Pendekezo: Prof. Lipumba awe mgombea wa upinzani Igunga

lipumba akíombea halafu akakosa si heshima yake itashuka sana jamani? tumwache tu kwa ajili ya 2015 urais.
 
SAMAHANI WAKUU WANA JF,
naomba ufafanuzi katika hili,
Baadhi wanasema CCM na CUF wana ndoa ya pamoja,
nijuavyo mimi katika ndoa kuna mwoaji na mwolewaji (Kiswahili),
Katika hilo la ndoa ya CCM na CUF (kama baadhi wanavyotamka),
je ni nani mwolewaji? na nani mwoaji?,inanitatiza sana.
 
CDM ilimshinikiza DK Slaa kuwa mgombea urais japo mwenyewe alikuwa hataki. Tumeona faida yake kuingiza wabunge wengi upinzani.

Kwa hivyo kwanini tusichukue nafasi ile kumshinikiza Mh Lipumba ili agombee ubunge Jimbo la Igunga:
  • Ni mzaliwa wa Tabora
  • Ni mwenyekiti wa Chama cha CUF ili kuongeza nguvu za upinzani akisaidiana na kina Mbowe, Lissu na wengine
  • Itaijenga Cuf kisiasa na kujenga Upinzani wenye nguvu bungeni
  • CDM haina nguvu sana kulinganisha na CUF kwa kuwa lipumba ndipo anapotoka.

Hii dhana ya wapinzani kuungana kwenye kugombea nafasi za uongozi mimi kwa kweli huwa siielewi vizuri. Hivi wanaungana kwa lipi? Kwa sera, iitikadi, maslahi ya chama, maslahi binafsi ya wagombea, nafasi ya uongozi, au kwa malengo yao muda mrefu?

Hivi mfano wakiungana halafu Lipumba akashinda; je huu muungano utaendelea au baada ya muda mfupi tutamwona mbunge mpya akichukua msimamo tofauti katika masuala kitaifa yanayohitaji msimamo wa pamoja wa wapinzani? je kushinda kwa CUF Igunga mfano kutaiongezea nini CHADEMA, NCCR Mageuzi au TLP kimkakati kuelekea kwenye uchaguzi wa 2015.

Kuhusu suala la Igunga mtazamo wangu ni kuwa kama Lipumba ni mzaliwa wa Igunga na ameshaweka mizizi kwa wapiga kura wake anaweza akawa na nafasi ya kushinda hata bila ya ushirikiano na wapinzani wengine. Lakini kama anatoka wilaya tofauti na Igunga sidhani kama atakuwa na nafasi kubwa ya kushinda hasa ikizingatiwa kuwa hana historia ya kushinda ubunge kwenye jimbo lolote la uchaguzi Tanzania.

Iliwezekana kwa Mrema na Mbowe kwa sababu walikuwa na track record ya kushinda na kuwatumikia wananchi katika nafasi hiyo ya ubunge. Lakini kwa Lipumba let us wait and see anaweza akaandika historia mpya nchini na itampa credibility ya kugombea tena urais mwaka 2015.
 
Mkuu,

Tukiweka mbali ushabiki wa Chama tunahitaji mtu kama Lipumba bungeni. Hali ya uchumi wa nchi unaenda kombo na walioko bungeni sio wajuzi wa uchumi waliobobea Lipumba anaweza kuongeza nguvu bungeni kuzidi kuikosoa serikali iliyo madarakani.

Hapa mkuu unaongea mambo yaliyopitwa na wakati. Cuf hawawezi kuikosoa serikali ya ccm kwa sababu wameshakuwa mwili mmoja. Ndoa ilifungwa Zanzibar na ndiyo maana kwa muda sasa cuf hana makali tena wala ukali wowote mbele ya magamba. Utaona hata mjengoni cuf wanaongea kwa tahadhali sana wasije wakavunja ndoa yao na magamba.

Kwa hiyo unapoongea kuhusu wapinzani kuungana cuf hawamo katika kundi la wapinzani. Umeshuhudia mwenyewe yanayoendelea mjengoni kwamba cuf wanaongea against cdm.

Usisahau pia kuwa viko pia vyama vingine ambavyo vimepandikizwa na magamba. Unaweza kuvitambua kwa maneno yao
 
Jambo wana JF!

Ubunge igunga ni moja kati ya ajenda mpya yakufanyia kazi. Igunga ina wasomi kadhaa ambao wanafaa kuwa wawakilishi wa wananchi. Wasomi hawa ni pamoja na Dr. Kafumu Kamishna wa Madini- Nishati na Madini, mtaalamu aliyebonea katika madini, tunaye pia Bw. Mboje mtaalamu wa masuala ya uvuvi ambaye tunasikia yuko Marekani kwa sasa, Jafar Omari, Hamis Mapinda na Malembela Mashauri mwalimu wa sekondari.

Watu hawa wote waliwania ubunge awamu iliyopita na bw. Rostam. Naamini mmoja kati ya hawa anafaa awe mwakilishi wa wananchi kwa jimbo la Igunga. Kwa namna tulivyowasilikiliza wakati wa kampeni walikuwa moto wa kuotea mbali maana walieleza ukweli kila palipostahili. Nawashauri chama chochote kiwatafute hawa badala ya kufikiria mtu ambaye hajui haja za watu wa Igunga. Igunga kwanza mengine yafuate.

Igunga imekuwa wilaya ya mwisho kimaendeleo ukilinganisha na wilaya nyingine za mkoa huu wa Tabora. Hakuna maji, zahanati hovyo, shule hazina walimu, hakuna mikakati ya maendeleo. Nashangaa wanaosema rostam kaliliwa na watu si kweli hata kidogo labda kwa wale vibarua waliokuwa wanashiba kwake.

Nashauri Igunga iwatumie vijana hao niliowataja wanaweza kufanikisha maendeleo ya Igunga.

Kama kuna mwenye CV za hawa watu azianike jamvini ili watu wasaidie kutoa mawazo ya kina Igunga ipate mtu wa kufaa.

Maoni yenu wana jamii yanasubiriwa.

Ituganhila Mashikolo
Igunga
 
Wewe unaamini CCM ya Rostam bado inaweza kutupatia mbunge? Kwa nini unasema "Chama chochote". Nashauri "chama chochote isipokuwa CCM" kiwatafute watu uliowataja na kuwaomba kugombea. Ndani ya CCM hata ungekuwa clean kiasi huwezi kuwawakilisha wananchi inavyotakiwa.
 
Igunga imekuwa wilaya ya mwisho kimaendeleo ukilinganisha na wilaya zingine za mkoa huu wa Tabora. Hakuna maji, zahanati hovyo, shule hazina walimu, hakuna mikakati ya maendeleo. Nashangaa wanaosema rostam kaliliwa na watu si kweli hata kidogo labda kwa wale vibarua waliokuwa wanashiba kwake.
Nahauri Igunga iwatumie vijana hao niliowataja wanaweza kufanikisha maendeleo ya Igunga.

ROSTAM AZIZ: Miongoni mwa mafanikio makubwa tuliyoyafikia kupitia ushirikiano wetu na uongozi wa pamoja ni kwamba, mwaka 1994 Igunga ilikuwa ni wilaya ya mwisho kwa maendeleo mkoani Tabora lakini leo ndiyo ya kwanza, taa za barabarani, bima ya afya kwa kila kaya, zahanati kila kijiji na shule nyingi kuliko idadi ya kata zilizomo kwenye wilaya.
 
Pesa za epa zimetumika kuijenga igunga wakati sehemu yote iliyobaki ya tanzania haina kitu.poor tanzania
 
sitashangaa pamoja na hali mbaya ya kimaisha iliyoko Igunga bado wanaweza wakachagua magamba tena akiwa ana ka ushombeshombe, mburushi, au muasia atapita kirahisi saaana si unajua wanyamwezi tena washazoea mateso toka enzi za kina Tippu tippu, na ule msemo MZIGO MZITO MPE MNYAMWEZI una ukweli kabisa
 
Taarifa nilizozipata sasa hivi, yule mwandishi wa habari mashuhuri nchini, Bw. Said Kubenea anatarajiwa kugombea ubunge katika jimbo la Igunga lililowachwa wazi na mbaya wake Rostam Aziz.

Tayari mazungumzo kati ya Kubenea ambaye mmoja wa wazazi wake wanatoka Igunga yamefanyika naye inasemekana amekubali ofa hiyo. Anatarajiwa kugombea kupitia chama cha magamba.

Mwingine anayetajwa kutaka kujitosa jimboni Igunga, ni Hussen Bashe na Peter Kafumo.
 
kwani kubenea ni muirani??hawezi chaguliwa na ccm APENDE ASIPENDE CCM IGUNGA INAONGOZWA NA NGOZI NYEUPE BWANA,LABDA AINGIE CDM
 
Nakwambia anagombea. Jana alikuwa na kikao kirefu na Membe na Msekwa. CCM wanaona njia pekee ya kushinda jimbo la Igunga ni kumuweka Kubenea. Wamemhakikishia vikao vya chama vitampitisha. Lakini mkakati mzima unaonekana kutaka kumyamazisha yeye na gazeti lake. Wanaamini kuwa akijitosa katika mbio za ubunge Igunga, basi hataweza tena kuwachapa.
 
kama hilo litatokea naamini litawezekana....huyo Kubenea si alinunuliwa mtambo wa magazeti na hao mafisadi na akaupokea?
 
TUYUKU- Acha kupakazia mwenzako. Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. Mtambo ule Kubenea ameuziwa na Mengi. Na mpaka sasa upo pale IPP Mikocheni, hajauondoa. Acheni kumchafua kwa mambo yasiyokuwa na kichwa wala miguu.
 
Back
Top Bottom