Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
Hii ni kauli ya Serikali kupitia kwa Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba.
----
Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Tanzania imekuwa ikichukuliwa kama nchi ya mfano Duniani ukilinganisha na mataifa mengine Barani Afrika kutokana na hatua kubwa na ya haraka iliyopiga kwenye sekta mbalimbali kama vile afya, nishati hususani umeme, maji na elimu suala ambalo linaashiria kufikiwa viashiria vya malengo iliyojiwekea
Dkt. Nchemba amesema hayo leo, Jumanne Machi 12.2024 wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi jengo la Taaluma la chuo cha Uhasibu Arusha (Kampasi ya Dodoma) linalojengwa kwenye eneo la Njedengwa, jijini Dodoma ambapo amesema tatizo kubwa linalotukabili hapa nchini ni suala la kujidharau wenyewe kwa vile tunavyofanya, lakini uhalisia ni kwamba Tanzania imekuwa ikichukuliwa kama mfano wa kuigwa miongoni mwa mataifa mengi Barani Afrika
Amesema hadi kufikia sasa asilimia kubwa ya maeneo ya nchi yameunganishwa kwa Barabara za lami, huku ajenda ya umeme sasa inajadiliwa kufikishwa kwenye ngazi za vitongoji na mtu mmoja mmoja, uwepo wa vituo vya afya kwenye kila tarafa, na suala la serikali kubeba gharama za elimu kuanzia ngazi ya awali hadi elimu ya juu ni ushahidi tosha wa kauli yake kwa kuwa bajeti ya elimu ya juu pekee inakaribia trilioni moja kila mwaka
Akizungumzia zoezi la uwasilishwaji wa mpango wa maendeleo ya Taifa na ukomo wa bajeti kwa mwaka ujao wa fedha wa 2024/25 Waziri Dkt. Nchemba amebainisha kuwa katika bajeti hiyo inayofikia trillioni 49 vipaumbele mbalimbali vimezingatiwa ambapo kati ya fedha hizo fedha za maendeleo ni trillioni 16, bajeti kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya mataifa huru ya Afrika (AFCON) inayotarajiwa kufanyika 2027 hapa nchini kwa ushirikiano wa Kenya na Uganda imetengwa shilingi bilioni 200, uchaguzi mkuu wa mwakani (2025) shilingi bilioni 600, wakati uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu (2024) ukiwekewa bilioni 300, sambamba na hilo amesema deni halisi la Taifa nje ya riba ni trilioni tano (5) lakini hata ukiweka na riba deni hilo halizidi trilioni 10 ambapo deni hilo linatokana na miradi mikubwa ikiwemo ujenzi wa reli, vivuko ikiwemo kivuko kikubwa cha Kigongo - Busisi, ujenzi wa vyuo vikuu, mabweni nk
Chanzo: Jambo Tv
----
Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Tanzania imekuwa ikichukuliwa kama nchi ya mfano Duniani ukilinganisha na mataifa mengine Barani Afrika kutokana na hatua kubwa na ya haraka iliyopiga kwenye sekta mbalimbali kama vile afya, nishati hususani umeme, maji na elimu suala ambalo linaashiria kufikiwa viashiria vya malengo iliyojiwekea
Dkt. Nchemba amesema hayo leo, Jumanne Machi 12.2024 wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi jengo la Taaluma la chuo cha Uhasibu Arusha (Kampasi ya Dodoma) linalojengwa kwenye eneo la Njedengwa, jijini Dodoma ambapo amesema tatizo kubwa linalotukabili hapa nchini ni suala la kujidharau wenyewe kwa vile tunavyofanya, lakini uhalisia ni kwamba Tanzania imekuwa ikichukuliwa kama mfano wa kuigwa miongoni mwa mataifa mengi Barani Afrika
Amesema hadi kufikia sasa asilimia kubwa ya maeneo ya nchi yameunganishwa kwa Barabara za lami, huku ajenda ya umeme sasa inajadiliwa kufikishwa kwenye ngazi za vitongoji na mtu mmoja mmoja, uwepo wa vituo vya afya kwenye kila tarafa, na suala la serikali kubeba gharama za elimu kuanzia ngazi ya awali hadi elimu ya juu ni ushahidi tosha wa kauli yake kwa kuwa bajeti ya elimu ya juu pekee inakaribia trilioni moja kila mwaka
Akizungumzia zoezi la uwasilishwaji wa mpango wa maendeleo ya Taifa na ukomo wa bajeti kwa mwaka ujao wa fedha wa 2024/25 Waziri Dkt. Nchemba amebainisha kuwa katika bajeti hiyo inayofikia trillioni 49 vipaumbele mbalimbali vimezingatiwa ambapo kati ya fedha hizo fedha za maendeleo ni trillioni 16, bajeti kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya mataifa huru ya Afrika (AFCON) inayotarajiwa kufanyika 2027 hapa nchini kwa ushirikiano wa Kenya na Uganda imetengwa shilingi bilioni 200, uchaguzi mkuu wa mwakani (2025) shilingi bilioni 600, wakati uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu (2024) ukiwekewa bilioni 300, sambamba na hilo amesema deni halisi la Taifa nje ya riba ni trilioni tano (5) lakini hata ukiweka na riba deni hilo halizidi trilioni 10 ambapo deni hilo linatokana na miradi mikubwa ikiwemo ujenzi wa reli, vivuko ikiwemo kivuko kikubwa cha Kigongo - Busisi, ujenzi wa vyuo vikuu, mabweni nk
Chanzo: Jambo Tv