. Tunataka kuwa na haki ya kuhusiana na OIC kama vile tunavyohusiana na taasisi nyingine za kimataifa. Tayari tuna balozi kwenye Umoja wa Mataifa na yupo anayetuwakilisha kwenye taasisi za Umoja huo na vyombo vya fedha kule Uswisi. Kwanini tusiwe na balozi wa OIC sielewi. Kwanini option pekee tunayopewa ni "kujiunga au kutokujiunga"? Hakuna anayetoa jibu wakati options nyingine za uhusiano rasmi zipo?
 
Maswali ya kujiuliza ni
kujiunga na OIC Tanzania au Zanzibar inavunja kipengele gani cha Sheria.
Je kujiunga na OIC ni sheria gani za kimatifa zinavunjwa. Hivi kunafaida kujiunga na jumuiya yenye wanachama 57 jumuiya ya pili kwa ukubwa duniani baada ya Umoja wa Mataifa.

Mbona tayari tuna mahusiano ya kibalozi karibu na nchi zote zilizoko kwenye OIC tayari? Na kama faida inakuja kwa kujiunga tu, je Somalia imefaidika vipi na kuwa mwanachama wa OIC kwa zaidi ya miaka 40?
Je hakuna faida za kiuchumi kwa wanachama wa juiya yenye Pato la wastani wa U$D 10,140,000,000/=.

Hizi faida za kiuchumi zinakuja kwa njia ya mnunurisho? yaani tukijiunga tu tutapata faida za kiuchumi. Kama hilo lingekuwa kweli taasisi zote ambazo tayari Tanzania inashirikiana nazo na nchi zote tunazohusiana nazo ikiwemo UK, Saudia, Iran, US, n.k na bado hatujapata faida kubwa za kiuchumi, sasa zitakuja tu ghafla bin vuup kwa sababu leo tumekuwa wanachama wa OIC? Haya ni matamanio yasiyo na msingi.






Swali la kujiuliza ni je kwa Tanzania/Zanziba kiujiunga na OIC je mamlaka ya nchi itakuwa inafanyakazi ya kutangaza dini, kueneza dini, kufanya ibada au inajishughulisha na uendeshaji wa Jumuiya za dini.

Hili ni suali zuri ambalo unalijibu mwenyewe hapa:


Jibu si kweli kwasababu moja tu kuu, OIC sio Shirika linalofanyakazi ya kutangaza dini, kueneza dini, kufanya ibada au linalojishughulisha na uendeshaji wa Jumuiya za dini. Na hii inathibitishwa na malengo ya Shirika la OIC ebu yapitie bila chuki binafsi za kidini wala uzandiki. Malengo yanasema hivi:

Chini ya Mkataba, Shirika lina malengo yafuatayo:
1. Kuboresha na kuimarisha kwa Mahusiano ya udugu na mshikamano kati ya Nchi Wanachama;

Kwa makusudi umekwepa kutafrisi Katiba ya OIC inavyosema hasa kwa kuondoa baadhi ya maneno. Naomba niyarejeshe:

to be guided by the noble Islamic values of unity and fraternity, and affirming the essentiality of promoting and consolidating the unity and solidarity among the Member States in securing their common interests at the international arena

sehemu ya pili unasema lengo ni:

2. Kuhifadhi na kulinda maslahi ya pamoja na kulinda harakati halali za nchi wanachama na kuratibu na kuunganisha juhudi za Nchi Wanachama katika mtazamo wa changamoto zinazokabili hasa ulimwengu wa nchi za Kiislamu na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla;

Kwa maneno yako mwenyewe unaona kuwa msisitizo wa pekee uko kwa nchi za Kiislamu!

3. Kuheshimu haki ya maamuzi binafsi na yasiyoingiliwa katika mambo ya ndani na kuheshimu uhuru, na uadilifu na uhuru wa mipaka wa eneo la kila nchi wanachama.

4. Kuhakikisha ushiriki wa Nchi Wanachama katika kisiasa za dunia, kiuchumi na kijamii na kushiriki katika mchakato wa maamuzi ya kijamii kupata maslahi yao ya kawaida;
5. Kuthibitisha uungaji mkono wake kwa haki za watu kama ilivyoelezewa katika Mkataba wa Umoja wa Mataifa na sheria za kimataifa.
6. kuimarisha mahusiano ya chumi za kiislamu na ushirikiano wa kibiashara, ili kufikia muungano wa kiuchumi kupelekea kuanzishwa soko la pamoja la kiislamu.
7. Kuweka juhudi za kufikia maendeleo endelevu na mapana ya kibinadamu na maendeleo na ustawi wa kiuchumi kwa nchi wanachama.
8. Kulinda na kutetea sura ya kweli ya Uislamu, ili kukabiliana na udhalilishaji wa Uislamu na kuhimiza mazungumzo kati ya staarabu mbalimbali na dini.
9. Kuimarisha na kuendeleza sayansi na teknolojia na kuhimiza utafiti na ushirikiano kati ya nchi wanachama katika maeneo hayo.

Haya maneno uliyoyaandika kwa Kiswahili ni matamu lakini siyo kilichomo moja kwa moja kwenye Katiba ya OIC. Ngoja niweke hapa kama kilivyo kwani kuna mtu mwingine ameshakiweka huko nyuma vile vile.

to adhere our commitment to the principles of the United Nations Charter, the
present Charter and International Law;
to preserve and promote the lofty Islamic values of peace, compassion,
tolerance, equality, justice and human dignity;
to endeavour to work for revitalizing Islam's pioneering role in the world
while ensuring sustainable development, progress and prosperity for the
peoples of Member States;
to enhance and strengthen the bond of unity and solidarity among the Muslim
peoples and Member States;
to respect, safeguard and defend the national sovereignty, independence and
territorial integrity of all Member States;
to contribute to international peace and security, understanding and dialogue
among civilizations, cultures and religions and promote and encourage
friendly relations and good neighbourliness, mutual respect and cooperation;
to promote human rights and fundamental freedoms, good governance, rule of
law, democracy and accountability in Member States in accordance with their
constitutional and legal systems;
2
to promote confidence and encourage friendly relations, mutual respect and
cooperation between Member States and other States;
to foster noble Islamic values concerning moderation, tolerance, respect for
diversity, preservation of Islamic symbols and common heritage and to defend
the universality of Islamic religion;
to advance the acquisition and popularization of knowledge in consonance
with the lofty ideals of Islam to achieve intellectual excellence;
to promote cooperation among Member States to achieve sustained socioeconomic
development for effective integration in the global economy, in
conformity with the principles of partnership and equality;
to preserve and promote all aspects related to environment for present and
future generations;
to respect the right of self-determination and non-interference in the domestic
affairs and to respect sovereignty, independence and territorial integrity of
each Member State;
to support the struggle of the Palestinian people, who are presently under
foreign occupation, and to empower them to attain their inalienable rights,
including the right to self-determination, and to establish their sovereign state
with Al-Quds Al-Sharif as its capital, while safeguarding its historic and
Islamic character, and the holy places therein;
to safeguard and promote the rights of women and their participation in all
spheres of life, in accordance with the laws and legislation of Member States;
to create conducive conditions for sound upbringing of Muslim children and
youth, and to inculcate in them Islamic values through education for
strengthening their cultural, social, moral and ethical ideals;
to assist Muslim minorities and communities outside the Member States to
preserve their dignity, cultural and religious identity;
to uphold the objectives and principles of the present Charter, the Charter of
the United Nations and international law as well as international humanitarian
law while strictly adhering to the principle of non-interference in matters
which are essentially within the domestic jurisdiction of any State;
to strive to achieve good governance at the international level and the
democratization of the international relations based on the principles of
equality and mutual respect among States and non-interference in matters
which are within their domestic jurisdiction;
Sasa ebu niambie ni wapi katika malengo haya shirika la OIC linalofanyakazi ya kutangaza dini, kueneza dini, kufanya ibada au linalojishughulisha na uendeshaji wa Jumuiya za dini. Na Shirika kama hili haliwezi kufanya hivyo kwani limesha ainisha katika lengo namba 3 na 5.

Hayo ndio malengo yake! malengo yamezunguka katika kuulinda Uislamu na maslahi na tunu za Kiislamu na kwa kuzingatia mafundisho ya Kiislamu. Tanzania kama ilivyo haiwezi kuingia mkataba kuyasimamia hayo. Isipokuwa kama Mkataba huo utaweka wazi kabisa kuwa Tanzania haitayasimamia masuala yenye mlengo wa dini isipokuwa masuala hayo mengine ambayo tunakubaliana ni bora. Bila kuweka hivyo Tanzania haiwezi (najumlisha na Zanzibar hapa) kuwa sehemu ya OIC hadi OIC aidha ibadili Katiba yake au iweke exception clause ya kutoifunga Tanzania na masuala ya kidini ya malengo yake.

Wananchi wenzangu jaribuni basi hata kupitia Mkataba wa Umoja wa Mataifa na sheria za kimataifa kuhusu haki za binaadamu ambazo OIC wameahidi kuzilinda na kuzisimamia kati ya nchi wanachama.

MAAJABU
Mbali ya kukosekana sababu za Tanzania kutojiunga na OIC lakini miongoni mwetu bado tunaamini nchi kujiunga na OIC ni kinyume na Katiba na wapo wale wahafidhana wa chuki za kidini ambao wao kubwa ni kuwa kujiunga na OIC ni kutusilimisha KIAINA kwa jina la misaada

Chuki hizi au ufinyu huu wa mawazo unatokana na sababu kuu zifuatazo

Jina lenyewe ni Organization of "ISLAMIC" Conference. Yaani hawa chochote kile chenye kuashiria uislamu kwao ni sumu lakini sio dini nyingine ni uislamu tu. Vita yao ni dhidi ya Uislamu na waislamu na hapa nitatoa mfano. Tanzania kuana mengi yanafanyika yenye sura za dini lakini kundi hili sijawasikia wakikosoa mfano:
i. UWEPO WA UBALOZI WA HOLLY SEE:
Kuna wachangiaji wengi wameandika kuwa Tanzania inaubalozi na VATICAN napenda hapa kurekebisha Tanzania hatuna ubalozi na VATICAN kama vile ambavyo VATICA haina ubalozi na nchi yeyote.
Tanzania tuna ubalozi na Holly see. Holly see ipo chini ya utawala wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki la Roma, ambapo Askofu wake anajulikana kama Papa. Ni Maaskofu mtakatifu wa Kanisa Katoliki, anayetengeneza serikali kuu ya Kanisa.(Kwa maneno mepesi holly see ni serekali kuu ya kanisa katoliki)

Kwa maana hiyo Tanzania kuwa na ubalozi wa Holly see maana yake ndani ya jamhuri ya muungano tuano ubalozi wa serekali kuu ya kanisa katoliki


Hebu tizama :
Although it is often referred to by the ambiguous term "the Vatican", the Holy See is not the same entity as the Vatican City State, which came into existence only in 1929, while the Holy See dates back to early Christian times.
Ambassadors are officially accredited not to the Vatican City State but to "the Holy See", and papal representatives to states and international organizations are recognized as representing the Holy See, not the Vatican City State.

Tafsri binafsi:
Ingawa mara nyingi huitwa kwa jina lenye utata "Vatican", Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) ni kitu tofauti kabisa na serekali ya mji wa Vatican, Mji ambao (VATCAN) ulianza kuwepo tu mwaka 1929, wakati Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) ilianza mapema ulipoanza ukristo.
Mabalozi wenye vibali rasmi si kwa ajili ya kuwakilisha Taifa la mji wa VATICAN bali Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki)", na wawakilishi wa Papa kwa nchi na mashirika ya kimataifa wanatambuliwa kama wawakilishi wa Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) nasio serekali ya mji wa Vatican.
Tembelea website ya Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki): Bilateral and Multilateral Relations of the Holy See, update on October 22, 2009. imetaja nchi zenye ubalozi na Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki): Tanzania imetajwa ni nchi ya 159.
Lakini ukitaka kujua ubalozi huo upo wapi basi website hii Embassy of Vatican in Tanzania itakusaidia.
Ubalozi wa Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) Tanzania:
Apostolic Nunciature of Holy See (Vatican City) in Dar-es-Salaam, Tanzania
Plot N. 146
Haile Selasie Road
Oyesterbay
P.O. Box 480
Dar-es-Salaam
Tanzania
Phone:
+255-22-266 6422
+255-22-266 7771
Fax:
+255-22-266 8059
Email:
nunzio@cats-net.com
SWALI 1


Haya nimeyaeleza kwa kirefu kwenye jibu langu hapo juu. Ila kama wengine wasiyoyapata vyema umeyachanganya changanya mno.

Wale wazandiki wa dini na chuki za kimadhehebu ebu niambini serekali yetu kujiunga na Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) Tanzania tunafaidi kitu gani kiuchumi (Kijinchi chenyewe ni kina eneo za mraba kilometa 0.44),

Tanzania haijawhai kujiunga na kijinchi (angalau mwenzetu unakubali kuwa Vatican ni nchi). Tuna uhusiano wa kibalozi na Vatican kama tulivyo na uhusiano wa kibalozi na Nchi ya Kiislamu ya Saudia. Lakini hatusemi ati tumejiunga na Iran au Saudia!

Idadi ya watu wake kwa sense ya mwaka 2010 inakadiriwa kuwa na watu 829, Uchumi wake unategemea uuzaji wa stampu, na michango ya wakristu duniani, tambua ina bajeti ya wastani wa Trilioni 1.2 watatusaidia nini nchi yenye bajeti inayokadiriwa kufikia Trilioni 11

Nchi ni nchi! haijalishi idadi yake! Kwani nchi ya visiwa vya Malta ina watu wangapi? Zanzibar kabla ya kuungana ilikuwa ina watu wangapi ili iwe nchi, Slovania ni nchi yenye ukubwa wa wangapi? Monaco ina watu wangapi? Iceland ina watu wangapi? Nchi yaweza kuwa nchi hata kama ina watu 10 tu alimradi ni nchi halali.


SWALI 2
Je tunaijua misingi inayoongoza Holy See (serekali kuu ya kanisa katoliki) haipingani na Katiba yetu ibara niliyoitaja hapo juu. http://en.wikipedia.org/wiki/Canon_law_(Catholic_Church)

tutarudi pale pale, tuna uhusiano wa kibalozi na Holy See kama vile Morocco, Iran na Iraq zilivyonavyo!


ii. WIMBO WA TAIFA
Tanzania ni nchi yenye makabila mbali mbali na dini tofauti, swali la kujiuliza katika kuupata wimbo wa taifa ilitumika mbinu gani kuuchagua huu tulionao. Hivi kwa makabila zaidi ya 120 tuliyonayo na jadi na tamaduni zetu, watunzi wetu hatukuona inafaa mpaka kuutafuta kuutafsiri wimbo wa Enoch Sontonga Mnajua kuwa asili ya wimbo huu unatokana na wamishionari wa kanisa la Methodist.
Mnajua lakini asili ya wimbo huu Huko Finland wimbo huu unatokana na sala za makanisa makuu ya Finland.
Mbona sisi hatusemi huku ni kubatizwa au tatizo ni Uislamu ikiwa ukatoliki, Umethodist sawa kabisa na ni kwa mujibu wa sheria lakini islamu Marufuku?

Maswali mengine muwe mnafikiria mantiki yake. Mbona leo hii tunatumia majina ya siku za wiki kwa kufuata mfumo wa Kiislamu? Kwa mfano, Jumamosi, Jumapili, Jumatatu hadi Ijumaa ni mfuatano wa wiki ya Kiislamu na hatusemi kuwa Tanzania imesilimishwa? Kwa yahudi Jumamosi ndiyo siku ya Saba, kwa wa Europa ni Jumapili wakati sisi kwetu siku ya saba ni Ijumaa!

iii. MAPUMZIKO JUMAPILI NA JUMAMOSI
Kitaifa serekali ya jamhuri ya muungano hupumzika kufanya kazi za kitaifa Jumamosi na Jumapili. Lakini siku hizi mbili ni mapumziko kwa watu wa madhehebu ya Katoliki na Sabato. Hivi dini zingine waliulizwa au ndo hivyo tena la Mkiristo ndio sawa na sheria?
Mifano ipo mingi.....

siku moja tunapumzika kwa wiki, lakini mbona tunafuata sheria za mfumo wa Uingereza? Mbona tunazungumza Kiingereza lugha ya nchi ya Kikristu na tunatumia Kiswahili chenye misamiati ya kutoka kwa nchi za Kiarabu? Jamani maswali mengine yanakosa mantiki kwani yanaonesha kutokukomaa kwa hoja tu. Vinginevyo, tutafika mahali tufanye kama wanavyofranya North Korea, Tuchague siku zetu wenyewe, taratibu zetu zisizofanana na sehemu au utamaduni mwingine wowote duniani!
 
Kwanza nikushukuru kwa taarifa hizi nyingi na madai haya mengi juu ya Vatican na Ukatoliki ambayo umeyapendekeza kama ni ukweli kabisa. Ninaamini kuwa unayaamini uliyoyoyasema kuwa ni kweli na hivyo wengine wanaosoma wayapokee pia kama ni ukweli. Ni kusudio langu kuonesha kuwa yote uliyoyasema hayakubaliani na ukweli wa kihistoria na kihalisia kuhusu Vatican, Ukatoliki na Wakatoliki.

Umesema mambo kadhaa ambayo labda niyatenganishe kutoka insha fupi hapo juu. Umedai kwamba:


  1. Vatican ni Taasisi ambayo imeunda nchi ndani ya Italia baada ya kuchukua au kupewa ardhi ili Papa atawale dunia ya ukatoliki (hivyo Vatican siyo nchi)
  2. Vatican siyo nchi kwa sababu uraia wa wananchi wake hautokani na uzawa
  3. Mtu yeyote anaweza kuwa raia wa Vatican (kutumia maneno "hata wewe waweza"
  4. Vatican wanaishi viongozi wa dini
  5. Raia wake ni waumini wote wa Kanisa Katoliki sehemu yoyote duniani.

Hofu yangu ni kuwa baadhi ya watu ambao wamesoma maelezo yake yawezekana wameyachukulia kama ni ukweli bila kuhoji msingi wake au ukweli wake. Na kutoka katika kuyaamini kwa sababu yamekaa kama "facts" basi na wao wanaweza kujikuta wanayarudia kwa watu wengine na taarifa sahihi ikaendelea kupitisha kutoka mtu mmoja kwenda mwingine.

1. VATICAN NI TAASISI

Hili ni jibu rahisi ambalo mtu yeyote anaweza kuangalia kwa urahisi kwenye intaneti au maktaba. Jina kamili ni Nchi ya Vatican City (Vatican City State). Jina la "Vatican" ni la zamani na limetangulia Upapa kwani linatokana na jina la Kilatini "Mons Vaticanus" yaani "Mlima wa Vatican". Historia inasema ni katika mlima (kwa kweli ni kilima) ndipo Mt. Petro aliuawa kwa kusulubiwa kichwa chini miguu juu na ni juu ya kabuli lake ndipo kanisa la Mt. Petro lilijengwa ambalo baadaye limeendelea kukuzwa hadi kufikia hilo tunalolijua kama St. Peter's Basilica.

Mapapa kwa muda mrefu walikuwa na utawala wa Kanisa na utawala wa kisiasa (secular) na wakiwa na kazi hizo mbili waliweza kutawala maeneo mbalimbali ambayo yalijulikana kama "Majimbo ya Papa – Papal States". Mfumo huu wa upili (duality) wa Papa kuwa mtawala wa Kanisa na maeneo ulidumu kwa karibu miaka elfu hadi mwanzoni mwa karne ya 19 ambapo Ufalme wa Italia ulipoundwa. Tukumbuke kuwa Italia wakati huo ilikuwa ni mgawanyo wa falme na himaya ndogo ndogo kama za Sicily, Tuscany, Sardinia, Savoy, Nice n.k kila mmoja ikiwa na mkuu wake na Papa naye alikuwa na eneo lake.

Vita kati ya falme hizo na watawala wa Austria na Ufaransa na wenyewe kwa wenyewe ndizo zilizosababisha hatimaye Waitaliano kutaka kuungana chini ya kiongozi au uongozi mmoja. Hadi inafikia 1870 maeneo na mali ya Papa yalikuwa katika hatari ya kuchukuliwa na watawala wapya wakiongozwa na ufalme wa Piedmont (makao yake makuu Turin). Kuanzia wakati huo hadi 1929 kulikuwa na kile kinachoitwa na wanahistoria kuwa ni "Swali kuhusu Roma" yaani katika Italia hiyo mpya Papa (ambaye alikuwa anatawala pia maeneo yake akiwa na mabalozi na nchi nyingine zikiwa na ubalozi naye atakuwa nani wakati taifa sasa ni Ufalme wa Italia?

Na yeye Papa alikataa kuondoka hata Vatikani hadi suala hilo litatuliwe kwani kwa upande wake hakuwa tayari kumtambua mfalme mpya wa Italia. Kulikuwa na makubaliano ambayo yalimruhusu Papa kuendelea kufanya kazi zake kupokea mabalozi n.k kama wakuu wengine wa nchi.

Mfalme mpya wa Italia hakumnyanyasa sana Papa lakini alitaifisha mali kadhaa za Papa ikiwemo maskani yake ya Quirinal ambayo leo hii ndio maskani rasmi ya Rais wa Italia. Papa Pius IX ndiyo alikuwa mtawala wa mwisho wa tawala mbalimbali za kipapa (yale maeneo niliyoyataja hapo juu) baada ya Jiji la Roma nalo kuchukuliwa na kumfanya ajitangaze kuwa amekuwa "mfungwa ndani ya Kuta za Vatican".

Mgongano kati ya Ufalme wa Italia na Papa ulimalizika kwa makubaliano maarufu yajulikanayo kama Makubaliano ya Lateran (Unaweza kutafuta yanaitwa Lateran Treaty) ambayo yalimaliza swali la Uroma kwa kuitambua Vatican kama nchi hakimiya (sovereign state) na kuhakikisha mali zake nyingine hazichukuliwi n.k Kutokana na hilo Vatican siyo sehemu ya Italia ni nchi kamili iliyoundwa kwa mkataba halali uliouingiwa kati ya Benito Musolini kwa niaba ya Mfalme Victor Emmanuel III na Waziri wa Mambo ya Nje wa Papa Cardinali Gaspari kwa niaba ya Papa Pius IX.

Ni vizuri nitenganishe vitu ambavyo kwa mtu asiye Mkatoliki (na hata Wakatoliki wengine) hawavielewi. Kuna kitu tunakiita "Holy See" na kuna "Vatican City State". Mambo mengi tunayoyaona yanafanywa na Papa au Kanisa Katoliki n.k yanafanywa na Holy See na siyo nchi ya Vatican.

Holy See (Kiti cha Papa a.k.a Upapa) ni utawala wa kidini wa Baba Mtakatifu ndani ya Kanisa Katoliki ambao huundwa na Papa mwenyewe na Kuria ya Roma wakati Vatican City State inaongozwa na Gavana wa Vatican chini ya Papa. Vyote viwili vinahusiana lakini si kitu kimoja. Utawala wa Papa basi siyo jamhuri (yenye kuhitaji vyama vya siasa kupiga kura n.k) bali ni Ufalme kamili – absolute monarchy. Maana yake ni kuwa Papa ana mamlaka yote ya kutunga sheria, haki, na utawala. Kutokana na hili utaona kuwa mabalozi wote hupelekwa Holy See na siyo Vatican na hata kile tunachoita Ubalozi wa Vatican kimsingi ni ubalozi wa Upapa – mfalme.

Kanisa Katoliki la Tanzania au la mahali linauongozi wake katika mambo ya askofu wake. Hivyo balozi wa Holy See hayuko juu ya Pengo kwani yeye yuko kwa kumwakilisha mfalme (Papa) kwa serikali ya Tanzania na Tanzania inapeleka balozi wake huko. Kutokana na ukweli kuwa Holy See ndiyo yenye mlolongo wa huduma ya kibalozi ya zamani zaidi duniani kuliko nchi nyingine yeyote (kuanzia 325AD) nchi kadhaa zina mabalozi wake huko. Miongoni mwa nchi za Kiislamu ambazo zinatambua hili na zina uhusiano wa kibalozi na Holy See ni pamoja na:

Morocco
Misri
Iran
Iraq
Uturuki
Palestine
Azeirjabain

Tanzania kama nchi hizo nayo ina ubalozi kwa Papa na hili si tatizo kuwa na ubalozi na taifa la kidini. Tanzania ina balozi Saudi Arabia ambao ni ufalme, tuna ubalozi Jordani ambao ni Ufalme na tuna mahusiano ya kibalozi na Falme za Kiarabu. Hizi zote ni falme ambazo zina msingi wa kidini kama vile ulivyo Upapa na dini ya Kikatoliki. Hakuna mtu ambaye amewahi kuhoji kwanini Tanzania ina husiana na nchi hizi au kwanini Jordani ina ubalozi Tanzania wakati ni ufalme wa utawala wa Kiislamu? Kumbe la msingi ni kuwa kwa vile hizi zote ni nchi halali na tunazitambua hivyo hakuna tatizo la kuwa na balozi nazo. Hili ni kweli tangu wakati wa Nyerere hadi leo hii.
Kwa hiyo, Vatican siyo "taasisi" bali ni nchi kamili, iliyoundwa kufuatia mkataba wa Laterani ambaye mkuu wake ni Papa. Haijawahi kuchukua eneo la nchi nyingine au mtu mwingine ili liwe chini ya Papa bali Papa ndiye alinyang'anywa maeneo aliyokuwa akiyatawala kwa karibu miaka elfu kufuatia vita vya Waitalia vilivyoiunganisha Italia. Kwa mkataba wa Laterani na nyongeza yake aliachiwa hiyo Vatican City pamoja na maeneo mengine ambayo yako nje ya kuta za Vatican (kama maktaba, makanisa yaliyopo sehemu mbalimbali za Italia na magazi mengine ya kipapa).

Kwa mtu yeyote anayejisikia kubisha anatakiwa aeleze ni Vatican City imetoka wapi na ilikuwa taasisi kwa utaratibu gani?

2: HAKUNA URAIA WA KUZALIWA HIVYO SI NCHI

Kwanza, niseme si kweli; Uraia wa Vatican unaweza kupatikana kwa watoto na wenza wa maofisa wanaofanya kazi Vatican. Kwa watoto hadi watakapofikisha miaka 25. Uraia ni suala la kisheria na kila nchi ina utaratibu wake. Mkataba wa Laterani nilioutaja hapo juu ndio unasimamia uraia wa Vatican vile vile. Raia wa Vatican ambaye anapoteza uraia wa Vatican au wa nchi yake (kwa wale wenye uraia wa nchi mbili) basi kwa mujibu wa Laterani anapata uraia wa Italia automatically.

Hadi mwaka mwishoni mwa 2005 kulikuwa na watu 557 wenye uraia wa Vatican. Miongoni mwao ni:

Papa
58 -Makadinali (ambao wanaoishi au kufanya kazi karibu na Roma). Ni muhimu kutambua kuwa siyo makardinali wote wenye uraia wa Vatican. Kanisa Katoliki lina makardinali 199 walio hai (hadi naandika hii) ambao kati yao ni 109 ndio wanauwezo wa kupiga kura kumchagua papa (wapiga kura wanatakiwa wawe ni wale chini ya miaka 80).
293 Waklegi (mapadre, mashemasi) wanaofanya kazi katika balozi mbalimbali za Holy See pote duniani. Baadhi yao ndio kama yule Askofu Mkuu Novatus Rugambwa ambaye ameteuliwa mapema mwaka huu kuwa Balozi wa Papa huko Sao Tome na Principe.
62 Watendaji wengine wa kanisa wanaofanya kazi Vatican
101 Maafisa wa vikosi vya usalama vya Vatican wakiwemo wale Swiss Guard wanaomlinda Papa
43 Walei wengine wanaofanya kazi hapo au familia na watoto wao.

Na Vatican inatoa passport za utumishi na za kibalozi. Passport kama hizi hutolewa na taasisi kama Umoja wa Mataifa au na taasisi nyingine zinazotambulika kimataifa. Taasisi kama Umoja wa Afrika na yenyewe inatoa passport zake za utumishi na wakuu wa nchi zote 53 za Umoja huo wamepewa passport hizo pamoja na watendaji wake wengine na watu wengine mashuhuri. Kutolewa passport si lazima kuwa suala la uraia ni suala la kumtambulisha msafiri kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine na zinatumika kwa makubaliano ya kutambuliwa kwa taasisi inayotoa. Naamini hata OIC inatoa passport za namna hii kwa watendaji wake.


3: MTU YEYOTE ANAWEZA KUWA RAIA WA VATICAN
Ni kweli mtu yeyote anaweza kuwa "raia wa Vatican" endapo tu mtu huyo ametimiza masharti ya uraia huo kwa mujibu wa Katiba ya Vatican na makubaliano ya Vaticani. Siyo rahisi kuupata uraia wa Vatican. Kwani hautokani na damu tu au kuwa naturalized bali unatokana na huduma (service) au ofisi ya mtu na kutoka hapo ndipo kwa watoto au wenzi wanaweza kuupata uraia huo.

4: VATICAN WANAISHI VIONGOZI WA DINI
Hili ni kweli kiasi. Lakini siyo viongozi wa dini tu. Wanaishi wafanyakazi wa Taifa la Vatican na raia wake vile vile wakiwemo watoto wa wafanyakazi na watendaji wengine ambao si viongozi wa dini.


5:WAUMINI WAKATOLIKI POTE DUNIANI NI RAIA WA VATIKANI
Hii si kweli kabisa. Wakatoliki wote siyo raia wa Vatican. Kama nilivyosema hapo juu uraia wa Vatikani hauji kwa ubatizo au kwa kuitwa Mkatoliki unakuja kwa mujibu wa mkataba wa Laterani wa 1929. Hii ina maana kwamba Vaticani licha ya kuwa ni taifa dogo zaidi vile vile ni taifa lenye raia wachache zaidi (hawazidi 1000). Na Vatican City haina mamlaka ya aina yoyote juu ya Mkatoliki kuhusu uraia wake. Papa ana mamlaka katika masuala ya imani na dini kama kiongozi wa dini lakini siyo kama mfalme wa wakatoliki wote duniani.

Ni muhimu kutambua kuwa kama mfalme Papa ni sovereign (hakimiya) hivyo haitaji Vatican City ili kuwa sovereign. Lakini uwepo wa Vatican City unasaidia tu katika kutekeleza majukumu yake ya kisiasa na kiutawala.

Nitawaacha wengine waendelee kuchangia suala la kujiunga na OIC kwani nilishatoa maoni yangu miaka mitatu iliyopita na kujirudia itakuwa ni kurudia rudia kitu kile kile. Mjadala mzuri sana.

No comment mkuu. Umesema yote.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu kuwa wewe Mkatoliki haina maana unajua sana utawala wa Vatican.. huu ni uongo mkubwa sana unaojaribu kuujenga. Imani ya dini na utawala mzima wa katoliki au Vatican hauwezi kutokana na imani ya mtuisipokuwa kusoma muundo wa utawala huo.. Mwenyewe umesema hivi:- Ni vizuri nitenganishe vitu ambavyo kwa mtu asiye Mkatoliki (na hata Wakatoliki wengine) hawavielewi. Kuna kitu tunakiita “Holy See” na kuna “Vatican City State”. Mambo mengi tunayoyaona yanafanywa na Papa au Kanisa Katoliki n.k yanafanywa na Holy See na siyo nchi ya Vatican.

Hapa tayari mwenyewe umeisha tenganisha nchi na mamlaka ya Papa..haihitaji mjadala kabisa ikiwa wewe mwenyewe tena umesema kwamba kutambuliwa kwa Vatican City kumetokana na mkataba baina ya Musolini na Waziri wa Mambo ya Nje wa Papa Cardinali Gaspari kwa niaba ya Papa Pius IX. Huyu waziri wa Mambo ya nje alikuwaje waziri hali Vatican City haijakubaliwa kuwa nchi?..Au mwenzetu una tafsiri tofauti ya waziri wa mambo ya nje! kama sii wewe kujibu maswali yako mwenyewe.

Mkuu wangu Vatican is Holy see na ilikuwa na utawala wake kabla hata Vatican City haijawa nchi...Vatican City kama nchi huru ni distinct from Holy see (utawala wa Papa) ndio inatambuliwa kimataifa kama nchi chini ya rais wake Cardinali Giovanni Lajolo.

3. Wewe tena umesema Vatican City ina raia 557 kufikia mwaka 2005 nadhani wamefika 900 kwa record nilionazo mimi..halafu ukajikanyaga mwenyewe kwa kusema miongoni mwao ni Papa (raia) na - "Waklegi 293 (mapadre, mashemasi) wanaofanya kazi katika balozi mbalimbali za Holy See pote duniani. Baadhi yao ndio kama yule Askofu Mkuu Novatus Rugambwa ambaye ameteuliwa mapema mwaka huu kuwa Balozi wa Papa huko Sao Tome na Principe. "

Mkuu hawa ni mabalozi wa Holy see (wakimwakilisha Papa) inakuwaje iwe hivyo badala ya hawa kuwa mabalozi kuwakilisha nchi ya Vatican City?. Hata uki google ukaandika Vatican inakupeleka Holy see..Ushahidi tosha kabisa au bado tuendelee kubishana tu.

Hayo maswali mengine yoote siyaoni yanalenga kitu gani zaidi ya kubishana ili mradi kwa sababu swala tunalochambua hapa ni Vatican as a state na Vatican as a Holy see kwani mkataba tulokuwa nao unawakilisha Holy see na sio Vatican City state..
 
Mjadala umeshakuwa wa dini tena? basi mod peleka kitu hii kwenye dini. Hatutaki kujadili mambo ya dini huku. Mwisho tupate ban bure.
 
Jimmy K,
Mkuu hapo juu tu ume comment kwa kusifia hoja za MJJ nimeandika mimi imekuwa udini vipi? au nimekushika kooni babu?...Kanywe maji tulizoa koo, haya ni majadiliano tu..I respect dini ya Katoliki na hata siku moja siwezi kuingia mjadala unaoleta Udini, ikiwa na maana kudharau dini na imani ya watu wengine..Yangu mwenyewe yananishinda iwe ya wengine!
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu kuwa wewe Mkatoliki haina maana unajua sana utawala wa Vatican..

Hii ni kweli, ni sawasawa kabisa na mtu ambaye ni Muislamu kujiona ana mamlaka ya kuzungumzia uislamu kana kwamba kwa kuwa muislamu tu kunamfanya awe mjuzi wa Uislamu na mambo yanayohusu Uislamu. Sidai kuwa kwa sababu mimi ni Mkatoliki basi naujua Ukatoliki.


huu ni uongo mkubwa sana unaojaribu kuujenga.
Uongo siyo wa kwangu mimi ila wa wale wanaoamini kuwa Vatican siyo nchi! wakati ushahidi wote tumeweka kuwa Vaticani ni nchi.



Hapa tayari mwenyewe umeisha tenganisha nchi na mamlaka ya Papa..haihitaji mjadala kabisa ikiwa wewe mwenyewe tena umesema kwamba kutambuliwa kwa Vatican City kumetokana na mkataba baina ya Musolini na Waziri wa Mambo ya Nje wa Papa Cardinali Gaspari kwa niaba ya Papa Pius IX. Huyu waziri wa Mambo ya nje alikuwaje waziri hali Vatican City haijakubaliwa kuwa nchi?
Bado naona umemiss historia niliyokuwekeeni hapo, Vatican City ilikuwa tayari ni nchi kabla ya mkabana na Musolini ikiwa sehemju ya milki za kipapa (Papal States) ambazo alikuwa nazo kwa miaka zaidi ya 1000! Vita ya Kuiunganisha Italia ndio ilisababisha baadaye mkataba wa kutambua nafasi ya Vaticani na Papa kwani Mfalme Vincent na wenzake walichukua maeneo yaliyokuwa ya Kipapa na kumfanya awe mfungwa Vaticani. Makubaliano ya 1929 yalihakikisha tu uhuru wa Papa na Vatican na kutengeneza uhusiano wake wa kisheria na Ufalme mpya wa Italia ambayo baadaye yalibadilishwa kidogo Italia ilipoamua kuwa Jamhuri.

..Au mwenzetu una tafsiri tofauti ya waziri wa mambo ya nje! kama sii wewe kujibu maswali yako mwenyewe.
Nimesema toka awali kuwa Upapa kama sovereign umekuwa na huduma ya kibalozi ya zamani zaidi duniani tangu 325.


Mkuu wangu Vatican is Holy see na ilikuwa na utawala wake kabla hata Vatican City haijawa nchi...Vatican City kama nchi huru ni distinct from Holy see (utawala wa Papa) ndio inatambuliwa kimataifa kama nchi chini ya rais wake Cardinali Giovanni Lajolo.
Angalau umeanza kupata mwanga kidogo. Kwamba kuna nchi inaitwa Vatican City. Lakini umepotea kidogo kufikiria Rais wa Vatican City ni Giovanni Lajolo. Kardinali Lajolo ni Rais wa Kamisheni ya Utawala wa Vatican City. Huteuliwa na Papa pamoja na makardinali wengine kwa kipindi cha miaka 5. Madaraka yao yanatoka kwa Papa ambaye ndiye mtawala wa kifalme wa Vatican City State. Vatican City State haiko nje ya Upapa.

Unaweza kutembelea hapa kuweza kuelewa zaidi juu ya kazi na muundo wa Vatican City sehemu yake inasema hivi:

State Departments

SegreteriadiStato1.jpg
Vatican City State is governed as an absolute monarchy. The Head of State is the Pope who holds full legislative, executive and judicial powers.
During a sede vacante (between the death of a Pope and the election of his successor), these powers are exercised by the College of Cardinals.
The Pope is elected by the Cardinals who are under eighty years of age. He becomes Sovereign of Vatican City State the moment he accepts his election as Pope.
3. Wewe tena umesema Vatican City ina raia 557 kufikia mwaka 2005 nadhani wamefika 900 kwa record nilionazo mimi..halafu ukajikanyaga mwenyewe kwa kusema miongoni mwao ni Papa (raia) na - "Waklegi 293 (mapadre, mashemasi) wanaofanya kazi katika balozi mbalimbali za Holy See pote duniani. Baadhi yao ndio kama yule Askofu Mkuu Novatus Rugambwa ambaye ameteuliwa mapema mwaka huu kuwa Balozi wa Papa huko Sao Tome na Principe. "
Nilisema vile vile kuwa hawazidi 1000 kwa sasa!

Mkuu hawa ni mabalozi wa Holy see (wakimwakilisha Papa) inakuwaje iwe hivyo badala ya hawa kuwa mabalozi kuwakilisha nchi ya Vatican City?. Hata uki google ukaandika Vatican inakupeleka Holy see..Ushahidi tosha kabisa au bado tuendelee kubishana tu.
Ni lazima ujifunze kwanza uhusiano kati ya Holy See na Vatican City. Japo ni vitu viwili tofauti lakini vinahusiana. Kwenye hiyo link uliyoitoa na mimi kuirudia angalia suala la Origins and HIstory ya Vatican City.

Hayo maswali mengine yoote siyaoni yanalenga kitu gani zaidi ya kubishana ili mradi kwa sababu swala tunalochambua hapa ni Vatican as a state na Vatican as a Holy see kwani mkataba tulokuwa nao unawakilisha Holy see na sio Vatican City state..
Ni wewe ulisema tuna mkataba na taasisi ya Vatican! Nikasema hatuna jambo ambalo hatimaye umelikubali
Ni wewe ulisema kuwa VAtican siyo nchi ni taasisi na mimi nikakuonesha kuwa ni nchi jambo ambalo umekubali
Ni wewe ulisema kuwa hakuna raia wa Vatican na mimi nikakuonesha na wewe umekubali
Ni wewe uliyesema kuwa mtu yeyote anaweza kuwa raia na mimi nikaonesha hapana na wewe umekubali

Sasa nafurahi kuwa angalau tumekubaliana tunaweza kuendelea.
 
Mzee Mwanakijiji,
Acha kujikanyaga kanyaga mkuu wangu., Kuna nchi ambayo haikuwepo kabla?... Hata Tanganyika ilikuwepo kabla hatujapata Uhuru na Hata Ukerewe ipo zamani tukija pata uhuru wetu ndipo tunaanza kuhesabu Ukerewe kama nchi..Sikuelewi unazungumzia kitu gani kwani ubishi wote wa madai ya Vatican kuwa nchi yanaanzia siku ilipotambulika na kukubalika kama nchi..na ndicho tunachochambua hapa.

Pengine mpe mtu mwingine ayasome maandishi yangu hapo juu na akutafsirie upate kuelewa tofauti niloizungumzia ya kwamba Vatican sio nchi. Nchi ni Vatican City na links zao nimekuwekea, zisome na upate kuelewa nachozungumza. Hakuna mahala nimekubali ulosema wewe, na hakuna mahala nimeandika ya kwamba vitu hivi havihusiani! isipokuwa swala ni nani tumeingia naye mkataba..Kisha hakuna Mtanzania anayetumia neno Holy see katika mazungumzo ya ku address Vatican.

Vatican represent Holy see na hata huyo Rugambwa anawakilisha Holy see kama balozi wa Papa..Maadam unakubali kuna tofauti baina ya nchi na Taasisi, pamoja na kwamba ni zinaunda utawala mzima bado ni tofauti na ktk utofauti huo ndipo tunapogoingana nikisema ni uwakilishi wa Taasisi ndiyo tumeingia nayo mkataba...Sasa huu ubishi unakwenda wapi?..

Mkuu wangu, kama kuna mkataba baina ya CCM na mtu yeyote kitaifa mathlan jengo la Vijana. Mtu yeyote anaweza kusema ni serikali ya Tanzania imeingia mkataba wa huyo mdosi..Tunaweza tumia jina la utawala wa CCM kuzungumza mkataba wa nchi kutokana na wao watawala lakini ipo tofauti kubwa sana..
 
Back
Top Bottom