Social Networking/Mitandao ya ki-Jamii...

Anyways kwa sababu inajulikana wewe ni Rais wa wabeba boksi, sio mbaya kutoifahamu kivile...ipo karibu na chuo cha ustawi wa jamii...kijiwe maaruf cha totoz wa ustawi pale...

sasa turudi kwen topic ya Mbu bana....

Mi kitu kimoja kimenishangaza kidogo, ni kwa nini Mbu ameamua kuweka katika upande hasi (negative) peke yake...bila kuangalia pia upande positive? Inaweza kuwa uamuzi sahihi kabisa wa kwake, lakini nadhani ingekuwa more balanced kama angeuliza pia mchango wa hizi social networks katika:
  • "kustabilise" relationships
  • Kuestablish new relationships, watu kibao wameo na kuolewa. sembuse Bf/GF
  • Kupunguza 'real time' cheating, lol (hapo inategemea definition ya cheating...a 'new' topic altogether)
Mengineyo tunaweza kuongeza...kwa hiyo si kweli moja kwa moja kuwa "na hii haikuanzia kwa Facebook pekee, Friends Reunited, myspace, WAYN, Hi5, Twitter na hata Google + mitandao yote hii kwa namna moja au nyingine imegeuka hatarishi kwa usalama wa mahusiano, mapenzi urafiki na ndoa!"

Huo ni mtizamo wangu. tuendeleee

...la la la,....:)

...binafsi Facebook na hii mitandao ya kijamii imeniwezesha kunikutanisha tena na watu weeengi niliokuwa nimesoma nao, nimeishi nao na hata wale ex-gelo frendz niliojirusha nao miaka hiyooooo....

...kimbembe ni jinsi gani ya ku handle hizo rekindled flames bana japo tayari wengi wetu tushakuwa na minyama uzembe, lakini si unajua tena....mnaanza na "..hivi nimekumisije?" au "...hivi kwanini ulinichunia!?"...kisha mnaendelea "...bado nakumbukia maujuzi yako, bado upo vile vile....?! " ----kufumba na kufumbua mshabadilishana namba za simu na na ahadi za kupeana 'what you've been missing all those years!"

Balaaa!
 
Hizo options zinamisi 2 important ones, 'unstable' na 'unpredictable'
Hii mitandao hai-respond to clientele needs kabisa! Afadhali maxence hajaweka hii option ya marital status humu jf, kila mtu angekuwa single tena yenye bold,lol

...dahhh, umegusa patamu sana;

umegusia kama vile watu hawaelewi lengo, nia na madhumuni ya kujiunga kwenye hii mitandao ya kijamii ni tofauti na jinsi wanavyotumia uhuru wao wa maoni na uchangiaji, ndivyo sivyo?
...

Katika posts zako za juu, zinahitimishwa na hapo nyekundu. Ubaya wa teknolojia unakuja pale tunapozitumia vibaya. Imani yangu mimi ni kuwa hata hii mitandao ya kijamii tukitumia vizuri inakuwa na faida zake. Mfano, kwa kutumia mitandao hii hii, tumeweza kuwasiliana upya na marafiki zetu tulliopoteana miaka mingi iliyopita, wangapi wamepata ajira mitandao na kufanyakazi na watu wasiowajua (mmoja Tanzania mwengine Thailand) na ni waaminifu.

Kuhusu suala lako, ninakubaliana na wewe kuwa huyo mamsap alikuwa na lake alilokuwa anaficha hadi asitake kuku"add", lakini na wewe umefanya hilohilo ambalo yeye alikuwa anafanya - kudanganya -, ingwaje hapa tutasema kudanganya kwako kulikuwa "kwa nia nzuri".

Tukija kwenye suala la mitandao kuvunja mahusiano, ukiwachia kesi kama yako na nyengine za aina hiyo, ambapo ulikusudia kukamata mwizi wako, kuna mahusiano mengine huvunjika kwa sababu tu ya watu kutafsiri kila kinachoandikwa na wapenzi wao. Mfano aliotoa Lizzy wa kuandika "ninaumwa" unatosha. Mfano mwengine unaandika "Im bored" anakuja mtu anakwambia "Njoo kwangu nikuchangamshe", halafu comment hiyo aione mpenzi wako na aanze sokomoko, wewe kosa lako lipi? Tatizo letu ni kuwa tunaingia kichwa kichwa kila pahali kwa kutaka sifa tu. Utakutia mtu ana marafiki 4,000, What for? Pengine kati ya hao anaowajua 100 hawafiki na marafiki wa kweli hawazidi hawazidi 3.

....biashara matangazo, wewe huoni wengine wanavyopiga picha za mapozi ya mvuto wa kufa mtu japo ni mke/mume wa mtu?


hapo juu naona hujanielewa. What I mean ni kwamba mtu anajua kua ni makosa ila anaona ni kakosa kadogo. A private indulgence, like eating candies when you are overweighted. Huwezi kusema basi nile candies, ninenepe, alafu nikiridhika niache kabisa ndio nianze diet. Utamu wa hizo candies ni that mixed feeling unapo zila. Na huku unajua sio kosa kubwa sana kama kula junk food. do you get the reasoning now?
About my man and I it has not always been like that. Mwanzo I was resisting because I wanted to keep certain things to me, just to affirm a different personality. but mwishowe we had an agreement. Na siwezi kusema uongo, imetokea nifute a message fearing that if he sees it inaweza kuleta shida. but this is not because I enjoyed receiving the message, or because i feel guilty of anything, it is because I fear that he will not understand that I did not ask for the message. this is also wrong, i now, but imenitokea. I tell him that it happens sometimes, but simwambii ilitokea na nani na simwambii ilitokea lini.

...huu mfano kama kale katabia ka kudokoa nyama jikoni umenifurahisha sana.
 
Kulinda mahusiano yangu kuna mitandao nilishaachana nayo kabisa nisije nikaingia majaribuni. Lol.
Mbu, hii thread imenifanya nimfikirie mara mbili mbili rafiki yangu, ana mpenzi wake(ambae anamuita mume mtarajiwa) kila kukicha ana kazi ya kuweka picha mpya facebook tena nyingi akiwa kifua wazi. Wadada nao wanacomment kumwambia ana kifua kizuri. Rafiki yangu hapendi na kashamwambia jamaa ila hasikii.
Mdada naona anakufa na tai shingoni.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Duh, umeongea kwa hisia.
Hadi umenitisha hata kuwa hapa jf
ukiachia mbali fb ambapo napaogopa siku zote
sijui nilog off for good?!!

Mbona mi naona nimeongea kawaida tu!

Mimi naona niliyoyaongea ni mambo halisi yanayotokea katika dunia ya leo. Au wewe unaona ni mambo ya kufikirika zaidi?
 
Kulinda mahusiano yangu kuna mitandao nilishaachana nayo kabisa nisije nikaingia majaribuni. Lol.
Mbu, hii thread imenifanya nimfikirie mara mbili mbili rafiki yangu, ana mpenzi wake(ambae anamuita mume mtarajiwa) kila kukicha ana kazi ya kuweka picha mpya facebook tena nyingi akiwa kifua wazi. Wadada nao wanacomment kumwambia ana kifua kizuri. Rafiki yangu hapendi na kashamwambia jamaa ila hasikii.
Mdada naona anakufa na tai shingoni.

...hahaha...ndipo tulipo na huko tunakoelekea sijui kutazuka balaa gani yarabi,
heri yao kina mzee DC miaka yao kulikuwa na Autograph tu za kusaini kisha unamrudishia

mwenyewe...
 

DivorceBook3.jpg
 
watu wana-subscribe kwenye hii mitandao ya kijamii kwa malengo tofauti: kupashana habari, kujenga urafiki, kuinter-act na professionals wenzetu, kufuatilia watu na matukio etc; unfortunately, mitandao yenyewe iko so much open-ended kiasi kwamba huna au una control kidogo sana kuhusu yale unayo-upload; pia watu tuna-tend kujisahau sana na kujiachia as if nobody else is watching - nadhani ni muhimu kujiwekea mipaka on how far we can go with the flow hasa kwenye mambo ya mapenzi, flirting etc kabla wengi wetu hatujaumbuka
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Facebook noma kule,unaweza ukafa na presha tena kama couples,ndo mambo ya kulazimishana 2andike married to...au in a relationship with...,2pige picha kila mtu ajue wewe wangu.Kifupi facebuk ina disadvantages nyingi sana.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Facebook noma kule,unaweza ukafa na presha tena kama couples,ndo mambo ya kulazimishana 2andike married to...au in a relationship with...,2pige picha kila mtu ajue wewe wangu.Kifupi facebuk ina disadvantages nyingi sana.

...hahahaha, wengine wanataka kumjua mwenza wajue jinsi ya kujipanga likilipuka.

Tukiangalia upande wa faida twaweza jikuta unausoma na kuujua udhaifu wa mwenzako pitia facebook...
picha anazoweka, comments zake kutokana na moods, marafiki zake wapya na wazamani,....nk
 

...hahahaha, wengine wanataka kumjua mwenza wajue jinsi ya kujipanga likilipuka.

Tukiangalia upande wa faida twaweza jikuta unausoma na kuujua udhaifu wa mwenzako pitia facebook...
picha anazoweka, comments zake kutokana na moods, marafiki zake wapya na wazamani,....nk

Labda inabidi watu wawekeane sheri kabisa kuhusiana na hii mitandao.
1. Hamna kuweka picha zinazoreaveal sana.
2. Hamna kuupdate ulimwengu kuhusu mahusiano yalipo/yanapoelekea (leo complicated, kesho vile, status za leo "he/she is the best, kesho kaniboa".
3. Hamna kuadd Xs (kama mmoja anaona italeta matatizo).
4. Hamna kiandika status zinahusiana na mambo ya ndani (sex, financia issues, mipango n.k)
5. Kila mmoja anakua rafiki wa mwenzie.
6. . . . . . . . .
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Labda inabidi watu wawekeane sheri kabisa kuhusiana na hii mitandao.
1. Hamna kuweka picha zinazoreaveal sana.
2. Hamna kuupdate ulimwengu kuhusu mahusiano yalipo/yanapoelekea (leo complicated, kesho vile, status za leo "he/she is the best, kesho kaniboa".
3. Hamna kuadd Xs (kama mmoja anaona italeta matatizo).
4. Hamna kiandika status zinahusiana na mambo ya ndani (sex, financia issues, mipango n.k)
5. Kila mmoja anakua rafiki wa mwenzie.
6. . . . . . . . .

aaaaarrrggghh? Lizzy masharti gani hayo sasa? hahahaha....
hivi kuna ubaya gani kumu add ex kwa facebook au hizi social networks?
au utajuaje huyu ni ex wake, au huyu ana fling & flirt kwa sana?

...yaani relationship na mtu ndio mnakabana kabana namna hii? hahahaha
 
facebook

1.vijimama na serengeti
2.vizee na visichana
3.vijana kwa vijana
4.wote mnachanganyana.
vigezo picha ziwe photoshop au umepiga maeneo ya ukweli,au umezipiga kule majuu,mbona kitaeleweka tu kirahisi
 
...Halafu Lizzy umenikumbusha kitu, kuna watu kila siku wanaweka updates zao tangu wanaamka, wanachokula, wanapokwenda,
na mapicha yao ya kila siku, .....akipotea siku moja, siku ya pili anahadithia alipopotelea jana....!

...hivi tafsiri ya siri ya mambo ya ndani ni nini vile?
 
facebook

1.vijimama na serengeti
2.vizee na visichana
3.vijana kwa vijana
4.wote mnachanganyana.
vigezo picha ziwe photoshop au umepiga maeneo ya ukweli,au umezipiga kule majuu,mbona kitaeleweka tu kirahisi

...hahaha, jina halijengwi kwa ubao kaka,
linajengwa kwa pesa, ujiko au maskendeli!

watu wamegundua facebook, kama njia nyepesi ya kujijengea jina
ndio maana
Twitter bado ina washabiki wachache...
 
ni ukweli
na inatisha
ndo maana natamani kulof off fo good!

Mbona mi naona nimeongea kawaida tu!

Mimi naona niliyoyaongea ni mambo halisi yanayotokea katika dunia ya leo. Au wewe unaona ni mambo ya kufikirika zaidi?
 
...Mkuu Mbu kama humjui ex basi imekula kwako hahahahah lol! mawasiliano ya karibu kabisa kwa raha zao :):)...Kama unamfahamu basi hastahili kabisa kuwepo katika page ya mke/mume vinginevyo ndio mwanzo wa varangati ndani ya nyumba.


aaaaarrrggghh? Lizzy masharti gani hayo sasa? hahahaha....
hivi kuna ubaya gani kumu add ex kwa facebook au hizi social networks?
au utajuaje huyu ni ex wake, au huyu ana fling & flirt kwa sana?

...yaani relationship na mtu ndio mnakabana kabana namna hii? hahahaha
 
Last edited by a moderator:
...Mkuu Mbu kama humjui ex basi imekula kwako hahahahah lol! mawasiliano ya karibu kabisa kwa raha zao :):)...Kama unamfahamu basi hastahili kabisa kuwepo katika page ya mke/mume vinginevyo ndio mwanzo wa varangati ndani ya nyumba.

..hah? kiongozi hivi kuna umuhimu kumjua sijui kumfahamu ex wa mke/mume?
sasa wale one night stand utawa block vipi nao? nao wamo hao...
 

...hahaha, jina halijengwi kwa ubao kaka,
linajengwa kwa pesa, ujiko au maskendeli!

watu wamegundua facebook, kama njia nyepesi ya kujijengea jina
ndio maana
Twitter bado ina washabiki wachache...
twitter hata matumizi yake magumu.
facebook unakuwa na friends 5000 na zingine pendings yaani unafans sawa na msanii mwenye jina tz
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Back
Top Bottom