Paukwa... Pakawa!

Ukorofi wa Mchungaji unafikia hatua ya kuuliza, je tunashangilia nini cha msingi ikiwa ukweli ni kuwa hili ni changa la macho na Kampeni za CCM kushida uchaguzi wa 2010 kwa kishindo cha tufani ya Katrina umeanza?

Mkulu Kishoka,

Heshima mbele bro, kwa kweli kinachoendelea so far ni mapema mno kusema wazi kwamba exactly ni nini hasa, between sheria na siasa, lakini:-

1. Wananchi wa Tanzania, tumeonewa vya kutosha na tumenyanyaswa na viongozi hasa wezi kwa muda mrefu sana, wakati wa Sokoine na uhujumu uchumi tumeona dagaa wakiswekwa lupango, huku papa wakiendelea kunawiri na kutucheka, tunasikia Sokoine alitaka kufanya kweli lakini Mwalimu alikataa kabisa, sasa this time is for real tunaona papa wakiswekwa lupango.

- Tena ninaaambiwa kwamba hata kuwaweka rumande hii week end nzima imefanywa kwa makusudi makubwa na "someone", kwa sababu siku ya Ijumaa baada ya kuwakilishwa kwa kesi yao ya kuomba dhamana kule mahakama kuu, mawakili wa serikali walipotea kwa makusudi na kutoonekana kwa muda mrefu sana knowing kwamba ruling haiwezi kutolewa bila ya wao kuwepo. Familia ya Yona did all they could kuwatafuta ikiwa ni pamoja na kuwapelekea gari kama watakwua wamekwama mahali lakini nowhere they could be found!

- By the time wamepaetikana ilikuwa late tena wakajitokeza wenyewe mahakamani na kupelekea the judge kuwakaripia sana, wao wakiwa wanatabasamu tu as if nothing happened, sasa unajiuliza ni kwa nini hasa kwa sababu ninaambiwa kuwa kuchelewa kwao ni moja ya sababu kubwa zilizopelekea kutoachiliwa kwa watuhumiwa.

2. Binafsi ninaamini kwamba this thing is for real kwa angalau 75%, kwa sababu ukishawafikisha Mramba na Yona, kwenye sheria ni lazima uende all the way to the end huwezi kuwaacha wengine kama the Richimonduli waliotutia hasara kubwa bongo kuliko all hawa wengine combined. Ni kweli in private mawaziri wengi wanadai kuwa uamuzi wa kutoa msamaha ulikuwa wa cabinet rais included, lakini let sheria take its mkondo kwanza, na besides ninaambiwa kwamba Yona na Mramba they are in for a long shit kwa sababu wana kesi nyingi sana pending na hasa Mramba.

- Lets say hawa tu wawili ndio watafikishwa mahakamani, can you imagine huko NEC na CC itakuwaje, kwa sababu unafikiri hawa wawili hawana wajumbe wa kuwatetea huko ndani na kutaka kujua kwa nini wengine hawajafikishwa kwenye sheria? Tayari kumeshaanza maneno ya udini, ukabila, na u-mtandao kuhusiana na kushikwa hawa Yona na Mramba, sasa rais kweli anaweza ku-take hiyo risk, jawabu kwangu ni kwamba hawezi tena hawezi kabisaa ni lazima wote watinge kwenye sheria tena soon, nasikia by next week kutakua na big news, infact tayari kuna habari za el kutafuta njia ya kukimbia!

3. Kwa taifa letu haya yanayoendelea sasa hivi hatukutegemea hata siku moja kuwa yanawezekana, lakini hatimaye sasa ni clear kua yanawezekana meaning kwamba from now on hakuna kiongozi atakayekua immune na sheria tena asilani, rais anahitaji pongezi nzito sana kwa hili ambalo hata Mwalimu hakuwa na ubavu nalo, WHY ninasema hivyo:-

- Sokoine alikuwa tayari ana list ya viongozi wa juu mawaziri wakiwemo aliotaka wakamatwe, kwa kuhujumu uchumi na pia alimuhakikishia Mwalimu kwamba ana ushahidi wa kutosha, kati ya viongozi hao walikwemo Barongo, na Kahama, katika kutayarisha ushahidi wake Sokoine alishikirikiana sana na Kaisi, na Kolimba. Lakini Mwalimu alipokataa wasishikwe, Kaisi ambaye sasa alikuwa RC Bukoba was so upset kwamba akaamua kwa hasira kumuweka ndani Barongo alipofika Bukoba, na hata Kahama pia lakini Mwalimu akamlazimisha kumuacha haraka sana the minute alipojaribu kule Bukoba uwanja wa ndege, wakati sir George anashuka kutoka Dar. Kina balozi Magombe wamefanya mambo ya aibu sana huko majuu, kina Maryogo na wengine wengi sana, lakini ninampa heshima rais kwa kuimaliza hii tabia ya kulindana kwa viongozi, rais ameweka mfano sasa ni wajibu wetu wananchi ku-take it form there!

3. Kwa wale wote wanaomjua muungwana kwa karibu, watakubaliana nami kwamba wakati wa kampeni zake za urais, pembeni pembeni kabla ya kufikia kwenye uwazi siku zote alikuwa na hoja nyingi sana zinazomsumbua kuhusu utawala wetu, lakini za muhimu zilikuwa tatu, (1). Viongozi mafisadi kuwafikisha kwenye sheria, (2). Nyumba za serikali walizouziwa viongozi, (3). Viongozi waliokaa kwenye power kwa muda mrefu sana. Hizi ni ishus nimesikia mwenyewe akizilalamikia sana kwa pembeni na leo nimeona akizigusa zote, ingawa kwenye la nyumba bado anasua sua, lakini haya mengine amejitahidi sana na hasa hili la viongozi na sheria.

4. Dataz zaidi nilizozipata jana ni kwamba kabla ya kufikiria kuanza kwa hii operation, kuna watu wetu walienda Zambia kula darasa kidogo on how to go about it, kwa hiyo kuna ka-muongozo flani hivi, ingawa ninaambiwa kwamba hata kule Zambia, operation ilikwenda safi sana mpaka ilipofikia kumkamata mstaafu wao wa idara ndipo mchezo ukasimama hapo hapo maana Mwanawasa, naambiwa aliiba uchaguzi na aliyeuiba ni huyu bwana mstaafu anayeitwa Chungu. Sasa je hapa Tanzania itakua hivyo hivyo kwamba hatutafika kwa mstaafu wa idara? Maana tusipofika huko kazi yote ni bure!

- Again ninaomba ksuema kuwa tuko kwenye the right track, na huu ni wakati wa kumpa rais ushirikiano wetu, na hasa ningetegemea kuwaona upinzani waki -take charge, maana huu ndio hasa wakati wao, pale tunapoambiwa hakuna ushahidi wao ndio wanaopaswa kujitokeza na ushahidi mzito, maana sisi wananchi walipa kodi tunawalipa ruzuku kila mwezi, sasa tunawalipa ruzuku for what kama sio watusaidie wka mambo kama haya?

- Kuendelea kumlaumu rais after all this kwa kweli sioni kama ni productive, kwa sababu rais anatakiwa afanye nini zaidi ya haya aliyokwisha fanya tayari? Amefungua mlango sasa sisi wananchi tu-take a charge na pia tu-take advantage, Mramba na Yona wako rumande sio kwa sababu ya kushindwa dhamana, isipokuwa ni kuthibitisha kwamba wahusika wa ushitaki wako serious, binafsi ninataka kutoa pongezi nzito sana kwa rais na wahusika wote wa hii operation, na ningependa kuwapa moyo kwamba baadhi yetu wananchi tuko nyuma yao na tuko tayari kuwapa msaaada ikibidi, lakini nasema hvi rais amefanya ya kwake, sasa ni zamu yetu wananchi kumalizia na hasa ninategemea Upinzani kutuongoza hapa, maana ndio hasa sababu ya kuwapa ruzuku.

Ahsante Rev!
 
Yaani Rev kama ulikuwa Kichwani mwangu vile. Haki ikifuatwa bila mizengwe haki ya nani tena hakuna atakayesalimika kuanzia mkuu wa nchi mstaafu hadi huyu wa sasa. Is all that possible? That's the million buck question....
hee... kumbe na wewe unaongeaga mabo ya maana!
 
Mkuu Mkandara, heshima mbele.

Mkuu Nurujamii aliuliza na narudia, watu walitaka JK afanyeje(i.e alternative course of action) ili watu waone anashughulikia ufisadi???... So far sijaona jibu.

.

Sober, MKandara na wengine,

Kosa tunalolifanya ni kuona kama ni Kikwete pekee ndiye mwenye wajibu huu.

Ndiyo nilipojibu moja ya hoja, nimeonyesha wazi ni jinsi gani kulivyokuwa na mzunguko usio wa maana wa kuchukua hatua madhubuti kulishughulikia hili.

Maadam, mmemleta Kikwete kwa mtaji wa kusema angefanya nini au afanye nini, nitarudi kwenye ile mada yangu ya awali niliyosema kuwa Kikwete in ineffective, inneficient na ineptitude.

Kama Kikwete angekuwa mjasiri na asiyeonekana kuwa ni mwoga au kutokuwa na uamuzi thabiti, tusingepoteza zaidi ya miezi 18 kulalamika kuhusu suala hili.

Masuala kama ya Richmond, Rada na EPA ambayo yametawala vichwa vya wananchi kwa takriban miezi 24 kuchukuliwa hatua, vinaonyesha wazi kuwa ama Kikwete hana uhakika anachokifanya, anabahatisha au anajilinda.

Mnakumbuka kauli ya IGP Mwema na hata Manumba ambao walisema hadharani kuwa eti walioibe EPA ni hatari sana kuwa Serikali haina uwezo au itaweza kuzidiwa kete? Ni kiongozi gani wa nchi ambaye anatoa kauli dhaifu kama hiyo na hachukuliwi hatua?

Mnakumbuka nilihoji na kuuliza ikiwa tunavamiwa au tunapata janga na kitu cha kwanza Serikali yetu inasema ni kuwa eti maadui wana nguvu kubwa hatuna uwezo, je tuendeleeje kuwa na imani na Uongozi tulioupa mamlaka amb ao unaonyesha udhaifu.

Kuna kitu wazungu wanakiita swiftly au swify. Haya mambo ya kushikisha watu adabu kuhusiana na EPA, Richmond na Rada ambayo yalisababisha mawaziri tunaosema kuwa ni kwa mara ya kwanza imetokea yalifanyika si kwa ukali na umakini wa Serikali na kiongozi wake mkuu. Yalifanyika kwa ulegevu wa hali ya juu na mzaha mzaha.

Jiulizeni iweje Lowassa na Chenge waliamua kwa hiari zao kujiuzulu lakini wakajiandalia maandamano kupongezwa na wasichukuliwe hatua na Chama CCM?

Ikiwa leo ndani ya Bunge na CCM kuna mvutano mkubwa wa kushikisha adabu hata kufukuza uanachama wale wote waliotuhumiwa kwa uzembe na ufisadi, na watu kama kina Mama Killango, Mwakyembe, Seleli, Manyanya, Shelukindo wanaonekana wahaini ndani ya CCM na mchungaji anawaasa waachane na CCM, hamuoni kama kuna tatizo la uongozi?

Wakati Jumbe alipokurufisha, haikuchukua mwaka au miezi kwa yeye tena Rais wa sehemu ya Muungano kulazimishwa aachie ngazi na kuwekwa kizuizini. Vile vile Sefu Hamadi alipoboronga naye alifukuzwa uanachama na kuwekwa ndani. Ndiyo inawezekana kwa mtazamo mmoja kuwa walionewa, lakini maamuzi ya kuwachukulia hatua kutokana na "makosa" na "tuhuma" dhidi yao hayakuwa na ulegevu.

Narudia tena, si picha nzuri kusifia kazi ambayo inaonyesha kuwa ina udhaifu wa hali ya juu na haifanyiki kwa hiari au nia madhubuti.

Kama hatua hizi zingefanyika mapema na Serikali kutolaza damu palipoanza tetesi za uhujumu, basi tungelielewa kuwa kuna uwajibikaji.

Kama Serikali ingefanya kazi hii bila kutegeana au kutishwa na wafadhili tungesimama upande mmoja kusema sasa tunaona tumaini.

Lakini, kesi zote mbili zina mapengo na udhaifu mkubwa, sawa na ile kesi ya Kiula. Zaidi ni kule kujivutavuta kwa Serikali na kuonekana kuwa kuna namna ya kulindana, kuogopana na hata mbaya zaidi ni kwa waliopewa mamlaka ya kuchunguza, kupeleleza na kufungua mashitaka wanapotoa kauli za woga na kusubiri ruhusa ya Rais kufanya kazi walizolia viapo kuzifanya.

Sasa unapoona mambo yako mkao huu, kwa nini basi tusiwe na mashaka? Kwa nini tusiendelee kumhoji Kikwete na kutaka kujua kama kweli ana nguvu au anachotufanyia ni geresha?

Sasa labda niwakumbushe kitu kimoja. Uhujumu wa ATCL, ulianza wakati tumeshaanza ongelea Rada, Richmond, EPA na uhujumu na ufisadi mwingine. Jiulizeni kama Serikali ingekuwa inafanya kazi yake kwa umakini inavyopaswa, kina Mattaka na hata Chenge wangepata wapi misuli ya kuanza kuhujumu ATCL huku kukiwa na moshi na uvundo wa EPA, Rada na Richmond?

Kwa kuwa swali linasema mnataka Kikwete afanyeje, jibu langu ni kuwa Kikwete aache kujivutavuta. Hii mambo ya kusema tulichukua muda kufanya ushahidi au inabidi tufanye uchunguzi kwa umakini sana maana watuhumiwa wana pesa sana ni kauli inayoonyesha udhaifu.

Yeye Kikwete akiwa kama Rais na Mwenyekiti wa CCM, inabidi awe na msimamo usioyumba na awe mwenye uwezo wa kuchukua hatua kali bila kusita, iwe kwenye Serikali au ndani ya Chama.

Upuuzi wa kina Lowassa na Chenge kujifanyia maandamano, umeonyesha wazi kuwa wao, Lowassa na Chenge wana nguvu sana na hawamheshimu Rais na Mwenyekiti wao. Wao kama Mramba na Yona, wana tuhuma nyingi sana za uzembe ambazo zinaegemea kusema kuwa ni Ufisadi. Sasa wanaporandaranda Bungeni, Majimboni kwenye NEC na CC kama hakuna lililotokea, inabidi tujiulize, ni lini watachukuliwa hatua?

Kauli aliyotoa Kikwete kuwa hana mbia kwenye urais na uongozi wake, ifanyiwe kazi kwa kweli na si kwa kurembaremba au kujivutavuta.

Namlaumu Kikwete si kuwa na mchukia, bali ni kwa vitendo, kauli na maamuzi yake kama Kiongozi mkuu ambayo yanatoa mianya kwa wahujumu, mafisadi, wazembe, wavivu na wenginewe wasiolitakia Taifa letu maendeleo au mema waendelee kupeta au kujitengenezea michoro ya kuhujumu.

Hili linanikumbusha suala la Karamagi kwenda kutia sahihi mkataba wa Buzwagi, huku Rais akiwa ametutangazaia umma wa Tanzania kuwa mikataba yote ya madini itasiitishwa kusainiwa mpaka tutakapoweza kuja na mnyumbuliko bora wa kutuongezea Taifa pato letu. Swali ni kwa nini Karamagi alikwenda London kusaini mkataba? ni kwa nini ilichukua zaidi ya miezi sita ndipo alipochukuliwa hatua? kwa nini hakufukuzwa kazi kwa kukiuka agizo la Rais?

Kila upande una haki na uhuru wa kuona picha hii kwa mtazamo tofauti.Narudia tena kusema hili ni changa la macho kwangu, kwenu inawezekana ni diripu ya kuongeza tumaini, mimi bado siamini kuwa kuna nia ya kweli kusahihisha makosa yaliyotokea. Mbaya zaidi ni dhana inayotawala kuwa hatua hizi zinaanza chukuliwa sasa hivi si kwa ajili ya umakini au kufuatilia utendaji na uwajibikaji, bali ni za kisiasa.

Kampeni kujiandaa uchaguzi 2010 na shinikizo la wahisani.
 
Yote haya ameyarithi toka kwa Mkapa na kwa uhakika amefanya mengi kurekebisha hali iliyokuwepo pamoja na kwamba bado analishwa habari za UONGO kiasi kwamba ni vigumu kufahamu kuna kiongozi chini yake mwenye nia nzuri.

..Nina hakika kabisa kuwa hii mipango inachezwa na watu wengine kabisa nje ya Kikwete na analikishwa limbwata la Wapambe (Kusifiwa) unajua tena Kikwete muungwana lakini ni mtu wa sifa...(misifa).

lile wakti haya macheche ambayo yalikuwa hayawezekani yamefanyika..
Tuwe sote pamoja ktk hili kuijenga nchi badala ya kupotezana nguvu..Let's all play our part ikishindikana ndipo tunaweza kutoa hukumu zetu..Yeye binadamu na tumeona mapungufu yake kama binadamu hivyo tumsaidie kuondoa hiki kiwingu..

Mkandara,

Yaani hapo umenisaidia sana kujenga hoja mpya au kuongezea nilichomaliza kukisema hapo juu.

Swali ni kwa nini kuna mazoea ya kumlisha Kikwete Uongo? ni wasifu gani alionao binafsi kuwa watu wanadiriki kumlisha uongo kama vile ni kitu cha kawaida bila kuwa na woga?

La pili linakuja ni hili la kusifiwa, je ni kwa nini anapenda kupewa sifa na wasaidizi wake (mawaziri, makatibu,wabunge, wasemaji, wananchi) wanaendelea kumsifia hata pale inapoonekana si pa kutoa sifa? Sifa hizi ni kwa mantiki gani na manufaa gani?

Nilichoandika kwenye hii mada ni kuonyesha mapungufu ya Serikali yake ambayo yanajengeka uimara kutokana na udhaifu wake yeye kama kiongozi mkuu.

Watanzania tumechoshwa na uongozi dhaifu na wenye kuendelea kuwa na mapungufu kila siku. Ni lini ataziba viraka au kuamka na taswira mpya ambayo haitatupa picha au hisia kuwa ni mazingaombwe, mzaha, dhaifu au woga ili tupate faraja, tumaini na nguvu mpya?
 
Rev. Kishoka,
Mkuu nimekuelewa vizuri na labda nikufahamishe vizuri ni jinsi gani mimi nafikiria.. Kwanza nimegeuza hiyo shilingi kuitazama upnade wa pili kama alivyofanya Sober na nimeona mazuri yake..
Hizo kesi zote ulizozitaja ambazo zimechukua miezi 18, zimeweza kuonekana wakati wa Kikwete hali zilikuwepo miaka ya nyuma..Kuweza kufahamu tu tobo hizo imetokana na Utawala wa Kikwete. Ni sawa na maradhi ambayo tumeyajua baada ya kufanyiwa diagnosis!..Sasa kunyiwa matibabu haichukui muda mfupi kama tunavyopenda sote, kuna kuchukua damu, kuelewa virusi vimesambaa kiasi gani na kadhalika kisha dawa ipatikane..Mbali na dawa huyo Daktari atakaye kupa dawa pia inatakiwa mwenye ujuzi na uwezo laa sivyo anaweza kukupa kipimo cha dawa kisiyofaa na mwisho kuna phamacy ambako unaweza pewa dawa isiyo ama akazsema mbona dawa uloandikiwa hailingani na maradhi...
Kwa hiyo sifa ya kwanza ya Kikwete inaanzia pale tulipoweza kwenda hospital na kuyafahamu magonjwa ya Utawala.. Uwazi kaanzisha Mkapa lakini ni wakati wa Kikwete tumeweza kuona UWAZI huo ukifanya kazi kama vile Nyerere ndiye aliye introduce Ujamaa na Kushindwa kwake.. July 1984, Nyerere alitangaza rasmi RUKSA lakini utekelezaji wake ulifanywa na Mwinyi hadi akaitwa RUKSA..
Kwa hiyo hiyo miezi 18 kuna watu wamecheza sana karata kuhakikisha Kikwete ana fail..Ni katika muda huo tumeona Kikwete akibadilisha karibu baraza zima la mawaziri ambayo ni kazi yake kama rais kisha akawaachia sheria ichukue mkondo..Huko kumekuwa na Uzembe na sidhani kama ni Uongozi mzuri kwa rais kulivalia njuga swala la kina Mkapa na wengineo utafikiria ana Usongo nao yeye binafsi.
Sasa tumekuja kwenye sheria ambako pia tumeona akiwabadilisha viongozi wengi waliokuwa chini ya Mkapa kuhakikisha kwamba sheria inaweza kufanya kazi..Kina Mkapa, Apson, Lowassa hadi kesho mkuu wana nguvu za ajabu wala usije fikiria kuwa wameondoka ndio basi. sasa kama sote tungependa sheria ichukue mkondo wake ndicho Kikwete amekifanya badala ya kuchukulia maswala haya personal.. na Nina hakika wengi wangemshutumu na pengine kuingiza maswala mazito ya Ubaguzi..
Step by step na serikali hiyo mbovu tutafika..
Ebu wewe nambie kama Kikwete akimwondoa Hoisea ama said Mwema unafikira ni nani anaweza kujenga hoja vizuri kisheria na kwa muda mfupi zaidi?..sidhani na pia kubmuka swali la Sober.. huo upande wenu wa pili mlitaka Kikwete kama Rais afanye nini zaidi!.. nani alifaa kushughulikia kesi hizi ambaye nyie mnafikiria Mtandao hawana mkono ndani ya UWT, PCCB na hata Mahakama zetu!.
 
Rev. Kishoka,
Mkuu nimekuelewa vizuri na labda nikufahamishe vizuri ni jinsi gani mimi nafikiria.. sidhani na pia kubmuka swali la Sober.. huo upande wenu wa pili mlitaka Kikwete kama Rais afanye nini zaidi!.. nani alifaa kushughulikia kesi hizi ambaye nyie mnafikiria Mtandao hawana mkono ndani ya UWT, PCCB na hata Mahakama zetu!.

Mkandara,

Naomba nikupe nukuu ya nilichoandika humu ndani kati ya Mwezi wa 12/07 na 02/08 kukujibu na kuwajibu wengine wote.

I will admit that I have changed my soft approach and become millitant and radical.

Our situation and environment needs radical and drasting changes. Time for soft talk and gentler actions need to stop!

We are asking for our Commander in Chief, The Imperator to be strong and use his Auctoritas to execute his Imperium!

Right now it is not about CCM, CUF or CHADEMA, it is about Taifa! So the question becomes what is the best way to tackle the issues at hand?

I am suggesting that he (Jakaya Kikwete);

  1. Dissolves the parliament, and his cabinet.
  2. Create a transitional government (include wapinzani)which its responsibilities will be to govern and lead and not Politiking. Expediting the fight against poverty, diseases and ignorance.Upholding efficiency and accountability on all levels of government with emphasis on minimizing Government Bureaucracy.
  3. Suspend all political parties activities during transition period. This should include monetary contibution from "wafadhili" and such.
  4. Hold open discussions and referendum for New Katiba.
  5. Revisit the workable creeds on Azimio la Arusha so that he can stimulate production, efficiency and acocuntability for Wananchi.
  6. Create tough election laws and financing.
  7. Clean out deficiencies on Muungano.
  8. Establish strict leadership codes for all ranks from local governments, parliament and central government.
  9. Revamp Justice department and its partners; Police, PCCB, DPP, Mahakama
  10. Halting all investment negotiations, review signed contracts, re-negotiate government earnings from mining and foreign investments.
  11. Hold TRA and BRELA accountable for strict policies that will reduce incorporation of phony companies and Tax evasion. Ensure swift tax and revenue collection.
  12. Revoke all Tax and Duty incentives given to wawekezaji and anybody with exception of NGO that are primarily working on Social Development and can be audited to show results.
  13. Investigate, prosecute and cease property of all those who abused the powers vested in them for personal gain.
I will give him 36 months to do this and after that call in general election for paliamentary seats and presidential.

Only if he is serious to recharge Ari, Kasi na Nguvu Mpya kwa manufaa ya Taifa na si ya Chama au kikundi fulani! then I will support his move to clean the morbid decay of Serikali.

He is a THE President and he has powers. It is only this time I will advocate for him to become absulute and have conditional absolute powers!
 
Mkulu Kishoka,

Heshima mbele bro, kwa kweli kinachoendelea so far ni mapema mno kusema wazi kwamba exactly ni nini hasa, between sheria na siasa, lakini:-
- Again ninaomba ksuema kuwa tuko kwenye the right track, na huu ni wakati wa kumpa rais ushirikiano wetu, na hasa ningetegemea kuwaona upinzani waki -take charge, maana huu ndio hasa wakati wao, pale tunapoambiwa hakuna ushahidi wao ndio wanaopaswa kujitokeza na ushahidi mzito, maana sisi wananchi walipa kodi tunawalipa ruzuku kila mwezi, sasa tunawalipa ruzuku for what kama sio watusaidie wka mambo kama haya?

- Kuendelea kumlaumu rais after all this kwa kweli sioni kama ni productive, kwa sababu rais anatakiwa afanye nini zaidi ya haya aliyokwisha fanya tayari? Amefungua mlango sasa sisi wananchi tu-take a charge na pia tu-take advantage, Mramba na Yona wako rumande sio kwa sababu ya kushindwa dhamana, isipokuwa ni kuthibitisha kwamba wahusika wa ushitaki wako serious, binafsi ninataka kutoa pongezi nzito sana kwa rais na wahusika wote wa hii operation, na ningependa kuwapa moyo kwamba baadhi yetu wananchi tuko nyuma yao na tuko tayari kuwapa msaaada ikibidi, lakini nasema hvi rais amefanya ya kwake, sasa ni zamu yetu wananchi kumalizia na hasa ninategemea Upinzani kutuongoza hapa, maana ndio hasa sababu ya kuwapa ruzuku.

Ahsante Rev!


Mkuu FMES, Mkandara, Sober, Zakumi na Nurujamii,

Msimamo wangu wa kuhoji udhaifu wa kesi hizi na hata mazingira yake bado yako pale pale.

Lakini, kuna upande wa pili ambao nilimjibu Zakumi na naomba nijirudi na kujisahihisha baada ya kulitafakari jambo hili kwa mtazamo mwingine wa kisiasa na si kiutendaji.

Kama Mashitaka ya Uzembe na Matumizi mabaya ya Madaraka yatanasa kama nta ukutani au kwenye vidole, kwa mtaji wa kisiasa niko nyuma ya Kikwete na kumpa shinikizo aendeleze libeneke na kuwaingiza wale wengine wote wawe kina Meghji, Rostam, Chenge, Lowassa, Mzindkaya, Mkono, Karamagi, Msabaha hata kama itafikia kwa Mkapa!
 
Rev. Kishoka,
I am suggesting that he (Jakaya Kikwete);

  1. Dissolves the parliament, and his cabinet.
  2. Create a transitional government (include wapinzani)which its responsibilities will be to govern and lead and not Politiking. Expediting the fight against poverty, diseases and ignorance.Upholding efficiency and accountability on all levels of government with emphasis on minimizing Government Bureaucracy.
  3. Suspend all political parties activities during transition period. This should include monetary contibution from "wafadhili" and such.
  4. Hold open discussions and referendum for New Katiba.
  5. Revisit the workable creeds on Azimio la Arusha so that he can stimulate production, efficiency and acocuntability for Wananchi.
  6. Create tough election laws and financing.
  7. Clean out deficiencies on Muungano.
  8. Establish strict leadership codes for all ranks from local governments, parliament and central government.
  9. Revamp Justice department and its partners; Police, PCCB, DPP, Mahakama
  10. Halting all investment negotiations, review signed contracts, re-negotiate government earnings from mining and foreign investments.
  11. Hold TRA and BRELA accountable for strict policies that will reduce incorporation of phony companies and Tax evasion. Ensure swift tax and revenue collection.
  12. Revoke all Tax and Duty incentives given to wawekezaji and anybody with exception of NGO that are primarily working on Social Development and can be audited to show results.
  13. Investigate, prosecute and cease property of all those who abused the powers vested in them for personal gain.
I will give him 36 months to do this and after that call in general election for paliamentary seats and presidential.

Only if he is serious to recharge Ari, Kasi na Nguvu Mpya kwa manufaa ya Taifa na si ya Chama au kikundi fulani! then I will support his move to clean the morbid decay of Serikali.
Haya yote uliyoyahitaji ndiyo yanayoniweka mimi upande wa Upinzani kwa sababu ni matakwa nje ya chama CCM..Ni marekebisho ambayo hayakubaliani na mfumo wala sera za CCM hivyo Kikwete kuyafanya haya atakuwa anakiuka mwongozo wa chama chake.. Pia kumbuka kuwa huwezi kupigania Urais kama huna chama hivyo Maslahi ya Taifa yanaweza tu kupiganiwa kupitia vyama sio matakwa ya mtu mmoja hata kama ni kwa faida ya nchi nzima.

Kwa mtaji huo basi, nikitazama mapendekezo yako yote yananigusa mimi ktk Upinzani na mabadiliko hayo hayawezi kutokea kama CCM itaendelea kuwa madarakani hata kama Mwandosya, mama Kilango au Mwakyembe mmoja wao akishika kiti cha Ikulu..
Hivyo mkuu tunatazama uwezo wa Kikwete ndani ya Uongozi wa chama kilichoshika hatamu..Kafanya mengi ambayo hayakuwezekana kifikra!..hakuwa rais bila baraka za chama laa sivyo itakuwa anafanya Mapinduzi na sii changes, serikali sio yeye pekee ila wote wanaohusika ndani ya chama chake.
 
Rev. Kishoka,

Haya yote uliyoyahitaji ndiyo yanayoniweka mimi upande wa Upinzani kwa sababu ni matakwa nje ya chama CCM..Ni marekebisho ambayo hayakubaliani na mfumo wala sera za CCM hivyo Kikwete kuyafanya haya atakuwa anakiuka mwongozo wa chama chake.. Pia kumbuka kuwa huwezi kupigania Urais kama huna chama hivyo Maslahi ya Taifa yanaweza tu kupiganiwa kupitia vyama sio matakwa ya mtu mmoja hata kama ni kwa faida ya nchi nzima.

Kwa mtaji huo basi, nikitazama mapendekezo yako yote yananigusa mimi ktk Upinzani na mabadiliko hayo hayawezi kutokea kama CCM itaendelea kuwa madarakani hata kama Mwandosya, mama Kilango au Mwakyembe mmoja wao akishika kiti cha Ikulu..
Hivyo mkuu tunatazama uwezo wa Kikwete ndani ya Uongozi wa chama kilichoshika hatamu..Kafanya mengi ambayo hayakuwezekana kifikra!..hakuwa rais bila baraka za chama laa sivyo itakuwa anafanya Mapinduzi na sii changes, serikali sio yeye pekee ila wote wanaohusika ndani ya chama chake.

Kwa mtaji huu ambao ndio niliuona na kumtaka Kikwete avunje bunge na mfumo wa vyama, ndivyo ninavyoona kuingia kwa ile hoja ya CCM ni adui wa Tanzania na Watanzania na ile ya Mwakijiji ya CCM Kumeguka.

Kila kitu ili Tanzania tuendelee na kuwa na uongozi bora kinaashiria kuondoka au kuondolewa kwa CCM madarakani.
 
Mkuu FMES, Mkandara, Sober, Zakumi na Nurujamii,

Msimamo wangu wa kuhoji udhaifu wa kesi hizi na hata mazingira yake bado yako pale pale.

Lakini, kuna upande wa pili ambao nilimjibu Zakumi na naomba nijirudi na kujisahihisha baada ya kulitafakari jambo hili kwa mtazamo mwingine wa kisiasa na si kiutendaji.

Kama Mashitaka ya Uzembe na Matumizi mabaya ya Madaraka yatanasa kama nta ukutani au kwenye vidole, kwa mtaji wa kisiasa niko nyuma ya Kikwete na kumpa shinikizo aendeleze libeneke na kuwaingiza wale wengine wote wawe kina Meghji, Rostam, Chenge, Lowassa, Mzindkaya, Mkono, Karamagi, Msabaha hata kama itafikia kwa Mkapa!

Rev Kishoka:

wanyonge bado tuko mbali sana kwa sababu vyombo vya sheria vya Tanzania vina uhuru lakini sidhani kuwa majaji wetu wako tayari kuwatendea wanyonge haki bila kupata shinikizo la kisiasa.

Unayo haki kutia wasiwasi je yanayofanyika ni show au nia ya serikali. Kwa upande mwingine serikali inaweza kuwa na nia lakini majaji wako tayari kuendesha kesi na kutoa hukumu kulingana na ushahidi uliokuwepo?

Kuna kesi nzito Tanzania zinapigwa tarehe mpaka watu mnasahau na baadaye watu kushinda.
 
Mkandara,

Yaani hapo umenisaidia sana kujenga hoja mpya au kuongezea nilichomaliza kukisema hapo juu.

Swali ni kwa nini kuna mazoea ya kumlisha Kikwete Uongo? ni wasifu gani alionao binafsi kuwa watu wanadiriki kumlisha uongo kama vile ni kitu cha kawaida bila kuwa na woga?

La pili linakuja ni hili la kusifiwa, je ni kwa nini anapenda kupewa sifa na wasaidizi wake (mawaziri, makatibu,wabunge, wasemaji, wananchi) wanaendelea kumsifia hata pale inapoonekana si pa kutoa sifa? Sifa hizi ni kwa mantiki gani na manufaa gani?

Nilichoandika kwenye hii mada ni kuonyesha mapungufu ya Serikali yake ambayo yanajengeka uimara kutokana na udhaifu wake yeye kama kiongozi mkuu.

Watanzania tumechoshwa na uongozi dhaifu na wenye kuendelea kuwa na mapungufu kila siku. Ni lini ataziba viraka au kuamka na taswira mpya ambayo haitatupa picha au hisia kuwa ni mazingaombwe, mzaha, dhaifu au woga ili tupate faraja, tumaini na nguvu mpya?

Rev Kishoka:


Nikiwa shule nakumbuka tulilimishwa heka 10 za shamba la kahawa na kulipanda miche ya kahawa katika kipindi cha wiki moja. Wataalamu wa kilimo wanasema shamba la kahawa linaandaliwa kwa muda wa miaka mitatu kabla ya kupanda miche.

Sababu ya shule yetu kutumia wiki moja ilikuwa nia ya mwalimu mkuu kutumia shamba kama show case kwa ugeni wa ngazi za juu ukiongizwa na rais uliokuwa utembelea maeneo ya shuleni kwetu.

Baada ya ugeni kuondoka shamba lilisahuliwa na nguvu za wanafunzi zilipotea.

Hivyo, exaggeration na tabia ya uwongo ni sehemu kubwa iliyotawala viongozi wa Tanzania kwa maslahi ya kupanda vyeo.

Mfano mwingine ni Kamanda wa Polisi, Zombe. Huyu jamaa aliua watu innocent na kuwasingia kuwa ni majambazi hili kujipa sifa kuwa amepambana na majambazi.

Na kuhusu suala la kusifiwa. Mtu yoyote ambaye anamdanganya kiongozi na kumpa taarifa za uongo ndie anayekuwa wa kwanza kutoa sifa kubwakubwa.
 
Zakumi,
Tena kweli umenikumbusha kitu kimoja. Hawa majaji wa Kisutu walilalamika kuhusu usafiri na kusema kwamba tayari wamekwisha pokea message za kutishiwa maisha yao..Je, kumetokea lolote kuwapa usafiri na kinga hawa majaji?..
Pili, Kuna mtu yeyote anafahamu kama DPP hakukutana na vitisho kama hivi!...
Nimefikiria hili baada ya kusoma waraka wa Mchungaji kuhusiana na Usalama nchini.
 
Mkandara na zakumi mmezungumzia jambo muhimu.

Huyu Hezron Mwankenja kafanya kitu adimu sana! personally nampa eko! unajua kuna maamuzi ya mahakimu ambayo wanaweza wakaamua na bado wengi wakaridhika,

Mathalani, kusikia Yona na Mramba wamekamatwa kwa watanzania wengi ilikuwa sikukuu,

Mwankenja angewapa dhamana yenye mashart nafuu hakuna ambaye angelalamika, nijuavyo wengi wamefurahi tu kkukamatwa kwao

ILIPOKUJA MOVE NYINGINE YA HAWA JAMAA KWENDA KEKO, HAPO...... HALI ILIKUWA ZAIDI YA FURAHA.

HUYU HAKIMU ANAWEZA AKAUAWA ,WANAWEZA WASIWE MRAMBA AU YONA WATAKAOHUSIKA, BALI WENGINE AMBAO WANATARAJIA KUINGIA KWENYE HII 'SOMBA SOMBA'

KUMBUKA HAKIMU AKIUAWA STORY NZIMA ITABADILIKA TENA..........
 
Kuendelea kumlaumu rais after all this kwa kweli sioni kama ni productive, kwa sababu rais anatakiwa afanye nini zaidi ya haya aliyokwisha fanya tayari? Amefungua mlango sasa sisi wananchi tu-take a charge na pia tu-take advantage, Mramba na Yona wako rumande sio kwa sababu ya kushindwa dhamana, isipokuwa ni kuthibitisha kwamba wahusika wa ushitaki wako serious, binafsi ninataka kutoa pongezi nzito sana kwa rais na wahusika wote wa hii operation, na ningependa kuwapa moyo kwamba baadhi yetu wananchi tuko nyuma yao na tuko tayari kuwapa msaaada ikibidi, lakini nasema hvi rais amefanya ya kwake, sasa ni zamu yetu wananchi kumalizia na hasa ninategemea Upinzani kutuongoza hapa, maana ndio hasa sababu ya kuwapa ruzuku.

Ahsante Rev!
Kweli Kaka hapa Raisi anahitaji pongezi kutoka kwetu na wananchi wakionyesha kwamba wako nyuma yake ndio ataendelea na moyo wake wa kuhakikisha na wengine wanafuatia. Big Up JK, tunaomba uendelee na kazi uliyoianza.
 
Rev Kishoka:


Nikiwa shule nakumbuka tulilimishwa heka 10 za shamba la kahawa na kulipanda miche ya kahawa katika kipindi cha wiki moja. Wataalamu wa kilimo wanasema shamba la kahawa linaandaliwa kwa muda wa miaka mitatu kabla ya kupanda miche.

Sababu ya shule yetu kutumia wiki moja ilikuwa nia ya mwalimu mkuu kutumia shamba kama show case kwa ugeni wa ngazi za juu ukiongizwa na rais uliokuwa utembelea maeneo ya shuleni kwetu.

Baada ya ugeni kuondoka shamba lilisahuliwa na nguvu za wanafunzi zilipotea.

Hivyo, exaggeration na tabia ya uwongo ni sehemu kubwa iliyotawala viongozi wa Tanzania kwa maslahi ya kupanda vyeo.

Mfano mwingine ni Kamanda wa Polisi, Zombe. Huyu jamaa aliua watu innocent na kuwasingia kuwa ni majambazi hili kujipa sifa kuwa amepambana na majambazi.

Na kuhusu suala la kusifiwa. Mtu yoyote ambaye anamdanganya kiongozi na kumpa taarifa za uongo ndie anayekuwa wa kwanza kutoa sifa kubwakubwa.

Umenikumbusha safari ya Kikwete kwenda kufungua daraja la kwenda Msumbiji na kukuta daraja halijafikia hata nusu ya ujenzi kukamilika.

Sasa kama kuna watu wanadiriki kumlaghai Rais kwa kiwango hiki ambacho ni kumkosea heshima na utii, inabidi tujiulize je Rais wetu ana matatizo gani?

Why is our President credibility questionable and his authority mocked by his subbordinates? How can these people dare him and disrespect him with such magnitude?
 
Rev,
Umenikumbusha safari ya Kikwete kwenda kufungua daraja la kwenda Msumbiji na kukuta daraja halijafikia hata nusu ya ujenzi kukamilika
Hii kweli mkuu ama umeamua sasa kukipaka! nashindwa hata kuiweka akilini kumpeleka rais kufungua daraja ambalo halipo...Nimeona Picha nguzo tu zimesimama tena tayari zimeanza kuchoka...
 
Maarifa yamekaziwa kwa kiasi cha kuridhisha ktk wachangiaji wa habari hii ,wako wanaotupa matumaini kuwa yanayotendeka ni amini na kweli na tuko ambao tunatilia shaka.
Mimi nikiwa upande wa wanaotilia shaka nina sababu ya kuwa na hisia hizo kutokana na jinsi mambo yalivyokuwa yakiendeshwa kwa kipindi cha nyuma na kama wangine wanavyounganisha na shinikizo toka kwa nchi wahisani na maandalizi ya uchaguzi pia.Sasa basi hisia hizi zitabadilishwa na nini,Hakika yake hakuna mpaka mwisho wake ndio tutasima ni hakika hii ilikuwa si drama .
Ila kitu kimoja JK ambacho anatakiwa kufanya ni kuwa amepata chance nzuri sana ya kuwageuka ufisadi hata kama alinufaika nao kipindi fulana,hii sababu ya shindikizo la wahisani.By the way hii has nothing to loss,he is presidaaaa kwa hiyo .Kwa hiyo iwe sababu za uchaguzi,shinikizo ama ni nia dhabiti toka moyoni mwake sisi tutafurahi hili likitendeka kufata sheria bila kuyumbishwa.

Mimi naomba msaada wa kisheria jamani kwa swali hili.
Je kumfungulia mtu ama kiongozi mashtaka kunahitajika ruhusu toka kwa rais,kwa nini ktk hili rais tunampongeza.?
Vinginevyo inaonyesha viongozi ndio wamekuwa vikwazo ktk haya
 
Rev,

Hii kweli mkuu ama umeamua sasa kukipaka! nashindwa hata kuiweka akilini kumpeleka rais kufungua daraja ambalo halipo...Nimeona Picha nguzo tu zimesimama tena tayari zimeanza kuchoka...

Mkandara,

Ama alikuwa anakwenda fungua au kukagua kukamilika kwa ujenzi akakuta halijakamilika. Akawa avuke daraja kwenda Msumbiji kwenye sherehe ya Frelimo kwa mtumbwi, ndipo alipotoa ile kauli kuwa yeye ni Mkwere, hajui kuogelea. Badala yake Membe na Msekwa wakapandishwa mtumbwi.

This was barely 4 months ago!
 
Umenikumbusha safari ya Kikwete kwenda kufungua daraja la kwenda Msumbiji na kukuta daraja halijafikia hata nusu ya ujenzi kukamilika.

Sasa kama kuna watu wanadiriki kumlaghai Rais kwa kiwango hiki ambacho ni kumkosea heshima na utii, inabidi tujiulize je Rais wetu ana matatizo gani?

Why is our President credibility questionable and his authority mocked by his subbordinates? How can these people dare him and disrespect him with such magnitude?

Samahani kama nitawaudhi watu. Utamaduni huo ni wa nchi nzima. Wengine tumelizwa na members wa familia zetu kwenye miradi mbuzi huko nyumbani. Ukipiga simu unaambiwa vitu vinaendelea na ukirudi unakuta kibiriti tu kimesimama na sio nyumba.

Kuna mfano mmoja nilitoa kuwa inasemekana kuwa watu wa Ulaya wanapenda sana process (how you do things). Kwa upande mwingine waMarekani wanapenda results (How you accomplish things).

Attitudes hizi kwetu hatuna. Tunapenda tu kuzungumza big things and big Ideas.

Kuna uwezekano mkubwa JK aliwachagua baadhi ya washirika wake kwa sababu ya mazungumzo ya Big Ideas walipokuwa bar au shuleni. Kuzungumza mambo mazuri ni kitu kimoja na utendaji ni kitu kingine kabisa. Na hata leo, tukihamua tuanzishe virtual country (second life country) hapa JF, Rev unaweza kuchaguliwa kuwa rais kutokana mitazamo yako. Lakini hiyo mitazamo haina maana yoyote katika utendaji au kupata matokeo.

Mashirika ya binafsi wanatumia KPI kupima mafanikio. Na kutokana na longolongo zetu na mazoea yetu, baadhi ya nchi wahisani wanatumia KPI katika kupima ahadi ya matumizi ya misaada wanayotupa. Hivyo ukiona waDenmark wanalalamika kuhusu misaada, ujue tumechemsha katika indicators fulani.

Hili kufanya viongozi wawe wakweli labda wizara ziongozwe kama business enterprises na KPI itumike.

Na mazoea yetu yalivyo issues za sasa zinaweza kupotea kwenye radar kwa sababu watu wamesha-vent hasira zao.
 
Mutu,
Mimi naomba msaada wa kisheria jamani kwa swali hili.
Je kumfungulia mtu ama kiongozi mashtaka kunahitajika ruhusu toka kwa rais,kwa nini ktk hili rais tunampongeza.?
Vinginevyo inaonyesha viongozi ndio wamekuwa vikwazo ktk haya
Swali zuri sana mkuu wangu na ndio maana sote tunamlaumu ama kumpongeza Kikwete badala ya kutazama sheria butu za nchi yetu...Kama nilivyokwisha sema hawa jamaa walisha jijengea mahekalu ya Ufisadi na kusafishwa na Azimio la chama tawala hivyo mageuzi yoyote ya sheria ni kukiuka malengo yaliyokwisha pangwa...
 
Back
Top Bottom