Serikali imdhibiti Maulid Kitenge na kundi lake la wahuni wanaojiita Wasafi Jogging Group

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,891
155,887
Huyu jamaa Kwa kutambua kwamba nchi Sasa Ina mbululaz wengi wanaojipendekeza Kwa watu maarufu huku wakijiita machawa akaanzisha kundi la kukimbia mchakamchaka barabarani.

Mazoezi ni muhimu Kwa afya ya mwili na akili, lakini yasifanywe kihuni, yafanywe mahali sahihi na salama Kwa wafanya mazoezi wengine na jamii Kwa ujumla.

Kitenge na wahuni wenzake wamekuwa kero Kwa wakazi wa maeneo ya Oyster Bay na Masaki na watumiaji wengine wa Barbara wa maeneo hayo.

Kitenge na wahuni wenzake wamekuwa wakikimbia katikati ya barabara huku wakisababisha usumbufu Kwa watumiaji wengine wa barabara, hususani watumiaji wa vyombo vya moto, Kwa kuwazuia kutumia barabara kikamilifu.

Kitenge na wahuni wenzake wamekuwa wakitumia barabara kukimbia, barabara zinajengwa Kwa gharama kubwa ili zipitishe magari Kwa haraka.

Kitenge ni kero, huyu atakuja kusababaisha majanga Kwa hao wahuni wake, amini nawaamnia Kuna siku mtasikia hao mbuzi wa Kitenge wanaokimbia mabarabarani kama wehu wamegongwa na gari na wamekufa na wengine kujeruhika.

Kwa kuepusha haya yasitokee, Kitenge adhibitiwe haraka.
 
Back
Top Bottom