Sura ya dada iliyomfufua mtu kutoka kwenye kifo

Manyanza

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
9,520
14,383
IMG-20240301-WA0039.jpg

Dunia ina maajabu na hayajawahi kuisha maajabu hayo...kila unaposikia moja la kuajabisha jua kuna mambo elfu moja ya kuajabisha zaidi ya hilo lakini hujalijua..

Essie Dunbar.. mwanamke aliyekuwa na miaka 30 mwaka 1915 alikuwa anaugua ugonjwa kifafa (epilepsy attack).

Siku moja akadondoka ikawa hapumui ...familia ikawa haijui lakufanya......ikabidi ikamtafuta daktar aliyeitwa Dr. D.K. Briggs kutoka Blackville

Dr. D.K. Briggs alivyompima yule mgonjwa hakupata alama yoyote ya kuashiria kuwa mtu huyo alikuwa hai ...Essie Dunbar hakuwa anapumua na mapigo ya moyo yalikuwa yamesimama ...Dr. D.K. Briggs akaiambia familia kuwa mgonjwa amefariki

Baada ya kupata taarifa hiyo familia ikaamua kuanza mipango ya mazishi na mipango ya mazishi ikaenda haraka haraka.

Dada wa marehem alikuwa yupo nje ya mji ila kwa mujibu wa ratiba angewahi kutoa heshima kwa mdogo wake

Siku ya mazishi ikafika viongozi wa dini wakaongoza sala na taratibu zote zikawa zimekamilika lakini hadi muda huo dada wa marehemu alikuwa bado hajafika basi ikabidi azikwe

Muda mchache baada ya maziko dada wa marehem akawa amewasili, licha ya kuwa amechelewa na mdogo wake alikuwa ameshazikwa akaomba mwili ufukuliwe ili atoe heshima yake ya mwisho kwa mdogo wake

Hebu jiulize kwenye jamii yenu hilo lingewezekana?

Basi viongozi wa dini wakakubali ombi la dada mtu mwili ukafukuliwa na sanduku likafunguliwa kwa ajili ya dada mtu angalau atoe heshima zake za mwisho

La! Haula hakuna aliyeamini pale sanduku la mwili lilipofunguliwa na kukuta marehem ametoa smile kwa dada ake na kila mtu aliyekuwepo pale

Huwezi kuamini watu wengi waliokuwa pale walikimbia wakiamini kuwa Essie Dunbar alikuwa ni mzimu uliofufuka kutoka kuzimu

Hata viongozi wa watu dini nao walipata mawenge watatu wakadumbukia ndani ya kaburi ...na wawili walikanyagwa na watu

Lakin Essie Dunbar alikuwa hai tena ...na baada ya pale aliishi tena kwa miaka 47 mbele alikuja kufariki mwaka 1962 akiwa na miaka 77.........@bwana fact

Elewa hivi sio kila lenye kuwahi linakuwa sawa na sio kila lenye kuchelewa linakuwa baya ndio maana hadi leo waswahili bado wamechanganyikiwa juu ya kuwahi na kuchelewa...waliosema haraka haraka haina baraka ...ndio hao hao waliosema ngoja ngoja yaumiza matumbo
 

Dunia ina maajabu na hayajawahi kuisha maajabu hayo...kila unaposikia moja la kuajabisha jua kuna mambo elfu moja ya kuajabisha zaidi ya hilo lakini hujalijua..

Essie Dunbar.. mwanamke aliyekuwa na miaka 30 mwaka 1915 alikuwa anaugua ugonjwa kifafa (epilepsy attack).

Siku moja akadondoka ikawa hapumui ...familia ikawa haijui lakufanya......ikabidi ikamtafuta daktar aliyeitwa Dr. D.K. Briggs kutoka Blackville

Dr. D.K. Briggs alivyompima yule mgonjwa hakupata alama yoyote ya kuashiria kuwa mtu huyo alikuwa hai ...Essie Dunbar hakuwa anapumua na mapigo ya moyo yalikuwa yamesimama ...Dr. D.K. Briggs akaiambia familia kuwa mgonjwa amefariki

Baada ya kupata taarifa hiyo familia ikaamua kuanza mipango ya mazishi na mipango ya mazishi ikaenda haraka haraka.

Dada wa marehem alikuwa yupo nje ya mji ila kwa mujibu wa ratiba angewahi kutoa heshima kwa mdogo wake

Siku ya mazishi ikafika viongozi wa dini wakaongoza sala na taratibu zote zikawa zimekamilika lakini hadi muda huo dada wa marehemu alikuwa bado hajafika basi ikabidi azikwe

Muda mchache baada ya maziko dada wa marehem akawa amewasili, licha ya kuwa amechelewa na mdogo wake alikuwa ameshazikwa akaomba mwili ufukuliwe ili atoe heshima yake ya mwisho kwa mdogo wake

Hebu jiulize kwenye jamii yenu hilo lingewezekana?

Basi viongozi wa dini wakakubali ombi la dada mtu mwili ukafukuliwa na sanduku likafunguliwa kwa ajili ya dada mtu angalau atoe heshima zake za mwisho

La! Haula hakuna aliyeamini pale sanduku la mwili lilipofunguliwa na kukuta marehem ametoa smile kwa dada ake na kila mtu aliyekuwepo pale

Huwezi kuamini watu wengi waliokuwa pale walikimbia wakiamini kuwa Essie Dunbar alikuwa ni mzimu uliofufuka kutoka kuzimu

Hata viongozi wa watu dini nao walipata mawenge watatu wakadumbukia ndani ya kaburi ...na wawili walikanyagwa na watu

Lakin Essie Dunbar alikuwa hai tena ...na baada ya pale aliishi tena kwa miaka 47 mbele alikuja kufariki mwaka 1962 akiwa na miaka 77.........@bwana fact

Elewa hivi sio kila lenye kuwahi linakuwa sawa na sio kila lenye kuchelewa linakuwa baya ndio maana hadi leo waswahili bado wamechanganyikiwa juu ya kuwahi na kuchelewa...waliosema haraka haraka haina baraka ...ndio hao hao waliosema ngoja ngoja yaumiza matumbo
Kifo ni Siri kubwa, madaktari wenyewe hawajui kipimo halisi Cha kifo ni kipi!!
 
Kwny movie ya THE NUN huko Romania marehemu alikuwa anazikwa na kamba ya kengele,kengele inakuwa chini ya msalaba juu ya kaburi,incase mzikwaji km alikuwa hajafa anavuta kamba ,kengele inalia kwa nje ,anakuja kufukuliwa,ndo Priest wa kwny hiyo movie alivosema kwny Abbey ya st carter
 
Kwny movie ya THE NUN huko Romania marehemu alikuwa anazikwa na kamba ya kengele,kengele inakuwa chini ya msalaba juu ya kaburi,incase mzikwaji km alikuwa hajafa anavuta kamba ,kengele inalia kwa nje ,anakuja kufukuliwa,ndo Priest wa kwny hiyo movie alivosema kwny Abbey ya st carter
Pata picha hapa Wild man from the Hills
 
Back
Top Bottom