Posho za wabunge zapanda kimyakimya!

Tumepata tulicholipia! Si mliwachagua wenyewe sasa mwalalama nini?
Anyway...na zile nyumba walizokuwa wanajengewa zimefikia wapi?
UBUNGE NI BONGE LA DILI!

Sasa wewe ulitaka watu wasichague wabunge? Kumbuka hii siyo ishu ya CCM au Chadema, kila mbunge anakula posho sawa ya bunge.
 
Nimekubali hakuna biashara inayolipa vizuri kwa sasa kama ubunge. 200,000 kwa siku? Enough is enough!

bungeletu.jpg

Kikao cha Bunge kikiendelea mjini Dodoma


ZAPANDA KUTOKA SH70, 000 HADI 200,000, NI ZAIDI YA ASILIMIA 150
Fredy Azzah

HUKU mjadala wa kufutwa au kwa posho za wabunge na watumishi wengine wa Serikali ukiwa umefifia, posho za vikao (sitting allowance) za wabunge zimepanda kutoka Sh70,000 kwa siku hadi Sh200,000, imefahamika.

“Zimeongezeka kutoka Sh70,000 mpaka 200,000, wameanza kulipwa Bunge lililopita hili ni ongezeko la karibu mara tatu, yaani asilimia 154,” kilieleza chanzo chetu kutoka ndani ya Ofisi za Bunge.

Kutoka na ongezeko hilo, kwa sasa kila mbunge atakuwa akilipwa Sh80,000 ikiwa ni posho ya kujikimu (perdiem) anapokuwa nje jimbo lake, posho ya vikao (sitting allowance) Sh200,000 na mafuta ya gari Sh50,000 kila siku, ambazo jumla yake ni Sh330,000 kwa siku.

Kutokana na ongezeko hilo, Bajeti ya Bunge kwa ajili ya posho za vikao vya wabunge imepanda na kufikia Sh28 bilioni kwa mwaka.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alipoulizwa kuhusu taarifa hizo alisema hawezi kuzungumzia jambo hilo kwa sababu siyo msemaji wa wabunge, bali Ofisi ya Bunge.

“Ni nani kawapa hizo taarifa bwana, au ni vyanzo vyenu vya habari?” alihoji Dk Kashililah.

Baada ya kuelezwa kuwa taarifa hizo zimetoka kwenye vyanzo vyetu vya kuaminika alisema “Hao wana utaratibu wao bwana, labda mtafute Spika ndiye msemaji wa Wabunge.”

Juhudi za kumpata Spika, Anne Makinda kutoa ufafanuzi wa suala hili, hazikufanikiwa baada ya simu yake kuita wakati wote bila kupokewa hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu (sms) hakujibu. Hata simu zote za Naibu wake, Job Ndugai hazikupatikana.

Hata hivyo, Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe alisema kuongezeka kwa posho hizo kunatokana na wabunge kuwa wanalipwa mishahara midogo kulingana na kazi wanayofanya.

Alisema endapo wawakilishi hao wa wananchi wangekuwa wanalipwa mishahara inayolingana na kazi wanayofanya, kusingekuwa na sababu ya kuongezeka kwa posho hizo.

“Ninachosema mimi, siyo wabunge peke yao, lakini watumishi wote wa umma wanalipwa mishahara midogo sana mimi binafsi sitegemei posho za Bunge, kabla ya kuingia bungeni nilikuwa nimefanya kazi kwa miaka 14 na nilikuwa napata mshahara mzuri tu,” alisema Filikunjombe.

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alisema amezisikia taarifa hizo za kuongezeka kwa posho lakini siyo kwa undani. Hata hivyo alisema hakuwa katika nafasi nzuri ya kuzungumza suala hilo.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema walivyokuwa wakipinga posho hizo wakati zilivyokuwa Sh70,000 waandishi wa habari walichukua suala hilo kama ajenda ya Chadema, hivyo kupandishwa kwa posho hizo ni matokeo ya watu kuwapuuza walivyokuwa wakizipinga.

“Msimamo wetu sisi tulishautoa tangu wakati posho zikiwa Sh70,000 wakati sisi tukipinga hizi posho waandishi wa habari na Watanzania mlichukulia suala hili kama ajenda ya Chadema, sisi wenyewe tupo wachache bungeni, tulichotaka ni kuonyesha jinsi fedha za Watanzania zinavyotumika vibaya,” alisema na kuongeza:

“Achilia mbali hizo 200,000 za wabunge kuna watu huko serikalini wanalipwa mpaka Sh400,000 au Sh1 milioni kwa siku nyie ulizeni.”

Alipoulizwa kama amechukua posho hiyo ya Sh200,000 alisema hajafanya hivyo kwa sababu hazifuatilii.

“Sijui hata kama zimeanza kulipwa au la kwa sababu huwa sizifuatilii na haka kama suala la posho hilo zilijadiliwa wakati wa vikao vya mwanzo mimi sikuwepo kwa sababu tulikuwa kwenye kesi yetu Arusha na bungeni tulikuja mwishoni wakati wa Muswada wa Katiba,” alisema Mbowe.

Ongezeko hili la posho za wabunge limekuja wakati Watanzania wakiendelea kuishi kwenye maisha magumu yanayochangiwa na mfumuko wa bei ambao mpaka mwisho mwa Oktoba ulikuwa umefikia asilimia 17.9.

Pia ongezeko hili limekuja wakati Watanzania wakiwa na matumaini ya posho hizi kupunguzwa baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutangaza bungeni kuwa Serikali imekubali pendekezo la kutafakari na kuziangalia upya posho mbalimbali wanazolipwa wabunge na watumishi wote umma.

Mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali alisema kuwa hawezi kuzungumza chochote juu ya posho hizo kwa kuwa hajapata barua rasmi juu ya kupanda kwake.

“Sijapata barua yoyote, nikiuliza na kupata majibu kwa wahusika nitakuwa na uhakika na nitakupa maoni yangu na msimamo wangu vizuri kabisa, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote,” alisema Mkosamali.

Juni 7, mwaka huu Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Zitto Kabwe, aliwasilisha barua Ofisi ya Bunge akikataa posho akisema watumishi wa Serikali na wabunge, hawastahili kulipwa posho wanapohudhuria vikao rasmi vya uwajibikaji wao wa kawaida.

Zitto alisema posho hiyo haistahili kulipwa kwake, wabunge wengine wala watumishi wa umma kwa kuwa kuhudhuria vikao ni sehemu ya kazi zao.

Alisema kitendo cha Waziri Mkuu kueleza kuwa watatafakari na kuangalia upya na kwamba suala la posho ni sera ya taifa na Ilani ya Uchaguzi ya CCM, ni ishara ya kiongozi huyo wa juu kukubali wazo la Chadema na safari ya kufuta posho hizo.

Awali, mara baada ya Chadema kutangaza msimamo huo, Spika Makinda alipinga uamuzi wa kususia posho akisema suala hilo lipo kisheria na kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kuamua kuliondoa.

Alisema wabunge wa Chadema wataendelea kulipwa posho za vikao kupitia akaunti zao za benki na watatakiwa kusaini fomu ya mahudhurio ya Bunge, vinginevyo watajiweka katika wakati mbaya.

Hata hivyo, akihitimisha hoja za wabunge katika hotuba yake ya makadirio ya matumizi ya ofisi yake na zilizo chini yake juzi, Pinda alisema suala la posho lipo kwenye mchakato wa kuangaliwa upya.

Wana JF,
Nikitizama kwa makini nakuja kugundua hali ya umaskini na hali ya ugumu wa maisha katika taifa hili inasikitisha sana na halii hii inavyo endelea ni kuwafanya watanzania kuwazia kuwa ukiwa kiongozi serikalini kwenye siasa kama mbunge diwani mayor ni ulaji mzuri na wananchi wanawazia hilo kumbe wana sahau kuwa uongozi huo au nyadhifa hizo ni kuwajibika kwa jamii iliyo kuteuwa kuwa hapo na unapewa dhamana ya kusimamia shughuri zote na utekelezaji wake wote kwa wananchi na kuleta maendeleo katika jamii hiyo.

Kuwepo na mfumo mbaya au usimamiaji mbovu au uongozi potofu na duni wa viongozi walio pewa dhamana ya wananchi kumeleta ugonjwa mbaya sana wa kila mtanzania kufikilia kuwa ukiwa kiongozi katika nyadhifa nilizo zitaja ni kuukimbia umaskini hii inatujengea nini watanzania. ??? wananchi wote tumekodolea hiyo mishahara kwanini hakuna chochote bunge linacho kifanya linasimami nini kuhusu serikali??? Maisha ya wananchi bunge linalo simamia hiyo serikali ni magumu kupita maelezo serikali imeshindwa kudhibiti mfumuko wa bei ya vyakula nchini wananchi hawajui wale nini kesho?

Nchi zingine mkate ukipanda bei tu watu wako barabarani kupinga ongezo la bei nchi hii mkiingia barabarani police waja na mabomu alafu JK anasema nchi hii sio ya ki dectetor ???? wapi na wapi jamani


 
Kwa hiyo hadi Dr Lusinde Livingstone na Profesa Majimarefu watakuwa wanalamba hiyo pesa?! Duu 'ITS NOT FAIR'
 
Tanzania hatuwezi kuondokana na huu umaskini, kama tukiendelea kuongozwa na hawa viongozi walafi.
 
Sasa! pesa zote hizo mbona bado wapo wanaosinzia? ni aibu!!
Na mkumbuke wabunge hawazalishi chochote zaidi ya maneno ambayo nayo vilevile hawaelewani.Du! Mungu tunusuru!!!!
 
Halafu bado wanawalipa wenzao 100,000 kwa mwezi,pia na walimu wanaambiwa wasubiri kwanza serikali haina pesa.............ipo siku tutapigana risasi for greater good of the nation.
 
Wabunge hawana uchungu na watanzania, kweli nimekubali "mwenye nacho huongezewa".

Ok! Tanzania ni nchi maskini, sawa. Kwanini hiki kidogo tulicho nacho tusigawane kwa uwiano sawa. Kwanini wao wanajimegea kipande kikubwa ilihali wanajua kuwa tupo wengi tunaotegemea hicho kipande?.

Wanafunzi wangapi wa vyuo vikuu wamekosa kuripoti chuo kwa kukosa mikopo. Kwanini bunge lisingewafikiria hawa nao, japo nao wapate mgao kidogo. Je gharama za maisha zimepanda kwa wabunge tu au watanzania kwa ujumla?. Ugumu wa maisha unawahusu wabunge tu?.

Shule ngapi za kata hazna madawati, wanafunzi wanakaa chini. Je wabunge hili hawajaliona?.

Inasikitisha kuwa ubunge tena si kwa ajili ya kumwakilisha mtanzania bali kwa sasa imekuwa ni biashara.

Hebu we mbunge jifikirie, utajisikia faraja kupata posho ya 330,000/=@ sikuwa wakati kuna kundi kubwa la wapiga kura wako wanaishi chini ya dola moja.
Kipi kilicho washawishi kupandisha posho 154%?. Kama mnaona sifa tuongezeeni basi na sisi mishahara walau kwa 100% kwani hata hukvu kwetu gharama za maisha zimepanda.


Mungu awalaani nyote na familia zenu.
 
Hili ongezeko watalifidia vipi wakati bajeti imeshapita?. Huu ni uhuni.
 
duh, na mimi naanza kampeni kabla ya wakati niingie mjengoni 2015 muhula mmoja tu unanitosha.
 
Nimekubali hakuna biashara inayolipa vizuri kwa sasa kama ubunge. 200,000 kwa siku? Enough is enough!

bungeletu.jpg

Kikao cha Bunge kikiendelea mjini Dodoma


ZAPANDA KUTOKA SH70, 000 HADI 200,000, NI ZAIDI YA ASILIMIA 150
Fredy Azzah

HUKU mjadala wa kufutwa au kwa posho za wabunge na watumishi wengine wa Serikali ukiwa umefifia, posho za vikao (sitting allowance) za wabunge zimepanda kutoka Sh70,000 kwa siku hadi Sh200,000, imefahamika.

“Zimeongezeka kutoka Sh70,000 mpaka 200,000, wameanza kulipwa Bunge lililopita hili ni ongezeko la karibu mara tatu, yaani asilimia 154,” kilieleza chanzo chetu kutoka ndani ya Ofisi za Bunge.

Kutoka na ongezeko hilo, kwa sasa kila mbunge atakuwa akilipwa Sh80,000 ikiwa ni posho ya kujikimu (perdiem) anapokuwa nje jimbo lake, posho ya vikao (sitting allowance) Sh200,000 na mafuta ya gari Sh50,000 kila siku, ambazo jumla yake ni Sh330,000 kwa siku.

Kutokana na ongezeko hilo, Bajeti ya Bunge kwa ajili ya posho za vikao vya wabunge imepanda na kufikia Sh28 bilioni kwa mwaka.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alipoulizwa kuhusu taarifa hizo alisema hawezi kuzungumzia jambo hilo kwa sababu siyo msemaji wa wabunge, bali Ofisi ya Bunge.

“Ni nani kawapa hizo taarifa bwana, au ni vyanzo vyenu vya habari?” alihoji Dk Kashililah.

Baada ya kuelezwa kuwa taarifa hizo zimetoka kwenye vyanzo vyetu vya kuaminika alisema “Hao wana utaratibu wao bwana, labda mtafute Spika ndiye msemaji wa Wabunge.”

Juhudi za kumpata Spika, Anne Makinda kutoa ufafanuzi wa suala hili, hazikufanikiwa baada ya simu yake kuita wakati wote bila kupokewa hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu (sms) hakujibu. Hata simu zote za Naibu wake, Job Ndugai hazikupatikana.

Hata hivyo, Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe alisema kuongezeka kwa posho hizo kunatokana na wabunge kuwa wanalipwa mishahara midogo kulingana na kazi wanayofanya.

Alisema endapo wawakilishi hao wa wananchi wangekuwa wanalipwa mishahara inayolingana na kazi wanayofanya, kusingekuwa na sababu ya kuongezeka kwa posho hizo.

“Ninachosema mimi, siyo wabunge peke yao, lakini watumishi wote wa umma wanalipwa mishahara midogo sana mimi binafsi sitegemei posho za Bunge, kabla ya kuingia bungeni nilikuwa nimefanya kazi kwa miaka 14 na nilikuwa napata mshahara mzuri tu,” alisema Filikunjombe.

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alisema amezisikia taarifa hizo za kuongezeka kwa posho lakini siyo kwa undani. Hata hivyo alisema hakuwa katika nafasi nzuri ya kuzungumza suala hilo.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema walivyokuwa wakipinga posho hizo wakati zilivyokuwa Sh70,000 waandishi wa habari walichukua suala hilo kama ajenda ya Chadema, hivyo kupandishwa kwa posho hizo ni matokeo ya watu kuwapuuza walivyokuwa wakizipinga.

“Msimamo wetu sisi tulishautoa tangu wakati posho zikiwa Sh70,000 wakati sisi tukipinga hizi posho waandishi wa habari na Watanzania mlichukulia suala hili kama ajenda ya Chadema, sisi wenyewe tupo wachache bungeni, tulichotaka ni kuonyesha jinsi fedha za Watanzania zinavyotumika vibaya,” alisema na kuongeza:

“Achilia mbali hizo 200,000 za wabunge kuna watu huko serikalini wanalipwa mpaka Sh400,000 au Sh1 milioni kwa siku nyie ulizeni.”

Alipoulizwa kama amechukua posho hiyo ya Sh200,000 alisema hajafanya hivyo kwa sababu hazifuatilii.

“Sijui hata kama zimeanza kulipwa au la kwa sababu huwa sizifuatilii na haka kama suala la posho hilo zilijadiliwa wakati wa vikao vya mwanzo mimi sikuwepo kwa sababu tulikuwa kwenye kesi yetu Arusha na bungeni tulikuja mwishoni wakati wa Muswada wa Katiba,” alisema Mbowe.

Ongezeko hili la posho za wabunge limekuja wakati Watanzania wakiendelea kuishi kwenye maisha magumu yanayochangiwa na mfumuko wa bei ambao mpaka mwisho mwa Oktoba ulikuwa umefikia asilimia 17.9.

Pia ongezeko hili limekuja wakati Watanzania wakiwa na matumaini ya posho hizi kupunguzwa baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutangaza bungeni kuwa Serikali imekubali pendekezo la kutafakari na kuziangalia upya posho mbalimbali wanazolipwa wabunge na watumishi wote umma.

Mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali alisema kuwa hawezi kuzungumza chochote juu ya posho hizo kwa kuwa hajapata barua rasmi juu ya kupanda kwake.

“Sijapata barua yoyote, nikiuliza na kupata majibu kwa wahusika nitakuwa na uhakika na nitakupa maoni yangu na msimamo wangu vizuri kabisa, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote,” alisema Mkosamali.

Juni 7, mwaka huu Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Zitto Kabwe, aliwasilisha barua Ofisi ya Bunge akikataa posho akisema watumishi wa Serikali na wabunge, hawastahili kulipwa posho wanapohudhuria vikao rasmi vya uwajibikaji wao wa kawaida.

Zitto alisema posho hiyo haistahili kulipwa kwake, wabunge wengine wala watumishi wa umma kwa kuwa kuhudhuria vikao ni sehemu ya kazi zao.

Alisema kitendo cha Waziri Mkuu kueleza kuwa watatafakari na kuangalia upya na kwamba suala la posho ni sera ya taifa na Ilani ya Uchaguzi ya CCM, ni ishara ya kiongozi huyo wa juu kukubali wazo la Chadema na safari ya kufuta posho hizo.

Awali, mara baada ya Chadema kutangaza msimamo huo, Spika Makinda alipinga uamuzi wa kususia posho akisema suala hilo lipo kisheria na kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kuamua kuliondoa.

Alisema wabunge wa Chadema wataendelea kulipwa posho za vikao kupitia akaunti zao za benki na watatakiwa kusaini fomu ya mahudhurio ya Bunge, vinginevyo watajiweka katika wakati mbaya.

Hata hivyo, akihitimisha hoja za wabunge katika hotuba yake ya makadirio ya matumizi ya ofisi yake na zilizo ch
Wajinufaishe cha mwisho kwani mapinduzi yaja
 
Hili ongezeko watalifidia vipi wakati bajeti imeshapita?. Huu ni uhuni.


Mhhhh! Sikutegemea kusoma bandiko kama hili toka kwako hasa ukitilia maanani ulivyo mtetezi mkubwa wa magamba hapa jamvini. Mimi nimeguswa na msimamo wa huyu Makamba.

~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*

Makamba ashtushwa
Mbunge wa Bumbuli, January Makamba, alieleza kushangazwa na ongezeko hilo la ghafla akisema kamwe wabunge wasifikiri kuwa wanaweza kumaliza matatizo yao au ya wapigakura wao kwa fedha ya posho.
Alisema kitendo cha wabunge kuongezewa posho za vikao kwa asilimia 185.7, kinaleta jazba kwa wananchi ambao wanahangaika kila kukicha kwa ugumu wa maisha.

"Kwenye jamii lazima kuwe na usawa, kama watu tupo kwenye hali mbaya (ugumu wa maisha) lazima wote tuenende sawa. Wabunge kuongezewa posho kwa asilimia 185 siyo sawa kabisa, tunajiweka mbali na wananchi na wanatuona tunafaidika sana wakati wao wanateseka kwa ugumu wa maisha," alisema Makamba.

Alisema kuwa, kutokana na msimamo wake huo, Juni mwaka huu alikataa posho iliyotolewa na Wizara ya Nishati na Madini baada ya kuhudhuria semina iliyoandaliwa na wizara hiyo.

"Tulikaa kwenye semina kwa saa mbili, tunamaliza naletewa karatasi nisaini posho ya Sh280,000. Nilikataa. Nilikataa kwa sababu nilitambua kuwa ile ni kazi yangu kama mbunge, sasa unanilipa hela ya kazi gani?" alihoji Makamba.

SOURCE: Mwananchi


 
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema walivyokuwa wakipinga posho hizo wakati zilivyokuwa Sh70,000 waandishi wa habari walichukua suala hilo kama ajenda ya Chadema, hivyo kupandishwa kwa posho hizo ni matokeo ya watu kuwapuuza walivyokuwa wakizipinga.
 
naomba kujua hivi wabunge wakikataa hizi posho (eg ZITTO & MAKAMBA) pesa zinapelekwa wapi

maana kwenye halmashauri zetu mtu asipo chukua haki yake kuna uwezekano mkubwa sana watu kuzichuka na ku"sign''
 
Posho za wabunge zazua mjadala
Send to a friend
Monday, 28 November 2011 21:26


zitto%20kabwe%20top.jpg
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe

Waandishi Wetu
NYONGEZA ya posho za wabunge imewakera wasomi, wanasiasa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(Tucta) ambao kwa nyakati tofauti jana, walieleza kutoridhishwa na hatua hiyo.Posho za vikao vya wabunge imeongezeka kutoka Sh70,000 kwa siku walizokuwa wakilipwa awali, mpaka Sh200,000 fedha ambayo ilianza kulipwa tangu Mkutano wa Bunge uliopita.

Kutokana na ongezeko hilo, kwa sasa kila mbunge atakuwa akilipwa Sh80,000 kama posho ya kujikimu anapokuwa nje ya jimbo lake, posho ya vikao (sitting allowance) Sh200,000 na mafuta ya gari Sh50,000 kila siku sawa na Sh 330,000 kwa siku.

Nyongeza hiyo ya posho za vikao imefanya bajeti ya Bunge kwa ajili ya posho za vikao kufikia Sh28 bilioni kwa mwaka.

Zitto adai ni usaliti
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, alisema kuwa ameshtushwa na taarifa za kupandishwa kwa posho za vikao kwa wabunge huku wananchi wakiugulia ugumu wa maisha na kusema kuwa ipo siku Watanzania watawapiga mawe kwa usaliti huo.

"Nimeshtushwa zaidi kwamba posho hizi zimeanza kulipwa katika mkutano wa Bunge uliopita kabla hata Rais hajaamua, maana maslahi yote ya wabunge huamuliwa na Rais baada ya kupokea mapendekezo ya Bunge kupitia Tume ya Bunge," alisema Zitto.

Aliwataka wabunge wote kutambua kwamba, kuamua kujipandishia posho bila kuzingatia hali ya maisha ya mwananchi wa kawaida ni usaliti usio na mfano.

"Mbunge yeyote ambaye anabariki jambo hili labda anaishi hewani, haoni taabu za wananchi au ni mwizi tu na anaona ubunge ni kama nafasi ya kujitajirisha binafsi," alisema Zitto.

Aliwataka pia wabunge wa Chadema, wajue uamuzi kuhusu posho ni wa chama na ni wa kisera.
"Mbunge yeyote wa Chadema anayepokea posho za vikao anakwenda kinyume na maamuzi ya sera za chama tulizoahidi wananchi wakati wa uchaguzi," alisema Zitto.

Alisema kuwa amemwomba Katibu Mkuu wa chama chake kuitisha kikao maalumu cha Kamati Kuu ya chama kujadili suala hilo.
Alisema kuwa tangu Juni 8 mwaka huu, alikataa kupokea posho za vikao na kuwa, popote anapohudhuria vikao huwa anaomba risiti za posho anazokataa.

"Baadhi ya wabunge kama Januari Makamba wamekataa posho na hata kwenye semina ya kamati ya nishati alikataa na tumeona kwenye vyombo vya habari jina lake likiwa limekatwa ilhali viongozi wakubwa kabisa wamechukua posho," alisema Zitto.
Alieleza kwamba anampongeza Makamba kwa uzalendo wake na kuwataka wabunge wengine wenye moyo wa dhati kukataa siyo tu ongezeko la posho bali posho yote ya vikao.
" Kwa nini mbunge akubali kulipwa kwa kukaa? Tazama nchi hii, juzi Serikali ilipokea msaada wa Sh20 bilioni kwa ajili ya Sensa ya mwakani wakati wabunge wanalipwa Sh28 bilioni kama posho ya kukaa tu kwa mwaka," alisema Zitto.
Tucta wawaka

Akizungumza na Mwananchi jana, Katibu Mkuu wa Tucta, Nicolaus Mgaya alisema kitendo cha wabunge hao kujiongezea posho ni ishara ya kushindwa kutetea maslahi ya wananchi wao waliowapeleka bungeni.

"Tucta inalaani kitendo cha wabunge kujiongezea posho kubwa kama hizo huku wakijua kuwa wananchi waliowachagua wanawategemea wao, hasa katika kipindi hiki kigumu cha maisha. Jambo hilo linaonyesha wazi kuwa hawako kwa ajili ya kutetea maslahi ya wananchi, bali kujinufaisha wenyewe," alisema Mgaya.

Alisema wabunge hao wameshindwa kujali hali ya wananchi wao hasa katika kipindi hiki cha mfumuko wa bei, hali ngumu ya maisha na migongano ya hapa na pale, badala yake wameamua kujipigia debe ili waweze kunufaika wenyewe. "Nasema hawafai, huu ni unyonyaji,"alisema.

AlisemaTucta inapinga kitendo hicho na imeitaka Serikali kuangalia upya suala la posho ili kusiwe na matabaka kati ya wabunge na wafanyakazi wengine ambao ndio msingi wa uchumi wa taifa.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema uamuzi wa kuongeza posho kwa wabunge unatakiwa kuchukuliwa kwa umakini kwa kuwa suala hilo limepigiwa kelele kwa muda mrefu.

"Tanzania ni nchi masikini, vipaumbele vya kulikomboa taifa letu vipo vingi na bado havijatekelezwa. Ubunge ni utumishi na kama ni hivyo wabunge wanatakiwa kuishi kama wanavyoishi wananchi wengine," alisema Dk Bana.

Mhadhiri mwingine wa Chuo hicho, Bashiru Ally alisema suala hilo litatengeneza matabaka kati ya aliye nacho na asiye nacho.
"Tunapaswa tujenge taifa la kujitegemea kulingana na hali ya uchumi wetu na sio kuiga mambo ya watu, watawala kupenda kuwa katika nafasi za juu kwa misingi ya kupata fedha ni tatizo," alisema Bashiru.

Shibuda adai posho muhimu
Mbunge wa Maswa Mashariki (Chadema), John Shibuda alisema suala la wabunge kuongezewa posho halina ubaya wowote kwa kuwa litawafanya wasiwe ombaomba.

Shibuda ambaye katika mkutano wa Bunge la Bajeti alipingana na sera ya chama chake iliyokuwa katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010 kuhusu posho za vikao, alisema ili mbunge atekeleze majukumu yake vizuri ni lazima alipwe fedha ya kutosha.
"Umefikia wakati Waafrika tulinde fedheha kwa viongozi wetu ili wasiwe ombaomba. Viongozi wakilipwa vizuri wataweza kuitumikia nchi na jamii inayowazunguka, ipasavyo. Kutokulipwa vizuri ndio mwanzo wa viongozi kusaini mikataba mibovu," alisema Shibuda.

Makamba ashtushwa
Mbunge wa Bumbuli, January Makamba, alieleza kushangazwa na ongezeko hilo la ghafla akisema kamwe wabunge wasifikiri kuwa wanaweza kumaliza matatizo yao au ya wapigakura wao kwa fedha ya posho.
Alisema kitendo cha wabunge kuongezewa posho za vikao kwa asilimia 185.7, kinaleta jazba kwa wananchi ambao wanahangaika kila kukicha kwa ugumu wa maisha.

"Kwenye jamii lazima kuwe na usawa, kama watu tupo kwenye hali mbaya (ugumu wa maisha) lazima wote tuenende sawa. Wabunge kuongezewa posho kwa asilimia 185 siyo sawa kabisa, tunajiweka mbali na wananchi na wanatuona tunafaidika sana wakati wao wanateseka kwa ugumu wa maisha," alisema Makamba.

Alisema kuwa, kutokana na msimamo wake huo, Juni mwaka huu alikataa posho iliyotolewa na Wizara ya Nishati na Madini baada ya kuhudhuria semina iliyoandaliwa na wizara hiyo.

"Tulikaa kwenye semina kwa saa mbili, tunamaliza naletewa karatasi nisaini posho ya Sh280,000. Nilikataa. Nilikataa kwa sababu nilitambua kuwa ile ni kazi yangu kama mbunge, sasa unanilipa hela ya kazi gani?" alihoji Makamba.

Habari hii imeandaliwa na Fredy Azzah, Frederick Katulanda, Mwanza, Patricia Kimelemeta, Fidelis Butahe na Ellen Manyangu

 
Kuna taarifa kwamba wabunge wamejiongezea malipo ya vikao vya bunge kutoka sh 70,000 kwa siku hadi 200,000 kwa siku.Nataka kujua hivi wabunge wa CHADEMA nao wamejua hali hii na kukubali kweli kuchukua viwango vipya ?

Nataka jibu moja ,(Kati ya NDIYO Na HAPANA) kutoka kwa wanaojua ,sitaki maelezo !

nitarejea baada ya majibu
 
Miswaada bungeni huwa inapitishwa na Magamba wakitumia wingi wao na hili wamelipitisha kwa mtindo huo sasa wewe ulifikiri Chadema wafanyeje????
Usitake tu Ndiyo & Habana taka ufafanuzi Ila Kama Umetumwa gangamala na swali lako lakini cha msingi ungewauliza wabunge Wa Magamba wao wangekujibu.
 
Back
Top Bottom