PICHA: Hawa ndio waliomuua mwandishi wa Channel Ten (Daudi Mwangosi) huko Iringa

Sio kosa ilimradi ujiridhishe kwamba habari ni ya kweli pili iwe imetoka kwenye reliable source kama ina mashaka haina ushahidi wa kutosha na source haijulikani mute
Wacha hiyo, Mdogo wangu Ni afisa ugavi polisi, anapata shida kuli - concile accounts zake na wenzie kwa sababu wakubwa wanamletea invoice za vitu ambavyo hajawahi kupokea na kumwamrisha aidhinishe malipo.

Akuniletea makabrasha nikayatundika Ni kosa?
 
Hiii bada imenikumbusha mbali sana,huyo mwandishi alionewa sana yaaaani tr 25 Oct tusifanye kosa kuyachagua Haya massm
 
jamani Mwangosi uliuwawa kinyama sana...yani hii habari ni kati ya habari zilizowai kunihuzunisha mno lala salama baba Mungu aliye haki na kweli anaendelea kukulipia baba
 
Wana JF,

Naomba mniruhusu niweke picha zenye sura za walioshiriki kitendo hiki cha kihuni ambacho ni uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu kama kamera yangu ilivyokinasa.

Nina picha ambazo zimechukuliwa zinazoonyesha walioshiriki na jinsi walivyoshiriki. Hata RPC alikuwepo eneo la tukio.

Mods, naomba msiunganishe thread yangu plz.

Picha nyingine nimezituma kwa watetezi wa haki za binadamu na video nimeziweka YouTube (sitatoa link kwa sasa).

Wanahabari, ni wakati wa kuonyesha umoja wetu dhidi ya udhalimu huu.

-----​

attachment.php

Huyu askari alimwelekezea mtutu tumboni na kumsambaratisha marehemu. Ni wazi watu wa Iringa wanamfahamu askari huyu.


attachment.php

Pembeni ni shangingi la RPC, askari huyu naye kashuhudia kitendo hiki cha kikatili. Wanahabari tushirikiane kupiga kelele. Hapa walikuwa wamemaliza unyama wao wakimwondoa mwenzao aliyeumia eneo la tukio

Kama ni kesi, askari huyu anaweza kuhojiwa. Nimekata picha kusitiri mwili wa marehemu.

Marehemu kafa akipigania haki za wanahabari, ni wakati wa wanahabari kushirikiana vinginevyo wanasiasa wataendelea kutumia vibaya vyombo vya dola dhidi yetu.


Hii siyo rahisi kufutika-mwenye Camera tu haya yanamfika alafu chakuumiza sana aliyesimamia hili anapandishwa Cheo!
Kwa hili JK-huwezi kuepuka lawama na iko siku muumba wa bingu na ardhi atasikia kilio cha Watoto wa Marehemu na mama yao Mungu !

Haya yanaoendelea ni mwendelezo wa yaliyopita ambayo Mfumo wa ulinzi na usalama umeyaacha kwa faida ya wahusika!
 
hakika kuitegemea mahakama zilizo chini ya ccm hakuna jipya ni sisi wananchi kufanya maamuzi
 
..hivi kesi hii itaisha lini?

..serikali itailipa fidia familia ya Mwangosi kama ilivyofanya kwa familia ya Lt.Gen.Kombe?

..Je, Raisi Magufuli atatengua kupandishwa cheo na kumfukuza kazi kamanda wa polisi aliyekuwepo eneo la tukio siku Mwangosi ameuawa?

cc maggid, Pasco, Manyerere Jackton


Katika mafaili hiyo kesi huenda imeshafutwa kwa wino mweusi.

Hivyo usitegemee kuwa kuna wa kuajibishwa katika suala hili. Wauaji walifahamika lakini hakuna mwendelezo wa ile kesi hatujafahamishwa.

Labda kama kuna mwenye taarifa iliishia wapi na familiya ilipata chochote kwani aliacha mke na watoto, atueleze ili tujue.

Mimi nipo gizani...........
 
Joka Kuu, heshima yako mkuu. Huu msiba unaniuma saaaana. Na wote walioichagua CCM uchaguzi uliopita simply walifurahia mauaji ya Mwangosi
 
Joka Kuu, heshima yako mkuu. Huu msiba unaniuma saaaana. Na wote walioichagua CCM uchaguzi uliopita simply walifurahia mauaji ya Mwangosi

..POLE ndugu yangu.

..tusiwalaumu wananchi kwa kuichagua CCM.

..wapinzani hawakufanya kazi ya kutosha kuwahamasisha wananchi.

..kampeni za upinzani na mgombea wao hawakuwa na mvuto hata kidogo.

..pamoja na mgombea wetu kuwa mgonjwa na kushindwa kuhutubia kila mahali, bado wananchi walijitokeza kwa wingi kupigia kura wapinzani.

..wapinzani tujilaumu sisi wenyewe kwa kuweka mgombea dhaifa na kuendesha kampeni zisizo na mvuto.
 
..hivi kesi hii itaisha lini?

..serikali itailipa fidia familia ya Mwangosi kama ilivyofanya kwa familia ya Lt.Gen.Kombe?

..Je, Raisi Magufuli atatengua kupandishwa cheo na kumfukuza kazi kamanda wa polisi aliyekuwepo eneo la tukio siku Mwangosi ameuawa?

cc maggid, Pasco, Manyerere Jackton
Kamanda wa Polisi kipindi Mwangosi anauwawa, tayari kastaafu utumishi wa umma. Ni Ret. DCP kamuhanda
 
Kamanda wa Polisi kipindi Mwangosi anauwawa, tayari kastaafu utumishi wa umma. Ni Ret. DCP kamuhanda

..naamini bado anaweza kuchukuliwa hatua.

..kwa mfano serikali inaweza kukatisha pensheni na mafao yake.

..vilevile anaweza kushtakiwa mahakamani kutokana na mwenendo wake siku ya tukio.
 
....very sad...!.....but again, it's a high time people to be reminded, to know that, wherever in the world, police force in action is not precise tool...!RIP Mwangosi!
 
Back
Top Bottom