moneytalk
JF-Expert Member
- Jan 23, 2017
- 7,700
- 16,417
harakati za utafutaji dear zinaniweka bizeulipotea hadi nkawa na waswas
harakati za utafutaji dear zinaniweka bizeulipotea hadi nkawa na waswas
ok poa poaharakati za utafutaji dear zinaniweka bize
Mkuu shukrani,Leta vitu mzee babaSEHEMU YA NANE
Oyaa bro naomba nifungulie geti nitoke . Nilimlazisha mlinzi.
Aaah kaka, huu usumbufu sasa, wapi unaenda, ila nimejua kumbe kweli ulitaka kumbaka yule mwanamkeee, we jamaa kumbe fala eeh, yaani wanawake wooote waliojaa miaka hii unalazimisha mapenzi halafu ulivyo na nilichosikia hata haviendani.
aliongea yule mlinzi huku akinimulika na tochi yake usoni.
Hebu usinimulike bwana, hebu fungua geti na aliyekwambia nilikuwa namfuata mwanamke hapa ni nani, fanya habari zako, wewe kazi yako ni kufungua na kufunga geti acha upuuzi. nilitoa gari huku mlinzi akiendelea kunirushia maneno.
Kwahiyo kupewa na kuendesha magari ya serikali unajiona nani sijui, unafikia hatua ya kudhani Kila mtu atakupenda kisa gari, wewe ni mjinga tu lione kwanza. alikuwa ni dada wa mapokezi akiungana na mlinzi wakinitukana. hakika ilikuwa ni fedheha ya aina yake.
Nilitafuta gesti nyingine huku nikiwaza alichonifanyia yule mwanamke, hakika alikuwa kaniweza sana na sikutegemea kabisa.
Asubuhi na mapema niliamka na kuoga vizuri kisha nikawasha chombo na kuingia njia kuu huku nikiwa high speed lengo niwahishe gari ofisini.
Nikiwa njiani niliwaza sana,
Dah kiufupi heshima yangu imeshuka kwa nilichokuwa nataka kufanya Jana Sasa kwanini nilifanya vile dah kweli shetani ana nguvu sana.
Hivi kwa mfano yule mwanamke akanisimulia mumewe kuwa nilikuwa nataka kulazimisha penzi yule jamaa atanionaje halafu wanadai wote ni maaskari na Wana namba yangu, loh najuta kutoa namba, lakiniiiiiiii si rahisi mwanamke kusimulia kwa mumewe hizi habari labda kama hana akili timamu. nilijiuliza maswali na kujijibu mwenyewe.
Halafu umri wangu, cheo changu wala sipaswi kufanya mambo haya yaani kifupi jana nimechemka.nilijilaumu Kisha nikachungulia pembeni yangu kwenye siti ya abiria nikaona mfuko wa samaki pia nikauona mtandio wa yule mwanamke kumbe wakati anashuka Jana kwa pupa alijikuta anasahau vitu vyake.
Loh afadhali nimeona hivi vitu Sasa ndiyo mke wangu anauona huu mtandio itakuwaje na vile alivyo mbona nyumba itaharibika. nilichukua simu nikapiga namba ya yule mwanamke ikaita sana tu bila kupokelewa. nikaamua kuachana nayo huyooo nazidi kusogea , nilijua ndani ya masaa mawili nitakuwa Dar es salaam, baadaye simu iliita alikuwa ni mke wangu.
Tukasalimiana,
Enhee vipi jana watu tumekesha tukikusubiri nikijua atarudi, lakini haikuwa hivyo vipi kuna shida gani mume wangu. aliuliza
Wee acha tu mke wangu gari liliharibika likaja kupona usiku sana, hivyo nikaona siwezi kuendesha chombo ambacho Sina uhakika nacho kama kimetengamaa nikaamua nilale ila ndani ya muda mfupi nitafika hapo. Nilimjibu.
Haya pole na matatizo na nakuombea ufike salama, lakini Mimi nitatoka kidogo naenda kukutana na akina mama wenzangu si unajua tena kampeni zimepamba moto. na pia Mimi ni mmoja wa viongozi hivyo sipaswi kukosa. alisema huku akisikiliza nitasemaje.
Lakini mke wangu si nimekuwa nikikukataza hayo mambo ya vyama, hizo mambo kwanza huwa zinajenga matabaka mnajikuta mnachukiana bila sababu na watu, na pili sitaki mtu yeyote aijue familia yangu ipo chama gani, Sasa wewe kwenda huko pia mkapeana na uongozi yaani unanishangaza mno. niliweka kituo.
Mume wangu huwa nakushangaa sana tena sana tu, Kuna misimamo mingine sidhani kama ina ulazima sana, nakujua kuwa wewe huna kipaji cha siasa na pia na ndiyo maana umeshindwa ndani ya muda mfupi, lakini kila mtu ana kile ambacho ana interest nacho, na pia ni sehemu ambako unapanua wigo wa kufahamiana na watu kwani unadhani muda wote tutajadili jambo moja , Kuna watu tunakutana nao wenye ujuzi wa vitu mbalimbali, kilimo, biashara Kuna ufugaji na mambo mengi. Sasa mtazamo wako Mume wangu unanitisha.
Unadai hutaki matabaka na watu wasijue kwamba wewe upo upande gani,lakini tambua kuwa familia yetu ni ya kikristo, je wewe huelewani na watu?
Si unafanya nao kazi na watu wa Dini na madhehebu mbalimbali, kwa mara ya kwanza ulikuwa unafanya kazi ya umakenika kwa waarabu, je wale wengi wao si unajua Dini yao.
Huko uliko Sasa kwenye ajira yako boss wako ni wa Dini yako?
Mbona wewe hapa nyumbani unapenda mpira kuliko kawaida na hakuna anayekughasi, ungependa kiushabiki nisingesema lakini ulitoa pesa nyingi sana kwenye timu ya hapa mtaani kwetu, je ulipata faida gani? ile pesa ungefanyia mambo mengine si ungekuwa mbali?
Je nilikulaumu? si nilikushauri tu kuwa ni vyema kufanya tafiti za kutosha kabla ya kuanzisha mambo yako.
Hela zenyewe huna, inafikia hatua unapaki gari lako kwa kukosekana hela ya matengenezo ambayo ni kiasi Cha kawaida tu. ila nisiongee mengi si unarudi ninachokuomba ni ruhusa yako tu sitaki kwenda sehemu Ukiwa haupo radhi. aliweka kituo akiwa kanisimanga .
Haya wewe nenda ila zingatia muda na pia naomba heshima iwepo, mambo ya kupeana lift na watu nisiowajua sipendi na yule shoga yako mnene naye sihitaji mazoea ya kujakuja kwangu hapo najua huyo ndiye kakuvuta uende huko Sasa sitaki awe anakuja hapo kwangu kama siku ile. nilitahadharisha nikakata simu.
Baada ya muda niliona sms kutoka kwa mwanamke niliyekuwa naye Jana, akitaka nimpigie.
Nikapiga huku nikiwa na hasira nikipanga nimchane.
Niliangalia mfuko wake wa samaki nikaangalia na ule mtandio Kisha nikaguna kidogo huku nikiwa namsifu mbinu aliyotumia kwani alianza kwa kujilegeza kumbe kashapanga ni namna gani atanikataa. Huyu mwanamke loh simuwezi.
Akapokea simu na kunieleza kuwa yupo kwenye gari la abiria Coaster na nimewapita muda si mrefu ndiyo maana akanipigia ili nimsubiri achukue mizigo yake.
Nikaweka Chuma pembeni kisha nikashuka, nikaangalia saa ni saa moja kasoro. Huku coaster fulani ikiwa inapaki karibu yangu akashuka yule mwanamke huku konda akija kwa pupa kwenye gari yangu.
Oyaa sorry bro huyu dada anasema ana mizigo yake humu kwenye gari lako hebu nipe tuondoke maana tunakimbizana Kuna mchawi anakuja sitaki anikute hapa.
Itaendelea...............................
Unajitafutia kipigo tu kutoka kwa askariSEHEMU YA SABA
Gari ilisereka kidogo huku ikihama njia kabisa, Kisha nikatulia huku ng'ombe wengi sana wakipita, kulikuwa watu zaidi ya kumi na tano jamii ya wamang'ati wakiwa wanaume kwa wanawake huku wakionesha wanahama.
Sasa shemu Hawa watakuwa wanaenda wapi usiku huu, jamani tena wana watoto mgongoni, kwanini watembee usiku? yule mwanamke aliongea kwa mshangao sana.
Baada ya kuwa ng'ombe wamepita nilikanyaga mafuta huku nikiongeza speed tofauti na mwanzo, nafikiri yule mwanamke alikuwa ana hofu sana juu ya uendeshaji wangu lakini hakuwa na namna hangeweza kuniambia chochote.
Nadhani zile beer nne zilishachukua nafasi fulani kichwani nikakuta naanza kumtamani yule mwanamke, nikapanga lazima nitafute sababu yeyote ile ili tulale na najua naweza kufanya chochote na asinipinge nilijiamini sana.
Heeeeh shemu ina maana tushakaribia daraja la mkapa, umetembeaaaa, alisema yule mwanamke huku mwanga wa gari linalokuja mbele yetu likiwa Ukiwa unamtesa sana.
Yaani kuna watu sijui walisomea wapi udereva yaani anawasha taa namna hiyo tena tupo katikati ya daraja, namuashiria apunguze mwanga hataki,haya ni madhara ya kujulia gari mtaani kisha kupata leseni kwa njia ya magumashi hawa ndiyo wanaosababisha ajali kila kukicha. nililaumu .
Akili yangu juu ya yule mwanamke ilikuwa palepale lakini na ugumu nao ulikuwepo hivyo niliona siwezi kumuacha hivihivi ikabidi nianze kutafuta visingizio.
Yaani gari hili shemu silielewi kabisa , yaani breki inashika kwa mbali sana na muda mwingine nakanyaga hamna kitu kabisa na usiku huu tena sijui itakuwaje, afadhali ingekuwa mchana ningekokota hivihivi lakini usiku huu hapana. Yaani hizi gari za kupokezana mara aendeshe huyu mara yule ni shida sana. nilijifanya gari ni mbovu.
MUNGU wangu sasa itakuwaje shemu maana, mbona nitakuja kugawanywa vipande masikini mimi, shemu huwezi simama popote ili wakuangalizie nini tatizo?
alihoji yule mwanamke.
Hilo hakiwezekani shemu, kwanza kwenye vijiji hivi vya njiani hakuna mafundi wala gereji za kueleweka, hivyo unaweza Kuta unazidi kuipa matatizo zaidi gari ya watu. vyombo vya serikali hivi huwezi kubumba bumba ujuavyo wewe. nilizidi kujitengenezea mazingira.
Ndani ya muda mfupi tulikuwa Ikwiriri, nikapaki gari pembeni huku nikishuka,
Shemu twende tukapate chochote kitu basi, maana mimi naona tumbo halina kitu nilimsihi.
Shemu yaani acha tu hapa nilipo sina hata njaa, siisikii kabisaaa, naona kama nimechanganyikiwa tu, yaani hii siku ya leo nitasimulia jamani.
aliongea kwa uchungu huku akiwa kama vile kagundua Nia yangu ila akashuka kwenye gari na kuiegamia.
Niliingia bar ya pale njiani wanapaita Kivulini, nikaketi na kuulizia Chakula nikaletewa nikapiga huku nikimuona vizuri sana yule mwanamke ambapo simu ilikuwa sikioni akionekana anapiga huku na huko , alionekana mwenye haraka sana na hakupenda kitendo cha mimi kusimama pale ila hakuwa na namna.
Ubishani ulioendelea pale Kivulini bar kuhusu Mgombea wa ubunge wa Jimbo la Rufiji ambaye alikuwa chama tawala huku wakidai hawamfahamu na si mzaliwa wa pale, ule mjadala ulinivutia sana nikatamani kujua japo A B C kadhaa, hivyo nikajisogeza kumsikiliza jamaa mmoja ambaye alikuwa anawashawishi wenzake kuwa wasije wakampa kura hata moja
Simu yangu iliita , kuangalia namba ni yule mwanamke ambaye tulipeana namba kwaniaba ya kwenda kumchekia mifugo yake,
Hello shemu, samahani lakini nilikuwa naomba uniruhusu niondoke kwasababu ninatakiwa nifike leo hii hii sitakiwi kulala njiani kabisa, naziona Coaster zinazofika mpaka Mbagala rangi tatu hivyo , nakushukuru kwa msaada wako . aliweka kituo akiwa ananipa nafasi labda niongee chochote lakini nilikata simu.
Huyu demu vipi naye, anawahi wapi?
Saa tatu hii si bora tulale tu ,
Nilimuita muhudumu nipewe bia yangu ili nishushie na Chakula nilichokula, huku nikisikia simu inaita kwa mara nyingine, kuangalia mpigaji ni yeye lakini sikupokea lengo nimcheleweshe ili tulale wote.nilijua asingeondoka kwani begi lake lilikuwa kwenye gari.
Nilimaliza bia kwenye glass Kisha nikaingia msalani, Kisha nikaenda kwenye gari huku nikiacha bia nyingine ikiwa haijafunguliwa nikakuta mwanamke kabadilika sana, uso wake haukuwa na masikhara hata kidogo.
Samahani kaka yangu naomba nipe begi langu siwezi kukaa kama vile yatima aliyefiwa na wazazi wote wawili naomba niondoke bwana, yaani unanifanyia visa kibao mara gari haina breki mara sijui kitu gani halafu unashuka unastarehe tu, wewe ni mwanaume unaweza kujiamulia mambo mengi, lakini Mimi ni mke wa mtu nipo kwenye himaya na miliki ya mtu hivyo naomba tuheshimiane. aliongea huku akiwa serious na sauti ya juu huku akionesha amechukia.
Hapana Shemu usiseme hivyo, lakini kwani Kuna ulazima wa wewe kufika leo, kesho alfajiri tutajihimu shemeji yangu, Mimi nipo na chombo Cha watu ambacho nina tahadhari nacho,nikipata ajali usiku huu itakuwaje? Vitu vingine vinazuilika shemu. hebu twende ukale kabisa shemu usijisikie vibaya bwana. nilimwambia lakini hakuwa tayari alikataa katakata huku akiomba nimpatie begi lake.
Nilikuja nikamalizia bia huku nikimuona, anaongea na wanaume watatu ambao sikujua wamefikaje pale labda kwakuwa nilikuwa tungi,
Kisha baada ya kumalizana na wale jamaa ambapo sikujua wameongea nini, akawa anakuja usawa nilipo akaingia , huku akikaa meza nyingine akionesha ana mawazo sana. wakati huo mimi moyo ulidunda kwa furaha maana dhamira yangu ilikuwa inakwenda kutimia , aliagiza chipsi kavu na soda tu, Kisha alipomaliza akaja kwangu kwa mwendo wa madaha kabisa , mwanamke mrefu sura isiyokuwa na makeup, huku akiwa kavaa tisheti nyeupe na suruali nyeusi iliyomkaa vyema sana huku akiwa kavaa raba fulani za kike nzuri sana, akiwa kajifunga kanga yake kiunoni.
Ahsante sana Kwa chakula shemu , aliongea huku akiwa kasimama pembeni yangu , huku nikimkung'uta vumbi vumbi lililonasa kwenye nguo zake, hakika nilienjoy maana nilimshika popote huku akiwa haoneshi kuchukia, alitabasamu tu, laiti ningejua mawazo yake.ama kweli mjinga hajijui.
Sasa vipi si tunalala shemu, niliuliza kwa sauti ya kilevi .
Hakuna shida shemu wewe si umesema si vizuri kutembea usiku, hivyo nimeridhia kulala, na pia nishaulizia na lodge nimeambia ipo ambako Kuna parking za magari na pia ni self hivyo nahisi ni pazuri twende huko.
Aliongea kwa kudeka huku akichochea hisia zangu, nilimaliza bia kwa pupa huku tamaa ya ngono ikishika nafasi yake.
Niliendesha gari huku nikiwa naulizia kwa watu ambalo walionesha kuwa ni paleeee kwenye taa za kuzunguka , baada ya kufika alishuka haraka sana kwenye gari.
Shemu paki gari vizuri, Mimi ngoja nikachukue chumba , aliongea Kisha nikamuona anaelekea mapokezi,
Mlinzi alinielekeza sehemu ya kupaki huku akiniuliza kama nitatoka asubuhi sana basi nipaki karibu na geti na gari iangalie nje.huku nikimshangaa yule mlinzi anavyonichelewesha kila napopark anasema siyo, hali ile ikafanya nichelewe kidogo,
Kisha kwa mbwembwe na tembea ya kilevi nikaenda mapokezi, huku nikivuta picha yule mwanamke ambavyo atakuwa kashabadilika huko chumbani.
Kuna mwanamke kaingia siyo muda hapa kavaa (nikiwaambia alivyovaa)
Ndiyo kaingia kwani unamuitaje, aliuliza yule dada wa mapokezi.
Ni mke wangu yule,. nilidanganya
Weee acha uongo yule siyo mkeo na katuambia Kila kitu na Kuna watu walikuja kumchukulia chumba hapa,
na anadai wewe unataka kulala naye wakati yeye hayupo tayari, hivyo uchukue chumba chako ulale au uondoke, na ukilala hapa hatutaki fujo , tutapiga simu polisi. aliongea yule dada wa mapokezi huku nikishangaa sana , Kisha nikapiga namba ya yule mwanamke ikawa haipatikani. nilichukia sana na pombe zikakata
Itaendelea.......................
Shughuli inaanza,jamaa angalia usijeitwa mhujumu uchumi,kesi nzito na Yule polisi uliyetaka kumhujumu ,mhhhhhhh!!SEHEMU YA KUMI NA MOJA
Nashindwa kuelewa maelezo yako vizuri, sijui una maana gani. nilijifanya sijui chochote.
Aaaah nimestuka kidogo kaka kwasababu mimi nilitegemea utaingia jana, Dar es salaam lakini hata mke wangu alinihakikishia kuwa amefika ndiyo maana kanichanganya sana. aliongea kwa upole sana.
Mimi nadhani ni vema umuulize mkeo binafsi Sina majibu ya kukupa , ila nikuhakikishie tu kama mwanaume mwenzangu kuwa uwe na amani tu. nilimjibu huku simu ikiwa hewani bado na nikawa nasikia mabishano fulani, nikawa na hofu sana.
Watu wengine bwana wivu tu hadi lini ndiyo hawa huwa wanaishi maisha ya taabu kwa kuwaweka watu vifuani mwao, mtu mzima uliyekutana naye ukubwani unawezaje kumchunga , kama siyo uwendawazimu ni nini.
Maisha, ndoa na mahusiano ya sasa hayahitaji nguvu badala yake ni heshima baina ya watu wawili. Kila mtu atambue wajibu na nafasi yake katika familia, sasa kuna mijitu inaendekeza wivuuu, ah atakuwa mshamba tu yule.watu tuacha wake zetu miezi ,angekuwa yeye angeweza.niliwaza sana
Jioni sana mke wangu alirudi akiwa kapendeza sana akiwa ndani ya sare ya chama (jina kapuni) tulisalimiana juujuu huku akiwa na furaha fulani hivi nadhani yanayoendelea kwa wakati huo yalimpa hiyo hali haswa ukizingatia wanawake wengi huingia kwenye masuala mengi kwa miguu miwili.wakati sikutaka kwenda ndani mapema nilikuwa nje nikipunguza punguza majani huku akili yangu ikiwa si nzuri kutokana na jamaa alivyokuwa na hisia mbaya na ukweli alikuwa sahihi.
Hapa ipo siku nitapata matatizo na wanasema mwisho wa ubaya ni aibu, ukweli ni kama MUNGU anataka kunionesha ni njia ipi napaswa kuishika , hakukuwa na sababu ya kulala njiani jana, kwakweli nastahili kulaumiwa. nilijiwazia hiki nikiwa na panga kupunguza majani ya mti fulani ndani mwangu.
Naambiwa karudi lakini naingia ndani sikuoni kumbe upo huku, habari za siku mbili tatu na pole kwa matatizo ya hapa na pale. aliongea mke wangu huku akinisaidia kukusanya yale majani sehemu moja .
Mke wangu acha tu nilikoenda mazingira ni magumu sana kufanya kazi, pia gari likawa linasumbua
sana hivyo mambo yakawa magumu ili nilijitahidi kukamilisha kwa wakati, kimbembe wakati wa kurudi ilikuwa ni shida sana, hakuna usafiri wa uhakika uhakika ni hadi nilipoletewa
gari baada ya kufika barabara kuu. nilimjibu.
Poleee, ila ahsante kwa kutuletea samaki japo wanatoa harufu, sijui tunakulaje, sidanganyi nadhani wamekaa muda mrefu sana. aliongea huku akionesha hawataki wale samaki.
Hebu kama nyie hamtakula mnipikie mimi, ila msitupe nimenunua bei ghali sana tafadhalini bwana, niliongea kama utani lakini nikimaanisha.
Hakuna anayetupa na wote watakula ila mimi hapana, halafu mume wangu huwa unapenda sana kuvaa kapelo , zipo nimekuletea.niwaambie wakuletee uzijaribu? aliongea huku akitabasamu.
Zilete wewe mwenyewe unajua jinsi navyopenda , lakini baada ya kuziona tu kwa mbali nikamwambia dada wa kazi azirudishe ndani kwani huwa sivai vitu vile. niliongea huku tukicheka na mke wangu.
Unajua nini mke wangu hizo watu wengi huvaa kwenye matatizo, Ukiwa huna hela ya hospital unavaa hizo huku ukienda kuomba matibabu ya bure
Au mtaani kwenu kukiwa hakuna maji, umeme na miundombinu mingine unavaa hizo kofia au zile fulana mbele ya wenye mamlaka na mambo hayo ili tu kuwakumbusha madai yenu.lakini hivi hivi hapa licha ya kuwa ni shabiki wa timu X hapa nyumbani lakini ulishawahi kuona nina jezi yeyote? nipo radhi ninunue Kisha nimpe mtu lakini si kuvaa hadharani nilifafanua.
Yaani baba Jack kuna vitu vingine wala huwa kuweka misimamo sana tambua maisha ni hayahaya , usijibane sana utakuja kuugua magonjwa yasiyo yako kwani moyo unapotaka kitu na wewe akili yako inakataa basi kuna vitu unavitengeneza vinaweza kjkugharimu baadaye. alifafanua mke wangu Kisha simu yangu ikaita ni yule mke wa jamaa pot alipiga.
lakini mke wangu alitoka na kuingia ndani hivyo ikawa rahisi Mimi kuongea,
Nilitoka nje ya fence kwa tahadhari huku nikiangalia kulia na kushoto maana sometimes watu wanaweza kupeleleza wakapajua Hadi kwako teknolojia imekuwa juu sana.
Nilipokea Kisha nikawa naisikilizia ni sauti ya nani,
hello shemu samahani kwanza nikupongeze kwa jibu fupi ulilompa Mr, kuwa aniulize mwenyewe hapo angalau alishusha presha, nikushukuru sana. aliweka kituo
Sikuongea chochote ila nikamwambia asipige tena simu na ikiwezekana afute namba yangu kwakuwa hakuna umuhimu wa kuwasiliana na Mimi lakini pia niliona isije ikawa ni mtego saa nyingine wapo wote wananisikiliza.
nilitafuta sehemu ya block basi nikaipiga tofali ile namba ya yule mwanamke.
Maisha yaliendelea vizuri , siku zilikimbia huku serikali mpya ikiingia madarakani , malalamiko ya mtaani yaliongezeka lakini siye wengine hatukulalamika kwani hakuna kilichokuwa kimeongezeka wala kupungua kama ni maisha haya ya dollars kadhaa kwa siku basi ni Yale tunayoishi siku zote.wiki.
Siku zilikimbia huku nikiwaza mambo mengi maana nilihisi kadri siku zinavyokwenda mambo mengi yanaongezeka huku nikihisi napitwa na vitu vingi na siendani na muda.
Basi katika harakati za kutafuta maisha na kujiongezea kipato Kuna jamaa yangu alinishauri kuwa kuna biashara ya madini, ambapo soko lake lipo na mtu anayenunua yupo hapa hapa mjini.
Niliona ni dili zuri hasa ukizingatia nishapiga madili kibao na nilifanikiwa kwa kadri ya nilichowekeza. hivyo nikaona ni muda wa kukutana naye huyu jamaa , kesho nilitoka kazini Kisha tukaonana kama tulivyopanga.
Dani hii ishu inalipa , na hii ishu si kwamba wewe unaenda kuchimba au nini maana ile ni kama kamari kuweka vijana kuwahudumia, Chakula, na mambo kibao mwisho wa siku unakuta umetumia gharama nyingi kuliko unachopata , au usipate
Kabisa, kuna jamaa yangu alienda mwaka fulani kwenye machimbo ya dhahabu, alitumia zaidi ya million hamsini lakini hakupata kitu yaani Kila akichimba hakuupata ule mwamba jike. aliokusudia hapo gold mine ditector ilikuwa inasoma lakini mwamba ulikuwa dume.
Sasa nilichokuitia ni kwamba sisi tutakuwa tunanunua kwa wachimbaji wadogo Kisha tunampelekea tajiri ambaye yupo hapa hapa mjini. alifafanua mshikaji wangu aliyeitwa Jastini au Jax kama alivyopenda kuitwa.
Lakini Jax eeh, hii ishu kwanza nimeipenda na ningependa kujua, vibali vyake vikoje na unavipataje, pia unaweza kuanza na mtaji wa bei gani, lakini pia mimi si mtaalamu wa mambo ya madini, na huwa nasikia kuwa Kuna fake na original japo kwa jicho la kawaida unaweza kuona yanafanana. lakini pia wewe nakujua a_z kazi yako na mengine mengi, hizi mambo wewe umeziuaje?maana Sina uhakika kama wewe ni mtaalamu wa masuala haya
niliuliza.
Na ndiyo maana tupo hapa, akaingia kwenye gari yake na kutoa makaratasi fulani Kisha akaleta pale tulipo huku nikiyapitiapitia.kujiridhisha
Itaendelea...........................
Weka mkuu,akiendeleza nishtue