Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Sheria hii inabainisha muundo, majukumu, utaratibu wa upatikanaji wa Wajumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na sifa za Mkurugenzi wa Uchaguzi, kuweka utaratibu wa uendeshaji wa vikao vya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na kuweka masuala mengine yanayohusiana na hayo.
Kwa mujibu wa Sheria hii, Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano iliyoanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 74(1) ya Katiba ambayo pia itajulikana kama “Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi”.
Tume hii itakuwa na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wengine watano watakaoteuliwa
na Rais. Aidha, Rais atateua wajumbe wa Tume kama ifuatavyo:
Kwa mujibu wa Sheria hii, Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano iliyoanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 74(1) ya Katiba ambayo pia itajulikana kama “Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi”.
Tume hii itakuwa na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wengine watano watakaoteuliwa
na Rais. Aidha, Rais atateua wajumbe wa Tume kama ifuatavyo:
- Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Tume kutoka miongoni mwa majina yatakayopendekezwa na Kamati ya Usaili kwakuzingatia masharti ya Ibara ya 74(1)(a) na (b) na (2) ya Katiba na kanuni zitakazotengenezwa chini ya Sheria hii; na
- Wajumbe wengine wa Tume kutoka miongoni mwa majina yatakayowasilishwa na Kamati ya Usaili baada ya kufanyiwa usaili.
- Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi watashika madaraka
mara baada ya kuapishwa na Rais. - Uteuzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Tume utafanywa kwa misingi kwamba, endapo Mwenyekiti atateuliwa kutoka upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano, basi Makamu Mwenyekiti atateuliwa kutoka upande wa pili wa Jamhuri ya Muungano.
- Mkurugenzi wa Uchaguzi atakuwa Katibu na Mtendaji Mkuu wa Tume.