Papa Francis amtimua Askofu anayempinga kuhusu kuruhusu ndoa za jinsia moja, kutoa mimba na waliobadili jinsia

▪︎ Hatuabudu sanamu
Ila? Sanamu zilizojaa makanisani, mnayoibusu na kuisujudia??? Wake up, don't be a religious fool.

Mungu anabudiwa katika Roho na Kweli. Yohana 4:24.

▪︎ Hatuabudu wafu
Siku ya kuwaombea wafu inahusikaje na wokovu?

▪︎ Hatumwabudu Mama Bikra Maria mama wa Mungu
^Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu.^

Sala ya Ukatoliki inaenda namna hiyo. Hiyo ni ibada ya wafu.

👉Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo. ~ Matendo 4:12

▪︎ Hatuungami kwa Padre, tunaungama kwa Mungu kupitia kwa Padre kama alivyotuagiza

👉Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. ~1 Yohana 1:9

Hakuna padre aliyetajwa hapo wa kuungamiwa dhambi zetu wala kutumika kama kiunganishi kati ya mdhambi na Mungu.

Kwa sababu Kristu ndiye Kuhani Mkuu kwetu, nasi Wakristu woote kwa pamoja ni ^ukuhani wa kifalme^

👉Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake Yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu. 1Pet. 2:9

Shida yenu mkikariri vimistari viwili vitatu kutoka kwenye Biblia
Inasikitisha na ni aibu pia kwamba Ukatoliki unafundisha kinyume na hilo Neno.

👉Lakini Yeye [Kristu] alisema, Afadhali, heri walisikiao neno la Mungu na kulishika. Luka 11:28
 
Samahi kiongozi, unaweza nisaidia andiko linalotaka tupitie kwa kiongozi wa kiimani ili kuungama dhambi zetu?.

Ninatanguliza shukrani.
Hakuna andiko kama hilo, Mwanzo hadi Ufunuo.

Wewe binafsi ukimwomba Mungu kwa imani, kwa unyenyekevu, ukatubu dhambi zako zote, kwa neema ya Yesu Kristo anakusamehe na kukupa nguvu ya Roho Mtakatifu.

👉Mkiomba neno lolote kwa jina Langu, nitafanya. Yohana 14:14.

Mathayo 18:18
Hilo andiko halihusiani na mwanadamu kuomba msamaha kwa Mungu kupitia kuhani.
Majibu yake tu huonesha ni tapeli wa imani ya Ukristu. Hawana majibu, ndiyo maana wanafoka kama Mafarisayo na Masadukayo.

👉Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu. ~1Petro 3:15

Andika Biblia yako uweke maana zinazokufurahisha.
Hawa hawaujui Ukristu, hawaijui Biblia na wala hawamtambui Yesu, na wala hayumo mioyoni mwao wala karibu nao.

Wanachojua wao ni kulitumia jina la Kristu ili kujinufaisha na kujitajirisha kidunia.

👉Na siku hiyo wanawake saba watamshika mtu mume mmoja wakisema, Tutakula chakula chetu, na kuvaa nguo zetu wenyewe, lakini tuitwe tu kwa jina lako; utuondolee aibu yetu. ~Isaya 4:1
 
  • Thanks
Reactions: K11
Kwa kifupi Katoriki siyo Kanisa la Mungu! Asikudanganye mtu kabisa.
Katoriki ni dhehebu la Mpinga Kristo! Ndiyo dhehebu lililoongoza mauaji ya Watakatifu Wakristo kuliko unavyofikiri.
Papa siyo Mtumishi wa Mungu bali ni Kiongozi wa dini ya Kikatoriki duniani.
kwani mkatoliki anahubiri injili ya nani?
 
Ila? Sanamu zilizojaa makanisani, mnayoibusu na kuisujudia??? Wake up, don't be a religious fool.

Mungu anabudiwa katika Roho na Kweli. Yohana 4:24
Hatuabudu sanamu, hatujawahi kuabudu sanamu na kamwe hatutakuja kuabudu sanamu.

Tunamuabudu Mungu. Tunamuabudu asiyeonekana kupitia vielelezo vinavyoonekana kama wana wa Israel walivyofanya kupitia nyoka wa shaba (Rejea Hesabu 21:8).

Siku ya kuwaombea wafu inahusikaje na wokovu?
Kuombea wafu ni sawa na kuabudu wafu? Kwamba ombi ni sawa na ibada? Umesoma mpaka hatua ipi ya elimu mkuu?

^Bikra Maria, Mama wa Mungu tukumbuke sasa na saa ya hukumu.^

Sala ya Ukatoliki inaenda namna hiyo. Hiyo ni ibada ya wafu.

👉Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo. ~ Matendo 4:12
Kwa taarifa yako tu; hatuna sala ya hivyo. Fanya utafiti kabla ya kuja kutuhumu. JF is becoming a home of stupids.

👉Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. ~1 Yohana 1:9

Hakuna padre aliyetajwa hapo wa kuungamiwa dhambi zetu wala kutumika kama kiunganishi kati ya mdhambi na Mungu.

Kwa sababu Kristu ndiye Kuhani Mkuu kwetu, nasi Wakristu woote kwa pamoja ni ^ukuhani wa kifalme^

👉Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake Yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu. 1Pet. 2:9
Mathayo 18:18

Inasikitisha na ni aibu pia kwamba Ukatoliki unafundisha kinyume na hilo Neno.

👉Lakini Yeye [Kristu] alisema, Afadhali, heri walisikiao neno la Mungu na kulishika. Luka 11:28
Nina uhakika haujui chochote kuhusu Ukatoliki.


NB: Ukatoliki mnaouhangaikia na mnaoufahamu ni tofauti na Ukatoliki wetu... Kanisa pekee lililoanzishwa na Kristu.
 
Hakuna andiko kama hilo, Mwanzo hadi Ufunuo.

Wewe binafsi ukimwomba Mungu kwa imani, kwa unyenyekevu, ukatubu dhambi zako zote, kwa neema ya Yesu Kristo anakusamehe na kukupa nguvu ya Roho Mtakatifu.

👉Mkiomba neno lolote kwa jina Langu, nitafanya. Yohana 14:14.



Majibu yake tu huonesha ni tapeli wa imani ya Ukristu. Hawana majibu, ndiyo maana wanafoka kama Mafarisayo na Masadukayo.

👉Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu. ~1Petro 3:15


Hawa hawaujui Ukristu, hawaijui Biblia na wala hawamtambui Yesu, na wala hayumo mioyoni mwao wala karibu nao.

Wanachojua wao ni kulitumia jina la Kristu ili kujinufaisha na kujitajirisha kidunia.

👉Na siku hiyo wanawake saba watamshika mtu mume mmoja wakisema, Tutakula chakula chetu, na kuvaa nguo zetu wenyewe, lakini tuitwe tu kwa jina lako; utuondolee aibu yetu. ~Isaya 4:1
Haujui chochote kuhusu Ukatoliki.
 
Maoni ya Papa Francis Dhidi ya Muelekeo Mpya wa Kanisa kwenye masuala ya Kijamii.

Kwamba Kuna Baadhi ya Viongozi Wana mgado wa Kifikra hivyo Kanisa haliwezi kuendelea kuwa nyuma kifikra Kwa kile alichoita Haina manufaa Kwa Kanisa.

Hali hii imepelekea kuanza kutoa sakramenti Kwa watu wa Jinsia Moja,Kuruhusu utoaji Mimba na watu Waliobadili Jinsia.

Waumini wa RC mnasemaje?

View: https://twitter.com/bbcswahili/status/1723590466598309996?t=FG7rQLomW2Is3DgSfrBz3Q&s=19

Bora kuhamia RC maana huko hakuna dhambi.
 
Waumini wa kikatoliki wa afrika achaneni na ukatoliki anzisheni makanisa yenu yenye maadili. Mtaaibika na kufedheheshwa na kiongozi wenu huyo mkuu mwenye mamlaka makubwa kanisani. Mtaburuzwa sana na kuonekana nanyi ni wahuni tu na hamna Mungu
shida maokoto...........mapadre wengi wanalishwa na hao wazungu
 
Maoni ya Papa Francis Dhidi ya Muelekeo Mpya wa Kanisa kwenye masuala ya Kijamii.

Kwamba Kuna Baadhi ya Viongozi Wana mgado wa Kifikra hivyo Kanisa haliwezi kuendelea kuwa nyuma kifikra Kwa kile alichoita Haina manufaa Kwa Kanisa.

Hali hii imepelekea kuanza kutoa sakramenti Kwa watu wa Jinsia Moja,Kuruhusu utoaji Mimba na watu Waliobadili Jinsia.

Waumini wa RC mnasemaje?

View: https://twitter.com/bbcswahili/status/1723590466598309996?t=FG7rQLomW2Is3DgSfrBz3Q&s=19

Baadhi ya waumini nao wana mawazo mgando, hawabadiliki.
 
Ikumbukwe huyu Papa wa Vatican anaeongoza Kanisa la RC almaaufu Kanisa Takatifu la Mitume kama wanavyojiita wao ameamua kuwaburuza wenzake wafuate msimamo wake.

Baadhi ya mambo ambayo anataka Kanisa lake lifuate ni

-Kuwatambua Mashoga bila kukemea akisema wenye dhambi ndio wanatakiwa kwenda kanisani

-Kubariki Ndoa za mashoga

-Kufuhusu utoaji Mimba

-Kutambua watu Waliobadili Jinsia kinyume na maumbile Yao ya Asili

-Kuwa na msimamo legelege na kuficha taarifa za watawa wanaokumbwa na kashfa za kulawiti Watoto wadogo.

-Kufuhusu Baadhi ya Maaskofu wa RC huko Amerika ya Kusini kuoa kinyume na msimamo wa Kanisa lao Hilo la Mitume.

Haya wenye Kanisa lenu johnthebaptist mnaitwa huku 😁😁

==========≈=

Papa Francis amemfuta kazi askofu Joseph Strickland, ambaye ni mkosoaji mkubwa aliyeibua maswali juu ya uongozi wa Papa katika Kanisa Katoliki.

Kwa mujibu wa taarifa ya Vatican, askofu huyo ameondolewa madarakani kufuatia uchunguzi katika Jimbo Katoliki la Tyler, huko Texas, Marekani alilokuwa akiliongoza .

Askofu Strickland ni mmoja kati ya sauti kinara katika tawi la uongozi wa Kanisa Katoliki nchini Marekani ambalo linapinga vikali mabadiliko yanayopigiwa chapuo na Papa.

Kuondolewa kwake kunakuja baada ya Papa kuzungumzia juu ya hali “ya kuwa nyuma” kifikra ya baadhi ya viongozi wa Kikatoliki nchini Marekani.

Askofu Strickland mara kadhaa ameshambulia hatua za Papa kutaka kubadili msimamo wa Ukatoliki katika masuala kadhaa ya kijamii ikiwemo kutoa mimba, haki za waliobadili jinsia na ndoa za jinsi moja.

Mwezi Julai mwaka huu, alionya kuwa mafunzo mengi ya Ukatoliki ambayo ni ya “ukweli wa msingi” yalikuwa yanapingwa, ikiwemo kile alichokiita majaribio ya “kudunisha” ndoa “kama ilivyoundwa na Mungu” baina ya mwanamume na mwanamke tu.

Askofu huyo pia amekosoa majaribio hayo aliyoyaita ya “kuvunja miiko” na kusema wanaoyapigia chapuo “wanapinga utambulisho wao wa kibailojia waliopewa na Mungu”.

Katika barua yake ya mwezi Julai, askofu Strickland amedai kuwa majaribio “kubadilisha visivyobadilika” yatasababisha mfarakano mkubwa ndani ya Kanisa. Na wale wanaotaka mabadiliko, ameonya kuwa “ndio hasa wanaofarakanisha [Kanisa]".

Askofu Strickland alikuwa chini ya uchunguzi wa Vatican na hapo awali alitupilia mbali uwezekano wa kujiuzulu, na katika barua ya wazi mwezi Septemba alimtaka Papa amfute kazi.

"Siwezi kujiuzulu kama Askofu wa Tyler kwa sababu kufanya hivyo itakuwa ninawatelekeza wana kondoo,” alisema.

Kwa mujibu wa Vatican, uamuzi wa kumfukuza umefikiwa baada ya “ziara ya kitume katika Jimbo la Tyler iliyoagizwa na Papa mwezi Juni".

Vyombo vya habari vya Kikatoliki vinaeleza kuwa uchunguzi huo pia uliangazia masuala ya kifedha katika jimbo hilo.

Askofu Strickland, 65, aliteuliwa kuwa askofu mwaka 2012, wakati wa Papa Benedikto XVI.

Vatican imesema kuwa Jimbo la Tyler kwa sasa litaongozwa kwa mpito na Askofu Joe Vasquez wa Jimbo la Austin.

Hatua hii inafuatia hatua mahususi zinazochukuliwa na Papa ili kulifanya Kanisa Katoliki kuendana na wakati kwenye utawala wake.

Siku ya Alhamisi, Vatican ilitangaza kuwa watu waliobadili jinsia wanaweza kubatizwa katika Kanisa Katoliki ilimradi kwa kwa kufanya hivyo hakutazua kashfa ama “mchafuko”.

Mwezi Oktoba Papa alisema kuwa Kanisa linaweza kukubali kubariki wanandoa wa jinsi moja, huku akiwaeleza makardinali kuwa "hatuwezi kuwa majaji ambao tunachofanya ni kukana, kukataa na kutenga tu".

Akizungunza katika mkutano wa Siku ya Vijana Duniani jijini Lisbon Papa alisema kuwa mgando wa fikra wa baadhi ya watu “hauna manufaa”.

"Kwa kufanya hivyo unapoteza utamaduni halisi na utategemea itikadi ili kuungwa mkono. Kwa maana nyingine, itikadi inachukua nafasi ya imani,” aliongeza kusema.

Mabadiliko ya tabianchi pia imekuwa ni moja ya ajenda kuu ya utawala wa Papa Francis - ambapo mwaka 2015 alitoa chapisho muhimu kuhusu mazingira ambalo lilionya kuwa dunia ilikuwa inaelekea hatua mbaya zaidi kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Papa pia amewashutumu vikali wale wote wanaokanusha mabadiliko ya tabianchi na anatazamiwa kuwa katika mkutano wa mazingira wa Umoja wa Mataifa wa COP28 baadae mwezi huu huko Dubai.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Papa kuhudhuria toka mikutano hiyo ianzishwe mwaka 1995.

Chanzo: BBC
Huyu Papa ni FreeMason Mkubwa duniani anakubali madhambi ambayo Mungu ameyakataza katika vitabu vyake vitakatifu? Huyu Papa ni mpinga amri za Mungu amelaanika kweli.
 
Hatuabudu sanamu, hatujawahi kuabudu sanamu na kamwe hatutakuja kuabudu sanamu.
Kukana tu kwa maneno hakusaidii kuondoa ukweli ulio wazi kwamba Ukatoliki unasujudia na kuabudu sanamu ambazo Biblia imepiga marufuku mara nyingi sana, na kwa maneno makali kadiri iwezekanavyo.

👉 [3] Usiwe na miungu mingine ila Mimi.

👉 [4] Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

👉 [5] Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa Mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, ~ Kutoka 20

👉Isaya 44:9-20

Tunamuabudu Mungu. Tunamuabudu asiyeonekana kupitia vielelezo vinavyoonekana kama wana wa Israel walivyofanya kupitia nyoka wa shaba (Rejea Hesabu 21:8).
Kama ilivyoelezwa katika Kutoka 20 (hapo juu) Maandiko yamekataza kabisa KUJIFANYIA SANAMU ZA KUCHONGA, KUZISUJUDIA na KUZITUMIKIA.

Ukatoliki utambue kwamba umejifanyia sanamu hizo za kuchonga, na hiyo, kwa mujibu wa Biblia, ni ibada ya sanamu.

Kitendo chao cha kuzisujudia, kuzibusu, kuzikumbatia katika utashi wa kiroho, hiyo ni ibada ya sanamu.

Kitendo chao cha kuzihudumia, kuzipa heshima na umuhimu na umaana wowote wa kiroho, huko ni kuzitumikia. Biblia inataja suala hilo kuwa ni ibada ya sanamu.

Kumhusu nyoka wa shaba, Biblia imefafanua kikamilifu kwenye Injili ya Yohana: 3:

👉[14] Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;

[15] ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika Yeye.

Biblia haijasema sanamu ziinuliwe, bali Mwana wa Adamu (Yesu Kristu), ndiye apewe nafasi ya kuinuliwa na kutukuzwa mioyoni na maishani mwetu.
Kuombea wafu ni sawa na kuabudu wafu? Kwamba ombi ni sawa na ibada?
Ukatoliki unamwomba ^Bikra^ Maria. Hilo liko wazi kwenye ibada zao.

Hiyo siyo tu kwamba ni ibada ya wafu, lakini pia ni ibada ya sanamu.

Ukatoliki unaabudu mizimu, kwa sababu Mariamu, mamaye Yesu alikufa, akazikwa na hakuna kumbukumbu yoyote ya Biblia kwamba alifufuka na kupaa mbinguni.

Ukatoliki unaabudu miungu kwa sababu hata kama Mariamu angelikuwa hai mbinguni, bado hana sifa za kuombwa dua na kuabudiwa kama wafanyavyo Wakatoliki.

👉Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo. ~Matendo 4:12

Kama hakuna wokovu kwa mwingine awaye yote mbali na Kristu, kwa mujibu wa Biblia, sasa mahangaiko ni ya nini kwa Wakatoliki juu ya Mariamu, tena mtu ambaye ni mfu???

Maana yake, Ukatoliki umemgeuza Mariamu kuwa mungu wao, kwamba hajafa na kwamba anao uwezo wa kuwasaidia na kuwaokoa. Vinginevyo wasingethubutu kabisa kumwomba! Ibada ya sanamu!!!
Kwa taarifa yako tu; hatuna sala ya hivyo. Fanya utafiti kabla ya kuja kutuhumu.
Sala ya ^Bikra^ Maria ni uthibitisho mkubwa mojawapo kwamba Ukatoliki unaabudu mizimu na ibada ya sanamu. Hii ni kinyume kabisa na Maandiko Matakatifu ambayo ndiyo msingi mkuu wa Ukristu.

Mathayo 18:18
Ni wapi ambapo padre ametajwa katika andiko hili la Mathayo 18?

Katika agano jipya, baada ya kifo cha Yesu Msalabani, waumini wote wanahesabika kama makuhani wa Mungu.

👉Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu. ~1 Petro 2:9

Mfumo wa Agano la Kale wa ukuhani ambapo wana wa Israeli walipaswa kwenda kwa kuhani kwenye hema takatifu, maskani au hekaluni, wakiwa na dhabihu zao, ulikuwa kielelezo cha kumwakilisha Masihi Kristu ajaye.

Mfumo huo ulikoma baada ya kifo cha Yesu, ndiyo maana wakati Kristu akikata roho, pazia la hekalu lilipasuka vipande (Mathayo 27:50, 51), ikiashiria kwamb huduma hiyo sasa haina maana, kwa vile imetimia na kutimilika katika Kristu.

Mambo hayo yalikuwa ^kivuli cha mambo yajayo^ -- yaani yalilenga kwa Kristu Yesu (Kolosai 2:17).
Nina uhakika haujui chochote kuhusu Ukatoliki.
???🤔🤔🤔

NB: Ukatoliki mnaouhangaikia na mnaoufahamu ni tofauti na Ukatoliki wetu.
Ukatoliki tunaoupinga kwa nguvu zote ni ule ambao:
👉unafundisha kwamba papa ndiye mwenye mamlaka juu ya Ukristu duniani -- yaani ndiye kaimu wa Mungu.

👉unadai Mtume Petro ndiye papa wa kwanza na kwamba mapapa wote wamerithi na wanarithi mamlaka yao kutoka kwake.

👉unadai kwamba mapokeo ya kanisa na mafundisho ya maaskofu wao na miongozo ya mabaraza iko sambamba na Biblia kimamlaka.

👉unafundisha kwamba ubatizo siyo lazima kuzamisha majini, hata kunyunyiza ni sawa.

👉unadai kwamba katika huduma takatifu ya Meza ya Bwana, vielelezo vya mkate na divai hugeuka kuwa mwili na damu halisi ya Kristu.

👉unafundisha kwamba Maria, mlolongo wa watakatifu, hata waliokwishakufa tayari, wanachangia katika wokovu wetu, kwa kuombwa dua.

👉unafundisha fundisho potofu la toharani ama pagatoria, kwamba ni mahali pa mateso ya utakaso kwa muda kwa ajili ya waumini ambao si waovu sana kiasi cha kwenda jehanum na wala si wema vya kutosha kuingia mbinguni.

👉unafundisha kwamba una mamlaka ya kubadilisha na kubatilisha Maandiko Matakatifu kama upendavyo wenyewe.

👉unafundisha kwamba wokovu haupatikani kwa neema bali kwa matendo; kwamba kipimo cha wokovu ni kwamba tu matendo ya wema yazidi yale maovu; kwamba kadiri muumini anavyojitesa, anavyotoa pesa, juhudi na mali kumtumikia Mungu na kanisa, kadiri anavyofanya huduma na ibada, nk ndivyo anavyo anahesabiwa haki machoni pa Mungu. Ndiyo maana Ukatoliki na Uislamu ni mapacha na mapapa wawili wanaofanana.

👉unafundisha kuchonga, kusujudia, na kutumikia sanamu kwa kisingizio kwamba unatumia kama vielelezo tu vya ibada.

👉Kama mambo haya na mengine mengi yanayofanana nayo ni tofauti na Ukatoliki wenu, basi una haki ya kukaa pembeni, maana wewe hauhusiki hapo.

Kanisa pekee lililoanzishwa na Kristu.
👉Kamwe Ukatoliki hauwezi kuwa Kanisa la Mungu kwa sababu Kristu kwao hatoshelezi kwa wokovu, lazima asaidiwe na akina Maria na watakatifu wengine.

👉Kamwe Ukatoliki hauwezi kuwa Kanisa la Mungu kwa sababu unapingana waziwazi na Maandiko Matakatifu.

👉Kamwe Ukatoliki hauwezi kuwa Kanisa la Mungu kwa sababu umepoka mamlaka ya Kristu, na papa kujiweka kama mungu duniani.

👉Kamwe Ukatoliki hauwezi kuwa Kanisa la Mungu kwa sababu historia ya matendo yake, mauaji ya Wakritu uliyoyafanya, ukatili wake katika nyakati zote vinapingana kabisa na Ukristu.

👉Ni sahihi 100% kusema kwamba Ukatoliki ni wakala wa Shetani duniani, ambaye hujificha kwenye vazi la Ukristu na utu wema.

👉Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. ~ Mathayo 7:15

👉Wito wa Mungu kwa waumini na Wakristu wote, hata wale waliomo kwenye jumuia ya imani potofu ya Ukatoliki:👇

Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake. Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake. ~Ufunuo wa Yohana 18:4, 5
 
Ikumbukwe huyu Papa wa Vatican anaeongoza Kanisa la RC almaaufu Kanisa Takatifu la Mitume kama wanavyojiita wao ameamua kuwaburuza wenzake wafuate msimamo wake.

Baadhi ya mambo ambayo anataka Kanisa lake lifuate ni

-Kuwatambua Mashoga bila kukemea akisema wenye dhambi ndio wanatakiwa kwenda kanisani

-Kubariki Ndoa za mashoga

-Kufuhusu utoaji Mimba

-Kutambua watu Waliobadili Jinsia kinyume na maumbile Yao ya Asili

-Kuwa na msimamo legelege na kuficha taarifa za watawa wanaokumbwa na kashfa za kulawiti Watoto wadogo.

-Kufuhusu Baadhi ya Maaskofu wa RC huko Amerika ya Kusini kuoa kinyume na msimamo wa Kanisa lao Hilo la Mitume.

Haya wenye Kanisa lenu johnthebaptist mnaitwa huku 😁😁

==========≈=

Papa Francis amemfuta kazi askofu Joseph Strickland, ambaye ni mkosoaji mkubwa aliyeibua maswali juu ya uongozi wa Papa katika Kanisa Katoliki.

Kwa mujibu wa taarifa ya Vatican, askofu huyo ameondolewa madarakani kufuatia uchunguzi katika Jimbo Katoliki la Tyler, huko Texas, Marekani alilokuwa akiliongoza .

Askofu Strickland ni mmoja kati ya sauti kinara katika tawi la uongozi wa Kanisa Katoliki nchini Marekani ambalo linapinga vikali mabadiliko yanayopigiwa chapuo na Papa.

Kuondolewa kwake kunakuja baada ya Papa kuzungumzia juu ya hali “ya kuwa nyuma” kifikra ya baadhi ya viongozi wa Kikatoliki nchini Marekani.

Askofu Strickland mara kadhaa ameshambulia hatua za Papa kutaka kubadili msimamo wa Ukatoliki katika masuala kadhaa ya kijamii ikiwemo kutoa mimba, haki za waliobadili jinsia na ndoa za jinsi moja.

Mwezi Julai mwaka huu, alionya kuwa mafunzo mengi ya Ukatoliki ambayo ni ya “ukweli wa msingi” yalikuwa yanapingwa, ikiwemo kile alichokiita majaribio ya “kudunisha” ndoa “kama ilivyoundwa na Mungu” baina ya mwanamume na mwanamke tu.

Askofu huyo pia amekosoa majaribio hayo aliyoyaita ya “kuvunja miiko” na kusema wanaoyapigia chapuo “wanapinga utambulisho wao wa kibailojia waliopewa na Mungu”.

Katika barua yake ya mwezi Julai, askofu Strickland amedai kuwa majaribio “kubadilisha visivyobadilika” yatasababisha mfarakano mkubwa ndani ya Kanisa. Na wale wanaotaka mabadiliko, ameonya kuwa “ndio hasa wanaofarakanisha [Kanisa]".

Askofu Strickland alikuwa chini ya uchunguzi wa Vatican na hapo awali alitupilia mbali uwezekano wa kujiuzulu, na katika barua ya wazi mwezi Septemba alimtaka Papa amfute kazi.

"Siwezi kujiuzulu kama Askofu wa Tyler kwa sababu kufanya hivyo itakuwa ninawatelekeza wana kondoo,” alisema.

Kwa mujibu wa Vatican, uamuzi wa kumfukuza umefikiwa baada ya “ziara ya kitume katika Jimbo la Tyler iliyoagizwa na Papa mwezi Juni".

Vyombo vya habari vya Kikatoliki vinaeleza kuwa uchunguzi huo pia uliangazia masuala ya kifedha katika jimbo hilo.

Askofu Strickland, 65, aliteuliwa kuwa askofu mwaka 2012, wakati wa Papa Benedikto XVI.

Vatican imesema kuwa Jimbo la Tyler kwa sasa litaongozwa kwa mpito na Askofu Joe Vasquez wa Jimbo la Austin.

Hatua hii inafuatia hatua mahususi zinazochukuliwa na Papa ili kulifanya Kanisa Katoliki kuendana na wakati kwenye utawala wake.

Siku ya Alhamisi, Vatican ilitangaza kuwa watu waliobadili jinsia wanaweza kubatizwa katika Kanisa Katoliki ilimradi kwa kwa kufanya hivyo hakutazua kashfa ama “mchafuko”.

Mwezi Oktoba Papa alisema kuwa Kanisa linaweza kukubali kubariki wanandoa wa jinsi moja, huku akiwaeleza makardinali kuwa "hatuwezi kuwa majaji ambao tunachofanya ni kukana, kukataa na kutenga tu".

Akizungunza katika mkutano wa Siku ya Vijana Duniani jijini Lisbon Papa alisema kuwa mgando wa fikra wa baadhi ya watu “hauna manufaa”.

"Kwa kufanya hivyo unapoteza utamaduni halisi na utategemea itikadi ili kuungwa mkono. Kwa maana nyingine, itikadi inachukua nafasi ya imani,” aliongeza kusema.

Mabadiliko ya tabianchi pia imekuwa ni moja ya ajenda kuu ya utawala wa Papa Francis - ambapo mwaka 2015 alitoa chapisho muhimu kuhusu mazingira ambalo lilionya kuwa dunia ilikuwa inaelekea hatua mbaya zaidi kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Papa pia amewashutumu vikali wale wote wanaokanusha mabadiliko ya tabianchi na anatazamiwa kuwa katika mkutano wa mazingira wa Umoja wa Mataifa wa COP28 baadae mwezi huu huko Dubai.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Papa kuhudhuria toka mikutano hiyo ianzishwe mwaka 1995.

Chanzo: BBC
 

Attachments

  • IMG_20231109_231209.jpg
    IMG_20231109_231209.jpg
    124.7 KB · Views: 6
Msimamo wa Papa Francis nauelewa vizuri sana, hayupo mwenye dhambi anayetakiwa kutengwa, hata Yesu Kristu hakuja duniani kwa ajili ya wenye haki, alikuja kwa wenye dhambi ili wapate kuokoka.

Huyo bishop aliyesimamishwa kazi kwa ajili ya uchunguzi angetakiwa kutuambia, mtu mwenye dhambi ukishamtenga utakuwa umemsaidiaje kuachana na hiyo dhambi yake? atuambie ni biblia ipi iliyomfundisha hivyo?

Kuliko kujitetea kwa kusema tu hayo mambo ya ushoga yanaharibu nature, nature haiwezi kuharibiwa kwa sababu ya mambo yanayofanywa na wawili waliopotoka, nature inaharibiwa kama hiyo tabia ndio itageuka mfumo rasmi wa kukutana na mwenza duniani kote, jambo ambalo kiuhalisia haliko hivyo.

Siku zote mwenye dhambi sio wa kumnyooshea kidole na kumhukumu, ni wa kumuombea abadilike, ndio maana maandiko yanasema usihukumu ili nawe usije hukumiwa, huyo bishop anaonekana kabisa amepanic.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
miaka 12 ndani ya JF ila bado uandishi wako unakuwa na walakini mkubwa sana..

Hebu jitafakari mkuu unaweza kuwa na taarifa nzuri ila uwasilishaji ukawa mbovu mbovu tu.
Sina hakika humu ndani tunafundishwa kuandika
 
Msimamo wa Papa Francis nauelewa vizuri sana, hayupo mwenye dhambi anayetakiwa kutengwa, hata Yesu Kristu hakuja duniani kwa ajili ya wenye haki, alikuja kwa wenye dhambi ili wapate kuokoka...
Ndiyo maana wezi hawaishi
 
Back
Top Bottom