Sitta awasha moto mpya DOWANS

Hatu msemi kwa sababu ya kupinga malipo yasi lipwe tunamsema kutokana na unafiki wake, Alipokuwa Spika alikuwa nauwezo wa kulimaliza ili tatizo lakini baada ya walichokihitaji kutimia yaani EL kuutema U waziri mkuu, vita ikawaimeishia hapo. Hawakutaka kuangalia kisheria mkataba unaweza kuvunjwa au la! wao waliamua kusonga mbele wakati wanajua wazi kuwa mikataba yenyewe imeingiwa kifisadi hivyo hata conditions zilizomo kwenye mikataba hiyo ni ya kutuumiza sisi waTZ, kumbuka mwakyembe na sitta ni wanasheria lakini hilo wakalipuuza. Tuseme walipitiwa lakini BUNGE lilisha azimia waliotuingiza ktk dhahama hii waazibiwe serikali ikaanz kupiga danadana Badala ya Sitta kukomaa ili maazimio ya Bunge yatekelezwe akakubaliana na chama chake wakalimaliza suala hilo kisanii tulipo lalama yeye akadai maazimio yametekelezwa na yaliobaki yatatekelezwa mjadala umefungwa, sasa kiko wapi? Waliotuingiza mkenge wapo serikalini wanapeta, waliokuwa wanawalinda mf Mkurugenzi PCCB hadi leo anakula bata. Umeme hatuna hadi leo giza totoro, mitambo ileile ya dowans sasa imebadili jina ni symbion na tunalipishwa hela ndefu si tuna shida ! Kesi tumeshindwa tukiendelea kukata rufaa riba ndio inaongezeka kwa kwenda mbelle yeye anasema tusilipe. Je tusipo lipa nini kitafuata? inamaana Sitta hajui kuwa wenyewe tumeridhia sheria za kimataifa kwa kusaini makubaliano ya kuziheshimu, kuzitii na kuzitekeleza sheria za kimataifa pindi tutakapoingia ktk kuzitumia! Aoni kutuambia tusilipe anaongeza tatizo badala ya kulipunguza au kuliondoa? Soma maelezo yake yote hatoi suluhisho yeye anasema tusilipe tu basi, je tusipolipa nini kitatupata hazungumzii.
Mwisho RA anakusanya malipo yote tutakayolipa kama fidia lakini Sitta anajifanya haoni au hajui kuwa RA bado ni mwanaccm na yeye ndie kawafadhili helkopta ktk uchaguzi igunga, hivyo ni mwenzao na swahiba wao na ni mfadhili wao pia. Sasa kama yeye ni mkweli na anauchungu na taifa hili kwanini asitoke uko alipo ccm na kujiunga na CHAUSTA,SAU au NLD kama anaogopa kwenda CUF au CDM maana CCJ imejifia kifo cha mende, tunaitaji afanye maamuzi mazito kuonyesha kweli anapinga hayo malipo na si longolongo tu anazozitoa ktk media

Weka pembeni unafiki wa Sitta au hata ufisadi lakini kwa kauli hii aliyoitoa hastahili kulaumiwa hata kidogo. Wako wapi hao ambao si wanafiki na mafisadi ndani ya CCM watoe kauli kama ya Sitta kupinga malipo haya? Huyo Magufuli ambaye baadhi wameshaanza kumpigia debe la 2015 umemsikia katamka lolote kupinga malipo haya ya kifisadi? Hao akina Asha Migiro na Hussein Mwinyi ambao nao wanadhaniwa wanaweza kuingia Ikulu 2015 umeshawasikia kupinga kuhusu malipo hayo ya kifisadi yanayotaka kufanywa kwa Dowans. Pinda naye yuko kimya na huyo aliyekuwemo Ikulu sasa hivi wala hatii neno kama vile haoni uchungu dhidi ya wizi huu unaoataka kufanywa na kundi la mafisadi wachache. Unafiki wa Sitta na hata ufisadi wake ujadiliwe lakini hii kauli yake ya kutetea maslahi ya Tanzania haistahili kabisa kulaumiwa na Watanzania ila ni kuunga mkono na kuhakikisha malipo hayo ya kifisadi hayafanyiki.
 
Naomba tuelewane, mkirejea kwenye post yangu nimesema, sita ni mwadamu kama wewe, anayo mazuri na mabaya yake aliyoyafanya, lakini katika kazi aliyoifanya akiwa kama speaker, lazima tukiri amefanya mambo mengi ambayo mimi na wewe kwa namna yoyote lazima tukiri.

Yupi bora, anaekaa kwenye vikao akatoa hoja ikakataliwa na akanyamaza au anayejitokeza na kusema hadharan KUTORIDHISHWA KWAKE JUU YA MWENENDO FULANI! NANI AIYEJUA TANZANIA ILIVYOHARIBIKA?

NANI ASIYEJUA UMAFIA UNAOENDELEA?NANI ASIYEJUA SYNDICATE INANYOZUNGUMZWA? NA WANGAPI WAMESHIKA MADARAKA MAKUBWA KAMA SITA HAPA NCHINI? NA WANGAPI WALIKUWA NA MATEGEMEO MAKUBWA JUU YA UONGOZI ILA HAYAKUTIMIA LAKINI SOR FAR WAMEFANYA NINI?

UNAWASIKIA? KWA NINI SITA ANASIKIKA NA HARAKATI ZAKE SI ZA LEO WALA JANA WALA JUZI?HUYU MTU TUMUHUMU KWA HAKI!WATU WENGI WAPO NYUMA YAKE TENA WENGI NDANI YA CCM NADHANI NI MTU ANYEWEZA KUONEKANA LABDA NA MAGUFULI! WATU HUWA WANATELEZA!

NAKUMBUKA JUZI ALIWESEMA WAPINZANI KUWA NI VYAMA VYA MSIMU, WENYEWE NI KUBEZA TU HATA MIMI SIKUFURAHI KWANI MIMI NI MPINZANII LAKINI YULE NI MTU KAMA WEWE! NI SAWA NA MAGUFULI ALIPOKUWA ANAMPIGIA DEBE KAFUMU KUWA WAKIMCHAGUA ATAJENGA BARABARA!

HUO NI UTELEZI!AJALI ZA MANENO KAMA HIZI HUWA ZIPO! SITTA NA MSIFU SANA NI MJASIRI NA ANAWEZA KUDHUBUTU!KAWAFUNGUA MACHO WATANZANIA WALIO WENGI ALIPOKUWA SPEAKER, KARUHUSU MIJADALA MINGI SANA AMBAYO ILIFUNIKWA SIKU ZA NYUMA NA SASA TUNAONA INAFUNIKWA!YEYE ALIFANYA KAZI YAKE!

KAZI ILIYOBAKI YA UTEKELEZAJI HAIKUWA YA SITTA LAZIMA TUELEWE!KILA KITU KINA SEHEMU YAKE KWA SETUP YA HII NCHI!ULITAKA AWAFUNGE YEYE KAMA SPEAKER?SIDHANI KAMA ANA MAMLAKA HAYO!HUYU NI MTU MWENYE UDHUBUTU, ALISHAWAHI KUMWAMBIA RAIS ‘’ UWE MKALI’’JAMANI NANI ALISHAWAHI SEMA MANENO KAMA HAYA NDANI YA SYSTEM YAO????

TUKUBALI 6 NI MTU AMBAYE AIBA YAKE NA USHAWISHI VINARIDHISHA!

Nakuunga mkono Mkuu. Sitta pamoja na unafiki wake na ufisadi lakini kwa kauli hii aliyoitoa ya kutetea maslahi ya Tanzania hastahili kabisa kulaumiwa. Imenishangaza sana kuona watu wanavyomshambulia Sitta kwa kauli dhidi ya malipo fisadi yanayotaka kufanywa kwa Dowans. Cha kushangaza wale ambao wamekaa kimya ndani ya CCM/Serikali kuhusu malipo haya hawashambuliwi hata kidogo. Watu kama kina Pinda, Membe, Magufuli, Hussein Mwinyi, Asha Migiro wamekaa kimya kabisa bila kutoa kauli zao ili Watanzania tufahamu wanasimama upande gani katika ufisadi huu lakini huyu aliyekuwa mstari wa mbele kusimama kuhakikisha malipo fisasi hayo hayafanyaki kabisa ndiye anaandamwa. Kwa maana nyingine wanamtaka anyamaze ili kurahisisha malipo hayo yafanywe haraka iwezekanavyo bila kuwepo pingamizi lolote lile. Tukumbuke malipo haya yalitaka kufanywa tangu January 2011 lakini kwa kelele za Watanzania mafisadi wakaogopa kuyalipa na sasa tuko October na mimi naamini kabisa kama Watanzania popote pale walipo pamoja na hukumu hii iliyotolewa bado tunaweza kabisa kuyasimamisha malipo fisadi haya yasifanyike na hivyo kuokoa mabilioni ya pesa za walipa kodi wa Tanzania na kuhakikisha pesa hii inatumika kwa maendeleo ya nchi badala ya kuingia mifukoni mwa mafisadi.

Hivi ni nani aliyeweka sheria kwamba ili kuipinga CCM na kuweza kufanikiwa ni lazima uwe nje ya CCM? Mwacheni Sitta apambane humo humo ndani ya CCM na kama wakitaka kumfukuza basi wamfukuze kama wanataka kuuwafukuza mapacha watatu inakuwaje wanashindwa kumfukuza Sitta ambaye amekuwa mstari wa mbele kutoa kauli ambazo mafisadi wengi ndani ya CCM hawataki kuzisikia. Tuacheni unafiki wa kumshambulia Sitta, inawezekana kabisa huyu Sitta naye ana mabaya yake mengi tu, lakini kwa kauli hii ya kupinga malipo fisadi kwa Dowans hastahili kulaumiwa kwa namna yoyote ile na Watanzania ambao wameweka mbele maslahi ya nchi ila sitashangaa kama akilaumiwa na kushambuliwa na wote wale ambao watanufaika kwa namna moja na malipo hayo ya shilingi bilioni 13 akiwemo Rostam, Al Adawi, Lowassa na wengine wote ndani ya CCM au Serikali ambao wanasubiri mgao wao baada ya malipo hayo kufanyika.
 
Nakuunga mkono Mkuu. Sitta pamoja na unafiki wake na ufisadi lakini kwa kauli hii aliyoitoa ya kutetea maslahi ya Tanzania hastahili kabisa kulaumiwa. Imenishangaza sana kuona watu wanavyomshambulia Sitta kwa kauli dhidi ya malipo fisadi yanayotaka kufanywa kwa Dowans. Cha kushangaza wale ambao wamekaa kimya ndani ya CCM/Serikali kuhusu malipo haya hawashambuliwi hata kidogo. Watu kama kina Pinda, Membe, Magufuli, Hussein Mwinyi, Asha Migiro wamekaa kimya kabisa bila kutoa kauli zao ili Watanzania tufahamu wanasimama upande gani katika ufisadi huu lakini huyu aliyekuwa mstari wa mbele kusimama kuhakikisha malipo fisasi hayo hayafanyaki kabisa ndiye anaandamwa. Kwa maana nyingine wanamtaka anyamaze ili kurahisisha malipo hayo yafanywe haraka iwezekanavyo bila kuwepo pingamizi lolote lile. Tukumbuke malipo haya yalitaka kufanywa tangu January 2011 lakini kwa kelele za Watanzania mafisadi wakaogopa kuyalipa na sasa tuko October na mimi naamini kabisa kama Watanzania popote pale walipo pamoja na hukumu hii iliyotolewa bado tunaweza kabisa kuyasimamisha malipo fisadi haya yasifanyike na hivyo kuokoa mabilioni ya pesa za walipa kodi wa Tanzania na kuhakikisha pesa hii inatumika kwa maendeleo ya nchi badala ya kuingia mifukoni mwa mafisadi.

Hivi ni nani aliyeweka sheria kwamba ili kuipinga CCM na kuweza kufanikiwa ni lazima uwe nje ya CCM? Mwacheni Sitta apambane humo humo ndani ya CCM na kama wakitaka kumfukuza basi wamfukuze kama wanataka kuuwafukuza mapacha watatu inakuwaje wanashindwa kumfukuza Sitta ambaye amekuwa mstari wa mbele kutoa kauli ambazo mafisadi wengi ndani ya CCM hawataki kuzisikia. Tuacheni unafiki wa kumshambulia Sitta, inawezekana kabisa huyu Sitta naye ana mabaya yake mengi tu, lakini kwa kauli hii ya kupinga malipo fisadi kwa Dowans hastahili kulaumiwa kwa namna yoyote ile na Watanzania ambao wameweka mbele maslahi ya nchi ila sitashangaa kama akilaumiwa na kushambuliwa na wote wale ambao watanufaika kwa namna moja na malipo hayo ya shilingi bilioni 13 akiwemo Rostam, Al Adawi, Lowassa na wengine wote ndani ya CCM au Serikali ambao wanasubiri mgao wao baada ya malipo hayo kufanyika.

Tanzania inakizungumkuti chake cha kuwa na aina ya watu ambao wako tayri kumshambulia mtu bali kwa sababu ya kuwa yuko CDM na mwingine yuko CCM,au kumshambulia alie CCM kwa kua yeye yuko CDM.Na mchezo huu unaweza kuona kwenye timu ya TAIFA ambako kukiwa na wachezaji wa timu mbili za SIMBA na YANGA.Huwa kunaibuka uchafuzi wa wachezaji wa timu hizi mbili kuwa na maneno ya uchokonozi toka pande mbili kwa wachezaji kulushiwa madongo toka kila pande dhidi ya upande mwingine.

Kwa kiwango fulani TANZANIA limekuwa ni TAIFA kwa baadhi ya raia kupenda UNAFIKI na ujinga wa kushabikia madudu ya aina hii ya TAIFA la watu kuwa na ujanja ujanja wa kuliibia TAIFA na bado kuonekana kwenye jamii kama watu wnaostahiki pongezi kuwa walitumia akili nzuri na maarifa katika kufanikiwa kimaisha kumbe ni WIZI MTUPU.

Ebu angalia mtaani kwako mwanajamii ambae analitumikika TAIFA kwa uaminifu jinsi anavyopata shida kwa kumwagia kila aina ya matusi toka kwa wanafamilia wake na jamii kwa ujumla kuwa anachezea nafasi yake na yule mwingine aliye MWIZI kwenye shirika la umma ama chombo cha umma kuonekana ni bora na wakupigiwa mfano kuwa ndiye bora na ikibidi kuombwa na wanajamii kugombea nafasi ya uongozi kwenye ngazi ya jamii.

Hivyo swala la baadhi ya Wanajf kumwagia matusi na lawama kadha wa kadha SITA ni mzigo wa aina ya wale wale wanajamaii wanaowasifia wezi wetu kwenye jamii na kuwapa madaraka ili wawaongoze na kuwaondoa wale wote wenye kutenda haki.\

Siokuwa SITa hana mapungufu yake bali,tunaangalia mema ni yapi na mabaya yake yana ukubwa upi katika kipimo cha kumuona dhidi ya hoja zake katika kulipigigania TAIFA.

Yote ya yote uzuri wa Nchi hiii na Mama wa Nchi ni kuwa hatimae wezi wa TAIFA hili mwisho wake hata wao Uwa wanastaajabu jinsi wanavyoumbuka hakika uwa hawaamini imekuwaje kuwa kumbe wakati wanaiba au wakati wa matendo yao kullikuwa na watu wenye nguviu wa kuwaumbua lakini hawakufanya hivyo.Ukibahatika kukutana na mafisadi nina hakika ndani ya mioyo yao wanatamani WANGELUDI KUWA KAMA WATOTO WADOGO.Wanajaka moyo lisilo kwisha kwa kuwa ugeuka kuwa waigizaji wenye dukuduku kila siku na kuchezeshwa gwalide wasilolitaka,moja ya matokeo ya jaka moyo angalia wale waliokimbilia kwenye sura za makanisa au misikitini.Jaka moyo hilo ni kuanza kutafuta uwepo wa ufahamu wa UBINADAMU ambao hapo awari muhusika hakuwa nao.

Matendo ya KIFISADI ni zao la watu ambao kwa imani zao za ndani awari wakati wa matendo ya KIFISADI watendaji walikuwa hawana Moyo wala HAWAAMNI KAMA KUNA MUNGU,kwa kuwa wamekuwa na mamlaka ya kumilki mali na watu wanaowatumikia kiasi kuwa wanakufulu, na hawajitambui kuwa ni sehemu ya viumbe wa MUNGU kama wengine.

Inapofika kwenye hatua hii,basi kuna wale ambao taaratibu wanafunguka na kuona kuwa mengine pamoja na matamanio ya kumiliki mali bali kuna ubinadamu.HATIMAE WENGINE UFUNGUKA NA KUONA WATANGULIZE KIPI KATI YA HAY MAWILI KUWATUMIKA WATU [BINADAMU] NA SIO MALI AU WATUMIKIE MALI NA SIO KUWATUMIKIA BINADAMU.

Yote ya yote nae SITA atudhibitishie kwa kuweka msimamo wa dhati kuwa wakilipwa dowans anatoka CCM?
 
Tanzania inakizungumkuti chake cha kuwa na aina ya watu ambao wako tayri kumshambulia mtu bali kwa sababu ya kuwa yuko CDM na mwingine yuko CCM,au kumshambulia alie CCM kwa kua yeye yuko CDM.Na mchezo huu unaweza kuona kwenye timu ya TAIFA ambako kukiwa na wachezaji wa timu mbili za SIMBA na YANGA.Huwa kunaibuka uchafuzi wa wachezaji wa timu hizi mbili kuwa na maneno ya uchokonozi toka pande mbili kwa wachezaji kulushiwa madongo toka kila pande dhidi ya upande mwingine.
WEWE hujui mambo na mazingaumbwe ya SITTA
sitta alipingana na wapinzani walipotaka posho ifutwe just bcs pamoja na wengine SITTA ni mnufaika.
Angelikuwa mzalendo angeunga mkono hoja ya NO POSHO kuokoa matumizi mabaya ya serikali ambayo ni bil 900 kwa mwaka
Sitta alikuwa akionekana shujaa kwa misimamo yake lakini tokea siku hiyo ya kuunga mkono posho kwa kuwaita wapinzani ni wanafiki WATANZANIA wengi tukaanza kumwona JIZI JINGINE
SITTA alinyimwa uwaziri mkuu ndiyo sababu akamwandama LOWASSA
sitta AJIUZULU KAMA ISHARA YA KUPINGA MALIPO TUTAMWELEWA
 
viongozi wengi wa nchi hii ni wanafiki wanapiga kelele kwa maslahi yao watoto wao si kwa wananchi walowachagua
 
hana lolote huyo ,mnafiki mkubwa muda wote akiwa nje uspika ameendelea kukaa nyumba ya kupanga huku analipiwa ml 12 kwa mwezi za hao hao walala hoi! uko wa uzalendo wake ?
 
astaafu uwaziri kuonyesha kwamba anakerwa na mafisadi walio ktk chama chake na awe wa kwazna bungeni kuonyesha kupingana na sera za ccm ambazo hazina tija kwa wananchi,awe mstari wa mbele kuikosoa ccm popte pale na aanile maovu yao,anajua fika nani mwizi nani fisadi mkuu.
 
Nadhani sasa imetosha kusikia ni nini kilifanyika..., inabidi kutafuta mbinu ya nini kifanyike..

huu moto unaowashwa mpaka sasa sijaona makali yake
 
Sitta ni mwizi tu yeye! hana ubavu wowote au uwezo wa kufanya lolote! Kama kidume angejiunga na ccj...hahaha!

Sita hana lolote na endapo sheria itachukua mkondo wake Sita na kundi lake ndio wa kulaumiwa ndio yeye aliye sitisha mjadala wa richmond kwa kuangalia maslahi yake ya kukosa ulaji akinyany'anywa kadi ya magamba.CDC kupitia thinker Zito aliyaona haya mapemba akashauri serekali inunue mitambo hii,sitta na kundi lake wakaja juu.Leo hii anasubutu kuongea tena.HAFAI KUWA RAIS HATA CHEMBE BORA HATA MNYIKA AU ZITO ambao ni sawa na wajukuu wa sita ila wanaona mbali kuliko huu MLAFI.
HIVI ALISHAHAMA NYUMBA YA SPIKA?

Tatizo la nchi hii wana siasa hata wakiongea pumba huwa hakuna wakusema hizi ni pumba,Sheria ni sheria
 
mh. sita ni mnafiki sana.ata hao mafisadi anaopigana nao ni kwamba walimsshinda ujanja.kwanini hakutoka ccm baada ya kumshushua na kukaa kando na siasa au kwenda upinzani??pili,huyu ndiye anatumiwa na ccm kupiga madongo wapinzani wakti anakumbatia wafu.tatu, kama ni mjanja mbona hakwenda igunga???imedhihirisha kuwa yeye anatumiwa pasipokujijua. mikutano yake ya kuzunguka kila mkoa eti anataka mafisadi wajivue gamba imeishia wapi???tunataka damu mpya na si hawa wapayukaji
 
Sitta ni mzalendo tatizo lake yuko katikati ya magamba amebanwa, inatakiwa apambane nao ajinasue.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom