n00b
JF-Expert Member
- Apr 10, 2008
- 1,006
- 2,667
Wakuu,
Tetesi zilizonifikia ambazo SI NZURI (kwa tunaopenda kuona wenzetu hata tukiwa na tofauti nao) zinaashiria kama kuna kitu kisicho cha kawaida kimemkuta bwana huyu hii leo.
Vyanzo vyangu vya kuaminika vinanihabarisha kuwa bwana huyu yamemkuta ya kumkuta. Kuna mwenye kuwa na 'ukweli' au 'tetesi' zaidi?
==============
UPDATES:
==============
Taarifa za awali zinadai kamwagiwa Tindikali maeneo ya Msasani City Mall muda wa saa 2.
Ni jirani na Ubalozi wa Marekani na jirani kabisa na Police Oysterbay.
Jamaa aliyefanya kitendo hicho alitoka mbio, mlinzi akamkimbiza lakini bahati mbaya akateleza na kuanguka na jamaa akawahi pikipiki na kutoweka eneo la tukio.
Said amelazwa Trauma (AMI) Hosp - Masaki.
Kapata madhara macho yote mawili ila moja ndilo limeumia zaidi sehemu ya juu.
Mwenyewe anaweza kuzungumza japo amefungwa mashine sehemu ya pua na madaktari wanamhudumia.
Polisi wanahaha kutafuta wahusika kwa nguvu kubwa na huenda akakamatwa mhusika mapema sana.
==============
Some useful topics on JF:
Katika picha, ni eneo lilipotokea tukio la kumwagiwa Tindikali
Tetesi zilizonifikia ambazo SI NZURI (kwa tunaopenda kuona wenzetu hata tukiwa na tofauti nao) zinaashiria kama kuna kitu kisicho cha kawaida kimemkuta bwana huyu hii leo.
Vyanzo vyangu vya kuaminika vinanihabarisha kuwa bwana huyu yamemkuta ya kumkuta. Kuna mwenye kuwa na 'ukweli' au 'tetesi' zaidi?
==============
UPDATES:
==============
Taarifa za awali zinadai kamwagiwa Tindikali maeneo ya Msasani City Mall muda wa saa 2.
Ni jirani na Ubalozi wa Marekani na jirani kabisa na Police Oysterbay.
Jamaa aliyefanya kitendo hicho alitoka mbio, mlinzi akamkimbiza lakini bahati mbaya akateleza na kuanguka na jamaa akawahi pikipiki na kutoweka eneo la tukio.
Said amelazwa Trauma (AMI) Hosp - Masaki.
Kapata madhara macho yote mawili ila moja ndilo limeumia zaidi sehemu ya juu.
Mwenyewe anaweza kuzungumza japo amefungwa mashine sehemu ya pua na madaktari wanamhudumia.
Polisi wanahaha kutafuta wahusika kwa nguvu kubwa na huenda akakamatwa mhusika mapema sana.
==============
Some useful topics on JF:
- Mfanyabiashara Said Mohammed Saad wa Home Shopping Center
- Serikali imewekwa mfukoni na Said na Ghalib Saad wa Home Shopping Center?
==============Mmiliki wa Home Shopping Centre amwagiwa tindikali usoni|Dar es Salaam.
Mtu asiyejulikana juzi usiku alimvamia mmiliki wa maduka ya Home Shopping Centre, Said Mohammed Saad (pichani) na kumwagia maji usoni yanayodhaniwa kuwa ni tindikali.
Tukio hilo lililotokea juzi saa 1 usiku karibu na kituo cha Polisi cha Oysterbay, lilithibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Ally Mlege kwa kusema kuwa bado polisi wanaendelea na uchunguzi wao ili kuwabaini waliohusika.
"Ni kweli tukio hili limetokea ila polisi wanaendelea na uchunguzi. Tukikamilisha uchunguzi tunatarajia kutoa taarifa kamili za tukio zima," alisema na kuongeza;
"Hatuna haja ya kuficha ukweli wa tukio hili, uchunguzi wetu ukikamilika na watuhumiwa wakikamatwa kila mtu atajua."
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa mtu huyo, alimkuta Saad akiwa anazungumza na mmoja wa wafanyakazi wake katika duka lake jipya lililopo karibu na Kituo cha Polisi cha Oysterbay.
"Wakati akizungumza na mfanyakazi wake, huyo mtu alikuwa kama anapita na alichomoa kitu fulani na kummwagia Saad usoni na kisha kukimbia," zilieleza taarifa hizo na kuongeza;
"Baada ya tukio hilo alipelekwa katika Hospitali ya AMI, sasa hatujui kama bado yupo hapo au ameondoka, ila sisi tulizungumza naye na alitueleza mwonekano wa mtu aliyemwagia tindikali."
Taarifa hizo zilifafanua kwamba polisi wanazitumia taarifa hizo walizopewa na Saad, ili kuweza kumkamata mhusika.
Taarifa hizo zilifafanua kuwa polisi wanapanga tena siku ya kumhoji kwa mara ya pili Saad, kwamba watataka kufahamu kama mfanyabiashara huyo alikuwa akipewa vitisho au ujumbe wowote, kabla ya kukutwa na tukio hilo.
Hata hivyo, habari nyingine zilizolifikia Mwananchi Jumapili zilieleza kuwa mtu huyo baada ya kummwagia Saad tindikali, alipanda pikipiki na kutokomea eneo hilo.
"Walikuwa wawili, mmoja alikwenda kufanya unyama na mwingine alibakia katika pikipiki, baada tu ya kumwagia tindikali mtu yule alikimbia mpaka pale alipokuwa imesimama pikipiki, alipanda na kuondoka kwa kasi," zilieleza habari hizo.
Taarifa zilizopatikana jana asubuhi zilieleza kuwa ndugu na marafiki wa mfanyabiashara huyo, walikuwa katika mipango ya kumpeleka nje ya nchi kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.
Chanzo: Mwananchi
Katika picha, ni eneo lilipotokea tukio la kumwagiwa Tindikali