Siri kuhusu wajumbe wateule wa tume ya katiba

Paparazi Muwazi

JF-Expert Member
Dec 23, 2007
310
79
Huu ndio wakati wetu wanahabari na wachambuzi kuanika siri zote tunazozifahamu wajumbe wateule wa tume ya katiba kwa sababu ikulu imesema Rais atawaapisha ijumaa.

Siri hizi zitawezesha usalama wa taifa kumshauri Rais kuacha kuwaapisha wajumbe wenye mashaka, pia makundi ambayo Rais amedai kuwa yameridhika na mapendekezo yataweza kuweka pingamizi pale ambapo mteule hajatokana na ridhaa yao.

Tusiangalie dini wala makabila ya watu walioteuliwa, tuangalie namna walivyoteuliwa iwapo walitokana na makubaliano ya makundi kweli ya wanaowakilisha na tuangalie pia kama kweli wana uwezo na msimamo wa kuhakikisha maoni ya wananchi ndiyo yanayowekwa badala ya mawazo ya watawala.

Kulipaswa kuwe na waliopendekezwa na vyama vya siasa, waliopendekezwa na vyama vya wafanyakazi, asasi za kiraia, taasisi za dini, vyama vya wanataaluma, sekta binafsi na makundi mengine muhimu katika taifa letu.

Weka jina la mjumbe unayemjua katika orodha na siri unazozifahamu kuhusu mjumbe huo. Haya tuanze sasa?

Mimi naanza na Mwenyekiti, ana sifa zote za kuwa mjumbe wa tume lakini sio mwenyekiti kwa kuwa alishawahi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya rushwa lakini akakubali ripoti yake isitekelezwe na pia katika siku za karibuni amekuwa akitoa kauli za kikada kama mwanaCCM, Mwenyekiti wa tume hii alipaswa kuwa mtu neutral ingawa Mzee Warioba ana sifa za kuwa mjumbe.

PM
 
What are you trying to advocate here? Kizazi kabla ya miaka ya 90 kilikuwa na masharti ya ukada katika sekta zote.

Tunaomba utupe list mbadala ili tuweze kuchangia badala ya kuishia kukosoa ama kutoa hizo unazoita siri (kama ni siri sijui watu watajuaje)
 
Kwa Bara Mkiwapinga/wakataa walioteuliwa, basi hata wakiletwa Malaika mtawapinga!

Usiangalie majina makubwa manne, pitia mjumbe mmoja baada ya mwingine utaona vituko. Niende kwa huyu Richard Lyimo, huyu ndiye ambaye kwa miaka mingi amekuwa akitumiwa na usalama wa taifa na kundi la propaganda la CCM pale TLP dhidi ya upinzani.

Mwaka 2008 wakati huo nikiwa habari Corporation kuliletwa kazi maalum akakabidhiwa Balille ya kukutana na Bwana Lyimo ikapikwa hadithi ya Mbowe kushangilia kifo cha Chacha Wangwe kule Afrika Kusini. Kwa jinsi tulivyokutana na huyu bwana ni mtu asiye na msimamo wowote akilipwa aseme au afanye chochote kwake ni jambo la kawaida. Ndio taifa itabidi limtegemee kwenye kuandaa rasimu ya katiba.

Miezi michache iliyopita kwenye ukumbi wa idara ya habari maelezo alifanya kituko cha mwaka dhidi ya bwana Tao, pale alipokuja na mwenzake mmoja simfahmu jina, wakataka wanahabari tumpe karatasi tulizokuwa nazo za press release kwamba zina makosa atupe zingine. Akatupa taarifa iliyoghushiwa kuhusu Tao na Mrema.

Kuna mtu anamfahamu zaidi bwana Lyimo? Nitawaletea siri za wajumbe wengine ninaowafahamu.

PM
 
Unataka watu watoke dunia gani na hao ndio watanzania !!!! Wenye viwango !
 
Kutoa maoni hadi ujue siri zao tu?

Ukijua siri zao utajua kama maoni unayotoa yatazingatiwa au yataachwa kwa maagizo ya serikali. Kwa mfano kuna huyu Humphrey Polepole ambaye ameingia kama mwakilishi wa asasi za kiraia. Huyu mkutano wa kupendekeza jina lake kule Dodoma ulivurugika, pamoja kusaidiwa na Ikulu baada ya ya mkutano wake na Kikwete bado alishika nafasi ya tatu. Mapendekezo ya asasi za kiraia wa kwanza alikuwa John Ulanga, wa pili Profesa Ruth Meena wa TGNP lakini Kikwete amewaacha wote akamchukua huyu.

Msimamo wake unajulikana kabla kwa kuwa mara zote alivyozungumza na vyombo vya habari kuhusu muswada mbovu wa sheria ya katiba uliokataliwa na asasi za kiraia yeye alitofautiana na wenzake na kuunga mkono. Uchaguzi ule wa Dodoma tulishuhudia NGO zenye utii kwa serikali zikieleza kuwa haziwataki wanasheria kama Wakili Harold Sungusia wa LHRC kwenye tume ya katiba kwa kuwa atakwenda kupingana na serikali. Hivyo wakataka Kikwete amchague Polepole kutoka TYC ili NGO ambazo zimekuwa zikichochea wananchi nchini kuhusu katiba zisipate uwakilishi wenye nguvu ndani ya tume.

PM
 
Usiangalie majina makubwa manne, pitia mjumbe mmoja baada ya mwingine utaona vituko. Niende kwa huyu Richard Lyimo, huyu ndiye ambaye kwa miaka mingi amekuwa akitumiwa na usalama wa taifa na kundi la propaganda la CCM pale TLP dhidi ya upinzani.

Mwaka 2008 wakati huo nikiwa habari Corporation kuliletwa kazi maalum akakabidhiwa Balille ya kukutana na Bwana Lyimo ikapikwa hadithi ya Mbowe kushangilia kifo cha Chacha Wangwe kule Afrika Kusini. Kwa jinsi tulivyokutana na huyu bwana ni mtu asiye na msimamo wowote akilipwa aseme au afanye chochote kwake ni jambo la kawaida. Ndio taifa itabidi limtegemee kwenye kuandaa rasimu ya katiba.

Miezi michache iliyopita kwenye ukumbi wa idara ya habari maelezo alifanya kituko cha mwaka dhidi ya bwana Tao, pale alipokuja na mwenzake mmoja simfahmu jina, wakataka wanahabari tumpe karatasi tulizokuwa nazo za press release kwamba zina makosa atupe zingine. Akatupa taarifa iliyoghushiwa kuhusu Tao na Mrema.

Kuna mtu anamfahamu zaidi bwana Lyimo? Nitawaletea siri za wajumbe wengine ninaowafahamu.

PM
Lazima siku moja kuna watu watafikishwa the Hague.
 
nashangaa watanzania wengi kuishabikia tume hii aliyoiunda JK, siikandii na nakiri kuwa ina watu makini lakini tatizo langu linakuja kwenye uwakilishi wa makundi mbalimbali kama sheria inavyojipambanua. kama sikosei tume inaundwa 80% na wanasiasa na viongozi wastaafu kwa nini? wafanyakazi kma walipakodi wakubwa wa nchi hii wanawakilishwa na nani? vijana je? ebu tuangalie kundi lingine wazee uwakilishi wao upo wapi? au watasema kwa sababu akina butiku, warioba, ramadhani ni wazee wanatosha! hapana tunataka mzee yule anayejua jinsi wenzake wanavyosotea dawa pale mwananyamala hospitali na mwisho wa siku wanaambia wakanunue wakati tayari walishapewa msamaha watibiwe bure. wakulima je? vipi makundi ya dini?. jamani nchi hii siyo ya wanasiasa na viongozi wasitaafu na waliopo kwenye system. rais kajitahidi lakini azingatie uwakilishi wa makundi
 
wanasema wahenga mpe mchawi akulelee mtoto wako.so usihofu kiongozi mwisho wa siku hwa kazi yao ni kukusanya maoni tu na sio kutunga.tukiona wamechakachua maoni ya watu nguvu ya uma ipo
 
Ukijua siri zao utajua kama maoni unayotoa yatazingatiwa au yataachwa kwa maagizo ya serikali. Kwa mfano kuna huyu Humphrey Polepole ambaye ameingia kama mwakilishi wa asasi za kiraia. Huyu mkutano wa kupendekeza jina lake kule Dodoma ulivurugika, pamoja kusaidiwa na Ikulu baada ya ya mkutano wake na Kikwete bado alishika nafasi ya tatu. Mapendekezo ya asasi za kiraia wa kwanza alikuwa John Ulanga, wa pili Profesa Ruth Meena wa TGNP lakini Kikwete amewaacha wote akamchukua huyu.

Msimamo wake unajulikana kabla kwa kuwa mara zote alivyozungumza na vyombo vya habari kuhusu muswada mbovu wa sheria ya katiba uliokataliwa na asasi za kiraia yeye alitofautiana na wenzake na kuunga mkono. Uchaguzi ule wa Dodoma tulishuhudia NGO zenye utii kwa serikali zikieleza kuwa haziwataki wanasheria kama Wakili Harold Sungusia wa LHRC kwenye tume ya katiba kwa kuwa atakwenda kupingana na serikali. Hivyo wakataka Kikwete amchague Polepole kutoka TYC ili NGO ambazo zimekuwa zikichochea wananchi nchini kuhusu katiba zisipate uwakilishi wenye nguvu ndani ya tume.

PM

Kwa kuwa alipendekezwa ANAFAAA, na kama hakufaa basi msingempendekeza! FULL STOP
 
Ukijua siri zao utajua kama maoni unayotoa yatazingatiwa
au yataachwa kwa maagizo ya serikali. Kwa mfano kuna huyu Humphrey

Polepole ambaye ameingia kama mwakilishi wa asasi za kiraia. Huyu mkutano wa kupendekeza jina lake kule Dodoma ulivurugika, pamoja kusaidiwa na Ikulu baada ya ya mkutano wake na Kikwete bado alishika nafasi ya tatu. Mapendekezo ya asasi za kiraia wa kwanza alikuwa John Ulanga, wa pili Profesa Ruth Meena wa TGNP lakini Kikwete amewaacha wote akamchukua huyu.

Msimamo wake unajulikana kabla kwa kuwa mara zote alivyozungumza na vyombo vya habari kuhusu muswada mbovu wa sheria ya katiba uliokataliwa na asasi za kiraia yeye alitofautiana na wenzake na kuunga mkono. Uchaguzi ule wa Dodoma tulishuhudia NGO zenye utii kwa serikali zikieleza kuwa haziwataki wanasheria kama Wakili Harold Sungusia wa LHRC kwenye tume ya katiba kwa kuwa atakwenda kupingana na serikali. Hivyo wakataka Kikwete amchague Polepole kutoka TYC ili NGO ambazo zimekuwa zikichochea wananchi nchini kuhusu katiba zisipate uwakilishi wenye nguvu ndani ya tume.

PM

Haya ni matokeo ya vita ya makundi ndani ya hizi NGO na hili tulilitarajia sana hasa katika ile slogan ya Mwamba ngoma huvutia kwake.Ni vigumu asasi hizi za kiraia kucompromise kwani zinadiffer kimtizamo na ndio maana ziko nyingi sana japo kwa sehemu kubwa scope na parameters za operation zinashabihiana.

Mchakato ulitawaliwa na ubaguzi mpaka huyo kushika nafasi ya tatu haikuwa kazi nyepesi kwani asasi kubwa zinazopata misaada kutoka nje lazima zitakuwa ni zile zisizoipendeza Serikali kwa maana ya kile wanacho kisimamia na taarifa zao ambazo kwa sehemu kubwa zinaonekana kuipaka madoa Serikali.Kwa msingi huu ziliweza kuwa na ushawishi mkubwa kama chaguo la kwanza na la pili japo bado manung'uniko yalibakia kwa NGO ambazo zilihisi kupata fursa pia lakini kutokana na uwezo mdogo wa kiushawishi pamoja na kitaasisi hazikufua dafu.

Kifupi ni ngumu NGO kujikubali zenyewe na kuwa na uwakilishi wa pamoja zaidi ya kila moja kujali maslahi na status quo.Rais kupick mmoja kati ya top three naona ni sawa na malalamiko kwa NGO hizi hayawezi kuepukika kwani ni nyingi na nafasi ni moja.
 
Wote wanafaa, kwa amoni yangu uteuzi huu ni mwanzo mzuri, tumwombe Mungu tufikie huko tunakotarajia" Katiba Muafaka'
 
Wana Jamvi
Mawazo ya Paparazi Muwazi yasipuuzwe. Nimefuatilia na kugundua kuwa wale walioteuliwa kuwakilisha makundi ni wale walioshika nafasi ya tatu na ya nne. Wale waliopendekezwa wakiwa wa kwanza na wa pili wameachwa baada ya TISS kupeleka taarifa kwa JK kuwa waliopendekezwa wakiwa wa kwanza ni "wakali" sana kuhusu sheria ya katiba mpya. Baadhi ya wateule waliitwa na kuonana na maofisa wa TISS ama kuwekwa sawa au TISS kujihakikishia juu ya misimamo yao. Ushahidi kuhusu madai haya ni:
-Prof Baregu alipendekezwa akiwa namba tatu - wa kwanza alikuwa na Tundu Lissu akifuatiwa na Prof Safari
-Jesca Mkuchu alikuwa wa tatu kutoka CCT akiwa nyuma ya maaskofu wawili - mmoja wa Mbeya na mwingine wa Tanga, n.k.

Pamoja na uhuru wa Rais kuteua kutoka mapendekezo ya makundi, ni sahihi kuhoji kwa nini ateue chaguo la tatu na siyo la kwanza na la pili.

Naelewa tume haina kauli ya mwisho juu ya katiba, lakini wakiishaandika draft na kuacha mengine, inakua vigumu kuyaondoa. Serikali inafanya makosa kujaribu kudhibiti mchakato huu maana hakuna serikali ya milele mahali popote. Katiba ikiwa mbaya wajue itatumika kuwakandamiza wao watakapokuwa wapinzani.
 
Haya ni matokeo ya vita ya makundi ndani ya hizi NGO na hili tulilitarajia sana hasa katika ile slogan ya Mwamba ngoma huvutia kwake.Ni vigumu asasi hizi za kiraia kucompromise kwani zinadiffer kimtizamo na ndio maana ziko nyingi sana japo kwa sehemu kubwa scope na parameters za operation zinashabihiana.

Mchakato ulitawaliwa na ubaguzi mpaka huyo kushika nafasi ya tatu haikuwa kazi nyepesi kwani asasi kubwa zinazopata misaada kutoka nje lazima zitakuwa ni zile zisizoipendeza Serikali kwa maana ya kile wanacho kisimamia na taarifa zao ambazo kwa sehemu kubwa zinaonekana kuipaka madoa Serikali.Kwa msingi huu ziliweza kuwa na ushawishi mkubwa kama chaguo la kwanza na la pili japo bado manung'uniko yalibakia kwa NGO ambazo zilihisi kupata fursa pia lakini kutokana na uwezo mdogo wa kiushawishi pamoja na kitaasisi hazikufua dafu.

Kifupi ni ngumu NGO kujikubali zenyewe na kuwa na uwakilishi wa pamoja zaidi ya kila moja kujali maslahi na status quo.Rais kupick mmoja kati ya top three naona ni sawa na malalamiko kwa NGO hizi hayawezi kuepukika kwani ni nyingi na nafasi ni moja.

Mkuu nimekukubali ila kwa kuwa hujabofya likes kwa mtu yeyote tokea ujiunge JF na mimi nimekupa nusu LIKES na hakuna button ya aina hiyo JF
 
Kwa kuwa alipendekezwa ANAFAAA, na kama hakufaa basi msingempendekeza! FULL STOP

Unamuamini JK? Una uhakika gani kwamba aliowateuwa ni miongoni mwa wale waliopendekezwa na makundi?

Je ilichapishwa orodha ya hayo makundi ikionyesha majina ya watu wao waliopendekezwa?

Kama JK kachomeka wengine watu wake nani atajua iwapo hatujui ni akina nami waliopendekezwa?
 
Wana Jamvi
Mawazo ya Paparazi Muwazi yasipuuzwe. Nimefuatilia na kugundua kuwa wale walioteuliwa kuwakilisha makundi ni wale walioshika nafasi ya tatu na ya nne. Wale waliopendekezwa wakiwa wa kwanza na wa pili wameachwa baada ya TISS kupeleka taarifa kwa JK kuwa waliopendekezwa wakiwa wa kwanza ni "wakali" sana kuhusu sheria ya katiba mpya. Baadhi ya wateule waliitwa na kuonana na maofisa wa TISS ama kuwekwa sawa au TISS kujihakikishia juu ya misimamo yao. Ushahidi kuhusu madai haya ni:
-Prof Baregu alipendekezwa akiwa namba tatu - wa kwanza alikuwa na Tundu Lissu akifuatiwa na Prof Safari
-Jesca Mkuchu alikuwa wa tatu kutoka CCT akiwa nyuma ya maaskofu wawili - mmoja wa Mbeya na mwingine wa Tanga, n.k.

Pamoja na uhuru wa Rais kuteua kutoka mapendekezo ya makundi, ni sahihi kuhoji kwa nini ateue chaguo la tatu na siyo la kwanza na la pili.

Naelewa tume haina kauli ya mwisho juu ya katiba, lakini wakiishaandika draft na kuacha mengine, inakua vigumu kuyaondoa. Serikali inafanya makosa kujaribu kudhibiti mchakato huu maana hakuna serikali ya milele mahali popote. Katiba ikiwa mbaya wajue itatumika kuwakandamiza wao watakapokuwa wapinzani.

JK asipoangalia hili nalo litasababisha watu waende Ikulu kujadili mambo ambayo hayana msingi sana. Ni hatari watu wanapoonza kudoubt uwezo wa timu kabla ya hata mpambano kuanza.
 
Back
Top Bottom