Sakata la gesi Mtwara: Kauli ya Profesa Muhongo

Hivi watu kupelekwa VETA au kupewa bei nafuu ya kuunganishiwa umeme huwa ni hongo, fadhila, au ni wajibu wa serikali kuelimisha watu wake na kuendeleza jukumu la maendeleo ?
 
Huyu Mzee kweli ni PROFESSOR wa elimu ya kimagharibi au PROFESSOR kama yule Mbunge wa Korogwe vijijini Maji Marefu?Jamani nimesikia haya mahojiano yake;huyu kweli ni Professor wa darasani?Nitaendelea kuwa TOMASO hadi nihakikishiwe!Huyu jamaa msomi?

Majibu yake ni mepesi na hovyohovyo kwenye hoja nzito iliyokwisha anza hata kusababisha mauaji Mtwara/Lindi!
 
Hii ndo Tanzania, kauli ya profesa haina tofauti na kauli itakayotolewa na mtu wa darasa la saba! Ni jambo la ajabu sana kuona Waziri mzima, tena Profesa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu, anafananisha usafirishaji wa Korosho na usafirishaji wa gesi. Waziri Muhongo anataka kutuambia kuwa usafirishaji wa hiyo gesi uko sawa na namna korosho inavyosafirishwa kutoka Mtwara? Ama kweli dunia ina mambo! Yangu macho, ngoja tuone wanapotupeleka!

Kazi ishamshinda huyu jamaa, alishazoea kufundisha watukudesa, amewekwa under pressure akili zimemruka anaropoka ropoka tu.
 
Jk akiwaanamuachiachia huyu waziri aongeeongee ataharibu kabisa, yaani nje ya hayo ma jeolojia yake huwezi amini kama jamaa ni profesa inaonekana haelewi isues kabisa.


Huyu jamaaa mimi alinishangaza sana....professor mzima hajui hata historia ya taifa hili...unaweza kufikiri labda ni mtoto aliyezaliwa 1982....Eti mikoa ya Lindi na mtwara toka uhuru haina mchango kwenye pato la taifa this is nonsense!!!!!... Kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni duuu!!!! Kwakweli haya ni matusi ya Nguoni na dharau kubwa kabisa kwa wananchi wa Mtwara na Lindi.....na huyu jamaa atakuwa moja kati ya chachu za wao ..m kupoteza ngome zao za miaka nenda rudi....mlikuwa mnakula na vipofu maskini kwa ujinga wenu safari hii mmewagusa mikono!!!!
 
JK: kwa kweli sielewi tatizo la umasikini Tanzania linasababishwa na nini.
mramba: mtakula nyasi lakini ndege ya Rais lazima ininuliwe
Malecela: mkikoboa, hizo pumba mzihifadhi mtazitumia wakati wa njaa.
Msekwa: wana wivu wa kike
Chenge: ni vijisent tu
pombe J.M: Kama hamna nauli pigeni mbizi.
Muhongo: sielewi matatizo ya watu wa Mtwara
Mwema. Kesi ya Ulimboka ni siri ya Taifa.
Baba wa Taifa: ccm si mama yangu...!!!
 
Hivyo vikao vya posho wakishakula makaratasi yaliyojadiliwa inabaki mali yao wananchi wanaishia kuwaona kwenye TV tu.Mfumo wa mawasiliano kati ya watawala na watawaliwa kuna Gap kubwa ambalo ndiyo linaleta yote haya. Kama kweli hayo yote yalijadiliwa na yakaafikiwa iwe waendelee kuweka machapisho kwa Lugha ya Malkia ambayo walengwa wengi hawaielewi?
 
Hii ndo Tanzania, kauli ya profesa haina tofauti na kauli itakayotolewa na mtu wa darasa la saba! Ni jambo la ajabu sana kuona Waziri mzima, tena Profesa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu, anafananisha usafirishaji wa Korosho na usafirishaji wa gesi. Waziri Muhongo anataka kutuambia kuwa usafirishaji wa hiyo gesi uko sawa na namna korosho inavyosafirishwa kutoka Mtwara? Ama kweli dunia ina mambo! Yangu macho, ngoja tuone wanapotupeleka!

Hata mimi sikujuwa kuwa kuna bomba la kusafirisha Korosho toka Mtwara hadi Kinyerezi
 
JK: kwa kweli sielewi tatizo la umasikini Tanzania linasababishwa na nini.
mramba: mtakula nyasi lakini ndege ya Rais lazima ininuliwe
Malecela: mkikoboa, hizo pumba mzihifadhi mtazitumia wakati wa njaa.
Msekwa: wana wivu wa kike
Chenge: ni vijisent tu
pombe J.M: Kama hamna nauli pigeni mbizi.
Muhongo: sielewi matatizo ya watu wa Mtwara
Mwema. Kesi ya Ulimboka ni siri ya Taifa.
Baba wa Taifa: ccm si mama yangu...!!!

Wassira: Wakristo marufuku kuchinja vitoweo
 
Hii ndo Tanzania, kauli ya profesa haina tofauti na kauli itakayotolewa na mtu wa darasa la saba! Ni jambo la ajabu sana kuona Waziri mzima, tena Profesa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu, anafananisha usafirishaji wa Korosho na usafirishaji wa gesi. Waziri Muhongo anataka kutuambia kuwa usafirishaji wa hiyo gesi uko sawa na namna korosho inavyosafirishwa kutoka Mtwara? Ama kweli dunia ina mambo! Yangu macho, ngoja tuone wanapotupeleka!

Tusipende kuwa Wakomunisti wa maneno wakuu, alichosema Waziri ni sahihi. Nchi hii haina utaratibu wa ukanda au majindo, kwa hiyo kauli ya Waziri ni kuwakumbusha wakaazi wa Mtwara kuwa, kuna tofauti ya Korosho uliyolima na Gesi ambayo ni MALI YA ASILI.

Kuwa darasa la 7 haimaanishi kuwa huna akili, tazama wewe na madarasa yako umeshindwa kuelewa suala dogo sana. Waziri hafananishi usafirishaji, Waziri anahoji 'Korosho za Mtwara zinaenda sokoni, gesi ya Mtwara itashindwaje kwenda sokoni?' Shida ni kwamba unajaribu kutumia hisia kuelewa.

Haya anayoyasema Waziri Muhongo hata Zitto Kabwe aliyasema BBC (simaanishi hizo mnazoziita kejeli) kwamba kuna viongozi wa ngazi ya Mkoa, Wilaya, Halmashauri na Wabunge wa mikoa ya Kusini walipelekwa nje kujifunza mambo kadhaa juu ya gesi. Kama nia ni kuweka maazimio wazi kwa Wanamtwara, mbunge wa Mtwara mjini ambaye nasikia naye ni kinara wa maandamano, anataka kuieleza nini Tanzania juu ya ushiriki wake katika ziara na vikao hivyo?
 
Mwandishi: Tatizo la wakazi wa Mtwara ni lipi?

Waziri: Mimi sielewi, inabidi wao waulizwe. Watu wa Mtwara kitu walicho nacho haki ni Korosho... Hizo korosho ni mali zao kabisa, mbona hizo korosho zinasafirishwa? Watanzania tuwaulize kwa nini korosho zao zinasafirishwa kutoka Mtwara.
Nathani Mhe. WAziri haelewi pia kwanini yupo madarakani,
labda kwasababu kateuliwa hivyo hajui pia kwanini kateuliwa
kwa maana kuwa hamuji hata aliyemteua kushika nafasi aliyonayo
Nadhani hajui kusoma pia maana wadhifa alionao majukumu yake yameandikwa mahali
 
Kinachonishangaza nyinyi wenye mawazo haya ndio mnaothubutu kumuita Waziri kilaza aliyeishia darasa la saba. Sasa angalia ni nini umeandika:

Ukweli ni kwamba viwanda na shughuli zitokanzazo na gesi Kama usafishaji na usambazaji zilitzkiwa zifanyikie Mtwara

Si ndio haya Waziri anayaeleza saa zote kuwa yatafanyika huko? Watanzania hebu tuache ushabiki wa kijinga na angalau mara moja kwa mwaka tuwe serious na reasonable badala ya kupenda sifa za kijinga. Hivi kuna shida gani ya kutafuta facts badala yake tunaongea kishabiki tu na kusifiana mitandaoni?
IPECACUANHA, natural gas exploration ni shughuli ya kitaalam na ina principles zake. Ungejisumbua tu kutafuta elimu ya gesi ikichimbwa huwa ikoje usingekuwa na maswali kama itachakatwa Mtwara au Dar. Shida yetu ni kukurupuka na kutopenda kusikiliza. Kama tungemsikiliza Waziri kwa umakini, naamini tusingekuwa na mabishano ambayo mimi binafsi nayaona ni ya kipuuzi.

Waziri kasema, uchimbaji, uchakataji na usindikaji utafanyika huko huko Mtwara. Na mimi nakuongezea kuwa: hata kama Serikali ingetaka hayo yafanyike Dar es Salaam, ISINGEWEZA. IPECACUANHA, sour gas (as it comes from the well) ni corrosive, kwa hiyo kwa usalama wa mabomba na sababu zingine za kiuchumi, lazima ichakatwe ndio iwe salama kusafirishwa kwenye mabomba. Na ndio hicho Waziri anachokirudia kila mara kukisema. Hebu soma hii link kwa faida yako mwenyewe uone kwa nini ni lazima gesi ichakatwe Mtwara na sio tu Mtwara, bali inalazimu shughuli hiyo ifanyike karibu na mahali ilipochimbwa kadiri iwezekanavyo NaturalGas.org

Kaka unataka usambazaji wa gesi ufanyike Mtwara? Kama mawazo ya Waziri ni ya darasa la 7 haya ya kwako ya darasa la ngapi?
1. Twiga Cement watandike bomba la inchi 1 toka Mtwara mpaka Wazo Hill DSM ili kupata Gesi
2. Kwanza Bottlers watandike bomba lao toka Mtwara hadi Kawe Industrial Area
3. Murzah Oil Industries watandike bomba toka Mtwara hadi Port Access Industrial Area
4. East Coast Oils watandike bomba toka Mtwara hadi Kurasini
5. Serengeti Breweries watandike bomba toka Mtwara hadi Chang'ombe....
Au mimi sijaelewa usambazaji upi unaomaanisha wewe?

Ushabiki wa kijinga unatunyima nafasi ya kusikia facts, kwani wakati muda mtu anaongea sisi tuko bize kutafuta kitu cha kubisha mara atakapomaliza kuongea. Sasa linakuja hili suala la KINYEREZI. Hata hili jambo dogo tu nalo lizue debate?

Kinyerezi kunajengwa Power Plant (Mtambo wa kufua umeme). Uhusiano wa Gesi na Project ya Kinyerezi ni kwa kuwa huo Mtambo unaojengwa Kinyerezi utatumia gesi kufua umeme. Sasa ukisikiliza watu wengi hapa JF wanakwambia kwa nini gesi itolewe Mtwara ipelekwe Kinyerezi, sasa swali la kujiuliza nyie wenyewe, hiyo gesi tunanufaika nayo kwa kuiangalia au kwa kutumika?
Mambo ya Almasi ya Mwadui kwenda kukatiwa Iringa halina sababu katika duniani ya leo

Kuna mambo ya kuzingatia hapa, si kuongea tu kwa kuwa hakuna kodi ya mdomo. Unaweza kuniambia kwa nini NG'OMBE wasichinjiwe Dodoma, Singida na kwingineko wanakopatikana badala yake wanaletwa Dar wakiwa hai? Nauliza hivi kwa kuwa, tukiwa tunaangalia sababu moja tu kati ya 20 zinazo-determine business location tutakuwa watu wa ajabu. Ng'ombe wangechinjiwa Dodoma ni kweli machinjio yangetoa ajira kwa wenyeji wa huko, sasa kwa nini wanasafirishwa hai kuja Dar?
 
Last edited by a moderator:
KUNA PROFESA ALIWAHI NIAMBIA KUWA MAPROFESA WA KONGO NI WABOBEVU KATIKA VITABU... LAKINI UKIWASIKILIZA UNAWEZA FIKIRI UPO NA MTOTO MDOGO...SASA NAAMINI MUHONGO ATAKUWA ANATOKA KONGO....:target:
 
Kinachonishangaza nyinyi wenye mawazo haya ndio mnaothubutu kumuita Waziri kilaza aliyeishia darasa la saba. Sasa angalia ni nini umeandika:



Si ndio haya Waziri anayaeleza saa zote kuwa yatafanyika huko? Watanzania hebu tuache ushabiki wa kijinga na angalau mara moja kwa mwaka tuwe serious na reasonable badala ya kupenda sifa za kijinga. Hivi kuna shida gani ya kutafuta facts badala yake tunaongea kishabiki tu na kusifiana mitandaoni?
IPECACUANHA, natural gas exploration ni shughuli ya kitaalam na ina principles zake. Ungejisumbua tu kutafuta elimu ya gesi ikichimbwa huwa ikoje usingekuwa na maswali kama itachakatwa Mtwara au Dar. Shida yetu ni kukurupuka na kutopenda kusikiliza. Kama tungemsikiliza Waziri kwa umakini, naamini tusingekuwa na mabishano ambayo mimi binafsi nayaona ni ya kipuuzi.

Waziri kasema, uchimbaji, uchakataji na usindikaji utafanyika huko huko Mtwara. Na mimi nakuongezea kuwa: hata kama Serikali ingetaka hayo yafanyike Dar es Salaam, ISINGEWEZA. IPECACUANHA, sour gas (as it comes from the well) ni corrosive, kwa hiyo kwa usalama wa mabomba na sababu zingine za kiuchumi, lazima ichakatwe ndio iwe salama kusafirishwa kwenye mabomba. Na ndio hicho Waziri anachokirudia kila mara kukisema. Hebu soma hii link kwa faida yako mwenyewe uone kwa nini ni lazima gesi ichakatwe Mtwara na sio tu Mtwara, bali inalazimu shughuli hiyo ifanyike karibu na mahali ilipochimbwa kadiri iwezekanavyo NaturalGas.org

Kaka unataka usambazaji wa gesi ufanyike Mtwara? Kama mawazo ya Waziri ni ya darasa la 7 haya ya kwako ya darasa la ngapi?
1. Twiga Cement watandike bomba la inchi 1 toka Mtwara mpaka Wazo Hill DSM ili kupata Gesi
2. Kwanza Bottlers watandike bomba lao toka Mtwara hadi Kawe Industrial Area
3. Murzah Oil Industries watandike bomba toka Mtwara hadi Port Access Industrial Area
4. East Coast Oils watandike bomba toka Mtwara hadi Kurasini
5. Serengeti Breweries watandike bomba toka Mtwara hadi Chang'ombe....
Au mimi sijaelewa usambazaji upi unaomaanisha wewe?

Ushabiki wa kijinga unatunyima nafasi ya kusikia facts, kwani wakati muda mtu anaongea sisi tuko bize kutafuta kitu cha kubisha mara atakapomaliza kuongea. Sasa linakuja hili suala la KINYEREZI. Hata hili jambo dogo tu nalo lizue debate?

Kinyerezi kunajengwa Power Plant (Mtambo wa kufua umeme). Uhusiano wa Gesi na Project ya Kinyerezi ni kwa kuwa huo Mtambo unaojengwa Kinyerezi utatumia gesi kufua umeme. Sasa ukisikiliza watu wengi hapa JF wanakwambia kwa nini gesi itolewe Mtwara ipelekwe Kinyerezi, sasa swali la kujiuliza nyie wenyewe, hiyo gesi tunanufaika nayo kwa kuiangalia au kwa kutumika?


Kuna mambo ya kuzingatia hapa, si kuongea tu kwa kuwa hakuna kodi ya mdomo. Unaweza kuniambia kwa nini NG'OMBE wasichinjiwe Dodoma, Singida na kwingineko wanakopatikana badala yake wanaletwa Dar wakiwa hai? Nauliza hivi kwa kuwa, tukiwa tunaangalia sababu moja tu kati ya 20 zinazo-determine business location tutakuwa watu wa ajabu. Ng'ombe wangechinjiwa Dodoma ni kweli machinjio yangetoa ajira kwa wenyeji wa huko, sasa kwa nini wanasafirishwa hai kuja Dar?

kwa hiyo hii Gesi ikishafika Dar Viwanda vyote viko kwenye yadi moja tu??? Acha kutumika bwana!! Kwanza Watanzania wanataka Mkataba uwekwe wazi wa huu Mradi, pili uzalishaji waweza fanyika Mtwara na Dar kukawa na Center ya distribution. Mbona maji ya Ruvu kiwanda chake kiko pale Ruvu na yakifika Dar ndo yanasambazwa kwa matumizi.
 
Hana tofauti na Mulugo. Anaongea kwa kiwango kinachokatisha tamaa kabisa hana hata uwezo wa kupanga hoja na huyu ndiye tuliyeambiwa kwamba ni kichwa. Anaendelea kutoa kauli zilizojaa vitisho. Serikali bandia, Rais bandia na mawaziri bandia.

Huyu ndio anasifiwa kama kichwa mbona mimi namuaona kama ---- tuu
lbda anatumia masaburi kujibu hoja za msingi
 
Wakati Muhongo alipotoa maelezo bungeni kwamba mgao wa umeme ulikuwa wa kutengeneza, nguzo za umeme za TZ kupelekwa Mombasa na kupigwa Mihuri ili zionekane zimetoka SA, etc watu walimuona kama kiongozi shupavu na anayefaa hata kuwa Rais. Lakini kwa hili la gesi na mgao wa umeme unaoendelea, inaokena hafai hata uenyekiti wa mtaa.

Si kumpa credit ya kuwa Rais kwa sababu naye alionyesha udhaifu wa kutoshughulikia waliotengeneza huo mgao,watu wengi walifia hosp.hata mfumko
 
Isitoshe, wananchi wa Lindi na Mtwara wamepunguziwa bei ya umeme... Je, wanavyounganishiwa huo umeme kwa bei nafuu kuliko wananchi wengine, hawajiulizi? Pili, vijana wao tumewachukua wanakwenda kusoma VETA...


Huyu jamaa ni arrogant.. Hafai kuwa waziri. Anataka wananchi wa Lindi na Mtwara 'waote' kwa nini bei ya kuunganisha umeme ni ndogo? Hana hoja kabisa. Halafu wenzetu wanatengeneza wataalamu waliobobea, yeye anaweweseka na mchundo?
 
Kinachonishangaza nyinyi wenye mawazo haya ndio mnaothubutu kumuita Waziri kilaza aliyeishia darasa la saba. Sasa angalia ni nini umeandika:
"Ukweli ni kwamba viwanda na shughuli zitokanzazo na gesi Kama usafishaji na usambazaji zilitzkiwa zifanyikie Mtwara"Si ndio haya Waziri anayaeleza saa zote kuwa yatafanyika huko?

Wananchi wa mtwara wanataka vitendo, wameshachoka kupewa ahadi kedekede zisizotekelezeka.
Tangu kikwete aingie madarakani amewaahidi mambo mengi sana moijawapo ni ujenzi wa barabara lakini kwa muda wa miaka yake saba ameweza kujenga barabara yenye urefu wa kilometa 60 tu!!

Wananchi wa Lindi waliahidiwa kiwanda cha mbolea sasa ni miaka nenda rudi lakini hakuna dalili ya kiwanda hicho kujengwa. Kama hiyo haitoshi, ilani ya uchaguzi ya ccm 2010 ibara ya 63 kifungu h na k vinataja ujenzi wa mitambo ya kuzalisha umeme mtwara (300MW) kwa gesi ya mtwara bay na Kinyerezi (240MW) kwa gesi ya songosongo. Sasa imekuwaje tena ccm na serikali yake wanahamisha magoli? au kwakuwa wamezoea kuhamisha na wananchi hukaa kimya? Mwaka jana mwishoni raisi kikwete alipokea ripoti ya wachina na siemens juu ya ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Mtwara/Lindi hadi singida yenye urefu wa kilometa 1,100 je mradi huo umeshatekelezwa?

Kama hali yenyewe ndio hii, unadhani wananchi hawana haki ya kumdharau profesa Muhongo ambaye ameshindwa kabisa kujibainisha usomi wake na kuishia kuongea na kutoa mifano dhaifu ambayo huwezi kumtofautisha na lakairo ama profesa maji marefu walioishia darasa la pili!!??

Safari hii hata ccm ifanyeje wananchi wa mtwara hawatakubali kurudi nyuma. Serikali lazima ijenge mtambo wa kuzalisha umeme kwa gesi asilia mkoani mtwara na ndipo iuingize kwenye gridi ya taifa. No more no less!!
 
Back
Top Bottom