junior2008
JF-Expert Member
- Apr 27, 2009
- 528
- 42
Ni kweli polisi wameua watu watatu kwenye ghasia huko Ubaruku lakini chanzo cha ugomvi si mpaka wa shamba bali kuzuiwa kwa malori ya zaidi ya tani 8 kupita kwenye barabara hiyo kwenda kuchukua mpunga wa wakulima (hivyo wananchi wameshindwa kuuza mpunga wao) wakati mfanyabiashara wa mafuta ameruhusiwa kupitisha la lori lenye uzito zaidi ya huo kupeleka mafuta (kama kawaida wawekezaji kwanza wananchi baadae - inauma) huko Rujewa.
Wananchi waliamua kulizuia lori hilo ndipo polisi wakaja na kuanza kuwatawanya wananchi kwa kutumia mabomu ya machozi na kama kawaida yao wakawapiga risasi za moto na kuua watatu kwa uchache. Wananchi wakaamua kuchoma lori moto na kuunguza kituo cha mafuta pia.Nasikia vurugu zinaendelea na polisi wameomba msaada kutoka Mbeya baada ya kuzidiwa nguvu na wananchi.
Tangu hotuba ya kikwete ya kuuaga mwaka na kuonya juu ya vurugu, askari polisi wamekuwa hawasiti kuwasha risasi za moto kwa wananchi, jamaa ameamua kutoa kafara wananchi wake ( kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia)
Hivi kweli JK, Nahodha na Mwema bado wanaona wanastahili kuendelea na nyazifa zao?