PMNBuko
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 967
- 154
Tokea Jana Usiku tumeshuhudia Jeshi la Polisi likituonesha picha za video kuhusu tukio la Arusha, Januari 5 mwaka huu ambapo Mtangazaji wake anaonesha umma kwamba CHADEMA wanahitaji kulaumiwa kwa kuchochea vurugu. Taarifa hii imeacha maswali mengi kichwani mwangu bila majibu.
Je, kwa nini jeshi lisitaje sheria inasemaje kuhusu kuzuia maandamano muda mchache kabla ya maandamano kuanza?
Je, kwanini Jeshi la Polisi liue watu badala ya kutumia mabomu ya machozi na virungu kama ilivyozoeleka?
Wana JF nani anawajibika kwa vurugu za Arusha? Wananchi wanaweza kugeuza mawazo na maoni yao kutokana na taarifa ya Jeshi hilo linalojaribu kujisafisha kwa kutumia gharama kubwa za fedha za walipakodi ambao ndio baadhi yao wameuwawa na Jeshi hilo?
Je, kwa nini jeshi lisitaje sheria inasemaje kuhusu kuzuia maandamano muda mchache kabla ya maandamano kuanza?
Je, kwanini Jeshi la Polisi liue watu badala ya kutumia mabomu ya machozi na virungu kama ilivyozoeleka?
Wana JF nani anawajibika kwa vurugu za Arusha? Wananchi wanaweza kugeuza mawazo na maoni yao kutokana na taarifa ya Jeshi hilo linalojaribu kujisafisha kwa kutumia gharama kubwa za fedha za walipakodi ambao ndio baadhi yao wameuwawa na Jeshi hilo?