Shibuda ampokea Kikwete Dodoma

wana JF na wa-TZ wenzangu tuwe waangalifu, tofauti ya vyama haileti tofauti ya uraia na haki ya kukutana. Kikwete na Shibuda ni wa Tanzania na watakufa na kuzikwa Tanzania. Vilevile wote wawili ni viongozi wa kitaifa pamoja na ukweli kwamba wana majimbo yao, hivyo wanaweza wakakutana mahali popote pale ndani ya nchi yao.

Kuna uwezekano Shibuda alipokuwa CCM aliwahi kumpa Kikwete maoni au maonyo fulani fulani akayapuuza, hivyo si vibaya akienda kumkumbusha madhara ya kupuuza maoni yake ambayo yangeweza kukiokoa chama kisifike hapo kilipo hivi sasa. Kumbukeni Shibuda hakuichukia CCM bali alitofautiana na Katibu Mkuu wa chama wakati huo. Lakini vilevile si makosa akienda kumpa ushauri nasaha ili kunusuru nchi kuingia katika hali ya sintofahamu, kwa sababu madhara yake yatampata kila mtu akiwemo na yeye Mh Shibuda...

Sasa tuache speculations zitatufanya tupotoke. Tusianze kusema aah sasa Shibuda anataka kurudi CCM.. je tumejuwaje? Kusalimiana na mtu mnayetofautiana itikadi si vibaya na si haram, kesho na keshokutwa unaweza kumwona Shekh Mkuu akisalimiana na Karidinali Pengo, je tutasema Pengo anataka kuwa mu-Islam? Au Kakobe na Marasusa? au wa Upako na Mwingira...

Tuacheni speculations na tuendelee kubaki wa-Tanzania wenye tofauti ya makabila, dini, itikadi, elimu, maumbo ...lakini bado ni wamoja ndani ya Tanzania
 
Hapo naona mzee Msekwa hakuipenda hiyo move, halafu naona kwenye picha kuna ndugu wawili wa damu, mmoja aliwekewa nazi baada ya kuzaliwa bila kichwa , na huyo wa mtera aliwekewa dafu baada ya kuzaliwa bila kichwa, baba mmoja mama mbali mbali.Halafu kwa mbaali naona yule chapombe anakenua kama m/kiti wake.
Du kumbe lusinde ana kichwa cha dafu? huyu mtu sifa zitamuua lakini kwa hali yalofikia kwenye chama na darasa lake la saba ni lazima afanye kazi ya ziada hata kama ni kujidhalilisha nk.
 
Wadau hili la shibuda kwenda kumpokea Kikwete limekaaje?hili nao nafikiri ni Gamba lingine.

View attachment 41723

ni hivi mkuu siasa siyo vita wala ugomvi na siasa ni kusimamia kile unachokiamini nakushimdana kwa hoja kwahiyo kama mhesimiwa alikuwa dodoma na shibuda alikuwa hapo sioni ubaya kusalimiana katika siasa kuwakuta wanasiasa wanaotofautiana kwa hoja kuwaona wakinywa wakitembea pamoja ni kawaida na haimaanishi wanakubaliana kwa hoja kwamana hiyo unataka ngeleja kipindi hiki asiongee na wote waliochangia kumkandamiza kuwa aachie uwazili hapo itakuwaje siasa kama unahasira utaua wengi,utagombana na wengi pia utawachukia wengi so ni kawaida sana kwenye siasa zakistarabu na za watu waliokomaa kisiasa.
 
Hivi wale wadau waliokuwa wanatuletea habari kutoka jikoni kabisa siku hizi wako wapi? tunakata tusikie 'chenge akaangwa' au 'lowassa achinjiwa baharini'.....hata kama ni ushuzi tu...alimradi siku iende vizuri....teh teh..!
 
Ni kweli mleta thread jaribu kuiweka sawa hii thread yako..maana tunaweza kuchangia kitu ambacho si sahihi..tuambie alimpokea wapi? kwenye nini? na lini? ukitupa hayo majibu nadhani tutachangia kwa uwazi zaidi...

Picha inajieleza hiyo., uambiwe nini? Au mwenzetu kipofu?
 
hapo ilikuwa uwanja wa ndege dodoma...ndipo walipokutana hapo hakuna jingine

kama wamekutana uwanja wa ndege sioni tatizo kusalimiana kwasababu hata angekuwa kiongozi yeyote wa CDM yupo pale angesalimiana na rais.pili siyo kosa kwa wanasiasa wa vyama vyenye itikadi tofauti kuwa marafiki.tatu kwa wale ambao kila siku mnafuatilia Shibuda anafanya nini na anaongea nini nadhani hamumfahamu vizuri huyu jamaa.waulize hata CCM wenyewe mpaka anaondoka huko walikwisha mchoka,ni mwanasiasa mtatata!
 
Atakuwa labda anamfikishia ujumbe alioahidi kuwa kuna baadhi ya wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa utendaji wao ni mbovu na hawamsaidii chochote rais. Soma majira ya November 2 utakutana na hiyo ahadi ya Shibuda. Ila tu kwa kuwa Dr Dr Dr Dr Dr Kikwete huwa hasikilizi ushauri juhudi za Shibuda zitakuwa kama kumpigia mbuzi gitaa.
 
Hata kama Shibuda angekuwa ni mbunge wa Dodoma mjini lakini hakupaswa kuwepo pale, ile ni ziara ya kichama ya JK, PALE WA KUMPOKEA NI MKUU WA MKOA KWA SABABU NI KADA WA CCM, NA VIONGOZI WOTE WAKUU WA CCM.
Ila msisahau huenda kulikuwa na nyama pale ndicho kilichompeleka pale Shibuka maana msukuma yule ana uchu balaa.

Jalibu kufikiriai kwa mapana!!

Kwani ukishakua raisi,mbunge au mwanasiasa ni tiketi ya kukutoa kuwasiliana na wenzako hata kama wa chama ambacho sio chako?

Jamani tuache siasa za uadui na chuki!! upinzani sio vita na chuki kunamasuala mengine ya kijamii zaidi ya siasa!! .
 
kama wamekutana uwanja wa ndege sioni tatizo kusalimiana kwasababu hata angekuwa kiongozi yeyote wa CDM yupo pale angesalimiana na rais.pili siyo kosa kwa wanasiasa wa vyama vyenye itikadi tofauti kuwa marafiki.tatu kwa wale ambao kila siku mnafuatilia Shibuda anafanya nini na anaongea nini nadhani hamumfahamu vizuri huyu jamaa.waulize hata CCM wenyewe mpaka anaondoka huko walikwisha mchoka,ni mwanasiasa mtatata​

Na hapo Jk alikuja anaingia dodoma...na shibuda anakuja dar kwenye mkutano wa cdm..kule mbezi
 
msiwewashamba huyu alikuja kumjoki tu , alafu kumbuka usipofanya hivyo hata umaarufu unapungua Shibuda ni maarufu kufuatia mizaa yake , kama unakumbuka alitaka kung'oa Mkapa kwa kugombea naye mpaka mwisho , alipigwa mikwala mingi sana, kusalimiana sio shida mbona wabunge wakiwa nje ya ulingo wanakumbatiana sana wakati wa bunge wanachemshana , tuachane na unafiki kwani hatujengi uadui,
 
Nadhani lipo jambo au hatua anataka kuchukua katika mustakabali wa hali yake kisiasa. Ukimuona Shehe kanisani au Askofu msikitini ni lazima ujiulize maswali pamoja na kwamba Mungu wetu mwingi wa rehema ni mmoja bali yuko kwa majina tofauti. Nderemo na na vimbwanga vya Shibuda katika ulingo wa siasa huenda vikfikia ukomo pale atakapotangaza kuyarudia matapishi yake. Hii ikitokea haitashangaza kwani tangu achukue jimbo amekuwa na misimamo tofauti na maamuzi ya chama chake. Anachojivunia ni kuwa yeye anakubalika na anachagulika hata awe kwenye chama gani. Siasa ni mchezo mcahfu, anaweza ujikuta ameachwa solemba na huo utakuwa mwisho wa fasihi na mashairi yake ya mwambao. Tunamtakia safari njema.
 
Kwa maoni yangu huyu Shibuda CHADEMA walitakiwa wamfukuze siku nyingi sana. Huyu ni pandikizi na anaweza kabisa kuibua bomu ambalo likaiathiri sana CHADEMA. Sioni kwa nini CHADEMA inaendelea kumkumbatia pandikizi huyu.
 
Waungwana!
La msingi kujiuliza hapa ni iweje picha ya Shibuda kumpokea Kikwete ndiyo ipambe magazaeti yote hayo ukurasa wa mbele?
Wabunge na viongozi wangapi walikuwepo na wasitolewe kama pambo la magazeti?
Ni message gani media inataka kutoa?
Kwa vyovyote ile tufike mahali tukubaliane huyu Shibuda si muadilifu katika siasa za nchi hii!
 
Back
Top Bottom