Boniface Jacob: Polisi walioua Mlinzi wa Bar ya Boardroom Sinza wadaiwa kutumwa na RC Chalamila kukamata Wanaojiuza

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118




1. Polisi wawili waua kwa risasi mlinzi wa Bar maarufu ya Boardroom iliyopo Sinza Jijini Dar es Salaam.

2. Mlinzi waliyeuwawa kwa risasi anaitwa Razak Anan mwenye umri wa miaka 29 muajiriwa wa Bar ya Boardroom, Sinza

3. Polisi kutoka kituo cha Polisi Mabatini walifika na gari na kupaki nje ya Bar ya Board room na kuanza msako wa Dada poa kwa kusema ni agizo la Mkuu wa Mkoa.

4. Lakini Polisi hao walikuwa wakiwatoa nje wahudumu na wateja katika Bar hiyo ambao walikuwa na min skirt (sketi fupi) kwa kusema kuwa watu hao kwa mavazi yao walikuwa wanajiuza katika Bar hiyo ya usiku (night Club)

5. Wateja wengine walipona udhalilishaji na manyanyaso hayo walianza kuondoka katika Bar hiyo ya Boardroom na waliobakia waligoma kutolewaa nje ya Bar kwa muonekano wa mavazi yao.

5. CCTV za Bar ya Board room inayonyesha Polisi hao walipoona wadada wanakata kufananishwa na machangudoa walienda katika gari na kuchujua silaha aina ya bunduki (SMG) na kuanza kutishia wateja na kuelekezea katika meza za wateja waliokuwa wanakunywa katika Bar hiyo.

6. Polisi hao ambao walikuwa wanaonekana wametumia kilevi walifyatua risasi kadhaa kisha kuondoka na gari yao kutoka eneo hilo la Bar ya Boardroom na baada ya kuondoka wateja walirejea na kukuta mlinzi mmoja wapo akiwa amelala chini akiwa amepigwa risasi na kuvuja damu nyingi (video inaonyesha damu ya marehemu)

7. Mlinzi wa Board room alifariki njiani akiwa katika Bajaji anakimbizwa hospitali.

8. Matukio ya polisi kuvamia sehemu za starehe na nyumba za watu binafsi ni maagizo ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambaye anaendesha zoezi la kutafuta madanguro na kusaka madada poa.

9. Leo Mkuu wa Mkoa amesisitiza mauaji kufanywa na polisi ni Jambo la kawaida "Mtu akifia kituo cha polisi tunasema Polisi wameua, Mtu akifia hospitali tunasema ni Mapenzi ya Mungu" RC-DSM, Chalamila

10. Nawakumbusha kulaani tukio lolote la Polisi kuua raia kwa kisingizio chochote kile, Leo kwa huyu kesho kwake.

Boniface Jacob EX Mayor Ubungo
Pia soma >>> Polisi kuua mlinzi wa bar Dar: Je, Chalamila anakwepaje kuwajibika?
 
Chalamila ni mtu wa ajabu sana na sijui kwanini mama anamuamini. ni mtu anayependa kutumia mabavu, hapendi utawala wa sheria. sasa, kweli unaweza msako kuwinda machangudoa? na wakati ule alienda kuvunja vijumba vile vya wahaya, bila amri ya mahakama. sisi sote hatupendi uzinzi/umalaya, lakini huwezi kuchukua maamuzi mkononi kwenye nchi yenye sheria. anaamini hapo anapambana na machangudoa?

Kwenye mitandao ya simu amewafuata, anajua kuwa wanawake wengi wanaojiuza ni haohao wa maofisini na wanaojifanay wastaarabu, wanao uwezo kupanga wanaume hata watano kwa siku kwa njia ya simu tu, wala hajipangi barabarani. ni kweli kosa la uzururaji unaweza kuwakamata nalo na kujiuza, ila utajuaje, si kuharibu biashara za watu hiyo?

Rais kama anatusikia watanzania, na tulishamwambia, watu kama makonda, alli happy, chalamila, na yule mbunge wa misungwi hatuwataki hata kusikia wala kuwaona kwenye uongozi. sikieni maoni ya wananchi kama kikwete alivyosema.
 
Chalamila ni mtu wa ajabu sana na sijui kwanini mama anamuamini. ni mtu anayependa kutumia mabavu, hapendi utawala wa sheria. sasa, kweli unaweza msako kuwinda machangudoa? na wakati ule alienda kuvunja vijumba vile vya wahaya, bila amri ya mahakama. sisi sote hatupendi uzinzi/umalaya, lakini huwezi kuchukua maamuzi mkononi kwenye nchi yenye sheria. anaamini hapo anapambana na machangudoa? kwenye mitandao ya simu amewafuata, anajua kuwa wanawake wengi wanaojiuza ni haohao wa maofisini na wanaojifanay wastaarabu, wanao uwezo kupanga wanaume hata watano kwa siku kwa njia ya simu tu, wala hajipangi barabarani. ni kweli kosa la uzururaji unaweza kuwakamata nalo na kujiuza, ila utajuaje, si kuharibu biashara za watu hiyo? Rais kama anatusikia watanzania, na tulishamwambia, watu kama makonda, alli happy, chalamila, na yule mbunge wa misungwi hatuwataki hata kusikia wala kuwaona kwenye uongozi. sikieni maoni ya wananchi kama kikwete alivyosema.
Acha porojo
Chalamila ndo kafyetua risasi?
Muda huo alikuwa kwake na mkewe wakidumisha ndoa
 
20231129_205519.jpg
 
Back
Top Bottom