Orodha ya Watanzania maarufu waliokufa bila kujenga nyumba

mdukuzi

JF-Expert Member
Jan 4, 2014
16,274
36,635
1. Dkt. Omar Alli Juma
Huyu alikuwa VP kipindi cha BWM, baada ya kufariki akiwa madarakani, familia yake ilitakiwa kupisha nyumba rasmi ya VP iliyopo nyuma ya St Peters Oysterbay ili Dkt. Shein VP mteuliwa aweze kuingia humo, wakawa hawana pa kuweka vyombo, hawana nyumba, ikabidi lori la erikali liwatoe kinguvu na kwenda kusitiriwa kwenye magofu ya Serikali


2. Gilman Rutihinda
Huyu alikuwa gavana wa BoT enzi za Mwinyi, tulimzika Buguruni Malapa maana kwao Ngara hakuwa na nyumba bali kijumba.


3.Brigedia Moses Nnauye
Huyu alikufa mwaka 2000 kama sikosei, ilibidi msiba tuupeleke kwa mzee Makamba maana tulikosa sehemu ya kufunga turubai kwenye zile flats za NHC, utafunga turubai kwenye flats?
Aliwahi kuwa brigedia jeshini,Naibu Waziri ulinzi,Mkuu wa wilaya Bagamoyo,mkuu w mkoa Singida,mhamasishaji wa CCM,Katibu mwenezi CCM,naibu katibu mkuu CCM Nk


4. Profesa Shaba
Huyu sijui yupo hai au, anasifika kuufanyia post mortam mwili wa hayati Sokoine, mpaka anastaafu na kumaliza kiinua mgongo hakuwahi kujenga hata choo. Alipostaafu aliigomea Serikali kuachia nyumba iliyokuwa mitaa ya Shaaban Robert karibu na Gymkhkana DSM.

Akiwatisha kuwa ataanika kilichomuua Sokoine if at all they try to vacate him, wakampotezea.


5. Steven Kanumba
Pamoja na kumiliki gari ya mamilioni kadhaa alikufa hajawahi kujenga hata kiosk

6. Ray Kigosi(yuko hai)
Bado anaishi kwa mama yake Sinza hajui hata mfuko wa cement inatoa tofali ngapi

7.TiD Top in Dar,mwanamuziki maarufu sliyegima kuhana jwao kinondoni,alishasema kazaliwa pale so pale ni kwake na ni kwao pia,kila mtu arudi kwao,ikaonekana wazazi wake ndio wanastahi kuondka pale sio yeye,japo hajachangia hata bati moja

Itaendelea
 
Back
Top Bottom