Rais Kikwete aagiza flyovers zijengwe Dar haraka sana

kama hizo barabara za hewani zitashuka toka mbinguni its ok. kama ni mpango mkakati ita ok!
 


Huku akiwaacha watumishi wake wakiendelea kujimegea ardhi maeneo ya baharini JK anaota barabara kama hizi sijui hapa Bongo utapitisha wapi vitu kama hivi watalipa watu wangapi fidia kama Mbagala na air port wameshemsha kuwalipa je watakapo anza kujenga hizo road itakuwaje?
 
Kamuagiza nani!?

Hivi anaelewa hata 'feasibility study' ya hii kazi inachukua muda gani?

Majuzi hapa wamesema wapo njiani kuleta train ziendazo kasi ya ajabu (kupitia kwenye reli ile ile ya mjerumani!!?)

Hivi uchaguzi mkuu ni mwezi wa ngapi vile!!?

Nadhani imefika muda sasa tusiwe na president mwanasiasa


Hapo ndo tujue siasa zilivyo kiboko...
Hii ya treni ilizinduliwa kabisa...japo mpango ulikuwa ipite kwenye hizo reli za mjerumani.lakini walizindua na ikaenda safari moja,sasa ni mwaka wa tatu hakuna kilichoendelea,....
 
Hapo ndo tujue siasa zilivyo kiboko...
Hii ya treni ilizinduliwa kabisa...japo mpango ulikuwa ipite kwenye hizo reli za mjerumani.lakini walizindua na ikaenda safari moja,sasa ni mwaka wa tatu hakuna kilichoendelea,....

acha kupotosha.wewe unazijua hizo treni kweli?
 
Kuna mambo mengi ambayo Mh! anaagiza yafanywe na hayafanyiki. Mradi wa mabasi ya kasi umeyeyuka na hatuambiwi kinachoendelea. Lakini je flyovers ndio suluhisho pekee la trafic jam Dar Es Salaam? Hayo magari yatakuwa yanapita kwenye hizo flyovers kwenda kupaki wapi? Magari kutoka pande zote za Dar na miji jirani yote yanaingia katikati ya mji. Mheshimiwa angefikiria vile vile akisha jenga hizo flyover na magari yakapita bila foleni ndefu kuingia mjini yataenda kupaki wapi?

Kwa mawazo yangu mepesi lingetafutwa suluhisho la muda mrefu kwa "kuwalazimisha kwa kupenda" wenye magari kutoingia na magari katikati ya jiji. Hii inaweza kufanyika kwa kuweka usafiri wa uhakika kutoka nje ya mji na kuweka parking salama za magari nje ya mji ambako usafiri huo wa uhakika utakuwa unaanzia. Kwa mfano, stendi ya mabasi ya ubungo inaweza kuacha iwe parking ya magari na kuwe na train ya kwenda kasi kutoka Ubungo kuingia mjini. Watu wanapaki magari pale na kuingia kwenye treni. Akimaliza kazi anapanda treni mpaka ubungo na kuchukua gari lake huyo kuelekea kibaha, mbezi, mwenge, n.k. Kunaweza kuwa na vituo vy treni kadhaa hapo mjini. Kwa njia hii watu hawataona haja ya kuingia na magari mjini kwani hii mbali ya kusaidia kupunguza matumizi ya mafuta, itasaidia kuokoa muda ambao mtu angetumia kwenye trafic jam.

Ni mawazo yangu ambayo yako open for criticism.

Tiba
 
......... Then, hao maofisa wa mipango miji wanafanya kazi gani sasa? unaweza kukuta wengine hata wamepanga manzese,na kwa nini hadi wapate amri kutoja juu? Tukija kwenye swala la flyovers ni kwamba linatekelezeka au ni kampeni tu? isije ikawa kama ile ya maisha bora.

unauliza wakati unajua jibu lake? ... isije ikawa kama ile ya maisha bora
 
Tiba, mawazo mazuri. Nadhani pia ingesaidia kama jiji lingeweka congestion charge kwa magari madogo kuingia sehemu fulani za mji kiasi kwamba yale magari ya ulazima tu ndio yaruhusiwe e.g utility vans, taxis. Congestion charge iwe juu kidogo.

Pia misafara ya mawaziri isisimamishe magari mengine, kwani wao nani?
 
Kuna mambo mengi ambayo Mh! anaagiza yafanywe na hayafanyiki. Mradi wa mabasi ya kasi umeyeyuka na hatuambiwi kinachoendelea. Lakini je flyovers ndio suluhisho pekee la trafic jam Dar Es Salaam? Hayo magari yatakuwa yanapita kwenye hizo flyovers kwenda kupaki wapi? Magari kutoka pande zote za Dar na miji jirani yote yanaingia katikati ya mji. Mheshimiwa angefikiria vile vile akisha jenga hizo flyover na magari yakapita bila foleni ndefu kuingia mjini yataenda kupaki wapi?

Kwa mawazo yangu mepesi lingetafutwa suluhisho la muda mrefu kwa "kuwalazimisha kwa kupenda" wenye magari kutoingia na magari katikati ya jiji. Hii inaweza kufanyika kwa kuweka usafiri wa uhakika kutoka nje ya mji na kuweka parking salama za magari nje ya mji ambako usafiri huo wa uhakika utakuwa unaanzia. Kwa mfano, stendi ya mabasi ya ubungo inaweza kuacha iwe parking ya magari na kuwe na train ya kwenda kasi kutoka Ubungo kuingia mjini. Watu wanapaki magari pale na kuingia kwenye treni. Akimaliza kazi anapanda treni mpaka ubungo na kuchukua gari lake huyo kuelekea kibaha, mbezi, mwenge, n.k. Kunaweza kuwa na vituo vy treni kadhaa hapo mjini. Kwa njia hii watu hawataona haja ya kuingia na magari mjini kwani hii mbali ya kusaidia kupunguza matumizi ya mafuta, itasaidia kuokoa muda ambao mtu angetumia kwenye trafic jam.

Ni mawazo yangu ambayo yako open for criticism.

Tiba

Mkuu hilo swala la parking si tatizo kubwa sana .zinaweza kujengwa parking zenye floor hadi sita hapo mjini. hii nayo ni biashara,mnaweza mkawa hadi na kadi zenu kabisa kuepusha usumbufu kwenye hizo parking.hili linawezekana tatizo ni mipango na utekelezaji hakuna.
"SALUTE"
 
Uyu Mzee awa CCM wenzake wanamchanganya,kwanza huo mradi mrahisi wa mabasi yaendayo kasi umemshinda yeye na CCm wenzake sasa anataka kulingiza taifa kwenye garama nyingine.
kwanza navyojua mimi ujenzi wa flyover ni garama sana kwa nchi iliyo tambarale(DSM) hizo flyover zinajengwa kwenye nchi zenye milima milima kwaiyo kukutanisha pande mbili za nchi inakuwa rahisi lakini kwa nchi kama yetu inabidi ujenge mlima kwa cement,
 
Tiba, mawazo mazuri. Nadhani pia ingesaidia kama jiji lingeweka congestion charge kwa magari madogo kuingia sehemu fulani za mji kiasi kwamba yale magari ya ulazima tu ndio yaruhusiwe e.g utility vans, taxis. Congestion charge iwe juu kidogo.

Pia misafara ya mawaziri isisimamishe magari mengine, kwani wao nani?

Mkuu nchi za wenzetu kuna baadhi ya barabara magari yasiyokuwa ya abiria hayaruhusiwi kupita na hivyo kutoa nafasi magari ya abiria na ambulance kutokwama kwenye traffic jam. Congestion fee inaweza kusaidia kupunguza idadi ya magari kuingia mjini lakini ili hii ifanyike lazima kwanza kuwe na usafiri wa uhakika kwanza kuingia mjini.

Hili tatizo la viongozi kufunga huduma za barabara kwa watumiaji wengine mpaka wao wapite kwanza kwa kweli inakera kupita kiasi.

Tiba
 
Si tunaambiwa mji utahamia Kiluvya!
Hizi barabara zao wange anza kuzijenga pale Kiluvya ili mji utakavyo tanuka mpaka Kibaha mambo ya foleni yatakuwa hayapo kabisa.
 
Lol...kila siku watu humu mnamlalamikia Kikwete. Waafrika bana. Wanajua sana kulalamika na kutoa maelezo na visingizio. Ikija kwenye kufanya na kutenda, zero.
 
Aisee....sasa hapa JK ndo anaponishangaza mimi!Unajua tamko kama hili linakuwa la kisiasa zaidi.Kwanini asikae na watu wake na kujipanga halafu inapofika simu anasema project ya kwanza ya flyover itaanza kesho.Vitu kama hivi vinapokosa utekelezaji ndo mheshimiwa anaonekana bomu...!Khaa....naomba mtu amueleze hilo....
 
Back
Top Bottom