Siri kuhusu wajumbe wateule wa tume ya katiba



Pamoja na uhuru wa Rais kuteua kutoka mapendekezo ya makundi, ni sahihi kuhoji kwa nini ateue chaguo la tatu na siyo la kwanza na la pili.

Naelewa tume haina kauli ya mwisho juu ya katiba, lakini wakiishaandika draft na kuacha mengine, inakua vigumu kuyaondoa. Serikali inafanya makosa kujaribu kudhibiti mchakato huu maana hakuna serikali ya milele mahali popote. Katiba ikiwa mbaya wajue itatumika kuwakandamiza wao watakapokuwa wapinzani.

Mkuu wangu, haya ni matokeo ya kukubali CCM iendeshe mchakato wa Katiba Mpya kitu ambacho hakijawahi kuwa ajenda yao wala ilani yao. CDM na wale waliokubali Rais awe na nguvu alizonazo kwa kweli hawana haki ya kulalamika sasa. Ama waamue kushirikie na kupokea kitakacholetwa mezani au wakatae mapema kabla mchakato wenyewe haujaiva. Kwa mfano, kwanini walikubali sheria ambayo Rais anateua hadi mwenyekiti wa tume; kwanini asingeteua hao wajumbe wa tume na wao watakapokutana baada ya kuapishwa ndio wangechagua uongozi wao kutoka miongoni mwao?
 
Wana Jamvi
Mawazo ya Paparazi Muwazi yasipuuzwe. Nimefuatilia na kugundua kuwa wale walioteuliwa kuwakilisha makundi ni wale walioshika nafasi ya tatu na ya nne. Wale waliopendekezwa wakiwa wa kwanza na wa pili wameachwa baada ya TISS kupeleka taarifa kwa JK kuwa waliopendekezwa wakiwa wa kwanza ni "wakali" sana kuhusu sheria ya katiba mpya. Baadhi ya wateule waliitwa na kuonanaW na maofisa wa TISS ama kuwekwa sawa au TISS kujihakikishia juu ya misimamo yao. Ushahidi kuhusu madai haya ni:
-Prof Baregu alipendekezwa akiwa namba tatu - wa kwanza alikuwa na Tundu Lissu akifuatiwa na Prof Safari
-Jesca Mkuchu alikuwa wa tatu kutoka CCT akiwa nyuma ya maaskofu wawili - mmoja wa Mbeya na mwingine wa Tanga, n.k.

Pamoja na uhuru wa Rais kuteua kutoka mapendekezo ya makundi, ni sahihi kuhoji kwa nini ateue chaguo la tatu na siyo la kwanza na la pili.

Naelewa tume haina kauli ya mwisho juu ya katiba, lakini wakiishaandika draft na kuacha mengine, inakua vigumu kuyaondoa. Serikali inafanya makosa kujaribu kudhibiti mchakato huu maana hakuna serikali ya milele mahali popote. Katiba ikiwa mbaya wajue itatumika kuwakandamiza wao watakapokuwa wapinzani.

Unatakuwa kuwa kwenye tume wewe unaakili
 
Kwa kuwa alipendekezwa ANAFAAA, na kama hakufaa basi msingempendekeza! FULL STOP


Kuna Pendekezo No.1,Pendekezo No.2 na No:3,ukiona mtu anaacha no.1 na 2 anarukia 3 hiyo inasema kwamba kuna tatizo kwa huyo anakuja kuchukua mmoja katika waliyopendekezwa,usiniambie kama unaona hamna tatizo hapo!!
 
back to square one!
Hakuna katiba mpya hapa ni mwendo wa kuziba viraka tu.
 
Anayepinga tume hii ni adui mkubwa wa taifa hili pamoja na amani yetu

hata ingeundwa na malaika lazima kuna watu wangetoa maoni ya kuipinga!
Cha mihimu ni kuangalia wanachokipinga ni nini ili kiwe addressed.
Asiyependa kukosolewa ni adui namba moja wa maendeleo ya nchi yetu.
 
jaji mstaafu barbanas samata na prof shivji ni vichwa vilivyowekwa kando hawa wangetupatia katiba bora
 
Tango,

Kwani wakristo na wayahudi ni moja?

Mbona nyerere alifukuza Wa israel akakata mahusiano ya ki diplomasia? Hapo utasemaje?

Ndio maana tumefika hapa tulipo.
Nyerere mwenyewe anakikiri kuwa dhambi ya ubaguzi ni kama kula nyama ya mtu. Ukila nyama ya mtu utaendelea hivyo hivyo!
Wote wanaowachukia waisrael watendelea kubaguana mpaka wao kwa wao.
Huwezi kupinga ubaguzi katika jamii wakati wewe mwenyewe unawabagua wengine.
Kama Salimu anawachukia waisrael hafai kuwa mtetezi wa taifa letu.
 
Watanzania kila kitu mna doubt, sasa mnadhani hii katiba ni ya wananchi au ni ya vyama vya siasa. Kwahiyo mlitaka achaguliwe SLAA ndo mfurahi, lazima mjue kwamba si kila mtu aliyekomboka (conscious person) basi awe CHADEMA

Wakati wa giza umepita. Kila kitu lazima kipimwe na jamii kwa manufaa ya jamii. Mambo ya kufanyia kazi mawazo ya mtu mmoja umepita.
Tunataka uwazi kwenye masuala yanayotuhusu. Katiba ni makataba wetu na watakaotaka tuwape madaraka ya kutuongoza.
Msiwe kama Carl Peters alivyowadanganya wazee wetu zamani kwa mikataba mufilisi.
 
Pamoja na walakini hizo mlizotaja, naomba tuwape nafasi, binafsi nina imani nao; hasa ukizingatia Mhe. Jaji Augustino Ramadhani yupo ndani ya Tume.

Ndugu mtanzania, kumbuka hii nafasi ni nafasi nadra sana katika maisha ya nchi. Tusifanye kama majaribio: Tuifanye kazi hii kwa ufanisi wa hali ya juu ili nchi isiangamie au la tuache kabisa tusipoteze muda na nguvu zetu
 
Mkuu wangu, haya ni matokeo ya kukubali CCM iendeshe mchakato wa Katiba Mpya kitu ambacho hakijawahi kuwa ajenda yao wala ilani yao. CDM na wale waliokubali Rais awe na nguvu alizonazo kwa kweli hawana haki ya kulalamika sasa. Ama waamue kushirikie na kupokea kitakacholetwa mezani au wakatae mapema kabla mchakato wenyewe haujaiva. Kwa mfano, kwanini walikubali sheria ambayo Rais anateua hadi mwenyekiti wa tume; kwanini asingeteua hao wajumbe wa tume na wao watakapokutana baada ya kuapishwa ndio wangechagua uongozi wao kutoka miongoni mwao?

Rais kateua hadi watakaoandika minutes! Kuna siri gani kwenye hili zoezi?
 
Anayepinga tume hii ni adui mkubwa wa taifa hili pamoja na amani yetu

Bila shaka wewe unaongea kwa niaba ya CCM au una uhakika utanufaika na tume hii.
Sisi tusio na uhakika huu lazima tujiulize kwa nini hamkuchukua mapendekezo vipaombele vyake?
 
Usiangalie majina makubwa manne, pitia mjumbe mmoja baada ya mwingine utaona vituko. Niende kwa huyu Richard Lyimo, huyu ndiye ambaye kwa miaka mingi amekuwa akitumiwa na usalama wa taifa na kundi la propaganda la CCM pale TLP dhidi ya upinzani.

Mwaka 2008 wakati huo nikiwa habari Corporation kuliletwa kazi maalum akakabidhiwa Balille ya kukutana na Bwana Lyimo ikapikwa hadithi ya Mbowe kushangilia kifo cha Chacha Wangwe kule Afrika Kusini. Kwa jinsi tulivyokutana na huyu bwana ni mtu asiye na msimamo wowote akilipwa aseme au afanye chochote kwake ni jambo la kawaida. Ndio taifa itabidi limtegemee kwenye kuandaa rasimu ya katiba.

Miezi michache iliyopita kwenye ukumbi wa idara ya habari maelezo alifanya kituko cha mwaka dhidi ya bwana Tao, pale alipokuja na mwenzake mmoja simfahmu jina, wakataka wanahabari tumpe karatasi tulizokuwa nazo za press release kwamba zina makosa atupe zingine. Akatupa taarifa iliyoghushiwa kuhusu Tao na Mrema.

Kuna mtu anamfahamu zaidi bwana Lyimo? Nitawaletea siri za wajumbe wengine ninaowafahamu.

PM

Badala ya kuendekeza majungu andika barua haraka kwa Mh.Rais mueleze mabaya ya wajumbe unaowatuhumu kabla hawajaapishwa.vinginevyo unapoteza muda.Wewe unayo mabaya badala ya kutuma kunako husika unapiga miruzi na unaahidi utaleta na ya wengine.Huoni kama unapoteza muda
 
Wana Jamvi
Mawazo ya Paparazi Muwazi yasipuuzwe. Nimefuatilia na kugundua kuwa wale walioteuliwa kuwakilisha makundi ni wale walioshika nafasi ya tatu na ya nne. Wale waliopendekezwa wakiwa wa kwanza na wa pili wameachwa baada ya TISS kupeleka taarifa kwa JK kuwa waliopendekezwa wakiwa wa kwanza ni "wakali" sana kuhusu sheria ya katiba mpya. Baadhi ya wateule waliitwa na kuonana na maofisa wa TISS ama kuwekwa sawa au TISS kujihakikishia juu ya misimamo yao. Ushahidi kuhusu madai haya ni:
-Prof Baregu alipendekezwa akiwa namba tatu - wa kwanza alikuwa na Tundu Lissu akifuatiwa na Prof Safari
-Jesca Mkuchu alikuwa wa tatu kutoka CCT akiwa nyuma ya maaskofu wawili - mmoja wa Mbeya na mwingine wa Tanga, n.k.

Pamoja na uhuru wa Rais kuteua kutoka mapendekezo ya makundi, ni sahihi kuhoji kwa nini ateue chaguo la tatu na siyo la kwanza na la pili.

Naelewa tume haina kauli ya mwisho juu ya katiba, lakini wakiishaandika draft na kuacha mengine, inakua vigumu kuyaondoa. Serikali inafanya makosa kujaribu kudhibiti mchakato huu maana hakuna serikali ya milele mahali popote. Katiba ikiwa mbaya wajue itatumika kuwakandamiza wao watakapokuwa wapinzani.

kama inaanza kuingia akilini sasa, lakini kwa chadema walipeleka mapenekezo ya majembe tupu. kila jina lilikuwa la moto. tundu lisu wamefanya vyema kumuacha ili awashughulikie vizuri bungeni, naona ingekuwa vyema zaidi kama wangemuweka prof, safari ila baregu nae sio mtu wa kawaida kama walizani sio moto ngoja waone
 
Back
Top Bottom