Picha na stori za Loliondo- kwa Babu

wanajamvi nimeona nidofoe hizi picha kutoka threads mbalimbali, ila watu wapate picha kamili yanayojiri huku Loliondo kwa Babu mwenye tiba ya magonjwa sugu.....Kama wewe ni mgonjwa anza safari sasa ukapate uponyaji wa dawa za mimea usijekujilaumu baadae kuwa ungejua !

[/ATTACH]View attachment 24605View attachment 24606View attachment 24607View attachment 24608View attachment 24609View attachment 24610View attachment 24611View attachment 24612


View attachment 24613View attachment 24614View attachment 24615

Ama kweli Babu Kiboko
 
Nyani hauni kundule..!!mnavyomsema K. vibaya si ndio na nyie mnachonga hivyo, au kuchonga ni vipi??? Mwacheni na yy atibiwe mnataka afe!!! Shame on U!
 
Yule msemaji wa nchi ya Tanzania na anayedhani ni mjuaji wa kila kitu kinachoihusu Tanzania na watu wake, ameonekana kwenye foleni ya Loliondo. Haijajulikana mara moja ameenda kufanya nini. Mwenye tetesi kamili atujuze. Nafuatilia picha, nitaziweka soon.
ameenda lini? mbona wikendi yote alikua dar

can we leave this guy alone?
 
Nyani haoni kundule...!! Na nyie ndio mnachonga hivyo, vinginevyo mgekaa kimya. Mwacheni K. atibiwe ana haki kama wengine.:hand:
 
ndio maana simsikii jioni kwenye kile kipindi chao cha mipasho na wale wadada?
 
Ana matatizo gani huyu ndugu, kwa nini kila mara ni mtu wa kupondea tuuuuu???
Kwake hakuna jema hata kidogo.:blah:
 
jamani ustaarabu hata wa kuandika unatushinda???
sasa huko Loliondo kila mtu anaetaka anaenda, hata ndugu zetu wanaenda, ina maana Alivyoenda Kuyu kaka, maneno ya kashfa tunatukana na ndugu zetu pia.

Watu siku hizi wanajaribu kila kitu, kutegemeana na mazingira waliopo. Mfano, tiba za kichina, za kimila, za Forever living, miujiza ya kikristu, ya kiislamu, ya mazingaombwe nk.
Kama huendi kule unaenda huku.

kama wewe hutaki kwenda basi!!!!
 
Ishu ya Kibonde siyo kwenda ama kutokwenda kwa Babu,...ni tabia zake za utata hasa anapoongelea masuala yenye maslahi na jamii ya wengi, aidha kujifanya kusemea mambo ambayo pasi na shaka yamemzidi kwa mbali kiwango cha uelewa wake dumazi!
 
Ama kweli watu wana shida, hivi ni kweli kwamba dawa ya aina moja inatibu magnjwa ya aina mbali mbali .........au .......imani yako inakuponya.?......maana mambo mengine yanachanganya, unywe dawa aina moja tena kwa muda mfupi, upone ukimwi, kansa, kisukari.........eh.
 
naona post yangu imetupwa kulee

lets leave kibonde alone... enough is enough
 
Binafsi sijaenda Loliondo ,lakini haijaninyima kutafuta shuhuda za watu mbalimbali ili kujua nini kinaendelea . Mchungaji Mwasapile amepata ufunuo na kuoteshwa katika ndoto,akakabidhiwa kikombe ambacho atawapatia watu dawa nao watapona magonjwa mbalimbali yakiwamo ya kisukari,pumu,presha na hata ukimwi na magonjwa mengine sugu .kama una virusi ukishapatiwa dawa hiyo baada ya siku saba utaitajika kwenda kupima ili ukiri mwenyewe muujiza wako .


Kwangu sio tiba ya kisayansi na napinga wale wote wanaotaka kuingiza ubinadamu na hata usayansi wao katika hili . katika mambo haya ya kiroho hatua zozote za kibinadamu zitashindwa kabisa . kakobe kumpinga mchungaji huyu ilhali wapo mashuhuda wa miujiza hii ni anaonekana jinsi alivyo pindi anapokosa la kusema . Kama kakobe ataongea katika mlengo wa ushindani wa kibiashara katika huduma ya kiroho analipeleka wapi kanisa lake . Ina maana kama ni kweli yeye ( kakobe ) ana ufunuo wake ina maana hakuna mtu mwingine yeyote anaeweza kupata ufunuo kama wake na hata kumzidi .maneno yake dhidi ya mchungaji mwasapile hayana tija,hayafai kusikilizwa na anajivunjia heshima yake.

Jumapili katika vijiwe vyetu vya weekend tumepata watu wakishuhudia miujiza yao . Kuna mzee mmoja alikuwa na presha mbaya kabisa leo hii presha yake ipo normal .Sijapata shuhuda wa HIV lakini wapo na nimesoma kwenye vyombo vya habari . Jana tarehe saba nimekutana na mzee mmoja / mfanyabiashara katika maongezi yake amesema sukari yake kwa sasa ipo normal . Alikuwa dhaifu sana mwanzoni na katika safari yake ya kurudi kutoka Loliondo alipofika mto wa mbu alikula Chips mayai kitu ambacho ni nadra sana kwa watu wenye kisukari.

Katika maelezo haya tunapaswa kuelewa kwamba uwepo wa mungu ni dhahiri,hasa kwa wale wanaomtumaini . Waliokuwa na mizigo yao ya maradhi hatimaye mungu amekuja kiuhalisia kumtumia mtumishi wake Mwasapile ili kuponya .

Wagonjwa wote wenye matatizo sugu waanze kuelekea loliondo . Zipo Changamoto kadhaa hasa za usafiri na wingi wa watu . Wajasiriamali wameshatumia mwanya huu na nauli kwenda na kurudi Lolionda kutokea Arusha ni Sh 100,000 kwa sasa . Usisahau 500 ya mzee yeye hana makuu kwani ana roho mtakatifu na sio roho mtaka vitu .Katika 500 hiyo 200 ni kwa ajili ya wamama wanaochemsha dawa,200 ni kwa ajili ya kanisa na mia ndio ya kwake.

Leo asubui nimemsikia naibu waziri wa afya akiongea na waandishi wa habari anasema wizara haiwezi kutoa tamko juu ya tiba hiyo lakini wanafuatilia ubora wa tiba hiyo na mazingira inapotolewa. Hapa namshauri mheshimiwa waziri abadili mawazo yako ,aondoe huo uchunguzi wake. Atakuta anachunguza matendo ya mungu ambapo ni dhambi kubwa . Hakuna chembe ya ubinadamu katika hili . Dawa hiyo hiyo inaponyesha ukimwi,kisukari na hata presha .hashangai ! Asije akatuma na/au akaunda tume katika hili kwani atashindwa.

Natumaini Mmenisoma
 
Wajameni naomba mnijuze kuhusu huyu babu wa loliondo. Kuna mtu amepona? Kama kuna mtu naomba ushuhuda wake!
 
Back
Top Bottom