Salaam, Shalom!
Siku moja nilitoka nyumbani kwangu nilipanga kwenda mjini kununua baadhi ya mahitaji muhimu ya vifaa vya umeme,
Niliondoka nyumbani majira ya saa tisa hivi, baada ya nusu saa, nilifika mjini, Sasa Pana duka la vifaa vya umeme kubwa nililokuwa nikitumia kununua mahitaji yangu hapo mjini muda mrefu uliopita, nikiwa natembea nikasema, niende duka lile nikapate mahitaji yangu na kuokoa muda.
Nikapaki gari yangu pembeni kidogo ya sehemu lilipokuwapo duka lile, Nilishuka na kutembea kulikaribia duka lile.
Kilichonishangaza, nikakuta mazingira tofauti kabisa, nje Kuna huduma za chakula watu walionekana wanakula na kunywa Kwa furaha.
Nilikuta duka lile limeongezeka ukubwa na kuongewza urefu, nje alikaa afisa wa ulinzi smart, palifungwa camera za USALAMA, ofisi ilinakshiwa kisasa zaidi. Ndani palikuwa na wazungu kadhaa na wafanyakazi waliovalia mavazi nadhifu.
Nikavutiwa kuingia ndani ya ofisi hiyo kujua nini kinaendelea humo, pia nilitaka kujua muuza electronics alihamia wapi,
Kuingia ndani ya ofisi hiyo, nikakuta watu wenye Rika mbalimbali watanashati, wengi walikuwa vijana na wanawake Wachache,
Mle ndani palikuwa na utulivu wa kutosha, AC Kila Kona, kila mtu alikuwa ameshika kalamu na karatasi na alionekana kumakinika na kusoma kilicho kwenye karatasi,
Nikawaza hiki ni nini watu Hawa wanafanya, niliwaza, yaezakuwa wanafanya labda mtihani hivi, niliwaheshimu sana, nilipoona hali Ile, nami nikalazimika kusogea pembeni alipokuwa askari yule wa USALAMA na kuuliza watu wale wanafanya nini, na ofisi Ile inajishughulisha na nini,
Mlinzi yule alinijibu kuwa pale ni ofisi za BETTING, watu wanachukua mikeka kutabiri timu za mpira wa miguu.
Sura yangu ilifura ghafula, nilitoka haraka ndani ya ofisi Ile nikijilaumu kupoteza muda wangu kuingia ofisi ya ulaghai Kwa nguvukazi yetu ya Taifa inayowateka vijana kuamini kuwa maisha yaezapatikana Kwa Bahati nasibu.
OMBI: Atokee kiongozi mmoja mkorofi aina ya Magu, afute Ujinga huu unaopoteza nguvu KAZI ya Taifa.
Haiwezekani mchina anapokea coin Kwa wanafunzi wa shule za msingi mtaani Ili wabet, Taifa tunalipeleka wapi?
Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo Tanzania 🇹🇿.
Amen.
Siku moja nilitoka nyumbani kwangu nilipanga kwenda mjini kununua baadhi ya mahitaji muhimu ya vifaa vya umeme,
Niliondoka nyumbani majira ya saa tisa hivi, baada ya nusu saa, nilifika mjini, Sasa Pana duka la vifaa vya umeme kubwa nililokuwa nikitumia kununua mahitaji yangu hapo mjini muda mrefu uliopita, nikiwa natembea nikasema, niende duka lile nikapate mahitaji yangu na kuokoa muda.
Nikapaki gari yangu pembeni kidogo ya sehemu lilipokuwapo duka lile, Nilishuka na kutembea kulikaribia duka lile.
Kilichonishangaza, nikakuta mazingira tofauti kabisa, nje Kuna huduma za chakula watu walionekana wanakula na kunywa Kwa furaha.
Nilikuta duka lile limeongezeka ukubwa na kuongewza urefu, nje alikaa afisa wa ulinzi smart, palifungwa camera za USALAMA, ofisi ilinakshiwa kisasa zaidi. Ndani palikuwa na wazungu kadhaa na wafanyakazi waliovalia mavazi nadhifu.
Nikavutiwa kuingia ndani ya ofisi hiyo kujua nini kinaendelea humo, pia nilitaka kujua muuza electronics alihamia wapi,
Kuingia ndani ya ofisi hiyo, nikakuta watu wenye Rika mbalimbali watanashati, wengi walikuwa vijana na wanawake Wachache,
Mle ndani palikuwa na utulivu wa kutosha, AC Kila Kona, kila mtu alikuwa ameshika kalamu na karatasi na alionekana kumakinika na kusoma kilicho kwenye karatasi,
Nikawaza hiki ni nini watu Hawa wanafanya, niliwaza, yaezakuwa wanafanya labda mtihani hivi, niliwaheshimu sana, nilipoona hali Ile, nami nikalazimika kusogea pembeni alipokuwa askari yule wa USALAMA na kuuliza watu wale wanafanya nini, na ofisi Ile inajishughulisha na nini,
Mlinzi yule alinijibu kuwa pale ni ofisi za BETTING, watu wanachukua mikeka kutabiri timu za mpira wa miguu.
Sura yangu ilifura ghafula, nilitoka haraka ndani ya ofisi Ile nikijilaumu kupoteza muda wangu kuingia ofisi ya ulaghai Kwa nguvukazi yetu ya Taifa inayowateka vijana kuamini kuwa maisha yaezapatikana Kwa Bahati nasibu.
OMBI: Atokee kiongozi mmoja mkorofi aina ya Magu, afute Ujinga huu unaopoteza nguvu KAZI ya Taifa.
Haiwezekani mchina anapokea coin Kwa wanafunzi wa shule za msingi mtaani Ili wabet, Taifa tunalipeleka wapi?
Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo Tanzania 🇹🇿.
Amen.