Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,499
- 113,610
Wanabodi,
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi kuhusu Maslahi ya Taifa, ambazo ni kuhusu jambo lolote la Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii . Bandiko la leo ni pongezi kwa Rais Samia na serikali yake, kukubali kubadili sheria ya uchaguzi, na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi!. Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.
Nilipata fursa kuhudhuria kongamano la siku 3 la vyama vya siasa nchini, lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kujadili ripoti ya Kikosi Kazi cha Rais Samia, na mapendekezo yake kuelekea chaguzi za serikali za mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, uliofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, JNICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Naomba nianze kwa kutoa maoni yangu, kwanza nampongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi kutathmini hali ya siasa nchini, nakipongeza kikosi kazi kwa kazi nzuri, naipongeza serikali yetu kwa kukubali mapendekezo ya kikosi kazi, kukubali kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi kuunda Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi.
Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.
Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.
Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...
Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.
Pendekezo la pili, ni tufanye uchaguzi wote kwa siku moja, na kusimamiwa na Tume moja huru ya uchaguzi. Kama Zanzibar wanaweza kufanya chaguzi 5 kwa siku moja, Tanzania hatuwezi kushindwa kufanya chaguzi 4 kwa siku moja!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!
Hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 halafu uchaguzi Mkuu 2025, kwa sasa tufanye mabadiliko ya katiba na sheria, halafu 2025 tufanye chaguzi zote 4 kwa siku moja, Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa.
Kongamano hilo lilifunguliwa na Rais Samia ambaye ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa nchini kutumia mikutano ya hadhara kutoa hoja na fikra zenye tija zinazolenga kuimarisha utendaji serikalini.
Aidha, Rais Samia amevitaka vyama vya siasa kutumia mikutano ya hadhara kujitangaza ili kukua kisiasa na kuutumia uhuru wa kujieleza kutoa mawazo mbadala yatakayoendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.
Rais Samia pia amesema uhuru wa kutoa maoni kusisababishe kudhalilisha watu
wengine, kuibua hisia za kidini, ukabila au kubaguana kwa misingi yoyote ile.
Vile vile, Rais Samia amesisitiza kutumia uhuru huo vizuri bila kuingilia haki na
uhuru wa watu wengine pamoja na kufuata sheria, kanuni na taratibu.
“Katika shukrani nisisahau Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakiongozwa na Jaji Mutungi, Jaji Mutungi saa zingine ananipigia simu usiku we mama wee hii kazi uliyonipa nimekwama hapa na hapa, umeaminiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nenda na kazi yako, ukikwama fedha niambie lakini mengine fanya kazi yako, kwa hiyo nakushukuru umefanya kazi yako na mmefikia pazuri”, alisema Rais Samia.
Rais Samia amesema kuwa Serikali imepokea ripoti ya kikosi kazi ambapo Serikali imeyapitia mapendekezo hayo kupitia vikosi kadhaa vilivyongalia mambo kadhaa yanayohitaji wataalamu hususan yanayohusu sheria na Bunge likalo, itapeleka marekebisho ya sheria kadhaa ikiwemo sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Rais Samia amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi waliopendekezwa wamefanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea Watanzania na Wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulika na masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa ratiba ya utekelezaji itaanza na mabadiliko ya sheria kadha ambazo zitapelekwa Bungeni kwenye Bunge lijalo la October/November ili zifanyiwe mabadiliko.
Kwa vile msingi mkuu na matatizo makuu ya uendeshaji wa siasa zetu yako kwenye katiba, katiba ndio kichwa cha yote na mengine yote ni kiwiliwili.
Kwa vile kuna mchakato wa katiba mpya utakaanza hivi karibuni, lakini kwa minaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, tuanze na mabadiliko ya katiba hii hii iliyopo kwa kuibadilisha kwa hati ya dharura, ndipo tuje kwenye mabadiliko ya sheria za uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi tuunde Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.
Hili ni bandiko mwendelezo wa bandiko hili Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?
Paskali
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu elimishi kuhusu Maslahi ya Taifa, ambazo ni kuhusu jambo lolote la Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii . Bandiko la leo ni pongezi kwa Rais Samia na serikali yake, kukubali kubadili sheria ya uchaguzi, na kuunda Tume Huru ya Uchaguzi!. Swali ni Jee Tuanze na mabadiliko ya katiba kwanza ndipo turekebishe sheria au turekebishe tuu sheria, kisha tuingie kwenye uchaguzi Mkuu na katiba hii hii, kisha baada ya uchaguzi wa 2025 ndipo sasa tushughulikie mchakato wa katiba mpya?.
Nilipata fursa kuhudhuria kongamano la siku 3 la vyama vya siasa nchini, lililoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kujadili ripoti ya Kikosi Kazi cha Rais Samia, na mapendekezo yake kuelekea chaguzi za serikali za mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, uliofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, JNICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Naomba nianze kwa kutoa maoni yangu, kwanza nampongeza Rais Samia kuunda kikosi kazi kutathmini hali ya siasa nchini, nakipongeza kikosi kazi kwa kazi nzuri, naipongeza serikali yetu kwa kukubali mapendekezo ya kikosi kazi, kukubali kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi kuunda Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi.
Kama ulitaka kikubwa, ukapewa kidogo, shukuru kwanza kwa hicho kidogo ulichopewa kisha endelea kuomba kile kikubwa!.
Mzizi wa matatizo yetu yote ya uendeshaji wa siasa zetu, uko kwenye katiba, kwanza ndipo tuje kwenye sheria.
Kufanya mabadiliko ya sheria bila mabadiliko ya katiba, ni sawa na kula bila kunawa, au kuvaa nguo nzuri bila kuoga, ukila bila kunawa bado utashiba tuu, ila matokeo!. Ukivaa nguo nzuri bila kuoga, utapendeza tuu, ila...
Hivyo tunaipongeza serikali yetu kukubali kubadili sheria ya uchaguzi na kutupatia tume huru ya uchaguzi, ila nashauri tuanze kwanza mabadiliko ya katiba ndipo twende kwenye sheria!.
Pendekezo la pili, ni tufanye uchaguzi wote kwa siku moja, na kusimamiwa na Tume moja huru ya uchaguzi. Kama Zanzibar wanaweza kufanya chaguzi 5 kwa siku moja, Tanzania hatuwezi kushindwa kufanya chaguzi 4 kwa siku moja!. Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!
Hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 halafu uchaguzi Mkuu 2025, kwa sasa tufanye mabadiliko ya katiba na sheria, halafu 2025 tufanye chaguzi zote 4 kwa siku moja, Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa.
Kongamano hilo lilifunguliwa na Rais Samia ambaye ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa nchini kutumia mikutano ya hadhara kutoa hoja na fikra zenye tija zinazolenga kuimarisha utendaji serikalini.
Aidha, Rais Samia amevitaka vyama vya siasa kutumia mikutano ya hadhara kujitangaza ili kukua kisiasa na kuutumia uhuru wa kujieleza kutoa mawazo mbadala yatakayoendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.
Rais Samia pia amesema uhuru wa kutoa maoni kusisababishe kudhalilisha watu
wengine, kuibua hisia za kidini, ukabila au kubaguana kwa misingi yoyote ile.
Vile vile, Rais Samia amesisitiza kutumia uhuru huo vizuri bila kuingilia haki na
uhuru wa watu wengine pamoja na kufuata sheria, kanuni na taratibu.
“Katika shukrani nisisahau Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakiongozwa na Jaji Mutungi, Jaji Mutungi saa zingine ananipigia simu usiku we mama wee hii kazi uliyonipa nimekwama hapa na hapa, umeaminiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nenda na kazi yako, ukikwama fedha niambie lakini mengine fanya kazi yako, kwa hiyo nakushukuru umefanya kazi yako na mmefikia pazuri”, alisema Rais Samia.
Rais Samia amesema kuwa Serikali imepokea ripoti ya kikosi kazi ambapo Serikali imeyapitia mapendekezo hayo kupitia vikosi kadhaa vilivyongalia mambo kadhaa yanayohitaji wataalamu hususan yanayohusu sheria na Bunge likalo, itapeleka marekebisho ya sheria kadhaa ikiwemo sheria ya uchaguzi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Rais Samia amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi waliopendekezwa wamefanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea Watanzania na Wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulika na masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa ratiba ya utekelezaji itaanza na mabadiliko ya sheria kadha ambazo zitapelekwa Bungeni kwenye Bunge lijalo la October/November ili zifanyiwe mabadiliko.
Kwa vile msingi mkuu na matatizo makuu ya uendeshaji wa siasa zetu yako kwenye katiba, katiba ndio kichwa cha yote na mengine yote ni kiwiliwili.
Kwa vile kuna mchakato wa katiba mpya utakaanza hivi karibuni, lakini kwa minaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu wa 2025, tuanze na mabadiliko ya katiba hii hii iliyopo kwa kuibadilisha kwa hati ya dharura, ndipo tuje kwenye mabadiliko ya sheria za uchaguzi na kurekebisha Tume ya Uchaguzi tuunde Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi.
Hili ni bandiko mwendelezo wa bandiko hili Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?
Paskali