Regia Mtema

Status
Not open for further replies.
mada hii ni habari mchanganyiko au kwenye pongezi angekosea sana angeiweka kwenye celebrity. Ila habri mchanganyiko ndiko mahali pake.



Hivi hapa kuna hoja yeyote ya siasa? au Angalia hata comments 34 zilizopita kama kuna comment ina ideology yeyote sa siasa


teh teh teh

Nadhani kulikuwa na implied msg, mtoa hoja alitaka kumpongeza au kumuelezea Mh. Regia kutokana na nafasi yake kama mwanasiasa. Napingana na wazo kwamba ni celebrity. The mere fact kwamba ataenda kuchanganywa na Kanumba makes me shiver. Hapana Shy!! Kinachotakiwa kufanyika ni kuipanua hoja iwe 'Mh. Regia; mwanasiasa shupavu na hodari ambaye ni mfano wa kuigwa'. Hapo kwa kiasi fulani itaeleweka kwa nini hoja/mada yake ipo humu. Ni vizuri pia wanaomfahamu kama mwanasiasa wakatoa mchango wao kuonyesha uezo wake na pia kuchanganua mapungufu yake ili aweze kuyafanyia kazi na kuzidi kuwa bora. Ndio umuhimu wa jukwaa la siasa. Naamini kwamba hatufungwi na hoja za sera/itikadi peke yake. Na kwa leo tumechoka kufikiria Dowans na yanayohusiana nayo!! Angalau tumjadili yeye kwa mazuri!!

Jukwaa la siasa ni la wanasiasa!
 
Mie jamani pamoja nakuwa nakubaliana nanyie kuhusu sifa za Regia...lkn mimi namzimia mno hakyanani! yaani ananvutia mno hasa ile staili yake ya nywele kunyoa kawida inanifanya nione hana makuu hata nyumbani. hivi ameolewa jamani?
 
Sikuwahi kumuona tofauti na avatar yake hapa jf!
Nimemfahamu kupitia jf,na nilipojua anagombea ubunge,....to me she was and still is a hero!

Leo pale mabibo,nilitamani sana kumuona baada ya kujua atakuwepo pia!
Ilipofika mda wa zitto kumuita jukwaani nilishangazwa na swali alilo muuliza
"Utaweza kupanda hapa?" sikujua kwa nini,nilihisi labda kwa kuwa ni parefu sana!

Alipo panda na nikamuona,Sikuwahi kujua hali yake.
Kwa jinsi nilivo muona,.......REGIA MTEMA NI MWANAMKE JASIRI MWENYE UWEZO WA KUTHUBUTU NA NI MFANO WA KUIGWA KWA WAMAMA WOTE!

Am proud of you Regy....

Huyu Dada ni mpambanaji, hata JK anamuogopa, na ni kati ya wapambanaji-wanasiasa ambao JK na CCM wakimsikia wanajua moto aliowawashia hadi wakafikia kukimbiana ktk Jimbo la Kilombero.

God Bless You Regia, upo ktk role -models wa Real Politicians ktk ukombozi wa Taifa pamoja na makamanda halisi wa dira ya Taifa hili. Keep going and going...!
 
Punguzeni minyukano humu unnecessarily

Gad kulikoni? Roho ya huruma imekugusa! Kwa bahati mbaya Shy amegusa kipenzi cha watu! Mh. Regia bado ni mmoja wa viongozi ambao wako genuine na humble, hana makuu as a result ana wafuasi wengi wanaomuamini!!
 
mada hii ni habari mchanganyiko au kwenye pongezi angekosea sana angeiweka kwenye celebrity. Ila habri mchanganyiko ndiko mahali pake.



Hivi hapa kuna hoja yeyote ya siasa? au Angalia hata comments 34 zilizopita kama kuna comment ina ideology yeyote sa siasa


teh teh teh

mkuu ... kuwa mwepesi wa kujiri uhalisia... Regia ni mwanasiasa...hivyo ni part and parcel ya siasa..sio lazima itikadi au sera zijadiliwe katika jukwaa la siasa... hata chakula anachokula mwanasiasa kinaweza kujadiliwa katika jukwaa hili la siasa... je unamjua Regia Mtema kwa nini anapewa ujasiri ambao ni extraordinary...? mbona DOWANS ni kampuni ya kuzalisha umeme na inajadiliwa humu... si kwa sababu maamuzi yametolewa na wanasiasa..... there are direct and indirect attributes of situations
 
Namkubali sana Regia pia,ni kiongozi mwenye uchungu na watu wake,msikivu,mnyenyekevu na jasiri.

Nafurahi kuona amepambana kufika alipofika,anastahili na kweli ni mfano wa kuigwa na kinadada na kinamama.

Mungu azidi kumwinua,atuwakilishe vizuri na 2015 ashinde Kilombero awatumikie zaidi wananchi anaowapa kipaumbele.

Siongezi neno hapa
 
Regia sasa ni Mwana siasa. Na alikuwa kwenye Jukwaa la SIASA.

Unataka aweke wapi? Shy, acha kujifanya na wewe umekuwa KIRANJA ahhh Kiranga.

U-Kuhani si wa kuiga. Inabidi tu uwe hivyo siku zote na watu wakuzoee.

Speaker, usitishike na mtu hapa.

Regia ni kweli kabisa, katuaibisha hata sisi watani wake wa Sikonge
.

Hapo kwenye RED nimejitahidi kusoma na kurudia mara kumi, lakini sijaelewa kitu, labda mimi nina matatizo au wewe ndio tatizo zaidi. nitashukuru kama nitapata ufafanuzi.
 
Mie jamani pamoja nakuwa nakubaliana nanyie kuhusu sifa za Regia...lkn mimi namzimia mno hakyanani! yaani ananvutia mno hasa ile staili yake ya nywele kunyoa kawida inanifanya nione hana makuu hata nyumbani. hivi ameolewa jamani?

Mzizi, huwa sitetei kesi za mafumanizi. Sasa unachotafuta shauri yako! Mimi sijawahi kujiuliza kama ameolewa au la, wewe umethubutu! Kila la kheri na kuthubutu kwako!
 
Mzizi, huwa sitetei kesi za mafumanizi. Sasa unachotafuta shauri yako! Mimi sijawahi kujiuliza kama ameolewa au la, wewe umethubutu! Kila la kheri na kuthubutu kwako![/QUOT

Mkuu nikweli nimefika bei, ngoja...siku nikija kuonana nae ntamuuliza ikiwacameolewa au la, then ntajua pa kuanzia
 
Sikuwahi kumuona tofauti na avatar yake hapa jf!
Nimemfahamu kupitia jf,na nilipojua anagombea ubunge,....to me she was and still is a hero!

Leo pale mabibo,nilitamani sana kumuona baada ya kujua atakuwepo pia!
Ilipofika mda wa zitto kumuita jukwaani nilishangazwa na swali alilo muuliza
"Utaweza kupanda hapa?" sikujua kwa nini,nilihisi labda kwa kuwa ni parefu sana!

Alipo panda na nikamuona,Sikuwahi kujua hali yake.
Kwa jinsi nilivo muona,.......REGIA MTEMA NI MWANAMKE JASIRI MWENYE UWEZO WA KUTHUBUTU NA NI MFANO WA KUIGWA KWA WAMAMA WOTE!

Am proud of you Regy....

Lets respect sex please, lets describe her as a "Heroine" and not" Hero2
 
Huyu dada ni rafiki yangu wa karibu.Nimemfahamu tangu mwaka 2007,kwa kweli ni mfano wa kuigwa kwa kila jambo sio kisiasa peke yake.Ana akili sana,ana busara,ni mchapa kazi,mbunifu,ni muwazi na muadlifu yawezekana kuliko wanawake waote pale makao makuu ya chama.

Ni mpenda maendeleo na ni mwanamke mwenye kuthubutu kwa kila jambo.Kwa kweli binafsi namuadmire sana Regia,she is my role model.

Mnyika anaweza akamuelezea vizuri kuliko mtu mwingine yeyote pale Makao Makuu kwani yeye ndiye aliyemlea alipotua Makao Makuu.

Keep Going My Lady
 
Akina dada mnapaswa kuiga moyo na ujasiri wa mh mbunge Regia

Nina imani wale wadada machachari na cv zao humu waliopo ndani na nje ya nchi hii wakijitokeza kuwania ubunge wa kuchaguliuwa na hata viti maalum nina hakikia watashinda kwa 100%

Msiache nafasi zenu kuchukuliwa na waimba bongo flavour,taarabu,watangazaji na wale vimada wa wakulu

Hongera Regia umeonyesha njia nina hakika 2015 tutapata wengi kutoka humu wimbledon!
 
Hapo kwenye RED nimejitahidi kusoma na kurudia mara kumi, lakini sijaelewa kitu, labda mimi nina matatizo au wewe ndio tatizo zaidi. nitashukuru kama nitapata ufafanuzi.
mambo ya watani wa jadi!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom