Pinda hastahili kuwa PM, si mbunge wa kuchaguliwa

Mimi kama sijaelewa vizuri labda, lakini mi navyoona niboro kama inawezekana Pinda aendelee amalize tu ngwe hii ilobaki kwa CCM.
 
Hapa tupo pamoja! Katika analogy hii, tunaweza kusema katiba ndio 'ukweli'?

Hata katiba yenyewe, with all it's inconsistencies and inherent flaws haiwezi kuwa ukweli.Ukweli ni kwamba justice must be done, and if we claim to have representative democracy, it must actually be representative.

Sio tunasema tuna representative democracy kumbe huyo mtu tunayesema muwakilishi wa jimbo hata hakuchaguliwa na watu wa jimbo.
 
Mimi kama sijaelewa vizuri labda, lakini mi navyoona niboro kama inawezekana Pinda aendelee amalize tu ngwe hii ilobaki kwa CCM.

Swala sio Pinda aendelee au asiendelee, swala ni je Pinda ana sifa za kuendelea au hana. Haya maswala ni tofauti.
 
Topiki nzuri sana, niseme tu kuwa sheria zetu hazilengi matakwa ya jamii bali zinalenga matakwa ya watu wachache. Maoni ya Luteni ni sahihi 100%, na sio kwa suala la Pinda tu bali wabunge wengine wote 17 waliopitwa bila kupingwa wamepitishwa kwa sheria inayokinzana na Katiba. Kuchagua ina maana kusema ndio au hapana i.e. kukataa, hivyo basi hata kama mtu hana mpinzani mpeleke kwa wananchi waamue kumkubali au kumkataa simple and clear.

Haina ubishi kuwa kuna aina tano tu za wabunge:

(a) Wabunge waliochaguliwa kuwakilisha majimbo ya uchaguzi;

(b) Wabunge wanawake wa idadi inayoongezeka, watakaochaguliwa na vyama vya siasa vinavyowakilishwa Bungeni, kwa mujibu wa ibara
ya 78, na kwa kuzingatia masharti ya uwiano wa uwakilishi baina ya vyama hivyo;

(c) Wabunge watano waliochaguliwa na Baraza la Wawakilishi kutoka miongoni mwa wajumbe wake;

(d) Mwanasheria Mkuu;

(e) Wabunge wasiozidi kumi walioteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watu wenye sifa kwa mujibu wa ibara ya 67, isipokuwa sifa iliyotajwa
katika ibara ya 67(1)(b).

Bunge limeundwa na katiba na katiba inaeleza bayana aina za wabunge. Hivyo basi sheria yoyote inayoongeza idadi ya aina ya bunge ni sheria haramu kabisa na inastahili kufutwa na mahakama.

Kwa kutilia mkazo umuhimu wa kuchagua, Ibara ya 77 ya katiba inaelezea wazi kabisa kuwa :
Wabunge wanaowakilisha majimbo ya uchaguzi watachaguliwa na wananchi kwa kufuata masharti ya Katiba hii na vile vile
masharti ya Sheria iliyotungwa na Bunge kwa mujibu wa Katiba hii
inayoweka masharti kuhusu uchaguzi wa Wabunge anaowakilisha
majimbo ya uchaguzi.
 
Sheria hii inavunja katiba, katiba katika ibara yake ya 66 inaainisha jinsi mtu anavyopata ubunge. Sheria hii imevunja ibara ya 66 ya katiba.

Imevunja pia na haki ya msingi ( Basic right) ya wakazi wa majimbo yote ambayo watu wamepita bila kupingwa , haki ya kushiriki katika shughuli za umma inayosema:

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma:
(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na
kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya
kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa
hiari yao,
kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.

(2) Kila raia anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomhusu yeye, maisha yake au
yanayolihusu Taifa.
 
Sidhani kama hiyo interpretation ni sahihi. Kwani Pinda ni Mbunge wa kuteuliwa? Kateuliwa na nani? Nafikiri kwa kuwa amepita bila kupingwa ina maanisha ni mbunnge wa kuchaguliwa.
 
Sidhani kama hiyo interpretation ni sahihi. Kwani Pinda ni Mbunge wa kuteuliwa? Kateuliwa na nani? Nafikiri kwa kuwa amepita bila kupingwa ina maanisha ni mbunnge wa kuchaguliwa.

Pinda si Mzaramo, kwa sababu si Mzaramo basi lazima ni Mchagga. What kind of logic is this ?

Wapi na wapi!
 
Imevunja pia na haki ya msingi ( Basic right) ya wakazi wa majimbo yote ambayo watu wamepita bila kupingwa , haki ya kushiriki katika shughuli za umma inayosema:

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma:
(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na
kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya
kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa
hiari yao,
kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.

(2) Kila raia anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomhusu yeye, maisha yake au
yanayolihusu Taifa.

hapa ndipo zaidi panaponigusa mimi.

wananchi wameporwa haki yao ya kuchagua, haki waliyopewa kikatiba.

Tume ya uchaguzi imewachagulia wananchi wabunge na kuwanyima haki yao ya msingi kwa sababu tu vyama vya siasa havikuweka wagombea (au wagombe waliowekwa waliwekewa pingamizi)
 
Tume ya uchaguzi imewachagulia wananchi wabunge na kuwanyima haki yao ya msingi kwa sababu tu vyama vya siasa havikuweka wagombea (au wagombe waliowekwa waliwekewa pingamizi)

Gaijin, nadhani shida ilianzia bungeni wakati wa kutunga sheria. Tume ya uchaguzi inafuata sheria ambayo supposedly imeopitishwa/kubaliwa na wananchi (kupitia wawakilishi wao, wabunge!).
 
Gaijin, nadhani shida ilianzia bungeni wakati wa kutunga sheria. Tume ya uchaguzi inafuata sheria ambayo supposedly imeopitishwa/kubaliwa na wananchi (kupitia wawakilishi wao, wabunge!).

Wabunge wenyewe ndio hao wanaona kupata ubunge bahati, kwa nini wasitake mteremko zaidi wa kupitishwa bila chaguzi?
 
Gaijin, nadhani shida ilianzia bungeni wakati wa kutunga sheria. Tume ya uchaguzi inafuata sheria ambayo supposedly imeopitishwa/kubaliwa na wananchi (kupitia wawakilishi wao, wabunge!).

hivi bunge linawezaje kupitisha sheria ambayo inapingana na katiba?
 
hivi bunge linawezaje kupitisha sheria ambayo inapingana na katiba?
Hapo sasa!...wengi huwa wanachapa usingizi tu mjengoni. Ningetegemea vitu kama hivi kuleta debate kubwa tu mjengoni kabla havijapitishwa.
 
hivi bunge linawezaje kupitisha sheria ambayo inapingana na katiba?

Tanzania chochote kinawezekana, si watu wanajilegeza. Hiyo sheria ya uchaguzi imepitaje ?

In theory hili likitokea Mahakama inatakiwa kutoa muongozo nafikiri, lakini mahakama zetu ndiyo kwanza zinaanza kupata independency, kwa mbali.

Attorney General mwenyewe ni AG (Executive) MP by virtue of being AG (Legislature) na Judge (Judiciary)

Checks and balances zitaanzia wapi ziishie wapi? Kwa nini kusiwe na conflict of interest hapo?
 
Gaijin, nadhani shida ilianzia bungeni wakati wa kutunga sheria. Tume ya uchaguzi inafuata sheria ambayo supposedly imeopitishwa/kubaliwa na wananchi (kupitia wawakilishi wao, wabunge!).

Sheria yoyote ambayo inakinzana na Katiba haiwezi kuitwa sheria, uwezo wa bunge kutunga sheria uko limited kuwa watunge sheria ambazo zinaendana na katiba.
Ndio maana Mahakama kuu na Mahakama ya rufaa ya Tanzania zinawajibika kufuta kifungu cha sheria kinachoenda kinyume na katiba. Ingawa mara nyingi kwa kuogopa the powers who are wanakwepa kufanya hiyo kazi waliyopewa kikatiba, mfano halisi kesi ya Mtikila ya mgombea binafsi
 
Hatuwezi kujua mpaka tujaribu, unaweza kusema hutashinda halafu ukawa surprised na independent minded justices huko kwenye high courts.Unaweza kusema utashinda ukaenda kukutana na politics mahakamani.

Kinachoniuma ni ukweli kwamba hakuna mwanasheria aliyefuatilia hili. Na kuna watu wanaweza kuona hili jambo kama pedantic legalese zisizo na practical effect, nimetoa youtube clip ya Masha hapo juu, ilikuwa bado kidogo tu Masha apitishwe kwa style hii, baada ya kushindikana wananchi walipopiga kura tumeona kumbe Masha hakupendwa hivyo na wananchi, kiasi kwamba hata kama angekuwa mgombea pekee katika kura ya ndiyo/ hapana kuna uwezekano angeshindwa.

Kwa hiyo ni muhimu kubadilisha hii habari ya kupita bila kupingwa, even if it is only to ensure the integrity of our system. Ama sivyo Rostam anaweza kununua viti kibao vya ubunge akacontrol bunge lote.

Tunataka wawakilishi wa wananchi wawe wamechaguliwa na wananchi kweli, sio usani sanii fulani fulani tu.

Right tatizo la sheria tumeshaliona. So what is your recommendation? Iongezwe aina nyingine ya mbunge, i.e mbunge wa kupitishwa kwenye ibara husika? Au wananchi wapewe haki ya kumchagua hata mbunge ambaye hana mpinzani? Je hapo watakuwa wanachagua kweli kama atakuwepo mgombea mmoja?
 
asilimia 30 ya wabunge ni wa viti maalum ambao wengi wao wako pale kujaza nafasi wanazoita wenyewe za ulaji tu. Hata kuchambua kitu kidogo hawawezi.

asilimia nyengine 40 nyengine, wameenda bungeni ili kuhakikisha wanapata pensheni ya kutosha uzeeni. Nusu ya muda bungeni huwa wamelala.

nusu ya waliobaki wanajua wanafanya nini, ila wanafanya kwa kusudi kutumia loop holes kujihakikishia mambo yao yanafanikiwa.

hiyo sheria ya maana itatungwa saa ngapi!
 
"Sehemu hii ya Katiba hii" haimaanishi katiba yote counsellor, mwananchi ana haki ya kuishitaki sheria ya uchaguzi kwamba ime violate ibara ya 66 ya katiba.


Hata kama haimanishi katiba nzima still mpiga kura atababwa na clawbacks zilizopo kwenye ibara ya 5 (1) Kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka kumi na minane anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi unaofaywa Tanzania na wananchi. Na haki hii itatumiwa kwa kufuata masharti ya ibara ndogo ya (2) pamoja na masharti mengineyo ya Katiba hii na ya Sheria inayotumika nchini Tanzania kuhusu mambo ya uchaguzi. Sheria ipi inayotumika nchini Tanzania kuhusu mambo ya uchaguzi?
 
Kuna aina tano za wabunge, tunachojua Pinda aliteuliwa na chama chake lakini hajachaguliwa na wananchi wote kwa vile nchi yetu ni ya vyama vingi definitely ha-qualify kwenye aina hizo. Ingawa tunajua kuna wabunge wa kuteuliwa na rais hao wanakuwa wabunge halali lakini hawawezi kuwateuliwa kuwa mawaziri wakuu, sasa je huyu aliyeteuliwa na chama chake tu atawezaje kuwa waziri mkuu? Labda katiba iongeze aina za wabunge ziwe sita ama kuwe na wabunge waliopita bila kupingwa au wabunge waliopitishwa na vyama vyao bila kuchaguliwa na wananchi kama ilivyo kwa wabunge wa viti maalum.
 
Right tatizo la sheria tumeshaliona. So what is your recommendation? Iongezwe aina nyingine ya mbunge, i.e mbunge wa kupitishwa kwenye ibara husika? Au wananchi wapewe haki ya kumchagua hata mbunge ambaye hana mpinzani? Je hapo watakuwa wanachagua kweli kama atakuwepo mgombea mmoja?

Mbona nishasema several times hapo juu.

The spirit of the law is to give power to the people.

Wapeni wananchi uwezo wa kupiga kura ya Ndiyo/ Hapana pale ambapo pana mgombea mmoja tu.
 
Sheria yoyote ambayo inakinzana na Katiba haiwezi kuitwa sheria, uwezo wa bunge kutunga sheria uko limited kuwa watunge sheria ambazo zinaendana na katiba.
Ndio maana Mahakama kuu na Mahakama ya rufaa ya Tanzania zinawajibika kufuta kifungu cha sheria kinachoenda kinyume na katiba. Ingawa mara nyingi kwa kuogopa the powers who are wanakwepa kufanya hiyo kazi waliyopewa kikatiba, mfano halisi kesi ya Mtikila ya mgombea binafsi

Wanaotunga sheria na wanaotunga katiba ni 'wale wale'. Wakiona katiba inawaletea 'kauzibe' si wanaibadilisha tu..!
 
Back
Top Bottom