the Villag Story
New Member
- Feb 13, 2023
- 2
- 5
MWANDISHI: INNOCENT
Tulianza mapenzi yetu tangu tukiwa secondary na hatukuishia hapo penzi letu lilifanikiwa kufika mpaka chuo kikuu pale mzumbe tawi la mkoa wa Mbeya mungu mwema na hatimae tukaoana.
Lakini kama ningevizingatia vijitabia flani vidogo vidogo alivonionesha mume wangu Terry enzi za uchmba wetu wallah nisingejaribu kuolewa nae. Wahenga walisema ni “kheri uwe na mume mbaya kuliko kuwa na mama mkwe mbaya.”. ulikua ni msemo ambao kamwe sijawahi uamini, lakini sasa unajidhihirisha ndani ya maisha yangu.
Naitwa Dorice ungana na mimi nikupe kisa changu kilichokithiri chungu, chuki, dharau, vituko vya mama mkwe wangu, twende pamoja.
Ni hivi tangu zamani mpenzi wangu ambae kwa sasa ni mume halali wa ndoa. Mapenzi yetu yalianza kama utani tukiwa secondary kwani tulikua hatupendani kabisa yani tulikua maadui wakubwa.
Na hii ni baada ya Terry kunishtaki kwa mwalimu eti mimi namuibia majibu yake tukiwa na kidato cha kwenza kwenye mtihani wetu wa kwanza kabisa. Lakini cha ajabu mwisho wa siku tulikua wapenzi na hatimae kuja kuoana, nikikumbuka mpaka nacheka mwenyewe.
Kwa nini nilianza kumpenda Terry ni kwamba cha kwanza alikua ni mzuri wa sura yani bonge la handsome, alikua mwenye akili sana, msafi, mrefu na sifa nyingine nyingi yani kiufupi ni mtu mwenye sifa ambazo ni ndoto kwa wanawake wengi.
Na mimi sio kwamba najisifia nilikua mrembo na mpaka sasa ni mrembo MashAlah, na enzi tunasoma tulikua tunachuana yani akiwa wa kwanza mimi wa pili aakiwa pili basi mimi wa kwanza. Tulimaliza secondary na kutegana kwa muda kidogo baada ya kwenda A-level.
Hatimae tulihitimu A-level na kuomba chuo kimoja na tulifanikiwa kwenda chuo cha mzumbe. Pale chuo tulikua moja kati couple’s bora kabisa yani tulipewa jina la utani couple gold na watu wetu wa karibu. Yani tulikua tunagandana kila sehemu kama ruba, kwa nini?
Ni kwamba Terry alikua ni mwenye wivu kupitiliza akiniona na mwanaume yoyote basi ilikua ugomvi, niliona kawaida kwani nilijua ni upendo tu. Hayawi hayawi yakawa na hatimae tukaoana na hapa ndo picha lilipoanzia.
Aisee kuna hii tabia moja ambayo inanikwaza sana toka tumeingia ndani ya ndoa. Ni hivi Terry ni “mama boy” nikimaanisha ni mtoto wa mama yani hana maamuzi kama mwanaume mpaka najiuliza hivi nimeolewa na yeye au nimeolewa na mama mkwe.
Kwake mama yake ndo kila kitu, “sawa hakuna ubaya lakini hii mh…mh hapana imezidi”. Kuna baadhi ya vitu inatakiwa aamue yeye kama mwanaume na kiongozi wa familia na sio kuamuliwa na mama yake,
“Hii kwa kweli nashindwa kuivumilia” twende pamoja na mimi ndugu msomaji.
Nikiwa nimekaa sebleni huku nimeshika simu yangu nikiendelea kusoma siulizi inaiyoitwa NDOA YA SHETANI, iliyoandikwa na INNOCENT katika page yake ya Facebook inayoitwa the village story(TVS), ghafra nikaskia mlango unagongwa kuashiria kuna mtu anapiga hodi.
Niliweka simu pembeni haraka nikainuka na kwenda kufungua na kujua aliepo nje ni nani.
Ile nafungua mlango tu, nilihisi joto kubwa ndani ya mwili, huku nikihisi kama nashindwa kupumua na yote haya ni taharuki niliyoipata ndani ya moyo wangu baada kuona aliyekua mlangoni ni…..
Tukutane sehemu ya pili wapendwa. ni mwandishi na member mpya humu naomba mnipokee.
nimawaleteeni simulizi hii nina uhakika mtaipenda.