mirindimo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2009
- 821
- 1,343
Kutoka kwenye mtandao wa X, Akaunti ya Lisa Ildephonce (@LIldephoce)
“Tarehe 23/1/2023 Tulipata msiba wa dada angu alifariki katika mazingira ya kutatanisha aliolewa na kijana anaitwa Josephat Aron ambaye ni Police pale Ufundi (Kilwa Road) cheo Kopro
Kifo chake kilitupa mashaka kutokana na mgogoro wa ndoa waliokuwa nao na sababu hiyo hatujui mpaka leo hii dada yetu amekufa na tatizo gani kwani baada ya kufariki kijana huyo alitunyima kupima mwili pamoja na taarifa za hosptal juu ya kilichomuua dada yetu
Imefika hatua familia ya marehemu wanatishiwa na hawana amani
Siku ya kumuaga marehemu mdogo wa kike wa marehemu alinyimwa kwenda kumstiri dada yake badala yake alienda mume na kaka ake kumstiri dada yetu ndugu tulichukizwa na iko kitendo cha shemeji mtu kwenda kumstiri marehemu tukaingilia kati hilo mwisho wa siku wakamruhusu mdogo mtu kuingia lakini haikusaidia kwani mume na shemeji wa marehemu walikuwa wameshatangulia
Baada ya kuruhusiwa mdogo wa marehemu na mama zake wadogo wawili walinyimwa gloves kwaajili ya kumvalisha marehemu na walikuta dada yetu amezuriwa maeneo mengi
Ndugu wa mwanamke waliokuwa hospitalini walikatazwa kumuona mgonjwa aliyekuwa anaingia ni Josephat na ndugu yake anaitwa Mwinyi walimuamisha mochwari kutoka hospital alipofia (Hindu Mandal)na kumpeleka mochwari ya kazini kwao anapofanyia kazi ndugu wasiweze kupima mwili
Hii ni siku ya msiba [Video] baada ya ndugu wa mwanamke kutaka mwili ukafanyiwe vipimo ili kujua ndugu yetu kwa nini amepatwa na kifo ila tukaletewa mapolisi waliokuja na mwili wakashika na mabunduki kutaka kuyafwatua baada ya wananchi waliokuja msibani kuwaambia tuuweni tu kama hamtaki tumpime ndugu yetu. Kijana huyo Josephat Aron akaamuru Polisi waingie ndani ya gari. Tulimzika ndugu yetu chini ya ulinzi wa mapolisi waliotoka Dar es Salaam kuja Rombo na mwili tukiwa na majonzi”
“Tarehe 23/1/2023 Tulipata msiba wa dada angu alifariki katika mazingira ya kutatanisha aliolewa na kijana anaitwa Josephat Aron ambaye ni Police pale Ufundi (Kilwa Road) cheo Kopro
Kifo chake kilitupa mashaka kutokana na mgogoro wa ndoa waliokuwa nao na sababu hiyo hatujui mpaka leo hii dada yetu amekufa na tatizo gani kwani baada ya kufariki kijana huyo alitunyima kupima mwili pamoja na taarifa za hosptal juu ya kilichomuua dada yetu
Imefika hatua familia ya marehemu wanatishiwa na hawana amani
Siku ya kumuaga marehemu mdogo wa kike wa marehemu alinyimwa kwenda kumstiri dada yake badala yake alienda mume na kaka ake kumstiri dada yetu ndugu tulichukizwa na iko kitendo cha shemeji mtu kwenda kumstiri marehemu tukaingilia kati hilo mwisho wa siku wakamruhusu mdogo mtu kuingia lakini haikusaidia kwani mume na shemeji wa marehemu walikuwa wameshatangulia
Baada ya kuruhusiwa mdogo wa marehemu na mama zake wadogo wawili walinyimwa gloves kwaajili ya kumvalisha marehemu na walikuta dada yetu amezuriwa maeneo mengi
Ndugu wa mwanamke waliokuwa hospitalini walikatazwa kumuona mgonjwa aliyekuwa anaingia ni Josephat na ndugu yake anaitwa Mwinyi walimuamisha mochwari kutoka hospital alipofia (Hindu Mandal)na kumpeleka mochwari ya kazini kwao anapofanyia kazi ndugu wasiweze kupima mwili
Hii ni siku ya msiba [Video] baada ya ndugu wa mwanamke kutaka mwili ukafanyiwe vipimo ili kujua ndugu yetu kwa nini amepatwa na kifo ila tukaletewa mapolisi waliokuja na mwili wakashika na mabunduki kutaka kuyafwatua baada ya wananchi waliokuja msibani kuwaambia tuuweni tu kama hamtaki tumpime ndugu yetu. Kijana huyo Josephat Aron akaamuru Polisi waingie ndani ya gari. Tulimzika ndugu yetu chini ya ulinzi wa mapolisi waliotoka Dar es Salaam kuja Rombo na mwili tukiwa na majonzi”