fangfangjt
JF-Expert Member
- Apr 25, 2008
- 571
- 139
Wananchi Mbarari Mbeya wamechoma moto lori la mafuta na kituo cha mafuta. Polisi waingilia kati, mwananchi moja apigwa risasi na kufa
SOURCERADIO 1
SOURCERADIO 1
kisa ni nini? mpaka waamue kuchoma moto lori na kituo cha mafuta au ubabe wa ccm kama kawaida yako...Wananchi Mbarari Mbeya wamechoma moto lori la mafuta na kituo cha mafuta. Polisi waingilia kati, mwananchi moja apigwa risasi na kufa
SOURCERADIO 1
Lori la mafuta na kituo cha mafuta ni private property kwa hali yeyote ile waliochoma moto ni wahalifu waliokosa mlo ,hongera polisi kwa kuwakurupusha na kufanikiwa kumsimika umaiti mmoja wao.
Ndg zangu wana JF,
Nimetaarifiwa na mdau mmoja kutoka Rujewa Wilayani Mbarali kwamba umetokea ugomvi mkubwa wa mipaka ya mashamba ya mpunga kwenye maeneo ya Ubaruku kati ya wananchi waliopokonywa mashamba yao na mwekezaji. Nakumbuka Bw. Maggid alishaandika makala yake moja kuhusu suala hilo na kuonya serikali ichukue hatua haraka iwezekanavyo. Lakini kama kawaida ya serikali yetu inaonekana makala hiyo ilipuuzwa. Sasa leo ugomvi mkubwa umetokea. Polisi wameingilia kati na mpaka sasa wananchi 3 tayari wamepoteza maisha. Muda si mrefu DEFENDER 12 zikiwa na askali polisi kutoka Jijini Mbeya zimewasili Ubaruku tayari kukabiliana na wananchi wenye hasira kali. Tafadhali wadau mliopo huko mtupatie taarifa zaidi.
Ni kweli polisi wameua watu watatu kwenye ghasia huko Ubaruku lakini chanzo cha ugomvi si mpaka wa shamba bali kuzuiwa kwa malori ya zaidi ya tani 8 kupita kwenye barabara hiyo kwenda kuchukua mpunga wa wakulima (hivyo wananchi wameshindwa kuuza mpunga wao) wakati mfanyabiashara wa mafuta ameruhusiwa kupitisha la lori lenye uzito zaidi ya huo kupeleka mafuta (kama kawaida wawekezaji kwanza wananchi baadae - inauma) huko Rujewa.
Wananchi waliamua kulizuia lori hilo ndipo polisi wakaja na kuanza kuwatawanya wananchi kwa kutumia mabomu ya machozi na kama kawaida yao wakawapiga risasi za moto na kuua watatu kwa uchache. Wananchi wakaamua kuchoma lori moto na kuunguza kituo cha mafuta pia.Nasikia vurugu zinaendelea na polisi wameomba msaada kutoka Mbeya baada ya kuzidiwa nguvu na wananchi.
Tangu hotuba ya kikwete ya kuuaga mwaka na kuonya juu ya vurugu, askari polisi wamekuwa hawasiti kuwasha risasi za moto kwa wananchi, jamaa ameamua kutoa kafara wananchi wake ( kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia)