Elections 2010 Sumaye agoma kumchafua Dk Slaa

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Sumaye agoma kumchafua Slaa

Na Ezekiel Kamwaga

Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye ameingia katika kampeni za mgombea urais wa chama chake kwa sharti la kutomchafua Dr Willbrod Slaa.

Taarifa zilizofikia gazeti hili kutoka Moshi zinamnukuu Sumaye akisema, hatamchafua mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa vile kufanya hivyo kutamvunjia hadhi.

Sumaye ameingia kwenye kampeni kufuatia mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete, kuwaomba msaada viongozi wastaafu wanaodaiwa “kukacha” kampeni zake.

“Naweza kukuthibitishia pasipo shaka kwamba, Kikwete amewaangukia baadhi ya wazee wetu kumsaidia katika mikoa ambako CCM ina “hali mbaya,” ameeleza mtoa taarifa.

Chanzo hicho cha habari kimesema awali ilionekana Kikwete angeweza kushinda bila msaada wa wastaafu, lakini sasa ameona upepo umegeuka.

Taarifa zinasema Kikwete alimwomba Sumaye kumsaidia hasa katika mikoa ya kanda ya Kaskazini ambako imeelezwa kuna upinzani mkubwa.

“Awali, Sumaye alisita kukubali ombi hilo la rais, lakini baadayeakakubali kwa kutoa masharti ya mahala hasa anapoweza kwenda,” kimeeleza chanzo chetu cha habari.

Hata hivyo, alimwambia kikwete kwamba atakwenda tu katika maeneo ambayo anadhani anaweza kuroa msaada mzuri,” kimeeleza chanzo hicho.

Ofisa mmoja wa ofisi ndogo ya makao makuu, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam ameliambia gazeti hili kuwa awali Sumaye alielekezwa kwenda majimbo ya Moshi Mjini, Hai, Rombo, Moshi Vijijini na Vunjo.

MwanaHALISI lina taarifa kuwa Sumaye amekataa kufanya kampeni katika majimbo hayo, kwa maelezo kwamba anaamini wagombea ubunge wa Chadema huko “hawana matatizo.”

Haikufafanuliwa iwapo kwa “hawana matatizo” Sumaye alikuwa na maana ya kusema hawashikiki au wana uwezo wa kuwakilisha majimbo yao…………..

……..Kuna taarifa kwama ilibidi Sumaye awasiliane na Kikwete moja kwa moja kumweleza uamuzi wake huo. Imeripotiwa kuwa Kikwete amekubalkiana naye.

Taarifa zilizopatikana juzi Jumatatau zimesema Sumaye amekubali kufanya kampeni katika majimbo ya Vunjo na Hanang.

Aidha, imefahamika kuwa Sumaye amekubali kuingia katika kampeni kwa sharti la kutoshiriki katika kumkashifu mgombea wa urais wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, jambo ambalo amenukuliwa akisema linaweza kumuondolea hadhi.

Taarifa zaidi zinasema Sumaye amegoma kumfanyia kampeni mgombea ubunge wa jimbo la Rombo kupitia CCM, Basil Mramba, kwa vile ana wasiwasi ataonekana ni mtetetezi wa watuhumiwa wa ufisadi na anaweza kuanza kuandamwa baadaye…….

Habari zaidi katika MwanaHALISI ya leo.
 
Si Makamba alishasema kuwa JK anapendwa zaidi ya CCM, sasa msaada wa nini tena???
 
Nimejaribu sana kutafuta na kupata tuhuma za ufisadi za huyu Bwana, lakini sijafanikiwa. Hakuguswa na kashfa ya EPA, Meremeta, Twin Toweres, Deep Green etc -- inakuwaje? Inaonekana ni msafi ama sivyo saa hizi angekuwa anaogelea katika dimbwi la tuhuma.

Hata mwaka 2005 alipojaribu kugombea urais, sikusikia kashfa yoyote ya ufisadi dhidi yake.

Naamini ni kiongozi safi, na ndiyo maana hataki kumkashifu mtu msafi (Slaa) na kumtetea mtu mchafu (Mramba).
 
Muda wa kuomba msaada na kusaidiana umekwisha tusubiri tuone ni nini watanzania wataamua
 
Sumaye hakutakiwa kuomba msaada, hadi Kikwete na wanamtandao woote wamwombe radhi kwa kumchafua.......
 
Wanapoteza muda tu. Sumaye anaushawishi gani? Mkapa akitokea tu watu watapiga yowe. Ruksa ndo amekwisha kwani kila kitu kwake ni mzaa. Wangekuwa ni wanachama wa ccm ndo wanaoamua hatima ya tanzania ingewezekana kubadili upepo lakini hadi sasa decide group iko kwa slaa. nani hamtambui slaa, hata ccm wenyewe naimani slaa anaweza kuondoka na 30% ya vote zao.

TUMESEMWA SANA TUMETUKANA SANA NA MANENO YA TAARABU TOKA KWA JK SAA YAKE YA KUBWABWAJA IMEFIKIA UKINGO. kwani wako wapi akini ridhiwani na wengine alowaamini zaidi?
 
Nimejaribu sana kutafuta na kupata tuhuma za ufisadi za huyu Bwana, lakini sijafanikiwa. Hakuguswa na kashfa ya EPA, Meremeta, Twin Toweres, Deep Green etc -- inakuwaje? Inaonekana ni msafi ama sivyo saa hizi angekuwa anaogelea katika dimbwi la tuhuma.

Hata mwaka 2005 alipojaribu kugombea urais, sikusikia kashfa yoyote ya ufisadi dhidi yake.

Naamini ni kiongozi safi, na ndiyo maana hataki kumkashifu mtu msafi (Slaa) na kumtetea mtu mchafu (Mramba).
hukusikia wakati JK alitumia magazeti kama kawida yake kumchafua yeye pamoja na Dk Salim, hata hivyo tuhuma haziwa nzito kwani alikuja akatoa tamko kwamba atakae andika tuhuma za uongo zidi yake na kushindwa kuzibitisha atampeleka mahakamani na kumdai fidia ya Bil 1, tangu hapo sikusikia tena magazeti ya JK kuandika tuhuma hizo na inasemekana alikuwa na kinyongo sana na serikali ya JK lakini kwakuwa siasa sazingine ni unafiki siajabu kweli kuanza kumkampenia JK.....Alikuwa akidaiwa anaakaunti nje ya nchi yenye pesa zaidi ya bil 3.....ngoja watu wenye data zake watakuja kuzimwanga
 
Safi sana!Unaona elimu inavyoweza kumbadisha mtu!jamaa sasa yuko juu,anajua madhara ya siasa za maji taka,kwa sasa ni mtu makini kupita maelezo!
 
Taarifa zilizopatikana juzi Jumatatau zimesema Sumaye amekubali kufanya kampeni katika majimbo ya Vunjo na Hanang.

Huko Vunjo ni kwa mashemeji au kuna nini? Tunajua Hanang ni nyumbani ambako Dr. Slaa atalamba kura zote na hata Sumaye anawajua wa-Irak wenzie jinsi walivyo na msimamo.
 
Na ya kwake yaja. Kila mtu ataumbuka kwa kombola lake, hakuna kujichagulia. Kama Sumaye anategemea kombola lake kuwa kwenye mashamba, asubiri akishaanza kampeni ndo watampa vitu vyake.
 
mbona nilikwisha sikia alilazimishwa akopeshwe pesa toka PPF ili hali yy si mwanachama na akakopeshwa milion 500! kwani km ni kweli si kashfa hiyo!?
 
Juzi juzi nilisikia watu wakisema Sumaye aliwashauri wazee wa Hanang kuwa mwaka huu hakuna kukosea tena, akiwaambia wamchague Dr Slaa. Alifanya hivyo kwa siri.
 
Back
Top Bottom