benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Elimu bila ada kwa shule za shule za msingi na sekondari imeongezewa kwa asilimia 15.34 kwa mwaka ujao wa fedha 2023/24 ikilinganishwa na bajeti iliyoidhinishwa katika mwaka wa fedha wa unaomalizika wa 2022/23.
Hotuba ya Makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2023 /24 iliyowasilishwa bungeni na Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki imeonesha hilo.
Kairuki ameliomba Bunge liidhinishe Sh bilioni 399.64 kwa mwaka 2023/24 kwa ajili ya elimu bila ada ambazo kati yake, Sh bilioni 157.79 zimetengwa kwa shule za msingi na Sh bilioni 241.85 kwa sekondari.
Bajeti hiyo ni sawa na ongezeko la shilingi bilioni 53.15 ambayo ni sawa na asilimia 15.34
Ongezeko hilo limeelezwa kuwa linatokana na wanafunzi wa kidato cha tano na sita kujumuishwa katika Mpango wa Elimu Bila Ada.
Katika hatua nyingine, Kairuki amesema serikali itaendelea na mpango wa ujenzi wa matundu ya vyoo katika vituo shikizi ambako Sh bilioni 5.74 zimetengwa kwa ujenzi wa matundu 5,218 ya vyoo.
Aidha, zimetengwa Ujenzi wa mabweni 61 ya wanafunzi wenye mahitaji maalum umetengewa Shilingi bilioni 7.86
Hotuba ya Makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2023 /24 iliyowasilishwa bungeni na Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Angellah Kairuki imeonesha hilo.
Kairuki ameliomba Bunge liidhinishe Sh bilioni 399.64 kwa mwaka 2023/24 kwa ajili ya elimu bila ada ambazo kati yake, Sh bilioni 157.79 zimetengwa kwa shule za msingi na Sh bilioni 241.85 kwa sekondari.
Bajeti hiyo ni sawa na ongezeko la shilingi bilioni 53.15 ambayo ni sawa na asilimia 15.34
Ongezeko hilo limeelezwa kuwa linatokana na wanafunzi wa kidato cha tano na sita kujumuishwa katika Mpango wa Elimu Bila Ada.
Katika hatua nyingine, Kairuki amesema serikali itaendelea na mpango wa ujenzi wa matundu ya vyoo katika vituo shikizi ambako Sh bilioni 5.74 zimetengwa kwa ujenzi wa matundu 5,218 ya vyoo.
Aidha, zimetengwa Ujenzi wa mabweni 61 ya wanafunzi wenye mahitaji maalum umetengewa Shilingi bilioni 7.86