Obama: Tanzania ni mfano wa kuigwa

Watani zetu wa jadi wakiona hii interview nadhani wataanza tena yale makelele yao....
 
Pamoja na 'makaratasi' ya JK, zipo ripoti zinatoka Ubalozi wa Marekani nchini mwetu kuhusu Tanzania. Kwa jicho la 'jumla' Tanzania ni nchi ya Amani na Tulivu na yenye kutafuta maendeleo ya wananchi wake tangu nchi ilipopata Uhuru. Hilo peke yake linaweza kupelekea Rais yeyote anayelinganisha Tanzania na nchi zingine za Bara letu kuweza kusifia na kusema ni mfano wa kuingwa. Ukiweka kando uozo unaojitokeza hapa na pale bado nchi yetu ni mfano mzuri barani Africa. Obama hajakosea!

Ni kweli kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana. Ina kila kitu kinachohitajika kuwa bora zaidi na kuzidi. Vile vile ina watu wenye roho ya huruma na wakarimu kwa wageni na wenye matatizo. Ni nchi ambayo haijakumbwa na misukosuko ya kutisha na mikubwa ya hali ya hewa, vita vya wenyewe kwa wenyewe n.k. Ina ardhi nzuri yenye rutuba. Ni nchi yenye madini mengi na ya aina mbalimbali. Ina mbuga kubwa na nyingi za wanyama wanaoishi kwa utulivu mkubwa. Ni nchi yenye bahari yenye urefu wa kuzidi kilometer 1440. Ina maziwa, mabwawa na kadhalika. Mali halisi hizo, pamoja na watu wake, hazitumiki ipasavyo na hivyo bado zinaendelea kubaki virgin kama zilivyoumbwa. Hii inaifanya nchi hii kuwa kivutio cha wengi kutoka nje na hata Marekani (mfano Obama). Nyerere aliwahi kusema, tusipoangalia na kuhangaika kujikwamua kiuchumi, tutabaki duni na baadae tutakuwa kama zoo ambapo wengi watatusifia na kuja kutuangalia kama wanyama wanavyotembelewa mbugani. Labda hii ndio inaanza kujitokeza.

Tanzania hakuna la kujivunia kiutendaji (walau kwa sasa). Watu wake ni masikini wa kutupwa. Rasilimali zake zinaibiwa na wezi wa kimataifa na wa kila aina. Labda hili ndilo linalompa faraja Mhe. Obama. Anaona angalau anapo pakuanzia kunyanyua uchumi wa nchi yake. Kwani anaona kuna mahali anapoweza kupata rasilimali za kuinua uchumi kwa haraka. Hasa anaposikia kuwa kuna uwezekano wa kuwepo kwa mafuta huko Zanzibar.

Tusubiri tuone kauli zinavyotulevya.
 
Huyo Mzungu wako Masatu,
Amenyongwa au kajinyonga? Maana watu wamemzunguka na mama anamfokea utafiikiri jamaa alimuharibia mtoto wake wa Kiume (mambo ya UK na u-Pedo...).

Kama umejihangaisha kuweka picha ya mtu anajinyonga basi tafuta ya kweli na si MTU ANANYONGWA. Wee vipi bwana, yaani WWW zote hizi duniani umekosa picha hata moja ya mtu anajinyonga?

Juu ya Kikwete kusifia Obama au ukitaka geuza na kuwa Obama anamsifia Kikwete/Tanzania, si kila mara yuko kule? Anatoa ajira kwa USA kwenye mahoteli, Airports, highways, parkings etc. Pia investment zao kibao zipo pale Tz.

Labda niungane na Mtanzania. Nilishakutana na Lawyer mmoja kutoka Nigeria (mzee na umri wake) na nikaanza kupaka juu ya Tanzania. Akaniuliza kama nilishawahi kufika nchi yoyote ya Africa zaidi ya Tanzania, nikasema hapana (kumbuka Gabon niliishia Airport tu), akacheka kidogo na kuniambia:-
" I was in Tanzania, Dar es salaam. I have visited a lot of countries in Africa and i must tell you that, Tanzania you are much better than many other countries in Africa..."
Nikamwambia kuwa, wee uliishia Dar na hukuenda huko madongo kuinama.... akaongeza kuwa nchi nyingine hata hiyo Dar yao kwa kweli ni mzinga wa soo, sasa itakuwa huko Madongo kuinama??

Ila still sisi Watz tungelipenda walau tuwe tunalinganishwa na nchi kama SA, Egypt, Botwsana etc na siyo Sudan, Somalia, Ethiopia etc...

Sasa Masatu, maadamu tunajua tunachosema/kushutumu na tunafahamu kuwa mambo uozo upo pote, nani anyongwe? Wewe au sisi? Wahiwahi uje Tabora, ntakuandalia kabisa Ngoye ya Myombo chini ya Mangle tree pale shule ya Kanyenye itakusaida sana kukupunguzia hasira kwani siye ndiyo tumego.... tumegoma baba yangu kujinyonga wala kunyongwa.....

MkamaP, heheee , Lyongo (mhogo mchungu) anasema karoti wajinyinge. Walau angelisema Mpare Magimbi....... (maana yake ni Masatu hujambo?)
 
"alisema jana kuwa kila atakakopita ataziambia nchi hizo za Afrika ziige mfano wa Tanzania."
Kama habari hii ni ya kweli kabisa na si kwamba anatupiga changa la macho, naanza kudoubt credibility ya Obama. Hivi kweli Marekani inaye balozi hapa nchini, ina mashushushu kibao na vifaa vya kuangalia matukio yote duniani Rais wake anaweza asiwe makini kiasi hiki?
Eti nchi zingine ziige mfano wa TZ ; kwa yafatayo!:
-Viongozi walio madarakani kutokubali kushindwa? (angalia uchaguzi wa Biharamulo, Zanzibar) nk.
-Kuacha sumu ikawaua wananchi wake kwa kuthamini mno wawekezaji?(Angalia North Mara -au naye ana hisa humo?)
-Kufisadi hela za wananchi na kuwaacha mafukara wa kutisha?
Kufisadi hela za wafadhili? (angalia zile za maliasili)
-Kubwa zaidi ni kuitumbukiza nchi katika vita na migogoro ya kidini. Ebu asubiri islamic courts kama za Somalia zianzishwe Tz ndipo atajua kuwa kauli yake ilikuwa ya kipuuzi.

Nawasihi viongozi makini wa Africa, msiige Tanzania. Hata hiyo inayoitwa amani haipo bali ni ujinga tu. Msiige TZ kwa kuwafanya wananchi wenu wajinga na makondoo kama TZ.

Bahati mbaya wenzako sio mambumbumbu wa demokrasia! Hivi honnestly speaking, kuna siku Opposition imeshindwa kwenye uchaguzi ikakubali matokeo bila kulalamika CCM imeiba kura?

Acha Rais wa Marekani atoe credit kwa Tanzania. Ni kweli tunahitaji kufanya vizuri zaidi, ila panapostahili pongezi ni uungwana kupiga makofi kidogo!
 
Hujaelewa! soma kasome tena bandiko, kwa kifupi issue sio "utajiri" kama ni utajiri angezungumzia SA, Botswana, Nigeria etc.Kibaya zaidi issue pia sio yeye kazaliwa wapi!

Yaani huwezi kuchangia bila kuonyesha rangi yako.You are prejudicative really you are!
Masatu,nawasiwasi na credibility yako! kati yako wewe na mchukia ufisadi nani amefanya reflection ya post hapo juu?Nahisi mzee hukuwa na haja ya kuamua tu kumkosoa Mchukia ufisadi, kwa critical thinking yake na ndiyo maana tuko kwenye hii forum.


Kwa nini asiseme nchi yake ya kuzaliwa ya Kenya ambayo iko juu kiuchumi na kihuduma kuliko sisi?
Wale kwanza shule ni bure kabisa sisi tunalipa.
Hospitali ndio usiseme hadi viongozi wetu wengine wanakimbizwa huko.
Lakini mimi sishangai maana hawa wamarekani wanasifia mahali wanapodhani watapata maslahi. Si ajabu kapewa ahadi ya mgodi hapo.
Masatu umesikia?
Sisi si wamarekani wala hatusubiri wamarekani kuja kuwa kipimo cha maendeleo mfu yetu. Sisi waliwanchi ndio hasa kipimo chenyewe. Tunapima wenyewe Sisi hasa tunaoishi danganyika hii na si watanzania mlioamua kuishi ulaya au kuila nchi. Pole kama mnadhani Obama atakuwa mpima mafanikio yetu.
 
Kwa kusema ukweli kuwa Sisi tuna matatizo yetu hivyo wao hawajui kiundani yaani mfumo na Bunge letu hata demokrasi ya Kweli, Hata Ben naye walisema hivi hivi
 
obama anaposema nchi ya Tanzania iwe ndio mfano wa kuigwa na nchi zingine anazungumzia nini, anazungumzia Elimu duni tuliyonayo, hospitali zetu, au kesi za rushwa za EPA, NA WIZI W BOT, AU BARABARA MBOVU, AU BUNGE LENYE MAJUNGU, AMA NJAA, AU ANATAMANI TANZANIA KATIKA MTAZAMO UPI? simuelewi Obama
 
Huyo Mzungu wako Masatu,
Amenyongwa au kajinyonga? Maana watu wamemzunguka na mama anamfokea utafiikiri jamaa alimuharibia mtoto wake wa Kiume (mambo ya UK na u-Pedo...).

Kama umejihangaisha kuweka picha ya mtu anajinyonga basi tafuta ya kweli na si MTU ANANYONGWA. Wee vipi bwana, yaani WWW zote hizi duniani umekosa picha hata moja ya mtu anajinyonga?

Juu ya Kikwete kusifia Obama au ukitaka geuza na kuwa Obama anamsifia Kikwete/Tanzania, si kila mara yuko kule? Anatoa ajira kwa USA kwenye mahoteli, Airports, highways, parkings etc. Pia investment zao kibao zipo pale Tz.

Labda niungane na Mtanzania. Nilishakutana na Lawyer mmoja kutoka Nigeria (mzee na umri wake) na nikaanza kupaka juu ya Tanzania. Akaniuliza kama nilishawahi kufika nchi yoyote ya Africa zaidi ya Tanzania, nikasema hapana (kumbuka Gabon niliishia Airport tu), akacheka kidogo na kuniambia:-
" I was in Tanzania, Dar es salaam. I have visited a lot of countries in Africa and i must tell you that, Tanzania you are much better than many other countries in Africa..."
Nikamwambia kuwa, wee uliishia Dar na hukuenda huko madongo kuinama.... akaongeza kuwa nchi nyingine hata hiyo Dar yao kwa kweli ni mzinga wa soo, sasa itakuwa huko Madongo kuinama??

Ila still sisi Watz tungelipenda walau tuwe tunalinganishwa na nchi kama SA, Egypt, Botwsana etc na siyo Sudan, Somalia, Ethiopia etc...

Sasa Masatu, maadamu tunajua tunachosema/kushutumu na tunafahamu kuwa mambo uozo upo pote, nani anyongwe? Wewe au sisi? Wahiwahi uje Tabora, ntakuandalia kabisa Ngoye ya Myombo chini ya Mangle tree pale shule ya Kanyenye itakusaida sana kukupunguzia hasira kwani siye ndiyo tumego.... tumegoma baba yangu kujinyonga wala kunyongwa.....

MkamaP, heheee , Lyongo (mhogo mchungu) anasema karoti wajinyinge. Walau angelisema Mpare Magimbi....... (maana yake ni Masatu hujambo?)

Sikonge
NSansa imekuelemea nini mbona wachonga sana teh teh teh teh teh.

Watu tunachonga sana wakati ukweli nchi zingine za afrika hatujatembelea na kuona mambo yanakwenda je.

Ukitaka kuona zari wewe shukia tu uwanja wa jommo kinyata pale Nairobi kila kitu unachofanya lazima utowe ushuru wa Mgingiki.

Yani kama kwako una umeme lazima ulipe kwa serikali na kwa mungiki kama una daladala lazima ulipe ya kodi ya serikali na ya mungiki na kama una nyumba lazima ulipie ardhi ya serikali na ya mungiki.

Ukikosea ukatuwa Nigeria kule balaa tupu ,miji karibu yote huwa ukikaribia wanakuwa wameandika welcome Dar es salaa,....... lakini pale nigeria utakutana na kitu hiki THIS IS LAGOS hakuna cha welcome ndani ya Nigeria
 
Kwa kusema ukweli kuwa Sisi tuna matatizo yetu hivyo wao hawajui kiundani yaani mfumo na Bunge letu hata demokrasi ya Kweli, Hata Ben naye walisema hivi hivi

Wee sema kingine ,hawa wazungu wanajuwa mno mambo yetu kuliko sisi wenyewe tunavyojuwa mambo yetu hasa ya serikali.Hizo mikataba mnazoambiwa ni siri ya serikali wao ndio huanza kuisoma hiyo mikataba na kwao sio siri tena,sema kingine lakini eti ohoo jamaa anasema hajui kuhusu Tz hapo umelamba nyanda moja wa karanga
 
Asie jua maana haambiwi maana.na yeye karubuniwa tu ikosiku ataleta watuwake kutafiti atapata majibu.hawezi kusifia Kenya kwasababu wazungu watamkalia kichwani.
 
Masatu kweli usijari tu uzalondo na kusahau tabu na adha zilizomo nchini.Nikweli mafanikio yapo na siyakutisha pia kumbuka tembo akisifiwa .....Na pia kumbuka wenzetu wanateseka huko mara wanakunywa maji yenye chemicals isitoshe wanauana,shinyanga ukame ,kagera uaribifu wa mazingira na swala la ajira kwa vija nikawa wimbo wa taifa .think about it.
 
Wenzetu wanapotoa kauli kama hizo huwa hawa kurupuki kua mechanism in place. Kwa kuwa tumezoea siasa za Mwembe yanga na kupayuka ovyo tunadhani na wenzetu nao ndio hivyo hivyo
 
Kwa vyo vyote vile kuna maendeleo hapa. Lakini cha kushangaza jirani zetu katika magazeti yao hawataki kukubaliana na Credits alizotoa OBAMA. Wao wanadai eti kakandia waafrika wote wakati si kweli. ANGALIA HAPA CHINI

http://www.nation.co.ke/News/world/-/1068/622174/-/sy7r0q/-/index.html
 
You know the Italian Prim Minister already told them he got the h***s lines up, just say the word...


610x.jpg

mhhhhh


ap162166140807163421_big.jpg


agf162166590807163418_big.jpg

Sarkozy: Hit or miss?

Obama
"Id skeet all over her back!!!"

and this is the guy that probably set them up
silvio_berlusconi_10.jpg
 
GT,
Ikianza MAHAKAMA ya Kadhi, na uroho wako huo, utakiona cha moto.
Badala ya kusema ASTAKAFLILAH, wee ndiyo kwanza watuletea na sisi wengine tuingie majaribuni? Wee Muislaam mwenzao wee!!!!
 
Wenzetu wanapotoa kauli kama hizo huwa hawa kurupuki kua mechanism in place. Kwa kuwa tumezoea siasa za Mwembe yanga na kupayuka ovyo tunadhani na wenzetu nao ndio hivyo hivyo

Wenzetu unamaanisha wale waliosema kuwa Iraq in WMD?

Au wale walimuunga mkono Mobutu na utawala wake for yrs?

Hao wenzetu kweli ..... hawakurupuki
 
Back
Top Bottom