fikirikwanza
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 7,452
- 3,065
Huku akiwasilisha kwa mbwembwe zilizoonekana kuwa ni za kishabiki akipinga hoja zilizowalishwa na kambi ya upinzani bungeni, Werema alishindwa kuunga mkono hoja ya Upinzani kuhusu mstakabari wa TZ baada ya Zanzibar kuutangazia UMMA na dunia kuwa ni NCHI.
Werema alisema zanzibar ni nchi ndo maana ukaungana na Tanganyika ambayo pia ni nchi ili kutengeneza JMT. Werema alitumia maneno ya kejeli eti kiswahili sio lugha mama ya upinzani, hawajui kiswahili vizuri ambapo yeye pia alijifunza na kwa vile ni msomi mzuri alielewa kiswahili barabara.
Werema anashindwa kutofautisha wakati uliopita na uliopo ktk lugha ya kiswahili. Kwa wakati uliopita Zanzibar ilikuwa nchi, na kwa wakati uliopo zanzibar sio nchi, hivyo kunauwezekano mkubwa kuwa katiba ya JMT imevunjwa na rais wa JMT anastahili kujibu mashitaka ya kuvunjwa kwa katiba aliyoapa kuilinda.
Kama Zanzibar na Tanganyika bado ni nchi ktk sheria za leo, basi JMT sio nchi ni umoja wa nchi mbili znz na tgk.
HUKU akijua kuwa kauli yake hiyo inamburuza PINDA waziri wake mkuu, ambaye aliwahi kusema kwa ujasiri kuwa Znz sio nchi as we speak. Werema alitaka kuthibitisha kuwa wakati PINDA anasema vile hakuwa amepata ushauri wa AG kitu ambacho kinamfanya PINDA awe kituko ktk suala zima la uongozi wa nchi hii.
Hadi hapo tutakapopata ufafanuzi wa wanasheria wengine suala hili linabaki kuwa Werema, AG amemsihaki Pinda, PM kuhusu zanzibar kuwa nchi au la.
Wanasheria waliobobea kwenye masuala ya sheria na katiba please tutegulieni kitendawili hiki.
Nawasilisha.
Werema alisema zanzibar ni nchi ndo maana ukaungana na Tanganyika ambayo pia ni nchi ili kutengeneza JMT. Werema alitumia maneno ya kejeli eti kiswahili sio lugha mama ya upinzani, hawajui kiswahili vizuri ambapo yeye pia alijifunza na kwa vile ni msomi mzuri alielewa kiswahili barabara.
Werema anashindwa kutofautisha wakati uliopita na uliopo ktk lugha ya kiswahili. Kwa wakati uliopita Zanzibar ilikuwa nchi, na kwa wakati uliopo zanzibar sio nchi, hivyo kunauwezekano mkubwa kuwa katiba ya JMT imevunjwa na rais wa JMT anastahili kujibu mashitaka ya kuvunjwa kwa katiba aliyoapa kuilinda.
Kama Zanzibar na Tanganyika bado ni nchi ktk sheria za leo, basi JMT sio nchi ni umoja wa nchi mbili znz na tgk.
HUKU akijua kuwa kauli yake hiyo inamburuza PINDA waziri wake mkuu, ambaye aliwahi kusema kwa ujasiri kuwa Znz sio nchi as we speak. Werema alitaka kuthibitisha kuwa wakati PINDA anasema vile hakuwa amepata ushauri wa AG kitu ambacho kinamfanya PINDA awe kituko ktk suala zima la uongozi wa nchi hii.
Hadi hapo tutakapopata ufafanuzi wa wanasheria wengine suala hili linabaki kuwa Werema, AG amemsihaki Pinda, PM kuhusu zanzibar kuwa nchi au la.
Wanasheria waliobobea kwenye masuala ya sheria na katiba please tutegulieni kitendawili hiki.
Nawasilisha.