MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,604
Watanzania tuko zaidi ya Milioni 42. Ni vyema zaidi kukawapo na wigo mpana zaidi wa kuwafikia Watanzania wengi kadiri inavyowezekana hii habari ya "ghafla" na "dharura" sijui inatokea wapi.
Sitegemei wabunge wa CCM walio wengi kuukwamisha Muswaada huo. Na ikitokea wakafanya hivyo, kwa maana ya Wabunge hao wa CCM wakaukwamisha Muswaada huo wa sheria, basi, Wabunge hao wa CCM watakuwa wameanza kazi ya ' Chama kujivua magamba' na baadhi yao kunusurika na adhabu ya wapiga kura ifikapo 2015.
Hapa adhabu ya wapiga kura haitoshi. Huwezi kumtreat mtu anayekukosea heshima kwa kumheshimu. CCM wametukosea heshima na 2015 iko mbali sana kusubiri kuwaadhibu. WaTZ wanachemka kwa maghadhabu na madudu ya CCM.
Salama yao ni kufanya ukusanyaji wa maoni nchi nzima, kila kaya, kata, wilaya, mkoa. Katiba ni mali ya WaTZ na sio ya JK na mamluki wake.