Said Mohamed Saad - Mmiliki wa Home shopping Centre, amwagiwa tindikali!

so he deserve! mwisho wa ubaya ni aibu, sheria ilipindiashwa na kuwanyima haki wengine, sasa ni zamu yake. wanasema malipo ni hapa hapa
 
Ni kweli, amemwagiwa tindikali usiku huu na watu wasiojulikana. Ni Said Mohammed Mahmoud, mdogo wake Gharib.
sahihisho Said ndio mmiliki wa hiyo kampun akina Gharib, Abdallah, Swallah, na huyo mwingine ni ndugu zake wadogo yeye ndio mkubwa, kwa kifup wanamiliki Home shopping, Amana benk, kampun ya ujenz, Msasan Mall, kampun ya kuagiza na kupokea mizigo bandarin hizo ni chache kati ya msururu wa makampun walionayo, kwakifupi jamaa shule hajaenda ila hicho kichwa chake ni kama vichwa vya maprof 20 pale mliman, pamoja na kwamba kuna jins wameiweka ccm mfukon huyu jamaa anajituma balaa niliwah kufanya nae kaz flan yuko vizur sana kichwan, na kwa kias kikubwa anauendesha uchumi wa kariakoo.
 
Kwa hiyo wewe mtu akiwa mkorofi apigwe risasi ndiyo dawa.

Mkuu mbona unajitia upofu? umesahau kauli ya "liwalo na liwe" Kwamba "wa pigwe tu" kupigwa kupo kwa aina nyingi mkuu.

Inasikitisha sana huko tuendako ni kubaya sana....
 
Si tu mwalimu.
Hata mwanafunzi anaweza kuwa na access ya conc. HCL, H2SO4.
two decades ago as a student I used to "steal" a tinge of Conc.HCL and Iron II sulphide (FeS) bars nakuja nazo bwenini usiku namix nje ya bweni upepo unakotokea, harufu inayotokea hapo mtahama bweni.... (they used to describe it as a rotten egg)

Mkuu ulikuwa unajifunza ugaidi bila kujua. Tehe tehe tehe, just a joke.
 
Kweli polisi ni dhana tu kwa TZ. Ikumbukwe mpaka leo hii watuhumiwa wa milipuko huko AR bado kukamatwa

polisi ni watuhumiwa namba 1 mlipuko wa Arusha watajikamataje? 2015 ifike haraka tuyaondoe haya majizi Ccm.
 
SIKU HIZ ukiona mtu anakukaribia kashika dumu kimb ia jiami mapema hata kama amebeba maji utamsogelea ukishajua kwenye dumu kuna maji si tindikali
 
sahihisho Said ndio mmiliki wa hiyo kampun akina Gharib, Abdallah, Swallah, na huyo mwingine ni ndugu zake wadogo yeye ndio mkubwa, kwa kifup wanamiliki Home shopping, Amana benk, kampun ya ujenz, Msasan Mall, kampun ya kuagiza na kupokea mizigo bandarin hizo ni chache kati ya msururu wa makampun walionayo, kwakifupi jamaa shule hajaenda ila hicho kichwa chake ni kama vichwa vya maprof 20 pale mliman, pamoja na kwamba kuna jins wameiweka ccm mfukon huyu jamaa anajituma balaa niliwah kufanya nae kaz flan yuko vizur sana kichwan, na kwa kias kikubwa anauendesha uchumi wa kariakoo.

Kati ya watu wenye vichwa vibovu, maprofesa wapo. Fast learners hawasomagi hadi sijui degree tatu (PhD), wakijitahidi bachelor, then wanaingia mtaani kutatua matatizo ya jamii. Waangalie akina Bilgate.
 
Ni kweli amemwagiwa tindikali,nimethibitishiwa na wafanyakazi wa hapo.

Jamani hata mimi rafiki yangu ni mfanyakazi wa home shoping center nimempigia simu anithibitishie taarifa hizi na amethibitisha kwamba ni kweli. kwa sasa jamaa(mgonjwa) anafanyiwa utaratibu wa kusafirishwa kupelekwa Afrika kusini kwa matibabu.
 
Yupo Johannesburg anapata matibabu amesafirishwa asubuhi sana ,inasemekana amepata athari ya jicho mmoja na mkono umeunguzwa sana na tindikali ,inasemekana huenda ikawa vita vya kibiashara!!

Hii habari nimeipata asubuhi pia mkuu, ni kweli yupio Jberg na jicho moja limeharibika vibaya sana!
 
Nadhani hiki ni kile kikundi cha chadema red bregade kimeanza kazi, serikali inahitaji kukifuta hiki chama cha waasi mara moja, dr slaa na mbowe wafungwe kifungo cha maisha na adhabu nzito.huu ndio uwe msemo wetu wana J.F ''CHADEMA HAIKUBALIKI, TUIPIGE VITA''.

wewe kama huna comment weka mikono kwenye ma------ yako, sio kundika pumba, usione sifa kuitaja CHADEMa kwenye issue kama hii wakati unaju sio siasa. Kimtazamo tu inaelekea una uwezo mdogo sana wa kufikiri.
 
sahihisho Said ndio mmiliki wa hiyo kampun akina Gharib, Abdallah, Swallah, na huyo mwingine ni ndugu zake wadogo yeye ndio mkubwa, kwa kifup wanamiliki Home shopping, Amana benk, kampun ya ujenz, Msasan Mall, kampun ya kuagiza na kupokea mizigo bandarin hizo ni chache kati ya msururu wa makampun walionayo, kwakifupi jamaa shule hajaenda ila hicho kichwa chake ni kama vichwa vya maprof 20 pale mliman, pamoja na kwamba kuna jins wameiweka ccm mfukon huyu jamaa anajituma balaa niliwah kufanya nae kaz flan yuko vizur sana kichwan, na kwa kias kikubwa anauendesha uchumi wa kariakoo.

Sasa mtu tunaambiwa kaishia darasa la 6 lakini ana miliki Benki wapi na wapi?


Wadau,kuna habari za uhakika chini kutoka kwa wadau wangu wa karibu kuwa hali ya mfanyabiashara said wa home shopping center si nzuri kibiashara...

kama thread moja iliyowahi kuandika habari zake humu ndani,inasemekana zaidi ya makontena 860 yamezuiwa bandarini kwa kile kinachoelezwa kufanya uchunguzi zaidi,mengi ya makontena haya yamewekwa bidhaa nyingine huku documents zikionyesha bidhaa nyingine.

hv karibuni amekuwa na ugomvi na mfanyabiashara mwingine Said salim bakhresa,na pia ameshagombana na Manji na yule muhindi mwingine tajiri zakaria,pia amekorofishana na subhashi Patel pale alipoanza kuingilia biashara ya mabati yanayofanana na ya kiwanda cha subash.

kuna wachina kama mia mbili hv nao mizigo yao iko kwenye hiyo ya huyu bwana so sad,kumbe na wao wanakwepa kodi

ukwepaji kodi huu wa Said,unajulikana wazi na kila mtu,hata serikalini,sijafahamu hasa kwann this time wameamua kumgeuka mwenzao! labda ndio yale maneno ya magufuli kuwa anaeweza kumtoa ni rais tu,maana huyu jamaa keshahamisha maafisa wa tra kama mia na hv!

my take:crime doesn't pay



Sidhani kama bakhressa anaweza kutuma watu wamwagie tindikali huyu jamaa kuhusu akina Subash, Manji na hao wengine aliogombana nao sina hakika lakini mimi naweza kumwondoa bakhressa kwenye hilo...

Lete list ya ma suspect wengine.


Tetesi zainasema kuwa Home Shopping Centre ni mali ya mkuu wa kaya (tz) na ndio sababu mara nyingi makontena yake yamekuwa yakipita bandarini bila kutozwa ushuru wakati watanzania wa hali ya chini ambao wamempa dhamana wanaumizwa kwa kucheleweshewa mizigo yao bandarini kisa hakuna hela hazina.

Tetesi zinaendelea kusema kuwa hivi sasa kuna container zipatazo 30 bandarini zilizofojiwa detail kuwa zina vyandarua na kumbe sio. na badala yake zimegudnulika kuwa zina vitenge. (no wonder they are the cheapest shopping centre in TZ)
Ingawa sisuport fujo za Mtwara lakini tafakarini kama wananchi wa tanzania wanaojulikana ni waoga au niseme (waerevu wa kijinga) leo wanadhubutu kupambana na polisi kweli ni kwasababu ya Gas tu. Wananchi wamesikia mengi wamechoka na wamechoka sasa.

Naomba mwenye detail zaidi juu ya hili ambalo linasememkana lina uhusiano mkubwa na kikao cha leo wizara ya fedha atuhabarishe zaidi.


Kwa hili sina hakika kwani haiwezekani mkuu wa nchi awe na njaa ya kuwa na duka la kuuza vikombe kariakooo. hili ni tusi kubwa sana kwa mkuu wa nchi na nashauri uende ufanye homework yako. Labda jamaa zake lakini sio mkulu mwenyewe...


Hapa kuna issue nyeti...itaiva siku siyo nyingi. Hayo ya HSC na Ikulu yamesemwa mara nyingi sana, hata gazeti moja, bila shaka ni Mwanahalisi ilishaandika sana jinsi kampuni hii ilivyo na uhusiano wa karibu na Mama Salma na Riz...na jamaa huwa wanaingia Ikulu kama kwao na hakuwa wa kuwahoji..

- na huwa ma-container yao huwa hayaruhusiwi kuguswa na wakaguzi wa pale bandarini. na pia kuna wafanyabiashara wa mikoani walishakubali kusafirishiwa bidhaa zao kwa bei chee kupitia kampuni ya HSC ya clearing na Forwarding then bidhaa zao zilipofika Dar, huwa hawapewi BL na vibali vingine halisi, kwa kuwa hawakuwa na vibali toka kwa HSC waliishia kupoteza bidhaa zao kwa kukamatwa na ndio walikasirika na kupasua majipu na uozo wa hawa jamaa...wanaenda ikulu kila mara ndio wanaenda kujadili deals.
- Kkoo wameotesha nyumba kama upepo...mojawapo ni jumba linalotazamana na Ben Mkapa Sec
- wanamiliki Benki (Amana Bank) na wanafanya kila biashara sasa...!


Hata ingekuwa mimi nisingelipa pesa hivyo tatzo hapo sio Said bali ni :

WAZIRI WA BANDARI, MH MWAKYEMBE
WAZIRI WA FEDHA MH MGIMWA
BOSI WA TRA MH KITILYA

Hao ndio wa kuwauliza na sio huyo Mmmahra.


Kwa machache ninayo jua mimi....home shopping center ni mmiliki wa silent ocean,inayosafirisha mizigo kutoka nchini china pamoja na dubai kwa bei ya kutupa,inafikia hatua mpk wewe uneenda kutuma mizgo yako ama kontena lako huendi tena tra kushughulikia kontena lako bali unaenda chukua mzgo wako warehouse,na kama utahofia kusumbuliwa na police wana magari yao ya HSC yanakuletea mzgo wako mpaka mlangoni kwako,wakwepa ushuru wengi na masikini wanaitumia sana kampuni hii.

HSC ndiyo wanaoingiza hapa nchini cement ya lucky toka pakistan kwa kibari maalumu,wao na mwenzao mmoja mwenye kiwanda cha mafuta na mifuko mbagala.

HSC ndiyo waliopanga lile jengo lilikuwa nikitumiwa na tra pale samora enzi hizo na hapo kuna office zao za silent ocean.

kwa leo ni hayo tu,siku hizi humu watu tunatoa infor za watu afu usalama wanazitumia kujipatia kipato sababu issue nyingi zinakuwa ni 100%.

NOTE: Kampuni hii imesaidia masikini wengi kuwa matajiri nchini,pamoja na kukwepa kwake kodi ila inarudisha kwa jamii kwa style ya kutoa misaada.kazi kwako kuihukumu ama kuisupport


mhhhhhh





kwa kifup tu hawa jamaa mimi nimefanya nao kaz tangu mwaka 2007 wananisafirishia mizigo yangu toka china na dubai. ukwel kama alivyosema jamaa mmoja hapo juu ni kwamba kwa kias flan wanawasaidia Wtz masikin kupata hela na matajir pia ila njia anazotumia kuwapa utajir ni kwa kukwepa kodi kwa kusaidiana na baadhi ya watumish wa TRA wale wakubwa. wakat huo yeye kwa kuwaweka watu kati huko juu anapiga hela nyingi mno yaan unaibiwa mwenye mzigo na serikali hasa serikal. conteiner la nguo ni TshsMilion 17 kwa futi 20 lakn yeye anakuambia ni milion 19 au 20 lakn unatolewa on the sport ikifika. so kinachojitokeza serikalin wanabadilisha document wakishirikiana na watu wa TRA conteiner la nguo linabadilishwa linakuwa la cement so analipia milion 5 mpaka 7 za juu anawapa kidogo watumish nyingine zake. huu mchezo ameuanza cku akisaidiwa na Zakhia Megi kipindi akiwa wazir wa fedha. walichofanya wamemuuzia Riz 0ne hisa so wanaiba hela nyingi ni Mungu anajua. ingawaje ukwel mwingine mchungu ni kwamba kampun yake ndio inasuply karibu mizigo yote kkoo na posta so kumfungia ni kusababisha ombwe la mizigo sokon na pesa kupungua serikaln ushahd ni juz mwakiembe kakamata conteiner zake mia moja leo hii wamezuiliwa kutoa mizigo wk hiz mbili tu tayar imebid wazir wa fedha awaite wafanyabiashara aongee nao tatizo liko wapi. coz hazina haisomeki. na kwa kuwatonya nasikia hata mtoto wa mshua wakat anakamatwa china kama ni kweli hawa jamaa ofic yao ya china ndio iliratibu mazungumzo ya kuachiwa kwao.



Wonders shall never end in Tanzania. Mwezi wa kumi na mbili 2012 nilikuwa China kwenye jimbo la Guangzhou nilibahatika kufika katika ofisi ya HSC katik jimbo hilo. Ukweli mambo yanayoendelea pale ndo utajua Tanzania ni nchi ya viongozi mazuzu! Mtu anapeleka container pale amepakia vitu tofauti lakini wale jamaa wanadiklea vitu fotauti. Mfano, jamaa alikuwa na container 40 ft la vifaa vya umeme na decorations za nyumba. Wale HSC wakamwambia yeye atapokea mzigo wake katika yard yao Dar es salaam na kulipia siku hiyo ya kuondoka na mzigo. Wakamuuliza yule jamaa anachotaka ni kupokea mzigo au ni kusoma kwenye karatasi nini kimeandikwa! Wao wanajua mzigo utapita wapi, kwa nani, kwa bei gani hadi kwenye yard. Jaama alilipia chini ya nusu ya bei ya kawaida kwani alishaingiza mzigo km huo miezi kama 3 kabla ya tukio hilo. Hii ndo Tanzania.

KITILYA/MWAKYEMBE/MGIMWA

HSC wanakampuni kibao za Clearing bandarini pale, wafanyabiashara wanalazimika kuwatumia hawa jamaa kutokana na kuwa na mkono TRA na wakubwa wa wizara ya fedha.

Ukijifanya unatumia kampuni nyingine kwa wafanyabiashara wa nguo, viatu, pazia na vinginevyo utapigwa ushuru wa kufa mtu. Ila ukitumia HSC container la nguo au kitenge unalipa mil.28 tunaambiwa jamaa yeye anacheza na wakubwa wa TRA anasema container lina Tooth pick au toilet paper yeye analipa TRA mil.7 dah kumbe zigo linathamani ya dola 170,000/= ishu ya Mwakyembe kuanza kukagua container imeanza kumuumbua bwana HSC na wakubwa wa TRA imesababisha taharuki kwa wafanya biashara k.koo mizigo imezuiliwa na biashara imesimama.

Serikali imepoteza sana mapato juu ya hawa jamaa HSC wanakula pia na polisi wanasindikiza toilet paper kumbe nguo au vitenge au tv au friji.


KITILYA/MWAKYEMBE/MGIWA

Mimi ni mfanyabiashara na nimefanya biashara na maagent wengi na hawa maclering wanazingua sana mambo yangu hapa ni machache kama ifuatavyo...

1. Hapa tusichanganye mambo ya vita za madaraka ya ukamishna wa tra, vita ya maclearing na maisha ya maskini

2. Hakuna asiyejua masamaki alikuwa manager wa mafuta na alivyokuwa anapitisha mafuta bure! Leo mafuta yanapita na mzigo wote anahamishia kwenye makontena

3. Hakuna asiyejua ubabaishaji, wizi, utapeli na rushwa wa BAADHI ya maclearing, kama ametokea clearing mwaminifu lazma biashara itahamia kwake

4. Maclearing wengi ni mawakala wa rushwa za macustom officer ! Hawawezi kumpenda mtu straight.
Sasa vita zao wasiingize na sisi maskini watuache tufanye kazi vita zao wamalizane wao wenyewe ...

SAWA SAWA KABISA

Bado sijaona mtu wa "KUMFANYA KITU" huyu jamaa!


sI HIYO TINDIKALI kashamwagiwa au unataka nini tena?


Jama ni habari ya Said si ya uongo, kwani wafanyabiashara wote wa kariakoo polisi na TRA wakiwakamata na mzigo wakisema mzigo huu unatoka kwa Said wanaachiwa lakini wakisema vinginevyo sero ya msimbazi polisi ya kwako au utoe rushwa ndevu, manake wakubwa wote wanajuwa habari za said, kwa hiyo inawalazimu wafanyabiasha wote kariakoo kumtumia Said kutoa mizigo yao Bandarin ili kukwepa kodi, Pili kiwe kizingiti wakikatwa na polisi au TRA.Saidi alipoandaa sherehe mwaka juzi je ni mkubwa gani wa nchi hii hakuwepo? au kutuma mwakilishi? na kupokea bahasha nononono.... anayejua aseme, Said yupo juu ya sheria nashangaa kwanini wamemsaliti?

KITILYA/MWAKYEMBE wanaweza kutoa majibu


TUWE MAKINI NA KINACHOENDELEA TATIZO SIO HOME SHOPPING CENTRE WADAU

Kiukweli inasikitisha sana kuona watu wachache wanaosaidia wanyonge wanachukiwa kwa misingi yao ya kibiashara
mimi ni CHADEMA FOR LIFE ila kwa hili CCM haihusiki na watendaji wanamtia aibu MH.Jakaya hapa kuna mambo matatu.

1.Kariakoo ilishakuwa Dubai ya nchi zote kongo, burundi, zambia, malawi, rwanda! Leo wanaenda uganda na kenya

2. Kodi itapungua, ajira itapungua, sisi hatujasoma tutaenda wapi

3. Nchi hii wabaya sio viongozi, wabaya watendaji! Na sisi tukiumia chuki zote kwa viongozi na ccm wao hata ikija chama kingine watabaki tu.

Mkutano ulioitishwa na waziri kuhusiana na kukwama mizigo bandarini ni kutokana na bidhaa kuwekewa kodi kubwa sana ambazo hazilipiki mizigo iliyokwama sio ya HSC ni wafanyabiashara mbalimbali na mkutano uliwahusu hao wadau wote hali ni mbaya...
tuliyoyashuhudia katika mkutano huu ni kama yafuatayo nilihudhulia kama mfanyabiashara niliyeadhirika na hili

A. Sisi wafanyabiashara ndio tunaoumia na kulipa kodi kwa mizigo inayoingia nchini lakini ajabu kubwa ya kutoa maoni walipewa mawakala wa forodha kuongea badala ya sisi wafanyabiashara ambao ndio waadhirika wakubwa wa ucheleweshwaji huu, ambao kwa kiasi kikubwa pia unawaadhiri wafanyabiashara wadogo na wananchi wa kawaida ambo bidhaa zetu ni kariakoo sehemu ambayo hao makamishna na mawaziri hawaji kununua chochote mambo yao ni ulaya na maduka makubwa huko posta kariakoo yetu hawaijui.

B. Mawakala wa forodha katika mkutano huu badala ya kujikita kujadiri sababu za msingi zinazosababisha mizigo ichelewe kutoka bandarini wao walitumia muda mwingi kushambuliana wao kwa wao kuhusu nani anapata kazi nyingi (vita ya kibiashara) jambo ambalo halikuwa lengo la mkutano huu na wala hatudhani mizigo kuchelewa kutokana na kampuni moja kupata kazi nyingi kuliko nyingine bali ni matatizo ya kiutendaji kwa hili Mh.waziri hakuambiwa ukweli kabisa mi naomba afike kariakoo ajioneee mwenyeweee.\

NB: Kilio chetu kama wafanyabiashara kuhusu ucheleweshaji wa mizigo ni suala la uthaminishaji mizigo (valuation) ambao maafisa wa TRA wanaweka bei kubwa sana kuliko ukweli kusababisha kodiinayotolewa kuwa kubwa kiwango ambacho hakilipiki.

kazi mnayo wafanywa biashara

HSC wanatumia frusa waliopewa na Serikali ya ccm,kukwepa kodi.

ccm ndio inayofuga ujinga huu, je tungekua na serikali makini mtendaji gani wa Serikali angekula rushwa.?

Tatizo serikalini hakuna mwadilifu, ndio maana mtu badala ya kuwajibishwa tunaambiwa ni upepo utapita.

Dawa ni kuikataa ccm kwa nguvu zote.!!

dont hate the playa, HATE THE GAME


HSC WANAJUA WANACHOKIFANYA...WATANZANIA WENGI WAVIVU UBUNIFU WA HAWA JAMAA UNAWACHANGANYA
DONT HATE THE PLAYER, HATE THE GAME...
Wakurugenzi wa Kampuni Hii wana Asili ya Saudia na Yemen,Wana Uhusiano wa Karibu na Viongozi wa Saudia Mtakumbuka alipokuwepo Balozi aliyepita wa Saudia waliwahi kupitia yeye HSC kutoa Pampu 800 Za Maji Zilizosambazwa Nchi Nzima Kusaidia Mama Zetu na Dada Zetu Vijijini kwa USHAWISHI wao
Mmoja kati ya Matajiri wa Dunia hii wa Kisaudia TRILIONAIRE PRINCE TALAL AL SAUD AL WALEED alipozuru Nchini Walikuwa Wenyeji na Ndio walimpokea Airport na ht Kumpeleka Kwa Viongozi wa Serikali na walihudhuria Mazungumzo ya Uwekezaji
Sasa Ajabu gani kwa Mtu anayejua Medani za Biashara za kimataifa Vijana hawa kuwa Matajiri??!

Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.

Isije kuwa anapigwa vita na CHADEMA na WACHAGGA?


Mada ni Home Shopping Centre au mada ni makontena kukwama bandarini?

Hivi hawa kina Rished Bade hili limewashinda kabisa?

BADE ANA RIPOTI KWA NANI?


Udhaifu mkubwa wa hii serikali katika kulinda vyanzo vyake vya mapato vimetuumiza sana kama nchi, nashngaa sana viongozi wetu kuona ni sawa kuomba omba kama wendawazimu huku wakishindwa kudhibiti mapato halali yenye heshima na utu hapa nyumbani...

KITILYA

Habari nilizopata toka kwa wafabiashara wa kariakoo ambao ndio waathirika wa makontena yalioko bandarini ni kuwa...

1.hsc ni bingwa wa kukwepa kodi Tanzania.
2.wafanyabiashara wakiagiza vitenge,tv,jenereta au hardware yeye kwenye kulipa bandarini anaandika tishu au net za msaada hivyo kulipa kidogo au kutolipa kabisa.
3.hsc ni Kampuni toka ikulu na vigogo wastaafu.
4.hsc haijakamatwa kwa bahati mbaya, na Mwakyembe kubadili utawala bandarini sio bahati mbaya Bali ni mpango maalumu.

Na kilichofanya hiyo Kampuni kuanikwa hadhani ni kitendo cha kuingilia tenda za vigogo wenzie akiwemo Zakaria na ishu ya betri za taiga.
Zaidi ni kitendo cha kutukanwa Mwakyembe na mkurugenzi wa hsc kwa kuambiwa Siwezi kuongea na wewe (Mwakyembe) naongea na mkubwa wako (jk)
Hivyo Mwakyembe nae akaamua liwalo na liwe kama uwaziri nifukuzwe tu Makotena hayatoki mpaka yalipe kodi halali.

Lakini mpaka sasa baada ya sakata la takribani miezi miwili juzi makotena yameanza kutolewa.!


dOOOOOOOOH kumbe mwakyembe alishatukanwa?
Lete ushahidi wa video au sauti


Naona pumzi Inaanza kunikatika habar nzito!!!


wewe jali ya kwako kisha uende mbele.
 
Gazeti la freeman mbowe wa chadema nalo halikuwa mbali kwenye kumsakama said. Je mbowe anaweza kuwa naye ni mtuhumiwa?

kikao cha waziri mgimwa, tra balaa



na mwandishi wetu







mawakala wa ushuru wa forodha (clearing agents) wenye uzalendo wameshtukia njama za kuwatumia kukwepa kodi kifisadi kupitia bandari ya dar es salaam na kuibua kiwewe kwa wahusika, imefahamika.

Hayo yalibainika katika kikao cha mawakala hao wakiwakilishwa na maofisa waandamizi wa kampuni zao na waziri wa fedha, dk. William mgimwa, kikao kilichohudhuriwa pia na wakuu wa mamlaka ya mapato tanzania (tra).

Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kwamba mawakala hao wapatao 150 walishtukia njama za wenzao waliojaribu kumpotosha waziri ili wazuie operesheni ya tra ya kuhakiki upya makontena yaliyokuwa yapitishwe bila kukaguliwa.


Baada ya kuwasikiliza mawakala hao na tra, waziri mgimwa ambaye awali alionekana kutaka kulainika, alitaka sheria ifuate mkondo wake na operesheni ya kukagua upya makontena uendelee ili kujiridhisha hakuna ukwepaji kodi wowote na watakaobainika wachukuliwe hatua.


Baada ya tanzania daima kuandika habari za ukwepaji kodi kutumia utaratibu halali wa tra kutoa mizigo inayolipiwa kodi bila kukaguliwa, mamlaka hiyo ilisitisha ghafla utaratibu huo ili kuchunguza madai ya kuwapo ukwepaji kodi mkubwa unaotajwa kuwahusisha vigogo ndani ya serikali na watu wazito.

"wenzetu waliingia katika kikao hicho wakiwa na mbinu chafu za kutaka kumtumia waziri awatishe tra ili makontena yao yanayokaribia 500 yatoke. Tukashtukia na kumwambia waziri utaratibu ufuatwe na yote yakaguliwe upya kujua yana nini ndani.


"wamedanganya kuwa baadhi ya makontena wamedanganya yana viatu toka dubai lakini ndani kuna magari, mengine wanasema kuna nguo za watoto kumbe kuna vitenge na vifaa vya electronics. Sasa kisheria ukishusha thamani ya mzigo tra wanapandisha lakini udanganyifu wa aina ya mzigo ni kosa la jinai unataifishwa na kushtakiwa," anasema mtoa habari wetu.


Katika kikao hicho, mawakala hao walimpongeza kamishna mkuu wa tra na wizara kwa kazi nzuri, lakini walilalamikia kitendo cha baadhi ya vigogo wa juu kuwaingilia katika kazi zao na hivyo kusababisha uhalifu unaofanywa na wakwepa kodi kuendelea kufanyika.


"waliondoka wakiwa wameinamisha vichwa chini ila wanachofanya sasa ni kueneza propaganda kwenye magazeti kwamba kuna usumbufu unaosababishwa na tra bandarini kumbe ni kuwabana wasikwepe kodi, hata kama kunakuwa na usumbufu, lakini ni vizuri kuokoa kodi," anasema.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, wahusika walikuwa wakitumia mwanya huo kwa kuficha thamani halisi ya mizigo na wakati mwingine kudanganya hata aina ya mizigo iliyomo ndani ya makontena na mara nyingi kwa kutumia nyaraka za kughushi.


Kampuni inayotajwa kuhusika kwa kiasi kikubwa ni ile maarufu kwa uuzaji wa bidhaa za nyumbani na wahusika wanaelezwa kujisahau sana na kufanya hadharani kwa kutumia majina ya vigogo wa juu serikalini.


"nasikia mpango wa haraka walionao ni kuwahonga maofisa wa tra wanaopangwa kwenda kufanya ukaguzi ili wakubaliane na kilichokuwa kimeandikwa kwenye nyaraka zao," anaeleza mtoa habari wetu.

Hata hivyo hali inaelezwa kuwa tete ndani ya tra kutokana na taarifa hizo kuvuja na kuwafanya vigogo kuhaha na baadhi kutaka hata kuitelekeza mizigo yao na wengine kuwasababishia hasara kubwa wafanyabiashara waliowatumia.


"waziri harrison mwakyembe aliambiwa haya yote alipokutana na wakurugenzi wa clearing & forwarding lakini pamoja na kujiita mpambanaji wa ufisadi alipuuzia kwa sababu zake mwenyewe mpaka vyombo vya habari viliporipoti na ndipo tra wamechukua hatua," anaeleza mtoa habari huyo.

Kwa takriban miaka mitatu iliyopita serikali kama njia ya kuondoa mizigo bandarini mapema kwa kuepusha mlundikano na msongamano wa mizigo bandarini iliruhusu baadhi ya mizigo ya wateja wakubwa iwe inachukuliwa bandarini bila kukaguliwa.


Kitendo hiki japo kilionekana kuwa na lengo zuri kilikosolewa na wengi kwa madai kuwa kingeweza kutumika vibaya na baadhi ya hao wateja wakubwa kwa kukwepa kodi.


Mmoja wa wateja wakubwa aliyelalamikiwa hata na baadhi ya vyombo vya habari ambaye anajishughulisha na biashara ya vifaa vya nyumbani, sasa anafanya biashara ya uwakala wa mizigo.


Katika kikao ambacho waziri wa uchukuzi, dk. Harrison mwakyembe alifanya na wakurugenzi wa makampuni ya mawakala wa forodha moja ya mambo yaliyojitokeza ni kutaja kwa majina kampuni za mfanyabiashara huyo na nyingine yenye kumiliki bandari kavu (icd), kuwa zinalindwa na wakubwa.

Wakati icd hiyo ya kuweka magari ikituhumiwa kwa utawala wa kudhalilisha na kuwatisha watanzania bila aibu, kampuni hiyo ya vifaa vya nyumbani inatuhumiwa na mawakala wa forodha kwa ukwepaji wa kodi.


Inadaiwa kampuni hiyo inayomilikiwa na ndugu wawili wenye asili ya kiarabu kuwa imekuwa na mtindo wa kuingia makubaliano na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa na wadogo hasa wanaofanya kwenye eneo la kariakoo kwamba mara waagizapo mizigo yao hasa kutoka china na dubai watumie kampuni yake au kampuni zake dada ambazo zingine zina leseni za kutolea mizigo bandarini kama njia ya kulipa kodi kidogo.


Wateja wanaokubali kutumia mpango huu haramu hulipa kwao sh milioni 17 kwa kontena moja la futi 40 na sh milioni 12 kwa kontena moja la futi 20.

Kampuni hizo zinazodaiwa kulindwa na wakubwa zinalipia tra sh milioni nane kwa kontena la futi 40 na milioni nne kwa kontena la futi 20 pamoja na gharama za bandarini ambazo si zaidi ya sh milioni 1.2.


"inashangaza serikali kila siku inahaha kutafuta vyanzo vipya vya kuongeza mapato wakati hiki kilichoko tena chenye uhakika kikidhalilishwa na walafi wachache kwa kushirikiana na wenye mamlaka," alisema mtoa habari wetu.




Kikao cha Waziri Mgimwa, TRA balaa
 
Back
Top Bottom