Polisi yajitakasa isishitakiwe ICC kwa kuua

Golden opportunity ya kuafanya nini? kujitangaza kimataifa au? this is shit! EU wanashindwa kusimamisha mauaji ya halaiki palestina yanayofanywa na israel, waje kuisaidia CDM? you are not serious! hao EU una waona wasafi?

sana sana kuwaomba wasitoe misaada yao kwa TZ wataadhirika watanzania wote including wana CDM na hata sikumoja EU haiwezi kupindua serikali ya TZ! wala haitawapa umaarufu mnaofikiria.

ICC ndio kabisa haita saidia chochote maana kama wa kufungwa ni Dr. Slaa, maana amri katoa yeye watu wakavamie kituo cha police. wacha waende yetu macho kwanza CDM watafundishwa namna ya ku control mobs zao.

acha utetezi dhaifu wewe, mbona tumeshuhudia maandamano yakutisha nchi nyingi kama ufaransa juzi lakini hatujaona mauaji ya raia kwa makusudi na kupiga ovyo na kipuuzi raia.

unataka kuniambia Josephin mchumba wa dk Slaa alipigwa karibu na kituo cha polisi? Unataka kutuambia wale waliojeruhiwa kwa risai ni karibu na kituo cha polis?
Je magari yalipokuwa yanmavunjwa vioo ni kituo cha polisi?

acha kurubuniwa na taarifa ya utetezi ya polisi ambayo utetezi wake hauna tija wala ukweli wowote, waongee wazi walitumwa kuua na kuumiza waandamanaji na si kuzuia, wanaongea uongo na wewe na akili zako unakubali kama mdanganyika?

kwa sasa sisi ni WATANZANIA NA SI WADANGANYIKA, Mwema hana la kukwepa zigo hilo la lawama. Unamlauma Dk Slaa kwa kuchochea watu mbona hulaumu upuuzi wa polisi kukamata viongozi kabla ya mkutano, ndio intelijensia ilivyowaambia?

hawakujua kukamata hao viongozi b4 mkutano kunaweza kuleta madhara na kuamsha mihemko kama wanavyodai? Stupit inteligency...
 
Sio Tz ,yaani huko wanajua wakikubali madai ya Chaderma ,mirija yao itakatwa kiurahisi,hivi mnasahau kuwa hapa Tz ni sehemu inayowatilia faida hao mnaowapelekea kesi.
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, kimeelezewa kuandaa mashitaka dhidi ya Serikali katika Mahakama ya Kimataifa inayoshughulikia Makosa ya Jinai (ICC), kutokana na kusababisha mauaji ya raia watatu wasio na hatia akiwemo raia mmoja wa Kenya yaliyofanywa hivi karibuni na Jeshi la Polisi huko mkoani Arusha.

Pia chama hicho kimepanga kuifikisha na kuishitaki serikali kwenye Jumuiya ya Ulaya EU, iwapo haitawajibika kumfukuza kazi kama Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema, atashindwa kujiuzulu mwenyewe kutokana na kashfa hiyo.

Aidha, CHADEMA kinasema vielezo muhimu wanavyo zikiwemo picha za video na ushahidi wa wazi unaonyesha mauaji hayo yalikuwa na baraka kutoka kwa viongozi wa ngazi ya juu ya serikali ambao ndio waliomshauri Kamanda Mwema kuzuia maandamano hayo muda mfupi na kusababisha ghasia na mauaji hayo.

Tamko hilo limetolewa juzi na Mkurugenzi wa Oganizesheni wa chama hicho, Ignas Karashani, wakati akizungumza na waandishi wa habari kulaani mauaji hayo.

My take: Serikali isipuuzie hatua hii ya Chadema inaweza kuiweka serikali kwenye image mbaya kimataifa.[Only educated are free]
Hakika hili ni muhimu sana naamini CDM watafanya kweli ili kuionesha "sirikali" hii kuwa wakati wa ukombozi wa wanyonge umefika. Na huyu Nyantella ametumwa au ana matatizo ya akili, anaishi ulimwengu gani na je ni mtanzania kweli ana asili ya kule........ atupishe wenye uchungu na nchi yetu.
 
Sio Tz ,yaani huko wanajua wakikubali madai ya Chaderma ,mirija yao itakatwa kiurahisi,hivi mnasahau kuwa hapa Tz ni sehemu inayowatilia faida hao mnaowapelekea kesi.

mwiba ... habari ya weekend..... naona umetoka mashine kukoboa mahindi
 
hivi kweli watanzania tuna amini ICC iko fair? nani alisema hizi UN agencies na other intenrational chapters ziko fair?

we better sort our own problems
The same ICC fairness/not fairness judgements applied to Dowans will prevail.
 
Mara nyingi huwa nawaambia wachezaji wangu keep the ball away from your penalty area, acha wao wa-defend kuliko wewe ku-defend. Nimeona wameanza kujitetea kwa kuchakachua picha TBC 1 wakidhani itasaidia, labda ingekuwa zamani enzi za magazeti ya Uhuru na Mfanyakazi na RTD tu lakini leo hawamdanganyi mtu.
Sure
 
umenena bro, watamdanganya nani na teknolojia ilivyo juu sasa, watachakachua kwenyevyombo vyao, TBC,UHURU,Habari Leo, Dailynews, Rai na Mzalendo.

lakini wengine wote tumeona upuuzi na mauji ya kijinga pale Arusha, gazeti la Reutes limeonyesha askari wetu bila aibu wakipiga vioo gari na mtu yumo ndani, je huku ndio kuzuia maandamano?

hata mchakachue vp, ukweli utabaki pale pale KILLERS or u may call them ASSASINS police
Kwa technologia ilivyosambaa wengi walishuhudia tukio live inawezekana hata Obama na Occambo walikuwa wanaangalia live, kadri serikali inavyochakachua ndivyo watu wanavyoona ubabaishaji wake afadhali ingeacha wananchi waamue ukweli uko wapi kuliko kuwalazimisha kukubali uongo, hizi siyo kura za NEC kila kitu kilikuwa wazi.
 
Sisi wa Arusha tulioona live hatudanganyiki na hizo picha za TBC 1
 
Golden opportunity ya kuafanya nini? kujitangaza kimataifa au? this is shit! EU wanashindwa kusimamisha mauaji ya halaiki palestina yanayofanywa na israel, waje kuisaidia CDM? you are not serious! hao EU una waona wasafi?

sana sana kuwaomba wasitoe misaada yao kwa TZ wataadhirika watanzania wote including wana CDM na hata sikumoja EU haiwezi kupindua serikali ya TZ! wala haitawapa umaarufu mnaofikiria.

ICC ndio kabisa haita saidia chochote maana kama wa kufungwa ni Dr. Slaa, maana amri katoa yeye watu wakavamie kituo cha police. wacha waende yetu macho kwanza CDM watafundishwa namna ya ku control mobs zao.

Mambo vipi mdogo wa Maria (Maleria) Sugu na mtoto wa Yusuph mauzi, mzee wa pumba
 
Tokea Jana Usiku tumeshuhudia Jeshi la Polisi likituonesha picha za video kuhusu tukio la Arusha, Januari 5 mwaka huu ambapo Mtangazaji wake anaonesha umma kwamba CHADEMA wanahitaji kulaumiwa kwa kuchochea vurugu. Taarifa hii imeacha maswali mengi kichwani mwangu bila majibu.

Je, kwa nini jeshi lisitaje sheria inasemaje kuhusu kuzuia maandamano muda mchache kabla ya maandamano kuanza?

Je, kwanini Jeshi la Polisi liue watu badala ya kutumia mabomu ya machozi na virungu kama ilivyozoeleka?

Wana JF nani anawajibika kwa vurugu za Arusha? Wananchi wanaweza kugeuza mawazo na maoni yao kutokana na taarifa ya Jeshi hilo linalojaribu kujisafisha kwa kutumia gharama kubwa za fedha za walipakodi ambao ndio baadhi yao wameuwawa na Jeshi hilo?

hata wajisafishe kwa sabuni ya ina gani, wao ni wauaji na wa kulaumiwa kwa yaliotokea Arusha, TBC wanajisumbua kabisa na polisi wao kwa teknolojia ya sasa watadanganya vichaa na wapuuzi tu.

uhakika ni kwamba wametimiza malengo ya wakubwa zao na sasa wanatafuta public concern waonekane hawana hatia, imekula kwao kila mtu kwenye jamii anawaona polisi wauwaji na si walindaji.
 
am watching,ni maneno tu au ndo action zinafuata?
maana watanzania kwa kuongea hatujambo
 
kizibao nikupe pole kwa sababu hujui ulitendalo,siku zote nguvu ya uma haina mpinzani subiri muda sio mrefu utagundua ulikuwa ni ushabiki na utoto unaokusumbua.
 
Polisi hawana tofauti na walinzi wa KK security, jinsi unavyowaajili walinzi wa kk watulinde majumbani kwetu ndivyo tulivyowaajili polisi, jinsi ambavyo haiwezekani mlinzi wako wa nyumbani kukupangia muda wa kurudi nyumbani ndivyo ambavyo polisi hawana mamlaka ya kutuzuia kuelezea hisi zetu.
 
Huo mkakati wapolisi na serikaliy yao pamoja na chama chao ni mzuri kwa sababu huo ni ushahidi tosha wana lao jambo la kuficha. Kweli kuna impact kuonyesha hiyo kwenye TV kwani watu ambao hawatataka kujua upande wa pili wataishia kuchukulia ndiyo ukweli. Lakini hiyo TV program itajibiwa na Tv program mbadala pamoja na ushahidi mwingine unaojitokeza. Kwa mfano hao waliouawa walikuwa umbali gani na kituo cha polisi? Walihatarisha nini kituo cha polisi? Walikuwa na silaha gani? Ndiyo hao wanaonyeshwa wakishambulia kituo au danganya toto?

Lakini hapa cha msingi aliyeua ndiye ana cha kujibu mauaji ya watu wasio na silaha kwa silaha za moto. Ushabiki wa akina Zombi utakuwepo tu kwa kuna maslahi yao; lakini ukweli huwezi ukauficha kwa kampeni chafu ya TV inayojulikana ni dhaifu.
 
Sio Tz ,yaani huko wanajua wakikubali madai ya Chaderma ,mirija yao itakatwa kiurahisi,hivi mnasahau kuwa hapa Tz ni sehemu inayowatilia faida hao mnaowapelekea kesi.

Unachanganya tena sasa. Mbona hatuendi mbali kuna tawi la ICC pale AICC ambao nao walishuhudia watawashangaa Chadema kama hawataishtaki serikali. Na hao hawahusiki na biashara za matapeli pamoja na kwamba sisi ni wanachama tulioridhia kuwepo kwa mahakama hiyo. Tujitayarishe kwa kitanza. Serikali? Na mauaji je?
 
Zomba kama unaweza kuangalia Euro news!(leo).nadhani utaona umuhimu na faida ya maandamano.Vile vile utaona jinsi gani polisi wanavyosaidia ili hayo maandamano yawe ya utulivu.
Zomba na Malaria Sugu
 
Arusha kama sikosei wanashughulikia kesi za Rwanda na Burundi tu.

Nafikiri kesi ya CHADEMA inabidi iende HAGUE na siyo hapo Arusha.

Kama kweli CHADEMA wanataka kufanya hivyo basi wafanye HARAKA SANA.

Wasisuesue kama kesi ya uchaguzi wa Rais. Ocampo, andaa CHAI ya Chadema.

Hahahaaa, watoto, ndugu na jamaa za Viongozi wa CCM/SIRIKALI matumbo moto.

Wahusika wa Mauwaji ya Arusha na Mbeya, kaeni mkao wa kula.

Unachanganya tena sasa. Mbona hatuendi mbali kuna tawi la ICC pale AICC ambao nao walishuhudia watawashangaa Chadema kama hawataishtaki serikali. Na hao hawahusiki na biashara za matapeli pamoja na kwamba sisi ni wanachama tulioridhia kuwepo kwa mahakama hiyo. Tujitayarishe kwa kitanza. Serikali? Na mauaji je?
 
Back
Top Bottom