Rais Magufuli, bila kuwajali Watumishi wa Umma utakutana na Magumu zaidi ya Kikwete

Kwa maoni yangu, mimi siamini hata kidogo kwamba mheshimiwa rais Magufuli hatawakumbuka watumishi wa umma. Hiki ni kipindi kifupi tu cha mpito, siku zote kipindi cha mpito huwa ni kigumu japo siyo sana. Imani yangu ni kwamba, MAGUFULI atakuwa ni rais pekee ambaye ataleta mabadiliko chanya makubwa katika nchi yetu. Huyu ni rais ambaye ataleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi na kimfumo katika nchi yetu. Naomba tumpe muda, tuwe wavumilivu kidogo katika kipindi hiki kama watanzania wenzetu walivyovumilia wakati na baada ya vita vya Tanzania na Uganda.

Unaota???
 
Ni lini Rais Magufuli alisema anawanyima mishahara watumishi wa umma? Wanaoshughulikiwa ni wezi, wavivu, na wazembe. Iweje wanaofanya kazi kwa uadilifu wanung'unike? Hivi wooote mnaolalamikia hatua zinazochukuliwa mmewahi kukumbwa na uzembe wa watumishi wa umma waliojisahau kwamba wao ni watumishi umma na sio vinginevyo!
wewe unataja Magufuli sijui kwa nini! Wakati mmoja Mwalimu Nyerere aliagiza maduka ya ushirika yafunguliwe kote nchini watendaji wakafunga maduka binafsi ili yafunguliwe ya ushirika likatokea tatizo la ugavi. Nyerere akasema " nilisema fungueni maduka sikusema fungeni maduka..." Hebu tafakari kidogo mwenendo uliopo sasa hivi mfano polisi kuzuia hata mikutano ... Wewe unasema tu Magufuli!
 
ulichokiandika ni ukweli mtupu mwenye masikio na asikie na mwenye akili na afikiri....kijiji chetu vijana ambao ni watumishi wa umma wanasidia sana ndugu zao hasa kuwajengea nyumba wazazi wao ,kusemesha ndugu zao na kutatua matatizo ya mbalimbali ....sasa watu wanawaamini sana ...unapo wabana unawabana hadi wategemezi wote......
Rais wetu Magufuli anawajali sana watumishi kuliko unavyofikiri.
 
Hata kama watumishi wana mapungufu nchi imesonga mbele kupitia haohao watumishi. Zaidi ya kuwa ofisini wanachangia kwa kushiriki shughuli nyingi za kiuchumi tena kitaalamu. Mfano kiliimo, ufugaji na biashara. Haifai kuwabembeleza japo pia haifai kuwapuunza. Ni kama vile watumishi wanaonekana wezi, wavivu na mafisadi mbele ya jamii. Hii inafanya wasio watumishi kushangilia kuona namna wanavyosemwa na kutumbuiwa. Ni wanafamilia tu wanaowanea huruma ndugu zao.
Ni kweli tupu mkuu, kinachotakiwa ni kusawazisha mambo.
 
Miongoni mwa mambo yanayosababisha CCM iendelee kupoteza ni kuwapuuza watumishi wa Umma ikiwa namengineyo. Linaonekana kama jambo dogo ila amini kuwa watumishi wamebeba mnyororo mkubwa wa wategemezi, na ikiwa hawa ni wategemezi wao yaani baba, mama, Mjomba, Kaka, Dada na wengine weeengi ujue pia hawa wategemezi wanaheshimu mawazo ya hao wanaowategemea angalao kuendesha maisha yako kiasi fulani.Na ikatokea huyu mtumishi akilalamika kuwa serikali haiwajali, kumbuka hasira yaho (Wategemezi) inahamia kwenye serikali maana mkate unakuwa haupatikani.

Sasa hivi watumishi wa Umma wanaonekana si kitu kwako Mheshimiwa, wanafanyakazi kwa vitisho, Mshahara uko palepale wakati bei za bidhaa ziko juu. Usitaraji utafanya jambo ambalo litasaidia kupunguza ukali wa maisha zaidi ya kuwawezesha uliyonao ili nao wawawezeshe wengine. Hii ni Afrika na si Ulaya,tunategemeana saana.

Mwisho, ikumbukwe waliyochangia saana kuiangusha CCM ni Watumisi hususani wa Umma maana ndiyo wanaaminiwa na jamii yao kuliko mwanasiasa yeyote yule. Tumia wataalam wako kulichunguza hili utajua ukweli wa haya. Njaa mbaya saana, na maskini haaminiki.

"Magufuli bila Kuwajali Watumishi wa Umma utakutana na Magumu zaidi ya Kikwete"
kikwete alisema hazitaki kura za watumishi wa umma na bado akashinda
 
Binafsi si mwanakilio cha ongezeko la mshahara kwani hakuna mshahara utoshao hasa kwa maisha tuliyoyazoea watanzania wengi.. Mimi ni mwanakilio wa Mfumuko holela wa bei za bidhaa muhimu sokoni.. Naomba kuona jitihada madhubuti kutoka mamlaka husika katika kusimamia swala hili ili walau kuwepo na ahuweni baina ya kipato na matumizi.
 
Uhanga wako wa kukosa ajira isiwe kero kwa wengine. Ni vema ukakaa kimya usiku haya yatakusaidia nawewe kula yako hapo ulipo kwa ndugu yako.
kwa nini usiombe kustaafu au acha kazi kama unaona magufuli hawajali...umelifanyia nini cha maana Taifa hili wewe
 
Mimi Mjumbe tu Mkuu, na Mjumbe hauwawi sijawakejeri wala kuwatukana. Zaidi ya yote ni kuwasaidia wao badala ya kutumia nguvu watumie akili.
Hawataki na wala hawapendi kuambiwa ukweli. Ukiwaambia ukweli wanona kama vile umewatusi. Ni watukufu zaidi ya miungu yao.
 
Mh.anaamin nchi hii inaeza pelekwa kwa fikra za mtu mmoja ..na nimwepesi wa kuhesabu madhambi kama vile yey ni malaika na hajawah kosea...hatukatai ukweli kwamba mamlaka yote niyake under the law lakn sio juu ya sheria ,,,kitendo cha kutengua watumishi wa umma (wakurugenzi) na jukum lake kikatiba ndio lakn sio kuwaacha pending tena bila hata barua ya maelekezo duuuh,, iv hio nikatba ya wapiii? Tena cheo iko sio ata chakisiasa kwaio wanahaki ya kubakia kua watumish katka majukum mengine ...ninavo amin mm kunatofaut kat ya kutumbua na kutengua uteuz ..mh,rudi mezani angalia unapo hisi unastahili kurekebisha
 
Vidampa kweli kweli hao, kuwa wahanga wa kukosa ajira ndiyo wanaropoka tu pasi kuwaza.

Hawa vijana ambao wanataka kupata ajira kwa wenzao kufukuzwa kazi wana shida sana, mshahara wa serikali ni mdogo sana wala haukidhi mahitaji muhimu. Hajui kwamba wanaotetea maslahi mazuri ya wafanyakazi pia wanamfaidisha yeye hapo baadae. Hajui kwamba hata yeye akipata ajira hapo serikalinimaisha yatakuwa magumu pia.
 
Usiwe na akili fupi kama mkia wa mbuzi.hivi nikifika ofisini saa 10 za usiku nikaanza kucheza games kwenye PC then saa 12 jioni natoka je nitakuwa nimefanya kazi? Kuwahi kazini na kuchelewa kutoka si kipimo cha ufanyakazi bora.
Sasa wewe unafikiri unaweza kuwahi kazini ukafika mapema na pia kwa makusudi usifanye kazi...point hapa ni wewe kutimiza wajibu wako kutokana na kazi unayoifanya utakua ni mtu gani uwahi kazini halafu uishie kucheza game...
 
JPM anatafuta fairness kwenye suala la ajira. Maisha ya magumashi yana mwisho wake. Mleta mada kama unao ndugu zako waliozoea kuishi maisha hayo ya njia za mkato nenda uwaambie warudi shuleni, wakaumizw vichwa na sio kutegemea mteremko. Haya maisha yaliyojaa uonevu ambapo mtu anafaidika na mifumo ya rushwa kwenye utoaji wa elimu, yana mwisho wake, na ndio huu umeshawadia.
 
JPM anatafuta fairness kwenye suala la ajira. Maisha ya magumashi yana mwisho wake. Mleta mada kama unao ndugu zako waliozoea kuishi maisha hayo ya njia za mkato nenda uwaambie warudi shuleni, wakaumizw vichwa na sio kutegemea mteremko. Haya maisha yaliyojaa uonevu ambapo mtu anafaidika na mifumo ya rushwa kwenye utoaji wa elimu, yana mwisho wake, na ndio huu umeshawadia.


post zingine bana!!!!
 
Sio jambo la kupuuza hata kidogo, ukiwa jemadari mwenye maono halafu jeshi lako halina morali hufiki popote, watumishi ni chain kubwa sana sababu nchi yetu ina high rate ya wategemezi na asilimia kubwa ya watumishi ndio wategemewa wakuu
 
Back
Top Bottom