Siri kuhusu wajumbe wateule wa tume ya katiba

Pamoja na walakini hizo mlizotaja, naomba tuwape nafasi, binafsi nina imani nao; hasa ukizingatia Mhe. Jaji Augustino Ramadhani yupo ndani ya Tume.
 
nashangaa watanzania wengi kuishabikia tume hii aliyoiunda JK, siikandii na nakiri kuwa ina watu makini lakini tatizo langu linakuja kwenye uwakilishi wa makundi mbalimbali kama sheria inavyojipambanua. kama sikosei tume inaundwa 80% na wanasiasa na viongozi wastaafu kwa nini? wafanyakazi kma walipakodi wakubwa wa nchi hii wanawakilishwa na nani? vijana je? ebu tuangalie kundi lingine wazee uwakilishi wao upo wapi? au watasema kwa sababu akina butiku, warioba, ramadhani ni wazee wanatosha! hapana tunataka mzee yule anayejua jinsi wenzake wanavyosotea dawa pale mwananyamala hospitali na mwisho wa siku wanaambia wakanunue wakati tayari walishapewa msamaha watibiwe bure. wakulima je? vipi makundi ya dini?. jamani nchi hii siyo ya wanasiasa na viongozi wasitaafu na waliopo kwenye system. rais kajitahidi lakini azingatie uwakilishi wa makundi
Mimi hii tume naipa only 40%. Ni watu wachache ninaowaamini. 1. Salim Ahmed Salim. 2. Prof Baregu 3. Dr sengondo.
Waryoba anaaongea sana kuhusu vita dhidi ya rushwa lakini hata siku moja hawezi kusaliti mapendekezo yanayobana chama chake hata kama yana maslahi kwa taifa. Jaji Ramadhan ndo simwamini kabisa hasa baada ya kushindwa kutoa uamuzi kuhusu mgombea binafsi kwamba ni swala la kisiasa wakati inajulikana kilichokuwa kinalindwa ni maslahi ya ccm.
 
Inafurahisha kuona magamba yanaaminika. Watanzania tu wasahaulifu sana, wengi tumesha sahau yale maneno ya waziri wa katiba na sheria.
Tuendelee na mchakato huu hadi mwisho ambapo waziri huyu atakapoibuka kidedea!
 
Ukijua siri zao utajua kama maoni unayotoa yatazingatiwa au yataachwa kwa maagizo ya serikali. Kwa mfano kuna huyu Humphrey Polepole ambaye ameingia kama mwakilishi wa asasi za kiraia. Huyu mkutano wa kupendekeza jina lake kule Dodoma ulivurugika, pamoja kusaidiwa na Ikulu baada ya ya mkutano wake na Kikwete bado alishika nafasi ya tatu. Mapendekezo ya asasi za kiraia wa kwanza alikuwa John Ulanga, wa pili Profesa Ruth Meena wa TGNP lakini Kikwete amewaacha wote akamchukua huyu.

Msimamo wake unajulikana kabla kwa kuwa mara zote alivyozungumza na vyombo vya habari kuhusu muswada mbovu wa sheria ya katiba uliokataliwa na asasi za kiraia yeye alitofautiana na wenzake na kuunga mkono. Uchaguzi ule wa Dodoma tulishuhudia NGO zenye utii kwa serikali zikieleza kuwa haziwataki wanasheria kama Wakili Harold Sungusia wa LHRC kwenye tume ya katiba kwa kuwa atakwenda kupingana na serikali. Hivyo wakataka Kikwete amchague Polepole kutoka TYC ili NGO ambazo zimekuwa zikichochea wananchi nchini kuhusu katiba zisipate uwakilishi wenye nguvu ndani ya tume.

PM




Kwa Kuongezea tu Kuhusu huyo ndugu Polepole alisoma Sekondari Azania Dar es salaam Mwaka 1997-2000 akachaguliwa kwenda Shule Benjamin William Mkapa Mwaka 2001,Katika Matokeo ya kidato cha Sita alipata 0(Zero),Kuthibitisha hili sio shida,Nenda Baraza la Mitihani pata matokeo ya Wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha 6 Mwaka 2003 BWM Secondary School!!


Katika Maisha yake ya Shule hasa Azania,aliwahi Kuongoza Azania Debating Society akisaidiwa na baadhi ya watu akiwemo Bwana Nyakia Ally(Sekretariet Member wa TYC) alikuwa ni Mzungumzaji Mzuri mbele ya hadhira na anapenda Kuongea Kiingereza!!!

Inasemekana in recent years,alisoma Chuo Cha Maendeleo Tengeru Arusha and some online course!!

Kuhusu kama atafanya kazi Nzuri kwenye hiyo Tume jibu ni HAPANA,Kwa sababu asasi anayoiongoza ya Tanzania Youth Coalition haifanyi kazi ya Utetezi wa Vijana ndiyo maana kwenye Mambo yote ya Msingi kuhusu Vijana,Polepole amekuwa mtu wa kuchukua msimamo Neutral au wenye mlengo wa kuitetea Serikali ya Ccm!!

Katika Chaguzi zote kuu ukianzia wa Mwaka 2005 hadi wa Mwaka 2010 TYC imekuwa bubu kana kwamba haifanyi kazi ya Uanaharakati!!

Asasi hii imegeuka tu kuwa genge la watu kupata fursa za kuhudhuria mikutano mbalimbali ya ndani na nje ya Nchi ili kupata senti za Kujikimu kwa wajumbe wasiobadilika Wa Sekretariet kama Vile Juma Mkuu,Nyakia Ally,Lenin Kazoba et all

Kwa haiba,ana uwezo mzuri wa kujieleza,Mwoga wa Changamoto kutoka kwa watu wanaonyesha Uwezo ndiyo maana anafanya kazi na watu walewale kwa zaidi ya Miaka 7 tangu ofisi zilipokuwa kwenye jengo la MS Upanga mpaka sasa pale Kijitonyama Karibu na shule ya Msingi kijitonyama,Kuna Jengo la Ghorofa ndipo zilipo Ofisi za Shirika hilo ambalo linajitambulisha kama Umbrella Organisation ya asasi za Vijana Tanzania!!


Itoshe kusema Polepole hawezi kusimamia Maslahi ya Taifa na hasa Vijana,ni Mtu wa Ccm ndiyo maana hata juzi katika kipindi cha Adam Sembeye cha This Week In Perspective alikuwa anaongea Porojo tu na hatoi Msimamo yabisi Kuhusu hatma ya Ajira za Vijana hapa Bongo!!

Humphrey Polepole atakuwepo pale kufanya Mapenzi ya aliyemchagua tu,kuhusu hili nina hakika kwa 100%
 
Watanzania kila kitu mna doubt, sasa mnadhani hii katiba ni ya wananchi au ni ya vyama vya siasa. Kwahiyo mlitaka achaguliwe SLAA ndo mfurahi, lazima mjue kwamba si kila mtu aliyekomboka (conscious person) basi awe CHADEMA
 
Hahaha hao madogo walikuwa wanataka sifa sana nilikuwa siwapendi kabisa. Mwenzake Nyakia nilimuona anasoma ustawi wa jamii certificate sijui...kweli shuleni si mahala pa kutafuta ujiko na kujifanya mnoko!
 
Wote wanafaa watanganyika na wazanzibar
wapeni nafasi
acheni majungu

DK Salim hafai, kwa sababu alipokuwa waziri wa mabo ya nje alimleta Alafat ktk nchi hii na kuhakikisha anawatukana wayahudi kila mwaka kwa miaka 15. hakututendea haki wakristo na watu wengine tunaowapenda wayahudi kama our spiritual brothers. sasa kama hakujali makundi ya watu wawapendao wayahudi , je atajali makundi mengine ktk jamii yasimlidhissha azma zake? naomba atolewe jinale na asiapishwe.
 
Tango,

Kwani wakristo na wayahudi ni moja?

Mbona nyerere alifukuza Wa israel akakata mahusiano ya ki diplomasia? Hapo utasemaje?
 
hawa watu hata mpirani hawaonekani, kweli wanajua kuishi pamoja na jamii ktk raha na shida? ukiziona shepu zote zilivyo utajua tuu wana kitu kiitwacho social distance na jamii waishio nayo. nani kamuona salimu au warioba akiingia kaunda stadium kuangalia mazoezi ya yanga?

nawahakikishia wenzanguni kuwa, hiyo katiba itakuwa ni katiba ya kujenga somalia enzi za siad bare na sio kujenga tz wakati huu.
 
Tango,

Kwani wakristo na wayahudi ni moja?

Mbona nyerere alifukuza Wa israel akakata mahusiano ya ki diplomasia? Hapo utasemaje?

wakristo wote duniani ni spiritual jews, halafu wayahudi wote ni active jews. hilo swali la nyerere na kuwafukuza wayahudi wewe naomba waulize baraza la maaskofu ambao wanataka kumpatia utakatifu nyerere. maana wanataka kumfanya mtakatifu wa kwanza duniani kuvunja amri ya mungu isemayo," nitampenda yeyote atakayekupenda na kumlaani yeyote atakayekulaani". hiyo ni ahadi ya mungu kwa Abrahamu alipokuwa nampatia ardhi ya kanaani.

sasa nyerere ingawa alikuwa mkristo aliipuuza agano la mungu na abrahamu. Ila mwenzake Kenyatta aliwapuuza waarabu walipomuomba awafukuze wayahudi. ona sasa nani anamtawala mwenzake kiuchumi kati ya Kenya na TZ?
 
Kuna msemo!Waoga hulewa hata soda!Hata wakiteua wapambe,watoto na wake zao,nguvu ya umma itaamua mustakabali mzima wa katiba mpya! Kumjua adui ni nusu ushindi.
 
Back
Top Bottom