emmanuel kajange
New Member
- Jan 29, 2014
- 1
- 1
Naunga Hoja hii biashara ya kuunda katiba ya kuridhishana tu itatu APTL na kutu ESCRO
Hatimaye hii hapa wadau! Jisomeeni.
ubarikiwe #professor umeniwezesha kupata rasmu ya ll na katiba pendekezwa ngoja nisome neno kwa neno maana hawa jamaa hawataki kutoa tujisomee mapema wanataka kutupiga kaunta ataki.
Mcheki Jaji Warioba nilimsikia akiichambua leo.
Hivi mtu na akili zake timamu anahusishaje katiba na vyama vya siasa,nadhani si haki hata kidogo mtu anapotaja chama fulani na kusema eti katiba ni ya chama hicho,huko ni kuwazarau watanzania,tuwatendee haki wananchi walioamua kuanzisha mchakato huu ambao ni watanzania wenyewe,hivyo juhudi hizi ni lazima ziungwe mkono
rasimu ii ya katiba mpya - sehemu ya kwanza
jina, mipaka, alama, lugha na tunu za taifa
ibara ya 1
ibara ndogo ya (1).
Jamhuri ya muungano wa tanzania ni nchi na shirikisho lenye mamlaka kamili ambalo limetokana na muungano wa nchi mbili za jamhuri ya tanganyika na jamhuri ya watu wa zanzibar, ambazo kabla ya hati ya makubaliano ya muungano ya mwaka 1964, zilikuwa nchi huru.
Ibara ndogo ya (2).
Jamhuri ya muungano wa tanzania ni shirikisho la kidemokrasia linalofuata mfumo wa vyama vingi vya siasa, usawa wa binadamu, kujitegemea, utawala wa sheria, kuheshimu haki za binadamu na lisilofungamana na dini.
Ibara ndogo ya (3).
Hati ya makubaliano ya muungano iliyorejewa katika ibara ndogo ya (1), ndio msingi mkuu wa jamhuri ya muungano wa tanzania na katiba hii, kwa kadri itakavyorekebishwa, itakuwa ni mwendelezo wa makubaliano hayo.
Tunu za Taifa 5. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaenzi na kuzingatia Tunu za Taifa zifuatazo: (a) lugha ya Kiswahili; (b) Muungano; (c) utu na udugu; na (d) amani na utulivu.
Je utoaju wa haki na kuenzi uwajibikaji sio tunu ya kutamaniwa? Nilidhani kuwa tukiwa na na tunu, kuzienzi pia kufuatane na kujenga tunu zitakazotupeleka mbele hasa vizazi vijavyo.
Katiba au mchi itakayoenzi na kupigania haki na uwajibikaji ndio yenye dalili ya kusonga mbele.
Nchi yetu iko mbioni kupoteza tunu ya amani, haki, uwajibikaji, lugha, utulivu n.k. ni muhimu sana kuziwekea mbele.
Ni aibu sana kiongozi kutokuwa na hisia ya kufungwa kuwa na hizi tunu.
Lazima mtanzania uweke mbele muungano, haki kwa wote, lugha, amani utulivu na uwajibikaji.
Huo ndio uzalendo.
Nadhani hii ni omission kubwa kimaadili kutoa uwajibikaji na utoaji wa haki katika tunu za taifa.
hiyo ni sura ya kwanza ya katiba yetu pendekezwa
eneo la jamhuri ya muungano wa tanzania 2.-(1) eneo la jamhuri ya muungano wa tanzania ni: (a) eneo lote la tanzania bara, ikiwa ni pamoja na eneo lake la bahari ambalo kabla ya muungano lilikuwa likiitwa jamhuri ya tanganyika pamoja na maeneo mengine yatakayoongezeka; na (b) eneo lote la zanzibar, ikiwa ni pamoja na eneo lake la bahari ambalo kabla ya muungano lilikuwa likiitwa jamhuri ya watu wa zanzibar pamoja na maeneo mengine yatakayoongezeka.
Kwa kuanzia hapa. Naomba kufahamishwa ilikuwaje jina tanganyika likatoka na zanzibar likabaki. Au tanzania bara likaanza na tanzania visiwani halikuanza?
2. Zanzibar ni visiwa vingapi?
Ubarikiwe #Professor umeniwezesha kupata rasmu ya ll na katiba pendekezwa ngoja nisome neno kwa neno maana hawa jamaa hawataki kutoa tujisomee mapema wanataka kutupiga kaunta ataki.
Hapo umenena USIEMPENDA KAJA. Zile Rasmu za Tume zimeshakuwa historical books inabidi zipelekwe maktaba na kwenye majumba ya makumbusho ya serikali. Na ikipendeza kwenye maktaba ya mwenyekigoda aliyekuwa akiongoza TMK.Sasa hivi tuna Katiba inayopendekezwa iliyopitishwa na BMK HIZO NYINGINE WALIZONAZOMWAKAFUNGIE VITUMBUA!