Einstein
Senior Member
- Dec 5, 2009
- 121
- 26
Siku za hivi karibuni, kumeibuka hisia kuwa India si mahala salama pa kusoma kwa watanzania.. Hisia hizi zimetokana na taarifa iliyotokea eneo la Bangalore, India ambapo kuna wanafunzi wa kitanzania walitaka kuchomewa nyumba waliyokuwa wakiishi(Ingawa sababu, binafsi sijaisikia)..
Kabla ya hapo pia kulikuwa na ile taarifa iliyohusu mtanzania mwenzetu aliefariki kwa kupoteza kichwa chake(Mungu ailaze roho yake mahali pema).
Lakini mi binafsi napinga kwa wanaosema kuwa India si mahali salama kwa kusoma!
Ntatoa sababu.
Kimsingi, ni kweli wahindi si watu wema sana kwa maana ya kitabia, kutokana na mila na desturi zao. Lakini tujiulize, sisi watanzania ni wema sana kuzidi wahindi? Jibu ni NO. Hata sisi tuna mapungufu yetu..
SABABU ZA KUSOMA INDIA..
1. Gharama ya Elimu katika nchi ya India ni ndogo ukilinganisha na Tanzania. Ni kweli kuna baadhi ya vyuo vya India ambavyo vina gharama kubwa kidogo, Lakini vyuo vingi India gharama si kubwa.. School fee, ina range kutoka $250 mpaka $700 kwa vyuo vya kawaida vinavyotambuliwa.
2. Gharama za kuishi India ni ndogo ukilinganisha na mahali pengine kama US na UK.. (US, UK na kadhalika ni kwa wenyenazo unless upate scholarship). Kwa mwezi ni, at least $250.
3. India ukilinganisha na Tanzania, they are much exposed kwenye maswala ya Technology(Hapa nagusia IT).. Makampuni mengi ya IT, kama Microsoft, IBM na kadhalika yamewekeza India. Miji kama Bangalore na Hyderabad ni baadhi kati ya miji inayofanya vizuri zaidi katika maswala ya IT.. Kwa hiyo ukisoma maeneo kama hayo accessibility ya Technology ni kubwa, kuliko ukiwa Bongo..
4. Admission ya vyuo vingi India (Si vyote), haihtaji uwe na credit nyingi ukilinganisha na Tanzania.. Maana Tanzania watu wakipata credit kidogo basi hupati admission inabidi urudishwe ukachunge ng'ombe.
5. Serikali ya Tanzania Imeshindwa kutoa mwongozo wa kuwafinyanga wanafunzi wasiojiweza kifedha (Ingawa wana academic background nzuri sana) wanaomaliza kidato cha sita (maana baadhi huacha masomo UDSM na kukimbilia Uhindini). Badala yake baadhi wanasomeshwa na scholarship toka India.
MATATIZO YA KUSOMA INDIA..
Hapa nitayagawanya matatizo ktk sehemu mbili..
Sehemu A: Kwa wanafunzi wanaotaka KUJINASUA.
Sehemu B: Kwa wanafunzi wanaotaka ANASA
Sehemu A:
Kwa wanafunzi wanaotaka KUJINASUA haya ndo baadhi ya matatizo wanayokumbana nayo..
1. Kuna kelele nyingi sana za wanafunzi madarasani (Wahindi husema wanapenda kupiga kelele just fo FUN), wakati wa lecture.
2. Mfumo wa ufundishaji uko tofauti na wa Tanzania maana mitihani huwa inafanyika kama vile mock na annual za Secondary school Tanzania(Ingawa si vyuo vyote)
3. Miji ya huku ina watu wengi, kwa hiyo kuna foleni kibao, Ingawa hawa jamaa wamejitahidi kupunguza kw kujenga flyovers ktk baadhi ya miji.
4. Wahindi ni wachafu(Ingawa si wote).
5. Degree colleges(Universities) zime kaa kaa kama Secondary za Bongo, kwa maana ya namna wana vyo wasimamia wanafunzi(Kuna vyuo vingine huwa wanafunga mageti ukichelewa kufika chuoni), pia baadhi ya vyuo majengo yake yamekaa ki ajabu ajabu utadhani majengo ya shule za msingi za Tanzania.
6. Wanafatilia sana mambo ya Attendance(Tofauti na UDSM, kwa baadhi ya kozi). Kama una attendance kidogo basi unaweza usifanye mitihani(India).
7. Chakula cha kihindi kina pilipili sana.
8. Wahindi wengi hawapendi kuchanganyika sana na foreigners, Ingawa si wote, wapo wanaopenda kuwa close na foreigners(Blacks).
9. N.K
Sehemu B:
Hawa ni kwa wanafunzi wanaotaka India iwe kama US. Hawa ni wale ambao wengi wao wanapenda starehe kuliko masomo.
Hawa pia wanapatwa na matatizo hayo hapo juu ila wao wana mengi zaidi
9. Inakuwa ni ngumu kwao kuchukua vimwana vya kihindi. Asilimia kubwa ya wasichana wa kihindi wanatunza bikra kama mboni ya macho yao. Kwa hiyo ikionekana uko karibu na mtoto wa kihindi unakuwa umejiweka kwenye matatizo(Kwa sehemu kubwa ya India).
10. Huwezi ukaachia mziki mzito mitaa unayokaa, unless kusiwe na familia za majirani wa kihindi karibu..
11. Ugomvi na police kwa sababu mbalimbali..
12. n.k
Conclusion:
Kuishi nchi za ugeni ni taabu, si kwa India tu. Ila kikubwa unatakiwa kufata sheria. Mila na desturi za kihindi zinaboa sana, ila kwa mtu unaetaka KUJINASUA matatizo ya 'sehemu A' yanavumilika.
Kwa 'sehemu B' kuna shida zaidi, maana India si kama US wala UK.. Huwezi ukawalazimisha wahindi uishi kama vile WESTERN COUNTRIES wanavyoishi, Hapa ndipo inapoonekana kuwa wahindi ni wabaya zaidi. Ndo maana kuna bango moja kubwa la kihindi mahala fulan Mumbai kwamba, INDIA WILL CHANGE U, U CAN'T CHANGE INDIA..
Kabla ya hapo pia kulikuwa na ile taarifa iliyohusu mtanzania mwenzetu aliefariki kwa kupoteza kichwa chake(Mungu ailaze roho yake mahali pema).
Lakini mi binafsi napinga kwa wanaosema kuwa India si mahali salama kwa kusoma!
Ntatoa sababu.
Kimsingi, ni kweli wahindi si watu wema sana kwa maana ya kitabia, kutokana na mila na desturi zao. Lakini tujiulize, sisi watanzania ni wema sana kuzidi wahindi? Jibu ni NO. Hata sisi tuna mapungufu yetu..
SABABU ZA KUSOMA INDIA..
1. Gharama ya Elimu katika nchi ya India ni ndogo ukilinganisha na Tanzania. Ni kweli kuna baadhi ya vyuo vya India ambavyo vina gharama kubwa kidogo, Lakini vyuo vingi India gharama si kubwa.. School fee, ina range kutoka $250 mpaka $700 kwa vyuo vya kawaida vinavyotambuliwa.
2. Gharama za kuishi India ni ndogo ukilinganisha na mahali pengine kama US na UK.. (US, UK na kadhalika ni kwa wenyenazo unless upate scholarship). Kwa mwezi ni, at least $250.
3. India ukilinganisha na Tanzania, they are much exposed kwenye maswala ya Technology(Hapa nagusia IT).. Makampuni mengi ya IT, kama Microsoft, IBM na kadhalika yamewekeza India. Miji kama Bangalore na Hyderabad ni baadhi kati ya miji inayofanya vizuri zaidi katika maswala ya IT.. Kwa hiyo ukisoma maeneo kama hayo accessibility ya Technology ni kubwa, kuliko ukiwa Bongo..
4. Admission ya vyuo vingi India (Si vyote), haihtaji uwe na credit nyingi ukilinganisha na Tanzania.. Maana Tanzania watu wakipata credit kidogo basi hupati admission inabidi urudishwe ukachunge ng'ombe.
5. Serikali ya Tanzania Imeshindwa kutoa mwongozo wa kuwafinyanga wanafunzi wasiojiweza kifedha (Ingawa wana academic background nzuri sana) wanaomaliza kidato cha sita (maana baadhi huacha masomo UDSM na kukimbilia Uhindini). Badala yake baadhi wanasomeshwa na scholarship toka India.
MATATIZO YA KUSOMA INDIA..
Hapa nitayagawanya matatizo ktk sehemu mbili..
Sehemu A: Kwa wanafunzi wanaotaka KUJINASUA.
Sehemu B: Kwa wanafunzi wanaotaka ANASA
Sehemu A:
Kwa wanafunzi wanaotaka KUJINASUA haya ndo baadhi ya matatizo wanayokumbana nayo..
1. Kuna kelele nyingi sana za wanafunzi madarasani (Wahindi husema wanapenda kupiga kelele just fo FUN), wakati wa lecture.
2. Mfumo wa ufundishaji uko tofauti na wa Tanzania maana mitihani huwa inafanyika kama vile mock na annual za Secondary school Tanzania(Ingawa si vyuo vyote)
3. Miji ya huku ina watu wengi, kwa hiyo kuna foleni kibao, Ingawa hawa jamaa wamejitahidi kupunguza kw kujenga flyovers ktk baadhi ya miji.
4. Wahindi ni wachafu(Ingawa si wote).
5. Degree colleges(Universities) zime kaa kaa kama Secondary za Bongo, kwa maana ya namna wana vyo wasimamia wanafunzi(Kuna vyuo vingine huwa wanafunga mageti ukichelewa kufika chuoni), pia baadhi ya vyuo majengo yake yamekaa ki ajabu ajabu utadhani majengo ya shule za msingi za Tanzania.
6. Wanafatilia sana mambo ya Attendance(Tofauti na UDSM, kwa baadhi ya kozi). Kama una attendance kidogo basi unaweza usifanye mitihani(India).
7. Chakula cha kihindi kina pilipili sana.
8. Wahindi wengi hawapendi kuchanganyika sana na foreigners, Ingawa si wote, wapo wanaopenda kuwa close na foreigners(Blacks).
9. N.K
Sehemu B:
Hawa ni kwa wanafunzi wanaotaka India iwe kama US. Hawa ni wale ambao wengi wao wanapenda starehe kuliko masomo.
Hawa pia wanapatwa na matatizo hayo hapo juu ila wao wana mengi zaidi
9. Inakuwa ni ngumu kwao kuchukua vimwana vya kihindi. Asilimia kubwa ya wasichana wa kihindi wanatunza bikra kama mboni ya macho yao. Kwa hiyo ikionekana uko karibu na mtoto wa kihindi unakuwa umejiweka kwenye matatizo(Kwa sehemu kubwa ya India).
10. Huwezi ukaachia mziki mzito mitaa unayokaa, unless kusiwe na familia za majirani wa kihindi karibu..
11. Ugomvi na police kwa sababu mbalimbali..
12. n.k
Conclusion:
Kuishi nchi za ugeni ni taabu, si kwa India tu. Ila kikubwa unatakiwa kufata sheria. Mila na desturi za kihindi zinaboa sana, ila kwa mtu unaetaka KUJINASUA matatizo ya 'sehemu A' yanavumilika.
Kwa 'sehemu B' kuna shida zaidi, maana India si kama US wala UK.. Huwezi ukawalazimisha wahindi uishi kama vile WESTERN COUNTRIES wanavyoishi, Hapa ndipo inapoonekana kuwa wahindi ni wabaya zaidi. Ndo maana kuna bango moja kubwa la kihindi mahala fulan Mumbai kwamba, INDIA WILL CHANGE U, U CAN'T CHANGE INDIA..