Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,715
- 41,488
Halafu tukutane nao EAC.Naunga mkono hoja. Na baada ya hiyo kura ya maoni, ikiwezekana waendelee tu na Taifa lao kama ilivyo kwa Comoro, nk.
Kitakachotokea:
1. Kama Samia atakuwa bado madarakani, italazimu Tanganyika kuongozwa na Rais wa mpito kwa mara ya pili.
2. DPW itabidi iende kue desha bandari za Zanzibar, maana imekuja Tanzania kama deal la wazanzibari.
3. Zanzibar litakuwa taifa la kwanza la kigeni kuuziwa umeme na TANESCO.
4. Mchele na ndizi toka Tanganyika zitaanza kuuzwa Zanzibar kwa kutumia sarafu ya Marekani.
5. Itakuwa patashika Tanganyika itakapotangaza wahamiaji toka Zanzibar kutakiwa kukamilisha taratibu za uhamiaji, huku wengi wakiamua kuukana uraia wa Zanzibar ili kukidhi sheria ya uhamiaji ya Tanganyika!!
Katika porojo ni rahisi sana kusema Muungano uvunjike, lakini kiuhalisia, hilo likitokea, inaweza kuchukua hata miaka 50 mpaka Zanzibar kutengamaa kama Taifa.