Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Akipokelewa mkoani Dar es Salaam kama Katibu Mwenezi na Itikadi wa CC, Paul Makonda amesema kazi ya CCM ni kusikiliza kuwa sikio la Serikali na kusema kuwa Sauti ya Wananchi
Amesema "Naomba nitumie fursa hii kutuma salamu kwa Mawaziri wote, Wakuu wa mikoa, na kwa Watendaji wote ya kwamba pale patakapobainika hamjafanya kazi yenu kwa ukamilifu, chama hakitasita kuchukua hatua"
"Bahati nzuri tunafahamiana, sitakuwa tayari kuwa Msemaji wa chama ambacho kimepewa dhamana na Wananchi na wanaomsaidia Mwenyikiti, nisimame hadharani kusema uongo, hapana!."
"Kila Kiongozi wa Serikali atabeba msalaba wake mwenyewe, sijahifadhiwa miaka mitatau na miezi mitatu kusema uongo, sijateuliwa na CCM kusema uongo na katika kiapo chetu kipo wazi, fitna, uongo na uzushi si sehemu ya CCM"
"Chama kimepewa dhamana na Wnanchi na kikaamini kwa kuunda Serikali, ni hakika Kiongozi yeyote atakayebainika na chama kikajiridhisha, kiongozi yeyote atakaye zembea chama kitachua hatua bila kusubiri kwa sababu ni wajibu wetu kukilinda, kukitea na kukipigania"
TAIFA HALINA UPINZANI
Aidha, amesema kuwa Tanzania hakuna Upinzani, yaani hakuna chama cha upinzani bali watoa taarifa walijikusanya kwa jina la vyama
"Ukimwona Tundu Lissu anaongea sio Chama ni mtu tu anatoa taarifa na wakati mwingine taarifa anayotoa inaweza kutoka kwenye chanzo ambacho si cha kweli au uhakika, lakini kwa sababu ni taarifa kazi ya chama chetu ni kusikiliza zile taarifa na badala ya kushughulika na mtoa taarifa tutashughulika na aliyesababisha taarifa kutoka"
"Naomba kusema kuanzia leo tarehe 26.10.2023 Taifa hili halina vyama vya upinzani bali kuna vyama vya watoa taarifa na sisi tutafanyia kazi taarifa zao maana ni chachu za maendeleo"
Amesema "Naomba nitumie fursa hii kutuma salamu kwa Mawaziri wote, Wakuu wa mikoa, na kwa Watendaji wote ya kwamba pale patakapobainika hamjafanya kazi yenu kwa ukamilifu, chama hakitasita kuchukua hatua"
"Bahati nzuri tunafahamiana, sitakuwa tayari kuwa Msemaji wa chama ambacho kimepewa dhamana na Wananchi na wanaomsaidia Mwenyikiti, nisimame hadharani kusema uongo, hapana!."
"Kila Kiongozi wa Serikali atabeba msalaba wake mwenyewe, sijahifadhiwa miaka mitatau na miezi mitatu kusema uongo, sijateuliwa na CCM kusema uongo na katika kiapo chetu kipo wazi, fitna, uongo na uzushi si sehemu ya CCM"
"Chama kimepewa dhamana na Wnanchi na kikaamini kwa kuunda Serikali, ni hakika Kiongozi yeyote atakayebainika na chama kikajiridhisha, kiongozi yeyote atakaye zembea chama kitachua hatua bila kusubiri kwa sababu ni wajibu wetu kukilinda, kukitea na kukipigania"
TAIFA HALINA UPINZANI
Aidha, amesema kuwa Tanzania hakuna Upinzani, yaani hakuna chama cha upinzani bali watoa taarifa walijikusanya kwa jina la vyama
"Ukimwona Tundu Lissu anaongea sio Chama ni mtu tu anatoa taarifa na wakati mwingine taarifa anayotoa inaweza kutoka kwenye chanzo ambacho si cha kweli au uhakika, lakini kwa sababu ni taarifa kazi ya chama chetu ni kusikiliza zile taarifa na badala ya kushughulika na mtoa taarifa tutashughulika na aliyesababisha taarifa kutoka"
"Naomba kusema kuanzia leo tarehe 26.10.2023 Taifa hili halina vyama vya upinzani bali kuna vyama vya watoa taarifa na sisi tutafanyia kazi taarifa zao maana ni chachu za maendeleo"