Rai: Waziri aliyetuma SMS kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo awajibishwe!

Mkuu mawasiliano ya sms si mapya. Kutuma sms si dhambi ya kumfukuza mtu, hata kama uko nje ya mawasiliano rasmi. Siku hizi ofisi zina Whatsapp Group ambazo wanatumiana matangazo na taarifa mbalimbali, sio rasmi lakini taarifa zinafika haraka.
Hili jambo nalifananisha na kiranja wa shule kumtaarifu kiranja wa darasa kwamba kesho mwalimu mkuu anakuja kufanya ukaguzi fulani. Ni hiari yako kufanya au kutofanya. Kesho mwalimu mkuu ukija, ukionekana na makosa usioneshe ulikuwa na mawasiliano na kiranja wa shule, maana alikufanyia favour, lakini hujabebeka.
Kama mtu alitaka ufanye jambo jema akakutumia sms, si mbaya ukamsitiri. Je, unadhani sms isingetumwa nani angeonekana hawezi kazi? Muhongo au huyo Mama? Bila shaka Muhongo haguswi hata chembe.

Mkuu hujui serikali yetu inafanya vipi kazi.... utakuwa uko UN au umejiajiri.... waziri akutumie msg uache kutekeleza? Hujipendi..... na pale yule mama asingesema kwamba alipewa maelekezo hayo yeye alikuwa ni jipu moja kwa moja na yawezekana hata asingepewa muda wa kuandika hiyo barua.... angefukuzwa palepale..... ni uungwana wa waziri mkuu kutaka kujua undani zaidi na mdo uziri wa kumpa mtu nafasi ya kujieleza....
 
Hata mdau yeyote, ukipigwa maswali ya kushtukiza na kimtego lazima ubabaike. Wapo watu jasiri hata umkazie vipi na maswali yako atakujibu tena bila woga. Watu wenye hulka na uwezo huo ni wachache
 
Simu za ofisini kazi yake ni nini? Ni kwa ajili ya mawasiliano ya kiofisi vinginevyo waziondoe.
Siku hizi maofisini wakubwa wanapewa simu za mikononi kwa ajili ya mawasiliano ya ofisi.Sasa kama huwezi kupiga hizo simu kutoa maagizo ya kiofisi au kuandika meseji ya kiofisi ukiagiza jambo fulani lifanyike tatizo liko wapi? Basi viongozi maofisi wasipewe simu wanapoteza pesa za walipa kodi bure za nini kama hazitumiki kwa mawasiliano ya kiofisi.Wazitoe wabakie kuandikiana na kuagizana kwenye makaratasi.

Mimi serious sioni tatizo la Muhongo kuagiza kwa SMS tatizo limalizike ndani ya saa 24.Na sioni tatizo la yule mama kusema katekeleza alichoagizwa kwenye SMS.

Mfano waziri mkuu kaagiza kwa mdomo kuwa wapeleke ripoti hajaweka katika maandishi.Ni agizo halali kabisa na litatekelezwa sawa na angeagiza kwa kupiga simu au kuandika Sms lazima wangetekeleza.Wasingesema tunasubiri atuandikie kwenye karatasi asaini alete kwa dispatch ndio tutekeleze.

Ila nilichogundua yule mama ana uongo fulani anasema hazifanyi kazi wakati Waziri mkuu kauliza mbona zile kule zinafanya ndio akasema aliagizwa kwa sms zifanye kazi.Yaani anajikanyaga kiaina fulani hivi.Ngoja akaandike maelezo labda ataeleweka vizuri.

Mkuu maelezo yako ni mazuri labda unifahamishe.... kwa nini for the past 5yrs flow meters zilikuwa hazifanyi kazi na zimeanza fanya kazi 24hrs tena kwa maelekezo ya sms kabla waziri mkuu hajatembelea eneo husika?
 
Namuaminia Magufuli, yeye yuko upande wa wananchi zaidi, ngoja wampe uenyekiti wa sisiemu ndo shughuli tutaiona!
Magu ajitoe kafara, awe shujaa atayekumbukwa daima, aipige chini katiba pendekezwa ya sisiemu na apitishe wa warioba watu tukaipigie kura za NDIO.

Kwa taarifa yako CCM ndani kwa ndani hawataki kumpa huo uwenyekiti maana wanajua ni shidaaaaaa yaani watu wanasema ngojeni mtasikilizia mziki wakimpa tuuu uwenyekiti kwisha CCM wezi wote wankimbia
 
Huyo Prof. Muhongo alikua akimuokoa huyo Mama, inaelekea walikaa Baraza la Mawaziri ku-discuss hii issue ndio Prof. Muhongo akavujisha taarifa kwa Mama (Mtuhumiwa). Huyu nae ni Jipu kama majipu mengine

Aliyevujisha siri awe Muhongo au la ni jipu na atakaethibitishwa hatua zichukuliwe. Huyo mama yeye ana kesi yake yake ya kujibu-hata kama kuna wanao myumbisha yeye ndie mwenye madaraka na waziri mkuu atamtaka awajibike. Je ni kweli aliomletea message alitaka kumuokoa huyu mama au alitaka kujiokoa yeye mwenyewe au watu wengine? Sidhani kama uamuzi wa kutumia kijiti ulikuwa wa huyu mama peke yake. Huenda kuna mtandao na JPM akifanya kazi yake vizuri huu mtandao utafahamika na kutumbuliwa. Yasiishie kwa huyu mama tu.
 
.......juzi yake nilikuwa namuangalia waziri wa viwanda mh mwijage alivyokuwa anajigamba kuwa hakuna ukwepaji kodi wowote wa mafuta bandarini .....sasa hivi sijui yupo wapi aje ajibu haya madudu ya serikali ya kazi tu....
Do u trust him?yeye mwenyewe muuza mafuta
 
Huyo chuwa aliulizwa na waziri mkuu, kama mliacha kupima mafuta kwa hizi mashine miaka 5 iliyopita kwa kuwa walikuwa wanalalamika mashine si sahihi kwa nini meanza kuzitumia jana wakati mimi nakuja leo, mehakiki kwa kikao gani kama hizi mashine sasa zianze kutumika? Chuwa akajiuma uma eti bado hazijaanza kutumika mh. huoni hii ina kutu, waziri mkuu akamuuliza na hiyo hapo mbona inafanya kazi ndipo akasema ameandikwa msg. na waziri mshine zianze kazi. Hapo ndipo shida mashine inafanya kazi cku moja wakati waziri kapanga kutembelea hapo. kuna majipu kati ya hawa mawaziri watumbuliwe.


Muhongo mus go.mzimu wa escrow unamuandama
 
Hapo ndo tutajua kwamba , Majipu
yote ni sawasawa ama la ,DOUBLE STANDARD
inaonekana
 
Tumeliwa vya kutosha mpaka damu zimekauka. Sasa imetosha, hivi vijipu uchungu vipo vingi sana na viendelee kutumbuliwa
 
Aliyevujisha siri awe Muhongo au la ni jipu na atakaethibitishwa hatua zichukuliwe. Huyo mama yeye ana kesi yake yake ya kujibu-hata kama kuna wanao myumbisha yeye ndie mwenye madaraka na waziri mkuu atamtaka awajibike. Je ni kweli aliomletea message alitaka kumuokoa huyu mama au alitaka kujiokoa yeye mwenyewe au watu wengine? Sidhani kama uamuzi wa kutumia kijiti ulikuwa wa huyu mama peke yake. Huenda kuna mtandao na JPM akifanya kazi yake vizuri huu mtandao utafahamika na kutumbuliwa. Yasiishie kwa huyu mama tu.
Ukitokea wizi nchi hii wanawajibishwa wa chini tu,wa juu na wafanyabiashara hubak salama salmin
 
JPM ameanza vizuri kwa kuhakikisha anajipanga na kutekenya ambapo kunaweza kukaleta fedha (BANDARI na TRA). Akimaliza kuweka mambo sawa ndani ndipo atembeze bakuli. Lakini hawezi kutembeza bakuli wakati limetoboka. Kuhusu katiba, piga ua laziama ile version ya Mzee Warioba irejewe. Mfano kama JPM angelikuwa na uwezo wa kupata mawaziri nje ya Bunge nadhani dhahama hizi zisingetokea. Haya ni mawazo yangu tu

Tanzania hii tusizungumze habari ya bakuli hata kidogo!
Uwezo wakujitegemea upo sana na kwa mwendo huu tutafika! Usimchekee nyani hata siku mmoja! Lakini tusishau naye anastahili kuishi. Wafanya biashara wakisimamiwa ni wadau wa Maendeleo wazuri tu-muhimu Watumishi wa Umma waache upolisi na mbaya mwisho wa siku ni kwa masilahi ya Mifuko yao Binafsi!

Ufisadi unatokana na Watumishi wa Bovu na wasiojali maendeleo ya Nchi!. Mkuu wa Nchi akiwa mfano na asiye na masihara tunaweza kusogea!. Lakini iwe ndiyo mfumo na siyo one man Show.


Mfano. CDM wanasema Sera ya Majimbo- lakini kama CCM hawataki hilo na Raisi kweli hakuna mbadala?
Kwa jinsi Ufisadi ulivyo tamalaki kushinda unahitaji jeshi dogo na kwa maana hiyo unafuta Ofisi zote za DC nchi nzima na kwa Mkurugenzi anayeteuliwa na Raisi anawajibika kwa Mkuu wa Mkoa ,kwa Waziri na Mwisho Raisi.
Kwa njia hiyo kila mhusika anafanya kazi 24hrs kuatafuta nini kinaendelea kila kona ya eneo lake la Mamlaka.
 
Katiba ni FASHENI tu sasa hivi ya kudai mabadiliko, ila trust me katiba hiyo hata tukiipata mambo yataendelea kuwa hivi hivi, maana kuna kina sisiemu alafu eti mbadala kuna kina mbowe, kizazi cha kuibadili tz bado wazazi wao hawajazaliwa.
Magufuli anajaribu ila kazungukwa na mamba sisiemu na pia ktk upinzani. Wee ebu jifikirie eti ukawa wanataka lowassa ndo alete mabadiliko, mfumo my asss!
Rasimu ya Warioba hata ikiwa katiba ya Tz itakuwa nzuri ktk makaratasi tu.
Namuombea sana Magufuli na Majaliwa na wachapa kazi wenzao Mungu awalinde na kuwajaza ujasiri wafanikiwe ktk kuleta maendeleo!

Hatu wazi miaka mitano au kumi-tunawaza miaka 100 na ushe ijayo!.
Leo mbowe kesho nani?
Leo Magufuli 2020 atakuwa nani?
Katiba sahihi inatoa mwanya wa Raia yeyote wa JMTZ kuweza kufikishwa mbele ya Mahakama bila kujali yeye nani!
Lakini pia inaipa mamlaka taasi kuu za Dola kila mmoja kuwa na nguvu yake bila kuingiliwa au kuwa na harufu ya kuingilwa katika utendaji wake!. Kwa kuanzia eneo la uteuzi,eneo la Bajeti nk.
 
Acha
Taarifa kuhusu hiyo mita kutokufanya kazi ziliandikwa kwenye gazeti vizuri sana.Waziri Muhongo akasoma akaliona hilo.Alipoliona akamwagiza mkuu wa Vipimo hakikisha mita inafanya kazi ndani ya masaa 24.Huyo mama mkuu wa vipimo akahakikisha inafanya kazi ndani ya masaa 24.Waziri mkuu kaenda kakuta tayari inafanya kazi .Tatizo la waziri Muhongo liko wapi?

Ila tatizo ninaloliona ni kwa nini Mita hizo hazikuwa zikifanya kazi kabla ya agizo la waziri Muhongo? Kulikuwa na nini? Nani mzembe hapo ndipo kimbembe kinabidi kianze na jipu husika litumbuliwe.



Acha upumbavu,unatumia nguvu nyingi kuuficha Ukweli lakini unasahau kuwa Ukweli hauhitaji mtetezi,unasimama wenyewe.

Mitambo hiyo haijafanya Kazi takribani miaka 5 iliyopita na ndani ya muda huo huyo unayejaribu kumtakasa kwa jiki,alihudumu katika Wizara hiyo kama Waziri wa nishati na madini.Kwa maana nyingine ni kwamba alikuwa bosi wa Wizara kipindi chote ambacho mitambo hiyo ilikuwa haifanyi Kazi.

Hoja hapa ni kwa nini mitambo hiyo ilizimwa?Ilizimwa kwa amri ya nani? Kwa nini huyo unayejaribu kumtakasa hapa na kamwe hatakasiki"labda ukamlambe kwa ulimi" alinyamanzia kuzimwa kwa mitambo hiyo?

Usifikiri sote tumezipeleka akili zetu likizo au tumelala,tupo macho tunausoma mchezo wenu kimyakimya.Endeleeni kuleta maigizo,kama kweli Magufuli ana nia ya dhati ya kutumbua majipu kama anavyojinasibu,basi anapaswa aitumbue CCM.

CCM ndiyo jipu kuu linaloitafuna na kuiozesha nchi yetu.Ili Taifa lipate uponyaji wa mwili,"ngariba wetu wa majipu" anapaswa alitumbue hili jipu kuku liitwalo CCM.Siku atakapoomba aombewe ili alitumbue hili jipu(CCM),nipo tayari kufunga na kuomba kwa ajili yake ili apewe nguvu na ujasiri wa kulitumbua hili jipu kuu liitwalo CCM.

Hakuna aliye msafi ndani ya CCM,uvundo wote unaotoa harufu kali zinazotishia uhai wa mapafu yetu,umefanywa na haohao ambao leo wanajaribu kutujia kwa jina la Malaika wa nuru,kumbe ni madhetani wenye mapembe.Eti wanatumbua majipu,thubutuuu,mwambieni huyo "ngariba wenu aende Wizara ya ujenzi na uchukuzi,mbona kila kukicha ni muhimbili na bandarini tu? Aende na huko alipotoka kama hajatokomea mazima.

Ni jambo la wakati tu,watanzania watazielewa hizi " muvi" za majipu,hapo ndipo watakapochachamaa na kuanza kuwadai waigizaji wa muvi hizi za majipu walipe kodi ya serikali kwani sanaa yao imeuza sana lakini serikali haijaambulia hata senti moja ya kodi ya muvi hizi za majipu.
 
Tuwe wakweli, hii issue kama ilivyokuwa kwa makontena si ya mtu mmoja au wawili, kuna mtandao mkubwa sana nyuma yake. Kumbe ndiyo maana hata vituo vya mafuta vilikuwa vinaota kama uyoga mpaka kwenye makazi ya watu. Hii nchi kweli ilioza
 
Taarifa kuhusu hiyo mita kutokufanya kazi ziliandikwa kwenye gazeti vizuri sana.Waziri Muhongo akasoma akaliona hilo.Alipoliona akamwagiza mkuu wa Vipimo hakikisha mita inafanya kazi ndani ya masaa 24.Huyo mama mkuu wa vipimo akahakikisha inafanya kazi ndani ya masaa 24.Waziri mkuu kaenda kakuta tayari inafanya kazi .Tatizo la waziri Muhongo liko wapi?

Ila tatizo ninaloliona ni kwa nini Mita hizo hazikuwa zikifanya kazi kabla ya agizo la waziri Muhongo? Kulikuwa na nini? Nani mzembe hapo ndipo kimbembe kinabidi kianze na jipu husika litumbuliwe.
Sijawah ona maagizo ya kiofisi yakitolewa kwa sms
 
Mkuu maelezo yako ni mazuri labda unifahamishe.... kwa nini for the past 5yrs flow meters zilikuwa hazifanyi kazi na zimeanza fanya kazi 24hrs tena kwa maelekezo ya sms kabla waziri mkuu hajatembelea eneo husika?

Siku za mwizi 40.Unaweza mtu kuwa kibaka weee miaka kibao hata 40.Kuna siku ya kudakwa.Ukidakwa kusema miaka yote hiyo mbona ulikuwa hujadakwa na uliokuwa ukishirikiana nao miaka yote mbona hawakudakwa? sio swala la msingi sana.Cha msingi vibaka wa meter Flow wamedakwa
 
Back
Top Bottom