PICHA: Mkutano wa Waislamu Mtwara wakipinga gesi isiende Dar es Salaam (leo)

Kwa kweli tupo pamoja na wanakusini ni wakati muafaka wa watanzania kuhakikisha kuwa rasilimali inayopatikani kwenye maeneo yao husika inawanufaisha haingii akili gesi inapatikana mtwara lakini watakaofaidika ni watu wa dar the same to areas like simanjiro tanzanite inapatikana huko lakini waliofaidika ni watu wa mkoa wa arusha barabara ya kwenda simanjiro ni shida likewise to other areas.
 
Mpaka kieleweke!!

Sultani Mangungo wa Bagamoyo amesema hajui hawa jamaa wanataka nini!!

Labda nimsaidie huyo sultani, watu wa ntwara wanachokitaka ni kutawanya uwekezaji wa viwanda katika nchi hii kwa kujenga kiwanda kikubwa cha kujengeneza malighafi ya gesi na kuwa bidhaa za gesi ntwara. Na hii itawavutia wawekezaji wengine kuja kuwekeza ntwara wakifuata hiyo bidhaa ya gesi. Nimetumia maneno malighafi ya gesi na bidhaa za gesi ili kumlahihishia kuelewa, nadhani sasa atafikiria sahihi na mteule wake Mhongo
 
Mti uliopandwa na WanaCCM wa Udini umemea na unatoa matunda haya. Wazee wa Jihad ndo kwanza wameanza.
udini hakuna mtwara/lindi leo waisilam na j'pili wakristo then j tatu wapo pamoja hii itakuwa vita ya bunduki vs zana za jadi na bila kusita zana za jadi zitashinda na kuandika historia mpya
 
Mkianza kujigawa kimakundi hamtafika popote...wekeni udini pembeni!

hakuna udini uliongelewa hapa zaidi ya viongozi wa dini kuongelea mambo ya kiuchumi ambayo yatagusa watu wote, wapagani , wakristo , waislamu nk, sawa sawa na cct au tec wanapotoa matamko ya kuwasaidia wa tz wote bila kujali dhehebu au asili ya mtu, haki bin haki
 
Wanamtwara msirudi nyuma!
Yani msikubali wakwere wachukue gas yenu!
 
Ni mkutano wa waislamu au wananchi wa Mtwara? Mbona huu mkutano ni kama umefanyika sehemu ya wazi? Mna uhakika gani umehudhuriwa na waislam pekee?
Kuna haja ya serikali ya Kikwete kutafuta maridhiano na hawa jamaa. Maana hapa hakuna mjanja, si wanamtwara wala JK. Hivi waliwahi kujiuliza kwamba itakuwaje iwapo serikali itabadilisha mpango wa kutumia gesi kwa ajili ya kuzalishia umeme, na badala yake wakaamua kuwekeza kwenye upepo na makaa ya mawe?
Mimi nafikiri wanamtwara wakubali manufaa waliyoahidiwa ya kuingiziwa umeme bure, na kulipa gharama ndogo ya umeme. Maana kukishakuwa na gharama ndogo ya umeme viwanda vingi vitaelekezwa huko kwa kuwa kutakuwa na gharama ndogo za uzalishaji. Lakini huu msimamo mkali wanaotaka kuuonyesha wanaMtwara sina uhakika kama una maslahi kwa taifa.
 
Hii inaonyesha kuwa wakifanya mkutano kama wananchi wanaambiwa ni siasa hasa cdm haya sasa ni kwa mwamvuli wa waislamu ingawa najua hapo huwezi wakosa wakristo kwakuwa hili halihusu dini. Kila la heri mtwara mnatufumbua ?acho si gesi kwanza sasa ni Mtwara kwanza Bwagamoyo ifuate
 
hatari ninayo ihisi
baada ya hapo wataunda Jeshi la Kiislamu la Kusini mwa Tanzania
 
Gesi ya watanzania wote, kama ilivyo maji ya mtera,dhahabu na almasi ya mwadui na tanzanite ya mererani
 
Mkianza kujigawa kimakundi hamtafika popote...wekeni udini pembeni!

Haya mnayoyashabikia subirini mtavuna mnalolitaka ,Mungu wa Yakobo atuepushe ,hamuelewi hatari mnayoipandikiza katika taifa kushabikia upuuzi unaofanywa .na wanamtwara na kuungwa mkono na akina zitto ,hautakua muda mrefu mtavuna machungu ,,,,,oooooh ole wa kizazi kilichopofuka na kushindwa kuyajua yaliyorohoni ,,,,,mmetegwa na Ibilisi na kuingia kichwakichwa
 
Kauli za kihaini

unajua uhain wewe hilo kontena la pembe za ndovo lililokatwa NAMANGA huo c uhain. waziri KAGASHEKI hawa tembo anataka waishe ndio ajiuzuru kwani ktk waziri wote walio pita huyu ndiyo anangoza kwa kugawa maliasili ye2 kila kukicha
 
Back
Top Bottom