Mwandishi wa habari akamatwa na Polisi akiwa katika majukumu yake mkoani Mwanza

Prof Koboko

JF-Expert Member
Aug 15, 2020
350
2,549
Taarifa ya kukamatwa kwa Mwandishi wa habari Shagata Suleiman na Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza.
.................................................

Ndugu waandishi wa Habari na Taasisi za kihabari Nchini Tanzania, nasikitika kuwataarifu kuwa, Mwandishi wa habari mwenzetu na mwanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza, Bwana Shagata Suleiman, ambaye pia anafanya kazi na Gazeti la Daily News na Habari Leo anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza na sasa ni zaidi ya masaa matatu tangia amekamtwa.

Mwandishi huyu amekamatwa kwa sababu alikwenda kituo cha polisi kati cha Mwanza kwa lengo la kutafuta mizania / ku balance habari ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kushikiliwa na Jeshi la Polisi.

Cha kushangaza alipofika kwenye lango kuu la kuingilia kituoni hapo alikamatwa kwa kuambiwa yeye ni msumbufu kwani alifika kituoni hapo zaidi ya mara tatu.

Klabu ya waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (MPC) imefuatilia kwa mhariri wa Chombo anachofanyia kazi mwandishi huyo na kubaini kuwa, Mwandishi huyu alikwenda awamu ya kwanza na aliambiwa arudi baadaye lakini aliporudi tena akiwa na wenzake aliambiwa yeye ni msumbufu, alikamatwa yeye pekee na kuwekwa chini ya ulinzi hadi sasa.

Nilipopata taarifa hii nilijitahidi sana kumtafuta RPC wa Mwanza Ramadhan Ngh'anzi kwa njia ya simu bila mafanikio, pia nilimtuma ujumbe mfupi ambao pia hakujibu.

Klabu ya waandishi wa habari ya Mkoa wa Mwanza tunaliomba Jeshi la Polisi kumwachia Mwandishi huyu na pia kutambua wajibu wa Mwandishi wa habari kwenye kutekeleza majukumu yake.

Kutafuta mizania ya habari ni jambo jema zaidi kuliko kurusha habari ya upande mmoja inayoweza kuzusha taharuki.

Hakuna sheria inayomkataza mwandishi wa habari kufuata chanzo mamlaka/ authoritative source kupata taarifa.

Mwisho MPC inatoa wito kwa RPC wa Mwanza na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Saimon Sirro kulishughulikia jambo hilo na kuzingatia azma ya Serikali ya sita ya kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari na wanahabari Tanzania kwa kuwashughulikia askari waliohusika kwenye kitendo hicho.

Waandishi wa habari Mkoa wa Mwanza tupo tayari kuacha kufanya kazi na Jeshi la Polisi kama vitendo vya kuwadhalilisha waandishi wa habari vitaendea kuungwa mkono na jeshi la Polisi Mkoani Mwanza.

Mwisho tunaomba taasisi za kihabari na watetezi wa haki Tanzania kuingilia jambo hilo.

Edwin Soko
Mwenyekiti
MPC
20.07.2021
 
Babati,

Unalo mwaka huu😂😂😂😂😂

Dume🔥🔥🔥 HAPA KAZI TUU💥💪
Jike 🔥🔥🔥 KAZI IENDELEE 💥💪

Rest well our hero President John Pombe Joseph Magufuli 🕊🕊🕊

Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake wote🙏
 
Wavifungie tu vyombo vya habari,mbona haya mambo yanarudi kwa kasi sana.
Mmemchokonoa sana, huenda anafanya hivyo Ili aone kama kweli mnauwezo wa kumnyoa kwa mujbu wa ahadi yenu,au kama kweli mnaubavu wa kukoromeana na Taasis ya Urais maana kuna mmoja alisema hawezi kumpa muda Rais.
 
Mmemchokonoa sana, huenda anafanya hivyo Ili aone kama kweli mnauwezo wa kumnyoa kwa mujbu wa ahadi yenu,au kama kweli mnaubavu wa kukoromeana na Taasis ya Urais maana kuna mmoja alisema hawezi kumpa muda Rais.
Tunapita tu duniani,usitegemee kutishia bunduki kwa walevi wakisiasa.JK alitamkiwa mengi sana tena makubwa,alibaki kucheka tu
 
Tunapita tu duniani,usitegemee kutishia bunduki kwa walevi wakisiasa.JK alitamkiwa mengi sana tena makubwa,alibaki kucheka tu
Ni sawa, lakini kumbuka Lila binadamu ana kiwango chake cha uvumilivu. Mtu kaingia madarakani kawatoa wafungwa wote wa kisiasa ambao wengi walikuwa ni CHADEMA, kawasikiliza kuhusu katiba akawaambia mmpe muda alafu mnamjibu "hamtampa muda" wengine wanasema watamnyoa wa wembe uleule waliotumia kwa mtangulizi wake.

Hata kama ni kuvumilia,lakini swala la mama kubadilika limechagizwa na dharau za CDM.
 
Hii mitihani ndo itamkomaza mama. Ila huo uandishi wa kufuatilia mpaka ndani ya Kambi ya jeshi duh!
Watu wameamua kufanya majaribio kwa utawala huu, mama akichemka tu mwanzoni itamsumbua sanaaa
 
Ni sawa, lakini kumbuka Lila binadamu ana kiwango chake cha uvumilivu. Mtu kaingia madarakani kawatoa wafungwa wote wa kisiasa ambao wengi walikuwa ni CHADEMA, kawasikiliza kuhusu katiba akawaambia mmpe muda alafu mnamjibu "hamtampa muda" wengine wanasema watamnyoa wa wembe uleule waliotumia kwa mtangulizi wake.

Hata kama ni kuvumilia,lakini swala la mama kubadilika limechagizwa na dharau za CDM.
Balance matamko ya wanasiasa.
1. Alisikika akisema tutamchoma sindano ya sumu.

2. Ukipigwa risasi 3 hujafa wewe sio askari.

Nadhani angekuwa anakamatwa mhusika kwa kumkashifu MTU kuliko kutegea/kuvizia kwa kukomoa taasisi.

Vyombo vya habari vinaeneza kwa haraka ujinga bila source.
 
Unalo mwaka huu😂😂😂😂😂

Dume🔥🔥🔥 HAPA KAZI TUU💥💪
Jike 🔥🔥🔥 KAZI IENDELEE 💥💪

Rest well our hero President John Pombe Joseph Magufuli 🕊🕊🕊

Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake wote🙏
Hahaaa...washaloweshwa nywele kwa maji na sabuni. Wembe unaandaliwa kuwanyoa. Walidhani Mama ni wakispotspoti
 
Hao makanjanja form four failure, hakuna habari yoyote aliyowahi kuitoa, wengi ndio wanamsikia leo, sio kila mwenye notebook na kalamu ni junalisti
 
Hasira zao za kutopandishwa cheo kwa miaka sita ndio wanamalizia kwa watu
 
Back
Top Bottom