rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 15,191
- 20,158
Toka tuanze mfumo wa vyama vingi nimekuwa nikivifatilia vyama vyote lakini chama tawala bado kimeendelea kuongoza kimuundo kwani kimekuwa na mizizi toka ngazi ya chini kulinganisha na vyama vingine pia ni chama ambacho kimeweza kusambaa tanzania nzima na ndio maana imeweza kuvishambulia vyama vingine ni vya kikabila au kidini.
Uimara wa CCM umechangiwa na kuwa chama pekee ambacho kina makada waliofundishwa ingawa baada ya kuingia vyama vingi walianza kupokea wanachama wa papo hapo mtindo ulioanzishwa na mrema huko kigoma wakati akiwa waziri wa mambo ya ndani vyama vingine vimeendelea kukusanya wanachama ambao wengi hawajui hata itikadi ya vyama husika kwani hawapewi mafunzo yoyote.
Pamoja na sifa zote hizo chama hicho kilianza kupoteza mwelekeo pale kilipovunja azimio la arusha na kuja na azimio la zanzibar ambalo kwa kiasi kikubwa kiliua maadili ya uongozi. Ingawa kiliua maadili ya uongozi kilizidi kupoteza mwelekeo pale kilipotengeneza mtandao wa kumwingiza rais aliyeko sasa madarakani.
Kwa sasa wale makada waliokuwa wakitetea chama hawapewi nafasi badala yake wapambe wa viongozi wamekuwa ndio wana sauti mtindo uliopewa nguvu wakati wa uongozi wa yusuph makamba.sasa hivi viongozi wengi wa CCM wamekuwa wakiwaza kutengeneza safu ya uongozi kwa ajili ya urais (mitandao) badala ya kutumikia wananchi na kwa wale waliopewa dhamana wamekuwa wakiwaza namna gani watajinufaisha wao binafsi, familia zao na jamaa zao imekuwa kawaida mtu anapoteuliwa kiongozi muda mfupi anakuwa na ukwasi wa ajabu. Pamoja na yote hayo bado chama hicho kimebaki na hazina ya viongozi kwani hata wakati wa uchaguzi wabunge wengi wa upinzani ni wale walioenguliwa toka ccm tukianzia na yule anayeisumbua CCM kwa sasa Dr. Slaa.
Pamoja na kuelewa vyama vya upinzani bado vichanga lakini kwa hali tuliyoifikia hivi sasa CCM haiwezi kujirekebisha mpaka tuiweke pembeni ili wajue ni nini wananchi walichokuwa wanahitaji toka kwao. Kwani sasa hivi nchi inaendeshwa kienyeji mno kuanzia ugawaji wa vyeo hauzingatii sifa bali kujuana na nani ni mpambe wangu.
Rushwa imehalarishwa kuanzia rushwa ya ngono sasa hivi tunashuhudia dada zetu na mama zetu wanavyojirahisi ili tu wapate nafasi za uongozi au kisiasa pamoja na rushwa nyingine na tatizo hili ni kuanzia ngazi ya chini hadi ya juu (mfumo mzima umeoza) wizi umehalalishwa kwa ngazi zote juu hadi chini leo hii ni fahari mtu kuoneka au kuwa tajiri bila kujulikana huu utajiri ameupata kihalali au la.serikali kuwa na kigugumizi cha kuchukua hatua hata pale inapoonekana makosa dhairi yametendeka kwa kutaja machache meremeta, kagoda,tbs, pesa zilizofichwa uswisi, rada.
Mmonyoko mkubwa wa kimaadili kupitia baadhi ya vyombo vya habari, kushindwa kulinda na kusimamia rasilimali za taifa kama madini, maji, gesi na ardhi na pia kushindwa kutoza kodi stahili kwa makampuni ya migodi na simu. Kuruhusu uchochezi wa kidini na pia kushindwa kusimamia muungano. Kuendelea kwa mauaji yanayofanywa na polisi bila kuchukua hatua za kimsingi.
Makosa yaliyopo yapo mengi sana lakini tukifanya kosa kuendelea kuichagua CCM haaitajirekebisha kamwe badala yake inabidi tuiweke kando ili wale walioivamia CCM wajichuje na kikirudi kiwe chama kilichozaliwa upya.
Uimara wa CCM umechangiwa na kuwa chama pekee ambacho kina makada waliofundishwa ingawa baada ya kuingia vyama vingi walianza kupokea wanachama wa papo hapo mtindo ulioanzishwa na mrema huko kigoma wakati akiwa waziri wa mambo ya ndani vyama vingine vimeendelea kukusanya wanachama ambao wengi hawajui hata itikadi ya vyama husika kwani hawapewi mafunzo yoyote.
Pamoja na sifa zote hizo chama hicho kilianza kupoteza mwelekeo pale kilipovunja azimio la arusha na kuja na azimio la zanzibar ambalo kwa kiasi kikubwa kiliua maadili ya uongozi. Ingawa kiliua maadili ya uongozi kilizidi kupoteza mwelekeo pale kilipotengeneza mtandao wa kumwingiza rais aliyeko sasa madarakani.
Kwa sasa wale makada waliokuwa wakitetea chama hawapewi nafasi badala yake wapambe wa viongozi wamekuwa ndio wana sauti mtindo uliopewa nguvu wakati wa uongozi wa yusuph makamba.sasa hivi viongozi wengi wa CCM wamekuwa wakiwaza kutengeneza safu ya uongozi kwa ajili ya urais (mitandao) badala ya kutumikia wananchi na kwa wale waliopewa dhamana wamekuwa wakiwaza namna gani watajinufaisha wao binafsi, familia zao na jamaa zao imekuwa kawaida mtu anapoteuliwa kiongozi muda mfupi anakuwa na ukwasi wa ajabu. Pamoja na yote hayo bado chama hicho kimebaki na hazina ya viongozi kwani hata wakati wa uchaguzi wabunge wengi wa upinzani ni wale walioenguliwa toka ccm tukianzia na yule anayeisumbua CCM kwa sasa Dr. Slaa.
Pamoja na kuelewa vyama vya upinzani bado vichanga lakini kwa hali tuliyoifikia hivi sasa CCM haiwezi kujirekebisha mpaka tuiweke pembeni ili wajue ni nini wananchi walichokuwa wanahitaji toka kwao. Kwani sasa hivi nchi inaendeshwa kienyeji mno kuanzia ugawaji wa vyeo hauzingatii sifa bali kujuana na nani ni mpambe wangu.
Rushwa imehalarishwa kuanzia rushwa ya ngono sasa hivi tunashuhudia dada zetu na mama zetu wanavyojirahisi ili tu wapate nafasi za uongozi au kisiasa pamoja na rushwa nyingine na tatizo hili ni kuanzia ngazi ya chini hadi ya juu (mfumo mzima umeoza) wizi umehalalishwa kwa ngazi zote juu hadi chini leo hii ni fahari mtu kuoneka au kuwa tajiri bila kujulikana huu utajiri ameupata kihalali au la.serikali kuwa na kigugumizi cha kuchukua hatua hata pale inapoonekana makosa dhairi yametendeka kwa kutaja machache meremeta, kagoda,tbs, pesa zilizofichwa uswisi, rada.
Mmonyoko mkubwa wa kimaadili kupitia baadhi ya vyombo vya habari, kushindwa kulinda na kusimamia rasilimali za taifa kama madini, maji, gesi na ardhi na pia kushindwa kutoza kodi stahili kwa makampuni ya migodi na simu. Kuruhusu uchochezi wa kidini na pia kushindwa kusimamia muungano. Kuendelea kwa mauaji yanayofanywa na polisi bila kuchukua hatua za kimsingi.
Makosa yaliyopo yapo mengi sana lakini tukifanya kosa kuendelea kuichagua CCM haaitajirekebisha kamwe badala yake inabidi tuiweke kando ili wale walioivamia CCM wajichuje na kikirudi kiwe chama kilichozaliwa upya.