Shule aliyosoma Mkapa yafungwa kwasababu ya udini (waislam vs wakristu) ni kasheshe!

Status
Not open for further replies.
Mambo mengi yanapaswa yatutoe kwenye jiza cha kufikiri.
1. Dhana ya udini: Hapa nitadodosa haya: kabla ya kutoa lawama kwa yeyote tafakari namna uchaguzi ulivyokwenda na ushiriki wa misikiti na makanisa katika kuwapandikiza wagombea. Hili huhitaji 'degree' wala 'diploma' kulibaini bali ubinadamu wa kawaida tuliojaliwa na Muumba.
2. Ndanda: Kanisa katoliki lilinyang'anywa ile shule pamoja na majengo ya shule si shule tu: ukweli ni kuwa kanisa lililojengwa pale lilikuwa la jumuiya yote ya waroma si wanafunzi pekee. Waislamu, ambao pia ni wanafunzi wa pale, walipa kodi wanahaki ya kuabudu, ila busara inahitajika, je mazingira ni mwafaka kwa msikiti? Wasio waroma lakini ni Wakristo wanasali wapi? Ndanda ni mahali ambapo shughuli zote za kanisa, pamoja na malezi ya masista na mapandri yanafanyika! Ni mahali palipotapakaa uturi wa bibilia!!! Waislamu nawashauri haya: a) Tumieni msikiti ulio nje ya maeneo hayo b) Zingatieni Masomo ili nanyi mfungue himaya zenu c) Mwambieni kiongozi wenu aandike barua ya kuomba mrudi shuleni na kuendelea na masomo d) Kama umbali wa msikiti unaathari kubwa kwa ibada zenu, ombeni chumba cha kudumu hapo shuleni! Mmenyimwa? Nawatakia uamuzi wenye busara katika suala hili.

Chumba cha kudumu hapo shuleni wanacho mbona pale kuna dhana fulani ya waislamu kuwa watawala wa kila kitu hicho kinachowafanya wakurupuke na kuona wanadai madai ya msingi kumbe Pumba tupu.
 
Mi nadhani tusifikirie vibaya, nadhani ni kuwa pale shule kuna vijana wa Kiislam, sasa wao wakaswali wapi jamani? Kuna ubaya gani kuomba watengewe sehemu ya kufanyia ibada. Tusilichulie hili swala ki udini udini tu...

Lazima kuna mahali wamepewa pa kuabudia kwani ni haki ya kila mtu kuabudu kulingana na Imani yake. Kwa mfano pale Tosamaganga wanafunzi wa kiislam wamepewa chumba na wanaswali hapo wale wa protestant(Lutherani, TAG, Agape NK ) wamepewa chumba pia na wameweka ratiba na kupeana ratiba ya matumizi ya chumba hicho then wao RC wanatumia kanisa lililopo nje ya eneo ambalo shule ilipewa. Sasa ni vema wakalizika na hiyo sehemu ya kuabudia waliopewa ila kama hawakupewa hapo ndo waombe uongozi wa shule uwaandalie hiyo sehemu. Wasijihusishe na ujenzi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom